Iyanii Aahidi Kutoa Mapato Yake ya Muziki Kwa Wafungwa

Iyanii Aahidi Kutoa Mapato Yake ya Muziki Kwa Wafungwa

Msanii wa muziki nchini Kenya, Iyanii, amewagusa wengi baada ya kutangaza uamuzi wake wa kusaidia wafungwa kupitia mapato ya muziki wake. Kupitia podcast ya Mic Check, Iyanii amesema ameahidi kutenga asilimia 20 ya mapato yote atakayopata kutokana na muziki wake ili kuwasaidia watu walioko magerezani. Msanii huyo amesema hatua hiyo inalenga kuwapa wafungwa matumaini na kuwasaidia kuboresha maisha yao wakiwa kifungoni, akisisitiza kuwa kila mtu anastahili nafasi ya pili maishani. Iyanii ameendelea kusisitiza kuwa muziki kwake si burudani pekee, bali ni njia ya kurudisha kwa jamii na kugusa maisha ya watu wanaohitaji msaada.

Read More
 Iyanii Ashinda Tuzo Mbili Kubwa

Iyanii Ashinda Tuzo Mbili Kubwa

Msanii nyota wa Afropop, Iyanii, ameendelea kung’ara kwenye tasnia ya muziki baada ya kushinda tuzo mbili katika hafla ya utoaji tuzo za Jamhuri mwaka huu Jijini Nairobi. Iyanii ametia kibindoni tuzo ya Best Male Artist of the Year, kutokana na mchango wake mkubwa na kazi zilizotamba nchini Kenya. Lakini pia ameshinda tuzo ya Music Collaboration of the Year kupitia single yake Donjo Maber, kazi iliyopokelewa kwa ukubwa na mashabiki. Kupitia Instastory yake, Iyanii amewashukuru mashabiki wake kwa kuamini safari yake ya muziki na kueleza kuwa ushindi huo ni hatua nyingine muhimu katika historia yao ya pamoja. Iyanii ambaye kwa muda amekuwa na njaa ya mafanikio, ameongeza kuwa kilicho mbele sasa ni malengo makubwa zaidi, ikiwemo kutazamia tuzo za kimataifa kama Grammy. Ushindi huu unathibitisha nafasi ya Iyanii kama mmoja wa wasanii wanaoendelea kuipa sura mpya muziki wa kizazi kipya nchini Kenya

Read More
 Msanii Iyanii Atoa Vifaa vya Muziki kwa Wafungwa Gerezani

Msanii Iyanii Atoa Vifaa vya Muziki kwa Wafungwa Gerezani

Msanii wa muziki nchini Kenya, Iyanii, ameonyesha moyo wa kutoa na kuunga mkono jamii baada ya kutembelea Gereza la Kamiti Medium kwa shughuli za Utoaji Huduma kwa Jamii (CSR). Katika ziara hiyo, msanii huyo ametoa seti kamili ya vifaa vya muziki (sound system) kwa madhumuni ya kusaidia na kukuza vipaji vya wafungwa. Msaada huo unatarajiwa kuboresha mazingira ya mafunzo ya muziki gerezani, na kutoa fursa kwa wafungwa kuendeleza talanta zao wanapohudumia vifungo vyao. Vifaa hivyo vitatumika kwenye shughuli za burudani, maonyesho ya ndani ya gereza na mafunzo ya uanamitindo wa sauti. Hatua ya Iyanii imepongezwa na uongozi wa gereza pamoja na mashabiki wake, wakisema kwamba mchango wake utawasaidia wafungwa kujenga ujuzi, kujiamini na kupata nafasi mpya za kujifunza kupitia sanaa. Ziara hiyo imeweka msanii huyo kwenye orodha ya wasanii wanaotumia sanaa na hadhi yao kuinua jamii na kuleta matumaini mahali ambapo wengi husahauliwa.

Read More
 Msanii Iyanii Afichua Kiasi cha Pesa Anachompa Mpenzi Wake Kila Mwezi

Msanii Iyanii Afichua Kiasi cha Pesa Anachompa Mpenzi Wake Kila Mwezi

Mwanamuziki Iyanii amefichua kuwa amekuwa akimpa mpenzi wake, anayejulikana kama Shes Kemunto, posho ya kila mwezi inayokadiriwa kuwa kati ya KSh150,000 hadi KSh200,000. Akizungumza kwenye mahojiano, Iyani alisema hatua hiyo ni sehemu ya kumtunza na kumthamini mpenzi wake kwa mchango wake katika maisha yake ya kila siku. Mkali huyo wa ngoma ya Donjo Maber, amesema kwamba anapenda kuhakikisha Kemunto anaishi kwa starehe bila kuwa na wasiwasi wa kifedha. Hata hivyo, Iyanii amesisitiza kuwa mapenzi sio maneno bali ni vitendo vinavyoonyesha kujali. Kauli hiyo imezua maoni mseto miongoni mwa mashabiki mitandaoni, wengine wakimsifu kwa ukarimu wake huku wengine wakidai ni matumizi ya kupindukia.

