VIDEO YA WIMBO WA MTASUBIRI WA DIAMOND PLATINUMZ YAPIGWA MARUFUKU TANZANIA
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imeagiza kusitishwa kwa video ya wimbo wa msanii Diamond Platnumz aliyomnshirikisha Zuchu “Mtasubiri” kutokana na kipande kinachomuonesha Zuchu akiimba kwaya kanisani na baadaye akaacha baada ya kupigiwa simu. TCRA imesema kipande hicho kimeibua ukakasi na hisia za dharau juu ya dini/madhehebu fulani, hivyo vyombo vyote vya utangazaji na mitandao ya kijamii nchini Tanzania vinatakiwa kutorusha video ya wimbo huo hadi pale Diamond Platnumz atakapo rekebisha sehemu hiyo ya video. Video ya wimbo “Mtasubiri” ilipandishwa kwenye mtandao wa Youtube Machi 29, mwaka huu
Read More