Dr. Ofweneke apata kigugumizi baada ya kuitishwa millioni 70 kumleta Burna Boy Kenya

Dr. Ofweneke apata kigugumizi baada ya kuitishwa millioni 70 kumleta Burna Boy Kenya

Mchekeshaji Dr. Ofweneke ameshangazwa na kiasi cha pesa alichotakiwa kulipa kwa ajili ya kumleta Burna Boy kutumbuiza nchini Kenya. Kupitia ukurasa wa Instagram Ofweneke amesema uongozi wa Burna Boy kupitia mama yake mzazi Bose Ogulu ulimtaka alipe kiasi cha shillingi millioni 70 kumpata msanii huyo kutumbuiza kwenye mkesha wa kukaribisha mwaka mpya wa 2023. “Weeh tried reaching out to the mum for a new year’s event … he is now charging Ksh 70 M,” alisema Dr. Ofweneke. Hata hivyo kauli hiyo imezua mjadala mzito miongoni watumiaji wa mitandao ya kijamii wengi wakitamtaka mchekeshaji huyo kuwapa nafasi wasanii wa Kenya kwenye onesho lake lijalo badala ya kuwazingatiwa wasanii wa nje ambao watamtoza kiasi kikubwa cha pesa.

Read More
 STEFFLON DON AKIRI BURNA BOY KUMUIMBIA WIMBO WA LAST LAST

STEFFLON DON AKIRI BURNA BOY KUMUIMBIA WIMBO WA LAST LAST

Mwimbaji Stefflon Don anaamini Burna Boy alimuimba kwenye wimbo wake maarufu “Last Last” ambao ulitoka Mei mwaka huu. Kwenye mahojiano na TT Torrez, Stefflon amesema alikuwa penzini na Burna Boy kwa miaka miwili na nusu na tangu wameachana mwaka mmoja uliopita hajaingia tena kwenye mahusiano mapya. Licha ya Stefflon Don kukubali kuwa Burna Boy alimlenga kwenye wimbo huo, amepingana na baadhi ya mistari kwa kusema mingine ambayo ameyazungumza Burna kwenye ngoma hiyo hayana ukweli.

Read More
 BURNA BOY AWATOLEA UVIVU MASHABIKI WA WIZKID KISA KUPONDA MAFANIKIO YA ALBUM YAKE

BURNA BOY AWATOLEA UVIVU MASHABIKI WA WIZKID KISA KUPONDA MAFANIKIO YA ALBUM YAKE

Msanii kutoka Nigeria Burna Boy ameendelea kurushiana maneno na mashabiki wa Wizkid, kupitia mtandao wa Twitter ameshambuliana nao tena hadi kutishia kumpiga Wizkid. Burna Boy alijikuta akiingia kwenye vita hiyo ya maneno baada ya mashabiki wa Wizkid kumvamia kwenye tweet yake ambayo aliweka mafanikio ya Album zake. Baada ya mashabulizi ya maneno kutoka kwa Wizkid FC, Burna Boy alikuja na kumwambia shabiki mmoja “Kama Wizkid asingekuwa rafiki yangu, basi kiukweli ningempiga ngumi ya uso papo hapo ili mashabiki zake wa Twitter wafahamu kwamba Mimi sio Davido. Lakini namshkuru Mungu ninafahamu na nimepevuka sana kufahamu (Wizkid) sio wewe.” aliandika Burna Boy kwenye tweet ambayo tayari imefutwa.

Read More
 BURNA BOY AWATOLEA UVUVI MASHABIKI WA WIZKID KWA KUMZUSHIA TAARIFA ZA UONGO

BURNA BOY AWATOLEA UVUVI MASHABIKI WA WIZKID KWA KUMZUSHIA TAARIFA ZA UONGO

Kumeibuka vita kati ya Burna Boy na mashabiki wa WizKid (Wizkid FC) kwenye mtandao wa Twitter. Burna Boy amewatupia vijembe kwamba wamekuwa wakimzushia vitu vya kijinga na kumtengenezea stori ambazo hazina ukweli wowote, na hii yote ni kutokana na kukosa elimu. “Niliwahi kusema kitu kama hichi kipindi cha nyuma lakini wafuasi wadanganyifu wa Wizkid (Wizkid FC) walisema nadanganya. Labda kama history ilikuwa inafundishwa kwenye shule zenu. Wizkid anapaswa kuwa na watu nadhifu hapa Twitter badala ya wajinga kama hawa.” aliandika Burna Boy na kuweka picha ya shabiki mmoja wa Wizkid. Shabiki mmoja alimuuliza kama zile insta stories zilizosambaa toka kwa Offset na ile iliyoonekana imetoka kwa Stefflon Don, zina ukweli? Burna Boy alijibu hapana, bali zilitengenezwa na mashabiki wapuuzi wa Wizkid FC. Burna alikuwa akiunga mkono kitu kilichosemwa na Professor aitwaye Wole Soyinka juu ya kuondolewa somo la Historia ya Nigeria kwenye mitaala ya elimu.

