Diamond Platnumz ataja sababu za kushindwa kutimiza ahadi ya kununua ndege

Diamond Platnumz ataja sababu za kushindwa kutimiza ahadi ya kununua ndege

Msanii wa Bongofleva kutoka WCB Wasafi, Diamond Platnumz ametaja sababu za kushindwa kutimiza ahadi yake ya kushusha ndege binafsi pamoja na helikopta yake kabla ya kuisha kwa mwaka huu 2022. Akizungumza na Wasafi FM, Diamond amesema wakala aliyemtumia akimtaja kwa jina ‘Mr T’ ndiye aliyemfanya asitimize ahadi hiyo baada ya wakala huyo kushindwa kuleta ndege hizo licha ya kulipwa kila kitu. Kwa mujibu wake, kwa sasa wameamua kufikishana katika vyombo vya sheria na suala lao litashughulikiwa huko. Mapema mwaka jana, baada ya Diamond maarufu kama Simba kufanikisha ahadi yake ya kununua gari aina ya Rolls Royce Cullinan 2021, aliweka bayana nia yake ya kununua ndege binafsi.

Read More
 Diamond Platnumz analipwa takriban millioni 12 za Kenya kwa show

Diamond Platnumz analipwa takriban millioni 12 za Kenya kwa show

Msanii maarufu wa Bongofleva na mmiliki wa Lebo ya WCB Wasafi, Diamond Platnumz analipwa takriban millioni 12 za Kenya kwa show za kimataifa anazofanya. Hayo ni kwa mujibu wa Meneja wa msanii huyo, Sallam SK akiongea kwenye mahojiano yake hivi karibuni ambapo amesema kwa show za Tanzania bei hiyo inapungua. “Milioni 230 hiyo ni nje ya Tanzania, hapa ndugu zetu lazima tutashusha. Kimsingi imewekwa kiwango hicho, kwa hiyo haziwezi kuwa show nyingi kama mwanzo” alisema Sallam SK. Katika hatua nyingine, Sallam SK amepuzilia mbali madai ya kwenda kuwa Meneja wa Harmonize na Konde Music kama ilivyodaiwa mtandaoni, amesema kufanya hivyo ni kujishusha kwa kuwa ameridhika na WCB Wasafi. Hata hivyo amekanusha stori za kuwahi kutoka kimapenzi na Baby mama wa Diamond Platnumz, Tanasha Donna ,kwa kusema kuwa yeye na mrembo huyo walikuwa marafiki wa muda mrefu.

Read More
 Hanstone adai kuibiwa wimbo na Diamond Platnumz

Hanstone adai kuibiwa wimbo na Diamond Platnumz

Msanii wa Bongofleva Hanstone ameibuka na madai ya kwamba Diamond Platnumz ameiba wimbo wake kwenye kazi yake mpya “CHITAKI” ambayo ameidokeza kwenye mitandao ya kijamii. Kupitia insta story yake, Hanstone ameanika wazi hilo kwa kuweka kipande cha wimbo wake uitwao “NATETEMEKA” ambapo kwenye file inaonesha aliufanya mwaka 2019. Utakumbuka Hanstone na Diamond walikuwa na ukaribu ambapo Hanstone alikuwa anatajwa kuwa angesainishwa na lebo ya WCB lakini baada ya kutokea utofauti wa pande zote mbili dili hilo lilitajwa halikuweza kukamilika.

Read More
 Babu Tale aburuzwa mahakamani kwa kushinda kulipa fidia ya Ksh millioni 13

Babu Tale aburuzwa mahakamani kwa kushinda kulipa fidia ya Ksh millioni 13

Meneja wa Msanii Diamond Platnumz, Babu Tale ambaye pia mmoja wa wakurugenzi wa kampuni inayojihusisha na shughuli za burudani, Tip Top Connections Company Limited yuko hatarini kufungwa jela kutokana na kushindwa kumlipa mhadhiri wa dini ya Kiislam, Sheikh Hashim Mbonde, fidia ya KSh milioni 13. Tayari Sheikh Mbonde ameshafungua maombi Mahakama Kuu akiiomba mahakama hiyo iamuru BabuTale akamatwe na afungwe kwa kushindwa kumlipa fidia hiyo. Sheikh Mbonde amefungua maombi hayo dhidi ya Tip Top na Babu Tale baada ya Mahakama ya Rufani kutupilia mbali taarifa yao ya kusudio la kukata rufaa kupinga hukumu ya Mahakama Kuu iliyowaamuru kulipa fidia hiyo, Agosti 17, 2022.

