Diamond Atoa Mtaji kwa Wafanyibiashara Wadogo kama Zawadi ya Siku ya Valentine’s
Staa wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, ameigeuza Siku ya Wapendanao Duniani kuwa siku ya matumaini kwa wafanyabiashara wadogo nchini kwao Tanzania baada ya kuamua kurudisha mkono kwa jamii. Kupitia video aliyochapisha mitandaoni, Diamond anaonekana akisimamisha gari lake kando ya barabara na kushuka kukutana na kundi la akina mama waliokuwa wakifanya biashara zao ndogo ndogo. Baada ya mazungumzo mafupi, msanii huyo alianza kutoa vibunda vya pesa kwa kila mama kama mtaji wa kuwawezesha kukuza biashara zao. Akina mama hao walionekana kushangazwa na kuguswa mno na kitendo hicho cha upendo, huku wakimshukuru kwa furaha. Wengi wao wameeleza kuwa msaada huo umekuja wakati muafaka na utasaidia kuboresha maisha yao pamoja na familia zinazowategemea.
Read More