Khadija Kopa Akanusha Kupiga Mnada Gari Lake
Mwimbaji mkongwe wa muziki wa taarab Khadija Kopa amekanusha taarifa zinazosambaa mitandaoni zikidai kuwa amepiga mnada gari lake aliyonunuliwa na binti yake Zuchu. Kopa amesema kuwa habari hizo si za kweli na hazina msingi wowote. Kwa mujibu wake, uvumi huo ulianza baada ya baadhi ya vijana kupiga picha ya gari lake likiwa limeegeshwa katika maegesho (parking) na kisha kuisambaza mtandaoni wakidai kuwa linauzwa. Msanii huyo amesema kuwa hana mpango wowote wa kuliuza kwa sasa huku akiweka bayana kwamba iwapo atakuwa na nia ya kuuza gari hilo siku zijazo, atatangaza hadharani bila kificha. Kauli ya Kopa imekuja kufuatia mjadala ulioibuka mtandaoni, ambapo baadhi ya watumiaji wa mitandao walidai gari hilo lipo sokoni. Hata hivyo, ufafanuzi wake umeondoa sintofahamu na kutuliza gumzo lililokuwa limeanza kushika kasi.
Read More