Donjo Maber: Wimbo Mpya wa Iyanii na Dufla Wateka Mitandao kwa Midundo ya Afro-Dancehall

Donjo Maber: Wimbo Mpya wa Iyanii na Dufla Wateka Mitandao kwa Midundo ya Afro-Dancehall

Wimbo mpya “Donjo Maber” wa wasanii wa Kenya Iyanii na Dufla Diligon unaendelea kutikisa mitandao ya kijamii na kuchezwa sana kwenye vituo vya redio. Donjo Maber, ni msemo wa jamii ya Luo unaomaanisha jambo limeweza au limetiki, kwenye hii single umetumika kama kauli ya ushindi na vibe nzuri mitaani. Wimbo huu ambao ni moja kati ya single itakayopatikana kwenye Album mpya ijayo ya Iyanii, unachanganya midundo ya Afrobeat na dancehall kwa ustadi mkubwa. Vocals za Dufla zinabeba hisia za mitaani huku Iyanii akitamba na uchezaji wa maneno unaonata. Beat ni kali na mashairi ni mepesi, yanayokaririka kirahisi, jambo ambalo limeufanya kuwa maarufu mitandaoni hasa kupitia #DonjoMaberChallenge kwenye TikTok na Instagram. Video rasmi ni ya rangi kali, nguo za kuvutia na densi zilizopangwa kitaalam. Ingawa haina hadithi nzito, inalenga vibe ya kusherehekea, jambo linaloifanya kuwavutia sana vijana. Tayari ndani ya siku 10 imevuma YouTube ikiwa na zaidi ya views laki 3 huku ikishikilia nafasi ya 6 kwenye trending tab nchini Kenya. Kwa ujumla, Donjo Maber ni ushahidi kuwa muziki wa Kenya unaendelea kukua na kuchukua nafasi katika soko la Afrika na dunia. Ushirikiano kati ya Iyanii na Dufla umeleta ladha ya kipekee ambayo inakonga nyoyo za mashabiki. Ni wimbo wa kujivunia, wa kufurahia, na bila shaka, una nafasi kubwa kuwa hitsong ya mwaka.

Read More
 Iyanii apokezwa tuzo mbili Boomplay baada ya kufikisha streams millioni 10

Iyanii apokezwa tuzo mbili Boomplay baada ya kufikisha streams millioni 10

Mwanamuziki Iyanii kutoka nchini Kenya anaendeleza ubabe upande wa Streaming Platforms hasa katika mtandao wa Boomplay, amepokea tuzo mbili za (plaque) kutoka Boomplay baada ya ya kufikisha zaidi ya streams milioni 10 kupitia nyimbo zake zote zinazopatikana kwenye mtandao huo. Iyaani ameamua ku-share plaque kutoka Boomplay kupitia ukurasa wake wa Instagram baada ya kufikia kiwango hicho ambapo amewashukuru mashabiki wake kwa upendo wanaoendelea kumuonyesha bila kuchoka kwenye muziki wake. Katika hatua nyingine Wimbo wake “Pombe”, umefanikiwa kufikisha zaidi ya streams milioni 5 kwenye mtandao wa Boomplay. Wimbo huo, ulitoka rasmi mwaka 2021 chini ya lebo ya muziki ya Utembe World inayomilikiwa na Arrow Boy.

Read More
 IYANII ANYOSHA MAELEZO KUHUSU ISHU YA KUWA NUSU UCHI KWENYE UZINDUZI WA ALBUM YA ARROW BOY

IYANII ANYOSHA MAELEZO KUHUSU ISHU YA KUWA NUSU UCHI KWENYE UZINDUZI WA ALBUM YA ARROW BOY

Msanii wa lebo ya Utembe World, Iyanii ametetea hatua yake ya kuwa nusu uchi kwenye hafla ya uzinduzi wa album mpya ya bosi wake Arrow Boy. Katika mahojiano yake ya hivi karibuni Iyanii amesema aliahamua kufanya hivyo kama njia ya kuonyesha ubunifu kwenye masuala ya mitindo na fasheini kwani ni kitu ambacho amekuwa akifanya tangu utotoni. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Pombe” amekanusha kutumia suala hilo kutengeneza mazingira ya kuzungumziwa kwenye vyombo vya habari nchini ikizingatiwa kwamba yeye ni moja kati ya wasanii wasiopenda kutumia kiki kutangaza muziki wake. Utakukumbuka Iyanii ni moja kati ya wasaniii waliotumbuza  kwenye hafla ya uzinduzi wa album ya Focus ya Arrow boy Usiku wa kuamkia Machi 13 Jijini Nairobi.

Read More
 IYANII ATHIBITISHA UJIO WA NGOMA YAKE MPYA NA SIZE 8

IYANII ATHIBITISHA UJIO WA NGOMA YAKE MPYA NA SIZE 8

Hitmaker wa “Pombe” msanii Iyanii ametangaza ujio wa ngoma yake mpya ambayo amemshirisha mwanamuziki wa nyimbo za Injili nchini Size 8. Iyanii amethibitisha hilo kupitia instastory ysake kwenyemtandao wa instagram kwa video clip fupi akiwa na Size 8 kwenye mazingira ya studio yenye caption inayoashiria kuwa kuna uwezekano wa Iyanii kufanya wimbo wa pamoja na himaker huyo wa Mateke. Hajafahamika kama wimbvo huo utakuwa wa injili au wa kidunia ila itakuwa ni kazi ya kwanza kwa Iyanii na Size 8 ikiziingatiwa kuwa wawili hao hawajahi fanya wimbo wa pamoja. Huu ni muendelezo mzuri kwa  Iyanii ambaye katika siku za hivi karibuni amekuwa akiachia nyimbo mfululizo bila kupoa.

Read More