Khadija Kopa Akanusha Kupiga Mnada Gari Lake

Khadija Kopa Akanusha Kupiga Mnada Gari Lake

Mwimbaji mkongwe wa muziki wa taarab Khadija Kopa amekanusha taarifa zinazosambaa mitandaoni zikidai kuwa amepiga mnada gari lake aliyonunuliwa na binti yake Zuchu. Kopa amesema kuwa habari hizo si za kweli na hazina msingi wowote. Kwa mujibu wake, uvumi huo ulianza baada ya baadhi ya vijana kupiga picha ya gari lake likiwa limeegeshwa katika maegesho (parking) na kisha kuisambaza mtandaoni wakidai kuwa linauzwa. Msanii huyo amesema kuwa hana mpango wowote wa kuliuza kwa sasa huku akiweka bayana kwamba iwapo atakuwa na nia ya kuuza gari hilo siku zijazo, atatangaza hadharani bila kificha. Kauli ya Kopa imekuja kufuatia mjadala ulioibuka mtandaoni, ambapo baadhi ya watumiaji wa mitandao walidai gari hilo lipo sokoni. Hata hivyo, ufafanuzi wake umeondoa sintofahamu na kutuliza gumzo lililokuwa limeanza kushika kasi.

Read More
 Khadija Kopa: Hakuna Aliyesusia Muziki wa Bongo Fleva

Khadija Kopa: Hakuna Aliyesusia Muziki wa Bongo Fleva

Msanii mkongwe wa muziki wa Taarab, Khadija Kopa, ameweka wazi msimamo wake kuhusu madai ya kuwepo kwa ususiaji wa muziki wa Bongo Fleva, akisisitiza kuwa hakuna mtu aliyesusia muziki huo bali ni wasanii wenyewe wanaojijengea hofu bila sababu ya msingi. Akizungumzia hali ya sasa ya tasnia ya muziki nchini Tanzania, Khadija amesema wasanii hawapaswi kuogopa, bali waendelee kufanya kazi zao kwa bidii na kuamini wanachokifanya. Ameongeza kuwa muziki mzuri hujipatia mashabiki wenyewe bila kulazimishwa, akisisitiza kuwa kila mtu ana uhuru wa kufanya anachotaka, ikiwemo kusikiliza au kutosikiliza muziki fulani. Kauli ya Khadija Kopa imeonekana kuwapa moyo wasanii wengi ndani ya tasnia ya Bongo Fleva, akiwataka kuacha hofu, kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kuzingatia ubora wa muziki wao kama njia kuu ya kuwafikia mashabiki na kuendeleza tasnia.

Read More
 Khadija Kopa Amkingia Kifua Diamond kwa Kuwataka Vijana Kufanya Kazi 

Khadija Kopa Amkingia Kifua Diamond kwa Kuwataka Vijana Kufanya Kazi 

Malkia wa taarab, Khadija Kopa, amemkingia kifua msanii wa Bongo Fleva Diamond Platnumz kufuatia kauli yake iliyozua mjadala kuhusu Watanzania kuhamasishwa kufanya kazi kwa bidii. Akizungumza na waandishi wa habari, Khadija Kopa amesema kuwa changamoto kubwa katika jamii ni kwamba watu wengi hawapendi kuambiwa ukweli, hata pale unaposemwa kwa nia njema ya kujenga. Kopa amewataka vijana waache kulalamika na wajikite katika kazi, akisisitiza kuwa wanapaswa wawe tayari kusikia ukweli hata unapoumiza. Ameeleza kuwa dunia ya sasa inahitaji juhudi na nidhamu ili kufanikisha malengo ya maisha. Mwanamama huyo ambaye pia ni mama mzazi wa Zuchu, amesisitiza kuwa kutafuta kipato si suala la jinsia, bali ni wajibu wa kila mtu mwenye uwezo. Amehimiza usawa katika kuwajibika, akisisitiza kuwa wanaume na wanawake wanapaswa kuwa na bidii na kujituma ili kujenga maisha bora na yenye heshima. Kwa ujumla, Khadija Kopa ameweka wazi kuwa kauli za Diamond Platnumz hazikuwa za dharau, bali ni mwito wa kuhamasisha vijana na jamii kwa ujumla kujituma na kuacha kulalamika bila kuchukua hatua.

Read More
 Khadija Kopa Akiri Kumkingia Kifua Diamond Anapogombana na Zuchu

Khadija Kopa Akiri Kumkingia Kifua Diamond Anapogombana na Zuchu

Malkia wa muziki wa Taarab, Khadija Kopa, amefunguka kuhusu uhusiano wake na mkwe wake Diamond Platnumz, akisema huwa anamkingia kifua kila mara anapokuwa na mgogoro na binti yake Zuchu. Akipiga stori na Juma Lokole, Kopa amesema huwa upande wa Diamond kwa sababu anamchukulia kama mwanae wa sasa na hataki kuvuruga ndoa yao. Amesema kuwa alianza kumpenda Diamond hata kabla hajaingia katika mahusiano ya kimapenzi na Zuchu, kutokana na heshima na bidii yake katika kazi ya muziki. Mwanamama huyo ameeleza pia kama mzazi, ni wajibu wake kuhakikisha amani na upendo vinatawala katika familia, hivyo anapochagua kumtetea Diamond, anafanya hivyo kwa nia njema ya kulinda ndoa ya mtoto wake.