Read More
 Meneja wa Diamond, Sallam SK ajibu disstrack ya Harmonize

Meneja wa Diamond, Sallam SK ajibu disstrack ya Harmonize

Meneja wa mwanamuziki Diamond Platnumz, Sallam SK amemjibu Harmonize kufuatia mashairi yake kwenye wimbo “Champion” alioshirikishwa na rapa Kontawa. Harmonize kwenye sehemu fupi ya wimbo huo aliimba kwamba, kwa sasa Konde Gang ni Jeshi la watu wawili akiwa na maana kwamba ni yeye na Ibraah pekee yaani baada Killy, Cheed na Anjella kujiondoa. Sallam ama Mendez leo Jumanne kupitia ukurasa wake wa Instagram amehoji kwamba, “Kwa hiyo kaua lebo kafungua kundi, wanajiita.. “Wagambo mtu mbili” au nimeelewa vibaya ” ameandika kupitia ukurasa wake. Utakumbuka tangu ameondoka WCB Wasafi, Harmonize hajawa na wakati mzuri na Lebo hiyo hasa Sallam SK ambaye mara kadhaa wameonekana kupisha kauli mtandaoni na hata walipokutana.

Read More
 Diamond Platnumz asema hawezi kumuoa Zuchu

Diamond Platnumz asema hawezi kumuoa Zuchu

Msanii nyota wa Bongofleva Diamond Platnumz ameamua kutoa ya moyoni baada ya meneja wake Babu Tale kumshinikiza amuoe Zuchu kutokana na video aliyoichapisha kwenye ukurasa wake Instagram akibusiana na hitmaker huyo wa “Sukari”. Kulingana na comment yake akimjibu Babu Tale, hawezi kumuoa msanii wake Zuchu kama ambavyo baadhi ya watu wamekuwa wakiamini. “Sasa nitamuoaje wakati ni Msanii wangu Bosi, hilo busu hapo lisiwatishe viongozi, ni salamu tu za Kijerumani” amesema Diamond. Utakumbuka wawili hao wamekuwa na ukaribu sana kiasi cha kuzawadiana zawadi jambo lililofanya baadhi ya watukuamini kuwa Diamond na Zuchu wapo katika mahusiano ya kimapenzi.

Read More
 DIAMOND PLATNUMZ AJIONDOA RASMI KWENYE TUZO ZA BONGO MUSIC AWARDS

DIAMOND PLATNUMZ AJIONDOA RASMI KWENYE TUZO ZA BONGO MUSIC AWARDS

Kampuni ya Millennium Stars Entertainment inayoratibu tuzo za Bongo Music Awards imepokea barua kutoka uongozi wa kampuni ya Wasafi Limited uliopendekeza kuondolewa kwenye mchakato wa Tuzo za Bongo Music Awards kwa msanii Diamond Platnumz kutokana na kuwa na ratiba ngumu itakayomzuia kupata muda wa kutosha kushiriki katika mchakato wa Tuzo za Bongo Music Awards 2022. Pamoja na mambo mengine uongozi wa Wasafi Limited wamepongeza na kushukuru kuona wapenzi wa muziki nchini Tanzania wamempendekeza kwa wingi msanii huyo. Kwa maana hiyo kampuni hiyo itamuondoa msanii Diamond Platnumz kwenye category zote alizokuwa amependekezwa muda wowote kuanzia sasa. Aidha, kampuni ya Millennium Stars Entertainment inaomba radhi kwa changamoto yoyote itakayojitokeza kwa mashabiki wa msanii Diamond Platnumz.

Read More
 LYNN AKIRI KUTOKA KIMAPENZI NA DIAMOND PLATNUMZ

LYNN AKIRI KUTOKA KIMAPENZI NA DIAMOND PLATNUMZ

Video vixen aliyegeukia muziki wa Bongofleva Lynn amemtaja ‘Simba’ kama ndiye Boyfriend wake kwa sasa. Jina la simba limeibua hisia mseto miongoni mwa mashabiki zake ambapo wengi wameenda mbali na kuhoji huenda mrembo huyo ana mahusiano na Diamond Platnumz ambaye amekuwa akitumia jina hilo. Katika hatua nyingine, Lyyn aliyetaja umri wake ni miaka 23, amesema hajawahi kuwa na mahusiano na msanii yeyote yule ingawa amekuwa akitongozwa sana na wasanii hao. Mrembo huyo ambaye kwa wakati mmoja amewahi kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na msanii Tommy Flavour amefunguka hayo wakati akijibu maswali ya mashabiki wake kupitia mtandao wa Instagram.

