CHAMELEONE AANIKA SIRI ZA BOBI WINE

CHAMELEONE AANIKA SIRI ZA BOBI WINE

Mwanamuziki kutoka nchini Uganda Jose Chameleone amefunguka tusiyoyajua kuhusu maisha ya msanii aligeukia siasa Bobi Wine. Kwenye moja ya performance yake juzi kati, Chameleone amedai kwamba Bobi Wine hawezi tena toka nje ya ndoa yake kwa sababu anaogopa kuwekewa sumu. Hitmaker huyo wa Bolingo ya Nzambe amesema Bobi Wine anahofia sana wanawake kwa kuwa wanaweza tumiwa na watesi wake kumuangamiza. “Bobi Wine alikuwa jambazi kama mimi lakini sasa hawezi tena kufurahia maisha ya usiku jijini Kampala. Hata aliomba usalama kutoka kwa vyombo vya usalama kuhudhuria tamasha la Fik Fameika. Anaogopa kufanya mapenzi na wanawake wengine kwa sababu anaweza kulishwa sumu,” alisema. . Mwimbaji huyo ameongeza kuwa Bobi Wine anakosa maisha yake ya muziki ambayo yalikuwa yanampa huru wa kutangamana na mashabiki bila uoga wowote.

Read More
 CHAMELEONE AFUNGUKA KUHUSU BIFU YAKE NA BOBI WINE

CHAMELEONE AFUNGUKA KUHUSU BIFU YAKE NA BOBI WINE

Msanii mkongwe nchini Uganda Jose Chameleone amefunguka uhusiano wake na Bobi Wine ambaye wamekuwa kwenye bifu kwa muda mrefu. Kwenye mahojiano yake hivi karibuni Chameleone amesema kwa sasa hana ugomvi wowote na msanii huyo aliyegeukia siasa kwa kuwa alishamsamehe zamani kwa hatua ya kunyima tiketi ya chama chake cha nup wakati alikuwa anawania wadhfa wa umeya wa jiji la kampala. “I have no problem with Bobi Wine and I cleansed my heart for whatever he did. I didn’t get the party ticket but I don’t mind about that anymore.” Amesema. Hitmaker huyo wa Forever ameeleza kuwa hawezi kubali  siasa iharibu uhusiano wake na Bobi Wine ambao wameujenga kwa kipindi kirefu ikizingatiwa kuwa wamekuwa kwenye tasnia ya muziki kwa zaidi ya miaka 20. “I have known Bobi Wine for twenty years and our relationship matters most,” he said in an interview with local television.” Ameongeza Utakumbuka Chameleone na Bobi Wine mara ya mwisho kukutana ilikuwa kwenye birthday party ya mwanamuziki mwenzao Eddy Yaawe ambayo ilifanyika mwezi meo mwaka huu viungani mwa jiji la Kampala.

Read More
 CHAMELEONE AFUNGUKA SABABU ZA KUTOWANIA URAIS UMA

CHAMELEONE AFUNGUKA SABABU ZA KUTOWANIA URAIS UMA

Msanii mkongwe nchini Uganda Jose Chameleone amevunja ukimya wake kuhusu kutowania urais katika chama cha wanamuziki nchini humo UMA. Katika mahojiano yake hivi karibuni Chameleone amesema ameshikika sana kwenye kazi zake za muziki hivyo atapata nafasi ya kutekeleza majukumu ya chama cha wanamuziki nchini Uganda. Hitmaker huyo wa ngoma ya Forever amedai kuwa wasanii wanahitaji mtu ambaye ameshikika kikazi lakini pia ana muda wa kujishughulisha na majukumu ya chama hicho. “I would have contested to be UMA President but honestly am very busy for that. We need to find artists that are busy but can run the post as well”, –Jose Chameleone. Hata hivyo hajabainika ni lini hasa uchaguzi wa chama cha wanamuziki nchini Uganda utafanyika baada ya Wizara ya Leba, jinsia na masuala kijamii kuahirisha uchaguzi huo bila kutoa maelezo.