Read More
 LOVE DAMINI YA BURNA BOY YAWEKA REKODI BOOMPLAY

LOVE DAMINI YA BURNA BOY YAWEKA REKODI BOOMPLAY

Mwanamuziki kutoka Nigeria Burna Boy anaendelea kufanya vizuri kupitia album yake mpya na ya sita katika muziki wake iitwayo “Love, Damini” ambayo ilitoka rasmi Julai 8 mwaka huu. Habari njema ni kwa mashabiki wa mkali huyo ni kwamba, ameweka rekodi katika mtandao wa Boomplay kwa album yake hiyo yenye mwezi mmoja na siku kadhaa tangu itoke kufikisha Streams zaidi ya Milioni 100. Kufuatia hilo Burna Boy anakuwa msanii mwenye jumla ya Streams nyingi katika akaunti yake ya Boomplay akiwa na Streams Milioni 402.4 Mbali na hayo, album ya “Love, Damini” yenye hits mbalimbali kama “Kilometre” inashikilia rekodi ya muda wote kwa kuingiza nyimbo nyingi mfululizo kwenye chart mpya za muziki za Billboard US Afrobeats. Burna ameingiza nyimbo 19 zote toka kwenye album yake “Love, Damini.”

Read More
 BURNA BOY AKIRI LAST LAST NDIO WIMBO ULIOMUINGIZIA PESA NYINGI KATIKA MUZIKI WAKE

BURNA BOY AKIRI LAST LAST NDIO WIMBO ULIOMUINGIZIA PESA NYINGI KATIKA MUZIKI WAKE

Burna Boy ameweka wazi kwamba wimbo wake “Last Last” umemuingizia pesa nyingi zaidi kuliko wimbo wake wowote ambao amewahi kuutoa. Wimbo huo ambao unapatikana kwenye album yake mpya ‘Love Damini’ uliachiwa rasmi mwezi Mei mwaka huu. Aidha asilimia 60 ya mapato ya wimbo huo yanaenda kwa Mwanamuziki wa Marekani Toni Braxton kwa kutumia kionjo cha wimbo wake ‘Not Man Enough’ wa mwaka 2000. Hata hivyo wimbo wa “Last Last” umeingia rasmi kwenye Chart za Billboard Hot 100, ngoma hiyo imechumpa na kukamata nafasi ya 86 kwenye chart hiyo wiki hii. Huu unakuwa wimbo wa kwanza kwa Burna Boy kufikia mafanikio makubwa kwenye chart hizo na pia ndio ingizo lake la kwanza. Aidha Album yake mpya (Love Damini) imechumpa hadi nafasi ya 14 kwenye chart za bora, Billboard 200.

Read More
 BURNA BOY AWEKA REKODI KUPITIA ALBUM YAKE MPYA LOVE DAMINI

BURNA BOY AWEKA REKODI KUPITIA ALBUM YAKE MPYA LOVE DAMINI

Mwanamuziki kutoka Nigeria Burna Boy ameachia rasmi album yake mpya “Love Damini” yenye jumla ya ngoma 19 ikiwa na kolabo 9 pekee, huku kubwa nikutoka kwa wasanii wa Kimataifa akiwemo Ed Sheeran, J Balvin na Khalid. Good news, Album mpya ya Burna Boy “Love, Damini” imekuwa Album ya Kiafrika iliyoshika nafasi za juu zaidi kwenye chart za US iTunes baada ya kukamata namba 2 ikiwa ni chini ya masaa machache tangu iachiwe rasmi leo Julai 8. “Love Damini” ni album ya sita kwa Burna Boy baada ya kupata mafanikio makubwa na album yake ‘Twice as Tall’ iliyotoka mwishoni mwa mwaka 2020.  

Read More
 BURNA BOY AACHIA RASMI TRACKLIST YA ALBUM YAKE

BURNA BOY AACHIA RASMI TRACKLIST YA ALBUM YAKE

Mwanamuziki kutoka Nigeria Burna Boy ameachia rasmi orodha ya ngoma zinazopatikana kwenye album yake mpya ya Love Damini ambapo ina jumla ya ngoma 19 ikiwa na collabo 9 pekee. Mkali huyo ambaye Julai 2 alisherehekea kumbukumbu ya kuzaliwa kwake, amewapa mashavu wasanii kama J Balvin, Ed Sheeran na wengine wengi kwenye album yake hii mpya. Album hiyo inatoka Julai 8, Ijumaa ya wiki hii. “Love Damini” inakuwa ni album ya sita kwa Burna Boy baada ya kupata mafanikio makubwa na album yake ‘Twice as Tall’ iliyotoka mwishoni mwa mwaka 2020.