Read More
 DIAMOND PLATNUMZ ADOKEZA KUMSAINI ASLAY WBC WASAFI

DIAMOND PLATNUMZ ADOKEZA KUMSAINI ASLAY WBC WASAFI

Moja kati ya vitu ambavyo Diamond Platnumz alivizungumza usiku wa kuamkia leo katika uzinduzi wa album mpya ya Barnaba “Love Sounds Different” ni kuhusiana na uwekezaji katika muziki hapa nchini unavyoyumba. Diamond ameeleza kwa undani namna wawekezaji wanavyosita kuingia katika muziki kwa sababu wakiangalia lebo kama WCB wakati fulani hali wanayoipitia hasa wasanii wake wakitaka kondoka inakua ni mshikemshike kitu ambacho Diamond amekisisitiza mbele ya Basata. Pia Diamond alimuongelea msanii aslayisihaka akisema kwamba ni mtu ambaye anamkubali na ana uwezo mkubwa sana na kama angekuwa chini ya usimamizi wake mwenyewe angefika mbali. “Kila mtu humu ndani anamjua Aslay, ana uwezo mkubwa sana, siongei kwa sababu niko hapa lakini Aslay angekuwa mikononi mwangu, asingekuwa huyu mnayemsikia, angefika mbali zaidi, au angepata mwekezaji mwingine hata kama siyo mimi, angefika mbali sana.” ameeleza Diamond Aidha, Aslay anatajwa kuwa ameshasaini na kampuni ya Sony Music na dili hilo lipo mbioni kutangazwa

Read More
 ZUCHU KULIPA MILLIONI 500 ZA KENYA KUONDOKA WCB

ZUCHU KULIPA MILLIONI 500 ZA KENYA KUONDOKA WCB

C.E.O wa WCB Wasafi, Diamond Platnumz ameweka wazi kuwa Zuchu kuondoka katika Lebo hiyo atalipa takriban shilingi milllioni 500 za Kenya. Kauli ya Diamond inakuja muda mfupi baada ya Babu Tale kutangaza Lebo hiyo itasaini wasanii wapya hivi karibuni. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Babu Tale ameandika “Hivi karibuni tutasaini wasanii wawili kujiunga lebo ya Wasafi ila safari hii tumeamua msanii atakua na mashaidi wawili kutoka COSOTA na BASATA” “Music ni biashara yetu na ni jukumu letu kukuza na kusimamia hii kazi, hatuwezi kuacha hata iwe vipi” amesema Tale. Hadi sasa WCB iliyoanza kusaini wasanii tangu mwaka 2015, ina wasanii kama Diamond Platnumz, Queen Darleen, Lava Lava, Mbosso na Zuchu. Utakumbuka WCB Wasafi haijasaini msanii mpya tangu Aprili 2020 walipomtangaza Zuchu ambaye alikuwa msanii wa pili wa Kike ndani ya lebo hiyo.

Read More
 DIAMOND PLATNUMZ ATHIBITISHA KUNUNUA PRIVATE JET

DIAMOND PLATNUMZ ATHIBITISHA KUNUNUA PRIVATE JET

Staa wa muziki wa Bongofleva Diamond Platnumz amethibitisha kuwa tayari ameshanunua ndege yake binafsi, “Private Jet”. Diamond amethibitisha hilo kwenye mahojiano yake na DW nchini Ujerumani, akiwa na mtangazaji Josey Mahachie, ambapo alikuwa anamueleza namna staa anavyotakiwa kuishi ili kupata heshima anayostahili. Diamond amesema yeye ametoka mtaani, ameshanunua magari yenye thamani hadi Shilingi Bilioni 2.3 (Rolls Royce, Black Bedge), anasema inabidi ufanye hivyo, usipofanya hivyo hawatakuona wewe ni wa thamani na sasa tayari ana ndege binafsi. Itakumbukwa, kwa mara ya kwanza Diamond kueleza mpango wake wa kununua ndege yake binafsi ilikuwa ni miezi miwili iliyopita akizungumza na wanahabari nchini Ivory Coast alipoenda kwenye show yake, ambapo alisema ndege yake hiyo itatua nchini kabla ya mwezi Oktoba.

Read More
 DIAMOND PLATNUMZ ATAJWA KUWANIA TUZO ZA MUZIKI NCHINI GHANA

DIAMOND PLATNUMZ ATAJWA KUWANIA TUZO ZA MUZIKI NCHINI GHANA

Staa wa muziki wa Bongofleva Diamond Platnumz ametajwa kuwania tuzo za muziki kutoka Ghana, ziitwazo Ghana Entertainment Awards USA. Majina ya wanaowania tuzo hizo yalianza kutangazwa, Mei 13 mwaka huu ambapo hadi sasa Diamond anashindania kipengele kimoja kwenye tuzo hizo. Katika tuzo za Ghana Entertainment Awards USA kwenye msimu wake huu wa nne, Diamond Platnumz anang’ang’ania kipengele cha Best African Entertainer ambacho ni maalum kwa wasanii wote Afrika. Wanamuziki na watu wengine wanaoshindania kipengele hicho ni Davido, Wizkid, Burna Boy, Tems, Focalistic, na wengine wengi. Tuzo za Ghana Entertainment Awards USA kwa mwaka huu zinafanyika kwa mara ya nne, na zinatarajiwa kutolewa Julai 8, mwaka 2022 huko jijini New York, nchini Marekani.

Read More