Read More
 CHAMELEONE NA BOBI WINE WAMALIZA TOFAUTI ZAO

CHAMELEONE NA BOBI WINE WAMALIZA TOFAUTI ZAO

Mastaa wa muziki kutoka Uganda Jose Chameleone na Bobi wine hatimaye wamemaliza ugomvi wao uliodumu kwa kipindi cha miaka miwili. Hii ni baada ya wawili hao kukutana kwenye hafla ya kusherekea kumbukizi ya kuzaliwa kwa mwanamuziki eddy yawe mapema wiki ambapo walipata wasaa mzuri wakuzungumza huku wakionekana wakiwa na nyuso za tabasamu. Taarifa za Bobi wine na Chameleone kumaliza bifu yao imethibitishwa na Eddy Yawe  ambaye ni kaka wa Bob Wine kwa kusema kwamba amefurahishwa na hatua ya wawili wao kuitikia mwaliko wake huku akisisitiza waendelee kuwa marafiki licha ya utofauti wao wa kisiasa. Hata hivyo mashabiki wa muziki nchini Uganda wamewapongeza wawili hao kwa hatua ya kumaliza tofauti zao huku  wakiwataka waachie wimbo wa pamoja utakaothibitisha kuwa wamemaliza ugomvi wao. Utakumbuka  Chameleone aliingia kwenye ugomvi na Bobi Wine mwaka wa 2020 baada ya Bobi Wine kumnyima tiketi ya kuwania kiti cha umeya wa jiji la kampala  kupitia chama cha kisiasa cha NUP. Tangu wakati huo Chameleone amekuwa akimshambulia Bobi Wine pamoja na watu wake wa karibu kwa hatua ya kuwa kizingiti kwenye azma yake ya kuwa mwanasiasa.

Read More
 CHAMELEONE ACHUKUA MAPUMZIKO MAFUPI KWENYE MUZIKI WAKE

CHAMELEONE ACHUKUA MAPUMZIKO MAFUPI KWENYE MUZIKI WAKE

Nguli wa muziki kutoka nchini Uganda Jose Chameleone amekuwa akifanya kazi ya muziki kwa takriban miongo mitatu bila kupoa. Baada ya kuachia nyimbo kali zilizokonga nyoyo za wapenzi wa muziki mzuri Afrika Mashariki, mkali huyo wa ngoma ya “Mama Mia” ametangaza kuchukua mapumziko ya miezi mitatu kwenye muziki wake. Vyanzo vya karibu na Jose Chameleone,vimedai kuwa msanii huyo amechukua hatua hiyo kwa ajili ya kusafiri nchini Marekani kuonana na familia yake kwani mara ya mwisho kutua nchini humo ilikuwa mwaka wa 2019. Taarifa hii inakuja mara baada ya bosi huyo wa Leone Island kupata VISA ya kwenda nchini Marekani wiki kadhaa zilizopita.

Read More
 CHAMELEONE AWAPA SOMO MASHABIKI

CHAMELEONE AWAPA SOMO MASHABIKI

Lejendari wa muziki kutoka nchini Uganda Jose Chameleone amewapa somo mashabiki wanaomkosoa kwa kufanya kazi na serikali ya rais Yoweri Museveni. Katika performance yake katika kumbukiza ya General. Muhoozi huko Cricket Oval, Lugogo chameleone amedai kuwa hatokubali kuvunjiwa heshima na mashabiki wanaomtaka afuate wanachokisema mtandaoni kwa kusema kwamba yeye ni mtu mzima na hawezi kupangiwa maisha. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Bei Kali” amesema hajali tena namna watu wanavyomchukulia kwenye mitandao ya kijamii kwa kuwa tayari ameshastaafu siasa. Inaripotiwa kuwa Chameleone na Bebe Cool ndio wasanii waliolipwa mkwanja mrefu kwenye hafla ya kumbukizi ya General. Muhoozi ambaye ni mwanawe Yoweri Museveni.