Read More
 Iyanii Alalamika Baada ya Kupuuzwa na Waandaaji wa Matamasha

Iyanii Alalamika Baada ya Kupuuzwa na Waandaaji wa Matamasha

Msanii nyota wa muziki wa Kenya, Iyanii, ameonyesha hisia zake baada ya kupuuzwa na waandaaji wa matamasha licha ya kuwa na nyimbo nyingi zilizovuma. Kupitia ujumbe wake, Iyanii amesema kuwa ni haki yake kama msanii kupata nafasi sawia na wengine, akieleza kuwa ni jambo lisilo la haki kuachwa nje ya matukio makubwa ya burudani. Hata hivyo, msanii huyo wa ngoma ya Donjo Maber amesema hatakata tamaa, akisisitiza kuwa anaamini muziki wake utazungumza kwa niaba yake na kuthibitisha thamani yake katika tasnia ya burudani. Kauli ya Iyanii imekuja baada ya mashabiki wake kuzindua kampeni mtandaoni iitwayo “Justice for Iyanii”, wakilalamikia namna waandaaji wa matamasha wanavyompuuza msanii huyo licha ya mafanikio yake makubwa. Mashabiki hao wamesema kuwa ni unyanyapaa na upendeleo unaoendelea katika sekta ya muziki, kwani Iyanii ameachia nyimbo nyingi zilizotamba katika kipindi cha mwaka moja uliopita, lakini bado hajapewa nafasi kwenye matamasha makubwa nchini Kenya.

Read More
 Msanii Iyanii Afichua Bado Ni Bikira, Asema Atasubiri Ndoa

Msanii Iyanii Afichua Bado Ni Bikira, Asema Atasubiri Ndoa

Msanii wa muziki kutoka Kenya, Iyanii, amefichua kuwa bado ni bikira na ameamua kuhifadhi ubikra wake hadi atakapoingia kwenye ndoa rasmi na mpenzi wake, Kemunto. Akizungumza katika mahojiano na mtangazaji Alex Mwakideu, Iyanii amesema kuwa yeye na mpenzi wake wamekubaliana kuishi maisha ya kutojihusisha na ngono kabla ya ndoa. Hitmaker huyo “Donjo Maber”, amesisitiza kuwa hatua hiyo ni sehemu ya maadili yake binafsi na pia ni ishara ya heshima kwa mpenzi wake. Iyanii, ameongeza kuwa uamuzi huo pia ni njia ya kuweka msingi imara kwa maisha yake ya kifamilia. Kauli ya msanii huyo imezua mjadala miongoni mwa mashabiki, wengine wakimsifia kwa ujasiri na msimamo wake, huku baadhi wakionesha mshangao kutokana na hadhi yake kama msanii maarufu wa burudani.

Read More
 Iyanii Aahidi Tamasha Maalum Bila Malipo Kupongeza Harambee Stars

Iyanii Aahidi Tamasha Maalum Bila Malipo Kupongeza Harambee Stars

Msanii Iyanii, ameahidi kuwatunuku wachezaji wa timu ya taifa ya Harambee Stars kwa kuandaa tamasha bure maalum, ikiwa ni njia yake ya kuwapongeza kwa uchezaji wao bora kwenye michuano ya CHAN 2024. Kupitia Ukurasa wake Instagram ameshindwa kuficha furaha yake kwa mafanikio ya timu hiyo na kupongeza kitendo cha wachezaji kumuonyesha upendo mkubwa kupitia hit single yake iitwayo Donjo Maber ambayo kwa mujibu wake ni moja kati ya ngoma pendwa zaidi kwa wachezaji wa timu ya taifa. Kauli ya Iyanii inakuja wakati ambapo Harambee Stars imekuwa ikionyesha matokeo mazuri katika mashindano hayo, hasa baada ya timu hiyo kupokea zawadi ya mamilioni ya fedha kutoka kwa Rais William Ruto kama motisha kwa mafanikio yao. Tamasha hilo linalopangwa litakuwa ishara ya kusherehekea juhudi na kujitolea kwa wachezaji wa Stars, huku pia likionekana kama hatua ya kuunganisha mashabiki wa soka na muziki nchini. Iwapo mipango itakamilika, hafla hiyo inatarajiwa kuwa moja ya matukio makubwa ya burudani mwaka huu, mashabiki wakisubiri kutangaziwa tarehe na mahali ambapo tamasha hilo litafanyika

Read More
 Donjo Maber: Wimbo Mpya wa Iyanii na Dufla Wateka Mitandao kwa Midundo ya Afro-Dancehall

Donjo Maber: Wimbo Mpya wa Iyanii na Dufla Wateka Mitandao kwa Midundo ya Afro-Dancehall

