LOVE DAMINI YA BURNA BOY YAWEKA REKODI BOOMPLAY

LOVE DAMINI YA BURNA BOY YAWEKA REKODI BOOMPLAY

Mwanamuziki kutoka Nigeria Burna Boy anaendelea kufanya vizuri kupitia album yake mpya na ya sita katika muziki wake iitwayo “Love, Damini” ambayo ilitoka rasmi Julai 8 mwaka huu. Habari njema ni kwa mashabiki wa mkali huyo ni kwamba, ameweka rekodi katika mtandao wa Boomplay kwa album yake hiyo yenye mwezi mmoja na siku kadhaa tangu itoke kufikisha Streams zaidi ya Milioni 100. Kufuatia hilo Burna Boy anakuwa msanii mwenye jumla ya Streams nyingi katika akaunti yake ya Boomplay akiwa na Streams Milioni 402.4 Mbali na hayo, album ya “Love, Damini” yenye hits mbalimbali kama “Kilometre” inashikilia rekodi ya muda wote kwa kuingiza nyimbo nyingi mfululizo kwenye chart mpya za muziki za Billboard US Afrobeats. Burna ameingiza nyimbo 19 zote toka kwenye album yake “Love, Damini.”

Read More
 BURNA BOY AKIRI LAST LAST NDIO WIMBO ULIOMUINGIZIA PESA NYINGI KATIKA MUZIKI WAKE

BURNA BOY AKIRI LAST LAST NDIO WIMBO ULIOMUINGIZIA PESA NYINGI KATIKA MUZIKI WAKE

Burna Boy ameweka wazi kwamba wimbo wake “Last Last” umemuingizia pesa nyingi zaidi kuliko wimbo wake wowote ambao amewahi kuutoa. Wimbo huo ambao unapatikana kwenye album yake mpya ‘Love Damini’ uliachiwa rasmi mwezi Mei mwaka huu. Aidha asilimia 60 ya mapato ya wimbo huo yanaenda kwa Mwanamuziki wa Marekani Toni Braxton kwa kutumia kionjo cha wimbo wake ‘Not Man Enough’ wa mwaka 2000. Hata hivyo wimbo wa “Last Last” umeingia rasmi kwenye Chart za Billboard Hot 100, ngoma hiyo imechumpa na kukamata nafasi ya 86 kwenye chart hiyo wiki hii. Huu unakuwa wimbo wa kwanza kwa Burna Boy kufikia mafanikio makubwa kwenye chart hizo na pia ndio ingizo lake la kwanza. Aidha Album yake mpya (Love Damini) imechumpa hadi nafasi ya 14 kwenye chart za bora, Billboard 200.

Read More
 BURNA BOY AWEKA REKODI KUPITIA ALBUM YAKE MPYA LOVE DAMINI

BURNA BOY AWEKA REKODI KUPITIA ALBUM YAKE MPYA LOVE DAMINI

Mwanamuziki kutoka Nigeria Burna Boy ameachia rasmi album yake mpya “Love Damini” yenye jumla ya ngoma 19 ikiwa na kolabo 9 pekee, huku kubwa nikutoka kwa wasanii wa Kimataifa akiwemo Ed Sheeran, J Balvin na Khalid. Good news, Album mpya ya Burna Boy “Love, Damini” imekuwa Album ya Kiafrika iliyoshika nafasi za juu zaidi kwenye chart za US iTunes baada ya kukamata namba 2 ikiwa ni chini ya masaa machache tangu iachiwe rasmi leo Julai 8. “Love Damini” ni album ya sita kwa Burna Boy baada ya kupata mafanikio makubwa na album yake ‘Twice as Tall’ iliyotoka mwishoni mwa mwaka 2020.  

Read More
 BURNA BOY AACHIA RASMI TRACKLIST YA ALBUM YAKE

BURNA BOY AACHIA RASMI TRACKLIST YA ALBUM YAKE

Mwanamuziki kutoka Nigeria Burna Boy ameachia rasmi orodha ya ngoma zinazopatikana kwenye album yake mpya ya Love Damini ambapo ina jumla ya ngoma 19 ikiwa na collabo 9 pekee. Mkali huyo ambaye Julai 2 alisherehekea kumbukumbu ya kuzaliwa kwake, amewapa mashavu wasanii kama J Balvin, Ed Sheeran na wengine wengi kwenye album yake hii mpya. Album hiyo inatoka Julai 8, Ijumaa ya wiki hii. “Love Damini” inakuwa ni album ya sita kwa Burna Boy baada ya kupata mafanikio makubwa na album yake ‘Twice as Tall’ iliyotoka mwishoni mwa mwaka 2020.