Read More
 CHAMELEONE AFUNGUKA CHANZO CHA UGOMVI WAKE NA BOBI WINE

CHAMELEONE AFUNGUKA CHANZO CHA UGOMVI WAKE NA BOBI WINE

Msanii mkongwe kwenye muziki nchini Uganda Jose Chameleone amekiri hadharani kwamba hana uhusiano mzuri na msanii mwenzake Bobi Wine ambaye aligeukia siasa. Akiwa kwenye moja ya onesho lake huko Kyengera Chameleone amedai kuwa Bobi wine alimnyima tiketi ya kugombea wadhfa wa umeya wa jiji la kampala kupitia chama chake cha NUP kwenye uchaguzi mkuu uliopita nchini uganda. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Forever” amesema jambo hilo lilimfanya apoteze imani kwenye siasa na sasa ameamua kuelekeza nguvu zake zote kwenye muziki kwani ni kitu anachokifahamu kwa undani. “Sitaki kumzungumzia alininyima tiketi ya chama chake. Nimepoteza imani kwenye wadhfa wa umeya. Kwa sasa nimelekeza nguvu zangu kwenye muziki kitu ninachokifahamu kwa undani,” Alisema. Chameleone ambaye ni bosi wa Lebo ya muziki ya Leone Island amesema anajihisi mwenye furaha zaidi akiwa karibu na wasanii kama Bebe Cool, Eddy Kenzo na David Lutalo na wengine wengi.

Read More
 JOSE CHAMELEONE AKIRI KUSHINDWA NA MASUALA YA SIASA

JOSE CHAMELEONE AKIRI KUSHINDWA NA MASUALA YA SIASA

Msanii nguli kutoka Uganda Jose Chameleone amekiri kutokuwa na bahati kwenye masuala ya siasa ikiwa ni mwaka mmoja tangu apoteze kiti cha umeya wa jiji la kampala kwa mpinzani wake Erias Lukwago katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2021. Akizungumza kwenye moja ya show huko Mukono Chameleone amesema amekubali hatma yake kwenye siasa huku akidai bado ana ari ya kutaka kujua kiini cha watu kutompigia kura kwenye wadhfa wa umeya licha ya kuwa na mashabiki wengi katika muziki wake. Bosi huyo wa Leone amethibitisha kutorudi tena kwenye masuala ya siasa na badala yake ataelekeza nguvu zake kufanya muziki ambao umekuwa ukimuingizia kipato kwa miaka nyingi. Hata hivyo amedokeza ujio wa show kubwa kati yake  na bebe  cool baada ya show yao iitwayo The Battle of champions iliyokuwa ikiwashindanisha huko Mukono nchini Uganda kupata mapokezi mazuri kutoka kwa mashabiki zao.

Read More
 CHAMELEONE: KOLABO ZA KIMATAIFA HAZINA MAANA KWA WASANII CHIPUKIZI

CHAMELEONE: KOLABO ZA KIMATAIFA HAZINA MAANA KWA WASANII CHIPUKIZI

Lejendari wa muziki kutoka nchini Uganda Jose Chameleone amedai kwamba kufanya kolabo na mastaa wa kubwa duniani haina faida yeyote kwa msanii. Katika mahojiano yake hivi karibuni Chameleone amesema haamini katika suala la kufanya kolabo na wasanii wakubwa duniani ili kupenya kwenye soko la kimataifa. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Forever” amesema kolabo hizo hazina maana kwa sababu mastaa hao hushindwa kuitangaza kolabo zenyewe kwenye nchini zao na badala yake mzigo wa kuitangaza project husika ubaki upande mmoja. Chameleone ni moja kati ya wasanii nchini uganda waliofanya kazi ya pamoja na mastaa kubwa duniani kama vile Beenie Man, Davido, Sizzla,Koffi Olomide na wengine wengi.

