Diamond Platnumz Aahidi Kutoa Sapoti Kwenye Live Streaming
Msanii wa Bongo Flava Diamond Platnumz ameonyesha kuthamini kazi ya muongozaji wa video za muziki Hanscana kwa juhudi zake katika ubunifu wa maudhui ya kidigitali, huku akiahidi kutoa sapoti kwenye harakati za live streaming anazofanya pamoja na Joowzey. Kupitia video iliyochapishwa mtandaoni na Hanscana, wawili hao walionekana wakizungumza na Diamond kwa njia ya simu. Katika mazungumzo hayo, bosi wa WCB Wasafi amewapongeza kwa ubunifu wao na kuwahimiza kuendelea kupambana huku akiahidi kuwaunga mkono. Hanscana ametoa shukrani kwa Diamond kwa kuwapa moyo, akisema sapoti hiyo inawapa nguvu ya kuendelea kusonga mbele katika safari yao ya kidigitali. Kwa sasa Hanscana na Joowzey wanafanya ziara ya live streaming katika jiji la Dar es Salaam, wakishirikiana na mashabiki wao kupitia majukwaa ya mtandaoni. Ingawa wamejulikana zaidi kama waongozaji wa video za muziki, sasa wanaonekana kuichangamkia pia fursa ya maudhui ya moja kwa moja mtandaoni.
Read More