Wimbo mpya “Donjo Maber” wa wasanii wa Kenya Iyanii na Dufla Diligon unaendelea kutikisa mitandao ya kijamii na kuchezwa sana kwenye vituo vya redio. Donjo Maber, ni msemo wa jamii ya Luo unaomaanisha jambo limeweza au limetiki, kwenye hii single umetumika kama kauli ya ushindi na vibe nzuri mitaani. Wimbo huu ambao ni moja kati ya single itakayopatikana kwenye Album mpya ijayo ya Iyanii, unachanganya midundo ya Afrobeat na dancehall kwa ustadi mkubwa. Vocals za Dufla zinabeba hisia za mitaani huku Iyanii akitamba na uchezaji wa maneno unaonata. Beat ni kali na mashairi ni mepesi, yanayokaririka kirahisi, jambo ambalo limeufanya kuwa maarufu mitandaoni hasa kupitia #DonjoMaberChallenge kwenye TikTok na Instagram. Video rasmi ni ya rangi kali, nguo za kuvutia na densi zilizopangwa kitaalam. Ingawa haina hadithi nzito, inalenga vibe ya kusherehekea, jambo linaloifanya kuwavutia sana vijana. Tayari ndani ya siku 10 imevuma YouTube ikiwa na zaidi ya views laki 3 huku ikishikilia nafasi ya 6 kwenye trending tab nchini Kenya. Kwa ujumla, Donjo Maber ni ushahidi kuwa muziki wa Kenya unaendelea kukua na kuchukua nafasi katika soko la Afrika na dunia. Ushirikiano kati ya Iyanii na Dufla umeleta ladha ya kipekee ambayo inakonga nyoyo za mashabiki. Ni wimbo wa kujivunia, wa kufurahia, na bila shaka, una nafasi kubwa kuwa hitsong ya mwaka.

Read More
 Iyanii apokezwa tuzo mbili Boomplay baada ya kufikisha streams millioni 10

Iyanii apokezwa tuzo mbili Boomplay baada ya kufikisha streams millioni 10

Mwanamuziki Iyanii kutoka nchini Kenya anaendeleza ubabe upande wa Streaming Platforms hasa katika mtandao wa Boomplay, amepokea tuzo mbili za (plaque) kutoka Boomplay baada ya ya kufikisha zaidi ya streams milioni 10 kupitia nyimbo zake zote zinazopatikana kwenye mtandao huo. Iyaani ameamua ku-share plaque kutoka Boomplay kupitia ukurasa wake wa Instagram baada ya kufikia kiwango hicho ambapo amewashukuru mashabiki wake kwa upendo wanaoendelea kumuonyesha bila kuchoka kwenye muziki wake. Katika hatua nyingine Wimbo wake “Pombe”, umefanikiwa kufikisha zaidi ya streams milioni 5 kwenye mtandao wa Boomplay. Wimbo huo, ulitoka rasmi mwaka 2021 chini ya lebo ya muziki ya Utembe World inayomilikiwa na Arrow Boy.

Read More
 IYANII ANYOSHA MAELEZO KUHUSU ISHU YA KUWA NUSU UCHI KWENYE UZINDUZI WA ALBUM YA ARROW BOY

IYANII ANYOSHA MAELEZO KUHUSU ISHU YA KUWA NUSU UCHI KWENYE UZINDUZI WA ALBUM YA ARROW BOY

Msanii wa lebo ya Utembe World, Iyanii ametetea hatua yake ya kuwa nusu uchi kwenye hafla ya uzinduzi wa album mpya ya bosi wake Arrow Boy. Katika mahojiano yake ya hivi karibuni Iyanii amesema aliahamua kufanya hivyo kama njia ya kuonyesha ubunifu kwenye masuala ya mitindo na fasheini kwani ni kitu ambacho amekuwa akifanya tangu utotoni. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Pombe” amekanusha kutumia suala hilo kutengeneza mazingira ya kuzungumziwa kwenye vyombo vya habari nchini ikizingatiwa kwamba yeye ni moja kati ya wasanii wasiopenda kutumia kiki kutangaza muziki wake. Utakukumbuka Iyanii ni moja kati ya wasaniii waliotumbuza  kwenye hafla ya uzinduzi wa album ya Focus ya Arrow boy Usiku wa kuamkia Machi 13 Jijini Nairobi.

Read More
 IYANII ATHIBITISHA UJIO WA NGOMA YAKE MPYA NA SIZE 8

IYANII ATHIBITISHA UJIO WA NGOMA YAKE MPYA NA SIZE 8

Hitmaker wa “Pombe” msanii Iyanii ametangaza ujio wa ngoma yake mpya ambayo amemshirisha mwanamuziki wa nyimbo za Injili nchini Size 8. Iyanii amethibitisha hilo kupitia instastory ysake kwenyemtandao wa instagram kwa video clip fupi akiwa na Size 8 kwenye mazingira ya studio yenye caption inayoashiria kuwa kuna uwezekano wa Iyanii kufanya wimbo wa pamoja na himaker huyo wa Mateke. Hajafahamika kama wimbvo huo utakuwa wa injili au wa kidunia ila itakuwa ni kazi ya kwanza kwa Iyanii na Size 8 ikiziingatiwa kuwa wawili hao hawajahi fanya wimbo wa pamoja. Huu ni muendelezo mzuri kwa  Iyanii ambaye katika siku za hivi karibuni amekuwa akiachia nyimbo mfululizo bila kupoa.

Read More