Read More
 BURNA BOY AWAKOSOA MASHABIKI KUHUSU MAPOKEZI YA WIMBO WAKE “LAST LAST”

BURNA BOY AWAKOSOA MASHABIKI KUHUSU MAPOKEZI YA WIMBO WAKE “LAST LAST”

Mwanamuziki wa Nigeria Burna Boy amejitokeza kukosoa mashabiki zake kwa jinsi wamepokea wimbo wake uitwao “Last Last”. Kupitia akaunti yake rasmi ya mtandao wa Tik Tok Burna Boy amesema watu wanafurahia wakichezea wimbo huo ilhali ni wa maumivu ya mapenzi. Ujumbe huo umewaaminisha walimwengu kuwa huenda mwanamuziki huyo anapitia wakati mgumu kuhusiana na maswala ya mapenzi jambo lilomsababisha kuandika na kuimba wimbo huo. Mwezi Januari mwaka huu burna boy alisema kwamba hataki tena kuwa na hisia kama binadamu na alikuwa tayari kulipa kiasi chochote cha fedha kwa yeyote ambaye angesaidia kumwondolea hisia. Lawama zake ziliambatanishwa na tukio la mwanamuziki huyo kuachana na mpenzi wake Stefflon Don ambaye pia ni mwanamuziki wa nchini Uingereza. Uvumi kuhusu kutengana kwa wawili hao ulisheheni mitandaoni mwezi Disemba mwaka 2021 na siku chache baadaye Burna Boy akathibitisha kupitia Instagram ambapo aliandika kwamba yeye hana mke.

Read More
 BURA BOY ATIANI, AHUSIKA NA MAUJI YA WATU NIGERIA

BURA BOY ATIANI, AHUSIKA NA MAUJI YA WATU NIGERIA

Staa wa muziki wa Nigeria Burna Boy ameingia kwenye msala mzito mno wa mauaji. Kwa mujibu wa Polisi wa Lagos nchini Nigeria, wanawashikilia maafisa watano wa Polisi wenye ukaribu na Burna Boy kwa tuhuma ya kuwapiga risasi watu wawili kwenye Klabu ya Cubana usiku wa Juni 8, mwaka huu. Taarifa hizo zinaeleza kuwa, Polisi hao wanaomlinda Burna Boy walifika kwenye klabu hiyo na staa huyo ambaye alikwenda moja kwa moja kwenye sehemu ya VIP akiwa na wanawake watatu. Lakini wakiwa wanaendelea na starehe, Burna Boy alimuona mwanamke mwingine mzuri ambapo bila kujua ni mke wa mtu, alimtuma Polisi mmoja amshawishi mwanamke huyo ili aungane naye kwenye kula bata. Hapo ndipo kulipotokea vurugu kubwa ambapo mmoja wa maafisa hao wa Polisi alimpiga risasi ya paja mume wa mwanamke huyo na mtu mwingine kichwani na wanaendelea na matibabu baada ya kutolewa risasi mwilini. Inaelezwa kwamba wakati risasi zikipigwa, Burna Boy alikuwa akiamrisha wapigwe risasi huku akifurahia. Hata hivyo, mara baada ya tukio hilo, Burna Boy anadaiwa kutorokea nchini Hispania ambapo anasakwa ili akamatwe kwa msala huo huku Polisi hao wawili wakiwa nyuma ya nondo za mahabusu.

Read More
 BURNA BOY KUACHIA ALBUM YAKE MPYA MWEZI JULAI

BURNA BOY KUACHIA ALBUM YAKE MPYA MWEZI JULAI

Staa wa muziki kutoka Nigeria Burna Boy ametangaza rasmi kuachia album yake ya sita baada ya kupata mafanikio makubwa na album ya ‘Twice as Tall’ iliyotoka mwishoni mwa mwaka 2020. Akizungumza na mchekeshaji Trevor Noah kwenye, Burna boy amesema ataachia album yake mpya kwenye siku ya kuzaliwa kwake Julai 2 mwaka huu. Ikumbukwe, Burna Boy kwa sasa yupo Jijini New York Marekani kwa ajili ya tour yake ya “Space Drift” ambapo anatarajia kufanya show yake leo kwenye ukumbi wa ‘Madison Square Garden’ ambao unaingiza watu elfu 20 huku akiwa msanii wa kwanza kutoka Afrika kufanya show kwenye ukumbi huo.

Read More
 KIJANA ALIYESUKUMWA NA BURNA BOY AAPA KUVAA SHATI MWAKA MZIMA

KIJANA ALIYESUKUMWA NA BURNA BOY AAPA KUVAA SHATI MWAKA MZIMA

Kijana aliyesukumwa stejini na  Burna Boy ameahidi kutovua shati mwaka mzima, shati ambalo alilivaa usiku ule aliosukumwa wakati akijaribu kuomba msaada kwa Staa huyo wa muziki kutoka nchini Nigeria. Kwenye mahojiano na vyombo vya habari nchini Nigeria kijana huyo amesema ni fahari sana kwake na alifurahishwa na lile tukio ndio maana ameapa kulitunza mwilini shati hilo mwaka mzima. Lakini pia amekiri mapenzi yake kwa Burna Boy ni makubwa sana na anamuomba msaada na wasanii wengine wa Nigeria wamsaidie kwani ana kipaji cha kuimba.