Read More
 JOSE CHAMELEONE AMWAGIA SIFA MSANII CHIPUKIZI ALLAN HENDRICK, AAHIDI KUSIMAMIA MUZIKI WAKE

JOSE CHAMELEONE AMWAGIA SIFA MSANII CHIPUKIZI ALLAN HENDRICK, AAHIDI KUSIMAMIA MUZIKI WAKE

Mkongwe wa muziki nchini uganda Jose Chameleone amehapa kukuza muziki wa msanii Allan Hendrick kwani ni kijana ambaye ana ari ya kutaka kufanya makubwa kwenye muziki wake. Katika mahojiano yake hivi karibuni Bosi huyo wa leone island amemwagia sifa msanii huyo chipukizi kwa kumtabiria mema kuwa atakuja kuwa msanii mkubwa kwenye kiwanda cha muziki nchini uganda kutokana na kipaji chake cha kipekee katika muziki wake. Kauli ya Chameleone imekuja mara baada ya kuonekana katika siku za hivi karibuni akitumia muda wake mwingi kukaa na Allan Hendrick ambaye ni kijana wa msanii mwenzake Bebe Cool. Utakumbuka msanii Bebe cool amekuwa akikosolewa na watu kwa kutompa support kijana wake Allan Hendrick  kutokana na hatua yake ya kumuacha akipambana mwenyewe kwenye muziki wake licha ya bebe cool kumiliki lebo ya muziki ya Gagamel ambayo ina uwezo wa kukuza kipaji cha msanii huyo.

Read More
 JOSE CHAMELEONE AKIRI BIFU LAKE NA WASANII GOODLYFE CREW LILIMSAIDI KUKUA KIMUZIKI

JOSE CHAMELEONE AKIRI BIFU LAKE NA WASANII GOODLYFE CREW LILIMSAIDI KUKUA KIMUZIKI

Msanii mkongwe kwenye muziki nchini Uganda Jose Chameleone amekiri kuwa bifu yake na wasanii wa Goodlyfe Crew Mozey Radio na  Weasel Manizo lilimsaidia kukua kimuziki. Katika mahojiano yake ya hivi karibuni Chameleone amesema kuwa bifu zinasaidia kukuza muziki kwani kipindi cha nyuma alipokuwa anajibu diss tracks za wasanii hao kwa kuachia ngoma alizungumziwa sana kwenye tasnia ya muziki nchini Uganda. Lakini pia ugomvi wake  na wasanii wa Goodlife Entertainmet uliwatengenezea wasanii hao brand yao ya muziki. Utakumbuka mwaka wa 2005 wasanii wa Goodlyf Crew walikuwa kwenye ugomvi mkali na chameleone jambo lilowafanya kuachia nyimbo za kumshambulia chameleone wakimtaja kama shetani lakini pia msanii wa mashinani. Hata hivyo walikuja baadae wakaweka kando tofauti zao kwa faidi ya wapenzi wa muziki mzuri nchini Uganda ambao waliingia kati na kuwataka wasanii hao waache ishu ya kuendekeza chuki na badala yake washirikiane kwenye shughuli zao za kimuziki.

Read More
 JOSE CHAMELEONE AFUNGUKA SABABU ZA KUTOACHA MUZIKI

JOSE CHAMELEONE AFUNGUKA SABABU ZA KUTOACHA MUZIKI

Msanii mkongwe kwenye muziki nchini Uganda Jose Chameleone amefunguka sababu za kutostaafu kwenye muziki licha ya kufanya kazi hiyo kwa zaidi ya miaka 20. Katika mahojiano yake ya hivi karibuni Chameleone amesema muziki upo ndani damu yake na hivyo haoni kabisa akiacha kuimba. Bosi huyo wa lebo ya Leone Island amesema hafanyi tena muziki kwa shinikizo za kupata pesa kama miaka ya hapo nyuma kwa sababu ana mali nyingi. “Sasa natoa muziki ninapojisikia kwa sababu sifanyi kwa ajili ya kujinufaisha kifedha. Tayari nina mali,” alisema katika mahojiano na runinga moja nchini Uganda. Ikumbukwe Jose Chameleone amejipatia mali nyingi kupitia muziki wake na anaendelea pia kuwekeza kwenye biashara mbali mbali. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Forever” ana mjengo wa kifahari huko Seguku nchini Uganda lakini pia inasemekana kuwa ana nyumba mbili nchini Marekani.

Read More