Read More
 BURNA BOY AWAKOSOA MASHABIKI KUHUSU MAPOKEZI YA WIMBO WAKE “LAST LAST”

BURNA BOY AWAKOSOA MASHABIKI KUHUSU MAPOKEZI YA WIMBO WAKE “LAST LAST”

Mwanamuziki wa Nigeria Burna Boy amejitokeza kukosoa mashabiki zake kwa jinsi wamepokea wimbo wake uitwao “Last Last”. Kupitia akaunti yake rasmi ya mtandao wa Tik Tok Burna Boy amesema watu wanafurahia wakichezea wimbo huo ilhali ni wa maumivu ya mapenzi. Ujumbe huo umewaaminisha walimwengu kuwa huenda mwanamuziki huyo anapitia wakati mgumu kuhusiana na maswala ya mapenzi jambo lilomsababisha kuandika na kuimba wimbo huo. Mwezi Januari mwaka huu burna boy alisema kwamba hataki tena kuwa na hisia kama binadamu na alikuwa tayari kulipa kiasi chochote cha fedha kwa yeyote ambaye angesaidia kumwondolea hisia. Lawama zake ziliambatanishwa na tukio la mwanamuziki huyo kuachana na mpenzi wake Stefflon Don ambaye pia ni mwanamuziki wa nchini Uingereza. Uvumi kuhusu kutengana kwa wawili hao ulisheheni mitandaoni mwezi Disemba mwaka 2021 na siku chache baadaye Burna Boy akathibitisha kupitia Instagram ambapo aliandika kwamba yeye hana mke.

Read More
 BURA BOY ATIANI, AHUSIKA NA MAUJI YA WATU NIGERIA

BURA BOY ATIANI, AHUSIKA NA MAUJI YA WATU NIGERIA

Staa wa muziki wa Nigeria Burna Boy ameingia kwenye msala mzito mno wa mauaji. Kwa mujibu wa Polisi wa Lagos nchini Nigeria, wanawashikilia maafisa watano wa Polisi wenye ukaribu na Burna Boy kwa tuhuma ya kuwapiga risasi watu wawili kwenye Klabu ya Cubana usiku wa Juni 8, mwaka huu. Taarifa hizo zinaeleza kuwa, Polisi hao wanaomlinda Burna Boy walifika kwenye klabu hiyo na staa huyo ambaye alikwenda moja kwa moja kwenye sehemu ya VIP akiwa na wanawake watatu. Lakini wakiwa wanaendelea na starehe, Burna Boy alimuona mwanamke mwingine mzuri ambapo bila kujua ni mke wa mtu, alimtuma Polisi mmoja amshawishi mwanamke huyo ili aungane naye kwenye kula bata. Hapo ndipo kulipotokea vurugu kubwa ambapo mmoja wa maafisa hao wa Polisi alimpiga risasi ya paja mume wa mwanamke huyo na mtu mwingine kichwani na wanaendelea na matibabu baada ya kutolewa risasi mwilini. Inaelezwa kwamba wakati risasi zikipigwa, Burna Boy alikuwa akiamrisha wapigwe risasi huku akifurahia. Hata hivyo, mara baada ya tukio hilo, Burna Boy anadaiwa kutorokea nchini Hispania ambapo anasakwa ili akamatwe kwa msala huo huku Polisi hao wawili wakiwa nyuma ya nondo za mahabusu.

Read More
 BURNA BOY KUACHIA ALBUM YAKE MPYA MWEZI JULAI

BURNA BOY KUACHIA ALBUM YAKE MPYA MWEZI JULAI

Staa wa muziki kutoka Nigeria Burna Boy ametangaza rasmi kuachia album yake ya sita baada ya kupata mafanikio makubwa na album ya ‘Twice as Tall’ iliyotoka mwishoni mwa mwaka 2020. Akizungumza na mchekeshaji Trevor Noah kwenye, Burna boy amesema ataachia album yake mpya kwenye siku ya kuzaliwa kwake Julai 2 mwaka huu. Ikumbukwe, Burna Boy kwa sasa yupo Jijini New York Marekani kwa ajili ya tour yake ya “Space Drift” ambapo anatarajia kufanya show yake leo kwenye ukumbi wa ‘Madison Square Garden’ ambao unaingiza watu elfu 20 huku akiwa msanii wa kwanza kutoka Afrika kufanya show kwenye ukumbi huo.

Read More
 KIJANA ALIYESUKUMWA NA BURNA BOY AAPA KUVAA SHATI MWAKA MZIMA

KIJANA ALIYESUKUMWA NA BURNA BOY AAPA KUVAA SHATI MWAKA MZIMA

Kijana aliyesukumwa stejini na  Burna Boy ameahidi kutovua shati mwaka mzima, shati ambalo alilivaa usiku ule aliosukumwa wakati akijaribu kuomba msaada kwa Staa huyo wa muziki kutoka nchini Nigeria. Kwenye mahojiano na vyombo vya habari nchini Nigeria kijana huyo amesema ni fahari sana kwake na alifurahishwa na lile tukio ndio maana ameapa kulitunza mwilini shati hilo mwaka mzima. Lakini pia amekiri mapenzi yake kwa Burna Boy ni makubwa sana na anamuomba msaada na wasanii wengine wa Nigeria wamsaidie kwani ana kipaji cha kuimba.

Read More