Read More
 SHATTA WALE AMVUA NGUO BURNA BOY, ATOA MATUSI MAZITO

SHATTA WALE AMVUA NGUO BURNA BOY, ATOA MATUSI MAZITO

Bifu la Shatta Wale wa Ghana na Burna Boy wa Nigeria linaendelea kushika kasi, Shatta Wale ameibuka na kuweka wazi kuwa yupo tayari kuingia ulingoni na African giant, Burna Boy. Kupitia mfululizo wa tweets za matusi katika mtandao wa Twitter  Shatta Wale alionekana mwenye hasira huku akitoa vitisho kwa Burna Boy asikanyaga kwenye ardhi ya Ghana kwani atamshushia kichapo cha mbwa kitakachoimuacha na majeraha. Shatta ametoa kauli hiyo mara baada ya Burna Boy kudai kuwa hatomvumilia msanii yeyote anayetaka kuigawanya tasnia ya muziki Afrika ambapo alienda mbali zaidi na kusema kwamba yupo tayari kuzichapa na Shatta Wale ambaye juzi kati amekuwa akiwashambulia mashabiki na wasanii wa Nigeria kwa kutosapoti muziki wa mataifa mengine ya Afrika. Hata hivyo Burna Boy hajajibu chochote mpaka sasa kuhusiana na ishu ya Shatta Wale kumtolea uvivu

Read More
 BURNA BOY KUICHAFUA MADISON SQUARE GARDEN APRIL 28, 2022

BURNA BOY KUICHAFUA MADISON SQUARE GARDEN APRIL 28, 2022

Burna Boy ametangaza rasmi onesho lake ambalo litafanyika katika ukumbi mkubwa na maarufu wa Madison Square Garden uliopo New York nchini Marekani. Onesho hilo ‘One Night In Space’ litafanyika April 28 mwaka 2022 ambapo Burna Boy ataweka rekodi ya kuwa msanii wa kwanza toka Afrika kuibariki steji hiyo kama msanii kinara. Uongozi wa Madison Square Garden pia umeutumia ukurasa wao wa Instagram kutangaza onesho hilo na tiketi zitaanza kuuzwa mnamo Disemba 16. Ukumbi wa MSG una uwezo wa kubeba watu 20,789. Justin Bieber ndiye anashikilia rekodi ya kuujaza ukumbi huo kwa haraka zaidi, show zake mbili za ‘Believe Tour’ zilikuwa Sold out ndani ya sekunde 30 mwaka 2012. Kabla, mwanadada Taylor Swift ndiye alikuwa akishikilia rekodi hiyo kwa kuujaza kwa sekunde 60 mwaka 2009

Read More
 BURNA BOY ATAKA BANGI IRUHUSIWE NIGERIA, ADAI HAINA MADHARA

BURNA BOY ATAKA BANGI IRUHUSIWE NIGERIA, ADAI HAINA MADHARA

Nyota wa muziki kutoka nchini Nigeria Burna Boy amesema kwamba ni vyema sheria ikaruhusu matumizi ya bangi nchini humo kwani haina madhara kama ambavyo wengi wanasema. Akihojiwa kwenye kipindi cha ‘Home Grown Radio’ jijini Los Angeles, Burna ameeleza kwamba watu wengi wanatumia bangi lakini hawataki kutangaza hadharini lakini kiukweli hamna madhara mabaya yoyote mtu akitumia. “Kila mtu anatumia bangi lakini hakuna anayetaka kusema au kukutwa nayo.” amesema Burna Boy. Lakini pia Hitmaker huyo wa Kilo metre amesema watu wazima na viongozi wamefanikiwa kutoa elimu kwa jamii kwamba endapo mtu akitumia bangi basi atakuwa chizi jambo ambalo yeye amelikataa na kusema kuwa ni uongo,  hivyo ni bora sheria iruhusu matumizi ya bangi.

Read More
 BURNA BOY AKAVA JARIDA LA ES MAGAZINE LA NCHINI UINGEREZA

BURNA BOY AKAVA JARIDA LA ES MAGAZINE LA NCHINI UINGEREZA

Staa wa muziki kutoka nchini Nigeria  Burna Boy ambaye anafanya vizuri kupitia kazi zake mbalimbali, ametokea mbele ya kava la Jarida la Es Magazine la nchini Uingereza. Jarida la Evening Standard Magazine ni jarida kutoka London, Uingereza ambalo hujihusisha kwa kutoa habari za burudani kutoka kwa mastaa wakubwa ulimwenguni. Kwenye Jarida hilo Burna Boy  amefunguka mengi kuhusiana na muziki wake, mpaka kufikia hapo alipo. Uwezo wake mkubwa wa kujaza kwenye Arena, dili mbalimbali alizozipata kama PEPSI, kukutana na mastaa wakubwa, kushiriki kwenye album za wasanii kutokea Marekani. Hata hivyo, Burna boy  anakuwa msanii wa tatu kutoka Afrika kupata nafasi ya kukava jarida la ES, mwaka 2019 WizKid alikava Jarida hilo na mwaka 2020 ikawa zamu ya Davido kutokea kwenye jarida hilo. Ikumbukwe, Burna Boy kupata nafasi ya kukava kwenye jarida hili kubwa ulimwenguni kunampa nafasi ya kuzingatiwa, kuongeza mashabiki na watu kupata nafasi ya kuweza kumfuatilia zaidi.

Read More