DRAKE AWACHEKA FORBES KWA ORODHA YAO YA WASANII WA HIPHOP WALIOINGIZA FEDHA NYINGI 2021

DRAKE AWACHEKA FORBES KWA ORODHA YAO YA WASANII WA HIPHOP WALIOINGIZA FEDHA NYINGI 2021

Rapa kutoka Marekani Drake ameonyesha wazi kuikataa orodha ya wasanii 10 wa Hip Hop walioingiza fedha nyingi kwa mwaka 2021, akitajwa namba 4, Jay-Z akiwa kinara kwenye orodha hiyo. Kwenye orodha hiyo Drake ametajwa kuingiza kiasi cha dola milioni 50 kwa mwaka 2021 kitu ambacho ameonesha hajakubaliana na tathmini hiyo. Drake amewajibu Forbes kwa kuangua kicheko kwa kuweka emoji ya kucheka katika taarifa hiyo kwenye mtandao wa Instagram. Inaelezwa kuwa watoa tathimini walikosea, kwani mapato ya mkali huyo yanadaiwa kuzidi kiasi cha dola milioni 50 walizoziweka. Ikumbukwe, Forbes walitoa orodha hiyo  Jumanne ya wiki iliyopita, ikiwa ni utaratibu wake wa kufanya hivyo kila mwaka.

Read More
 DRAKE ALIPITA NA MREMBO JULIA FOX KABLA YA KANYE WEST

DRAKE ALIPITA NA MREMBO JULIA FOX KABLA YA KANYE WEST

Kumbe Rapa Kanye West kutoka nchini Marekani amepita sehemu ambayo rapa mwenzake Drake alipita kitambo. Taarifa mpya mjini zinadai kwamba Drake aliwahi kuwa na mahusiano na mrembo Julia Fox ambaye kwa sasa yupo penzini na Kanye West. Kwa mujibu wa tovuti ya Page Six, penzi lao lilianza mwaka 2020 kufuatia ukaribu ulioanza mwaka 2019 baada ya Drizzy kumtelezea DM mrembo huyo na kumsifia kuhusu ushiriki wake kwenye filamu ya Uncut Gems. Julia Fox aliachana na mumewe Artemiev na Drake ndiye akawa tulizo lake la muda mfupi. Kumbuka kuwa kipindi cha nyuma kabla ya wawili hawa kuzika tofauti zao walikuwa kwenye bifu zito huku sababu kubwa ikitajwa kuwa Drake aliwahi kusema kuwa yupo kwenye mahusiano na Ex wa rapa Kanye West ambaye ni Kim Kardashian na kwa kuthibitisha hilo alim-follow Instagram pamoja na kutoa ngoma yake ya “In My Feeling” akimuimba “Kiki” ambalo ni jina lingine la mrembo huyo.

Read More
 DAVIDO MBIONI KUKAMILISHA COLLABO YAKE NA RAPPER DRAKE KUTOKA MAREKANI

DAVIDO MBIONI KUKAMILISHA COLLABO YAKE NA RAPPER DRAKE KUTOKA MAREKANI

Mwanamuziki nyota kutoka nchini Nigeria Davido amethibitisha uwepo wa collabo yake na rapa kutoka nchini Canada Drake mwaka wa 2022.Kupitia insta story yake kwenye mtandao wa Instagram Davido ameshare sehemu ya video akiwa anazungumza na rapa huyo kupitia video call na kusindikiza na ujumbe unao ashiria uwepo wa collabo kati yao ifikapo mwaka wa 2022. Kama collabo hiyo itafanikiwa basi Davido atakuwa msanii wa pili mkubwa kutoka Nigeria kufanya kazi na Drake ikizingatiwa kuwa kipindi cha nyuma alifanya kazi ya pamoja na WizKid kupitia nyimbo kama ‘Closer & One dance’

Read More