Read More
 Zuchu hana mpenzi wala mchumba -Khadija Kopa

Zuchu hana mpenzi wala mchumba -Khadija Kopa

Mama mzazi wa msanii Zuchu kutoka WCB Wasafi, Khadija Kopa amerejelea na kusisitiza kuwa mwanawe bado yuko singo na hana mwanaume yeyote awe mchumba au mpenzi. Kopa amesema kutokana na umaarufu wa Zuchu, siku akipata mchumba dunia nzima itajua na itakuwa ni habari ya mijini na vijijini, ila kwa watu wawe na subira na kutopotoshwa na kile ambacho wamekuwa wakikisikia mitandoani na kwenye mablogu ya udaku. “Zuchu bado yupo single, hana mpenzi wala Mchumba na wala hajanitambulisha kwa Mwanaume yoyote kwamba Mama huyu ndiye Mwanaume wangu, Zuchu ni maarufu hata mimi Mama yake ni maarufu siku atakapopata Mchumba akanitambulisha matajua tu muwe na subira,” alisema Khadija Kopa. Ikumbukwe Zuchu anatajwa kuwa na mahusiano na Diamond Platnumz lakini wenyewe wamekuwa wakikanusha hilo, ila mitandaoni wanaonekana kama wapenzi.

Read More
 Khadija Kopa achukizwa na ujumbe wa kaka yake Diamond

Khadija Kopa achukizwa na ujumbe wa kaka yake Diamond

Malikia wa mipasho Tanzania Khadija Kopa ambaye pia ni mama mzazi wa nyota wa muziki wa bongo fleva Zuchu, ameonesha kuchukizwa na ‘Komenti’ ya Romy Jons ambayo aliiandika kwenye ukurasa wa Instagram wa Zuchu. ‘Komenti’ hiyo iliandikwa baada ya Zuchu kuposti picha zake akita amevaa ‘Taiti fupi’, Romi aliandika, ‘’SHAPE NDIO HUNA MWAYA’. Kupitia ‘komenti’ hiyo Khadija Kopa alishindwa kuvumilia na kuamua kutoa neno kumtaka Mwanae asiende Uturuki ambapo wengi huwa wanaenda kufanya upasuaji ili kuongeza umbo. Khadija aliandika, ‘’Wala usiende Uturuki mwanangu alonacho yeye huna na ulonacho wewe yeye hana huyo ndio Mungu @romyjons’’ Ikumbukwe kuwa Romy amekuwa mtu wa utani mwingi katika mitandao ya kijamii hasa katika komenti zake ambazo huwa anaandika kwa baadhi ya kurasa za watu mbalimbali.

Read More
 BI KHADIJA KOPA AZUA GUMZO MTANDAONI BAADA YA KUMUANDIKIA MWANAE ZUCHU UJUMBE MZITO

BI KHADIJA KOPA AZUA GUMZO MTANDAONI BAADA YA KUMUANDIKIA MWANAE ZUCHU UJUMBE MZITO

Mkongwe wa muziki wa Taarab nchini Tanzania Bi Khadija Kopa ambaye ni mama mzazi wa msanii kutoka WCB Zuchu Ameweka ujumbe ambao umewaacha watu wengi na maswali mengi katika mitandao yake ya kijamii. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Khadija Kopa amendika Ujumbe wa kumtakia kheri mwanae Zuchu katika maisha yake mapya ambayo yataanza siku ya Valentine  Februari 14 ambapo amesema kila mwanamke ana ndoto ya kuishi maisha hayo. “Zuhura mwanangu Nimekulea kwenye maadili na Najua wewe ni binti mwenye maamuzi sahihi na mimi kama Mama yako niseme sina budi kukusapoti .Tarehe 14 inaenda kua siku yako kubwa hakuna mwanamke asie na ndoto hii.M/Mungu akakusimamie najua hutoniangusha .siku hii isiwe tu siku yako kubwa duniani basi pia ikawe ndo mwanzo wa maisha mapya yenye Furaha .M/Mungu Akulinde kiziwanda changu Amin” ameandika Bi Khadija Kopa. Hata hivyo walimwengu kwenye mitandao ya kijamii wameibuka na kuhoji kuwa huenda siku hiyo zuchu akavishwa pete ya uchumba na bosi wake diamod platinumz ambaye katika siku za hivi karibuni amehusishwa kutoka kimapenzi na hitmaker huyo wa “Sukari. Wengine wameenda mbali Zaidi na kusema kuwa huenda Zuchu akaachia album au E yake mpya siku hiyo ya wapendanao duniani ila ni jambo la kusibiriwa.

Read More
 KHADIJA KOPA AVUNJA KIMYA CHAKE KUHUSU ISHU YA DIAMOND KUTOKA KIMAPENZI NA ZUCHU

KHADIJA KOPA AVUNJA KIMYA CHAKE KUHUSU ISHU YA DIAMOND KUTOKA KIMAPENZI NA ZUCHU

Moja kati ya headlines zinazo gonga vichwa vya habari mtandaoni ni issue inayomtaja mwanamuziki diamond platnumz kutaka kumuoa mwanamuziki mwenzake zuchu , sakata ambalo kila mtu analizungumzia katika namna yake. Sasa mama mzazi wa zuchu, Khadija Kopa amezungumzia kile kinachoitwa penzi jipya mtandaoni kati ya binti yake, Zuchu na Diamond Platnumz. Kwenye mahojiano Kopa  ambaye ni Malkia wa muziki wa Taarab nchini tanzania amepuuzilia mbali madai hayo na kusema aliwasiliana na bintiye na akamueleza hali halisi kuwa huo ni uvumi tu usio na msingi. Zuchu alimhakikishia mama yake kuwa Diamond amekuwa akimuonyesha heshima kubwa na hakuna chochote kinachoendelea kati yao. “Wakati ule Zuhura aliniambia Diamond anamheshimu sana na hajawahi hata siku moja kuniambia vitu vya kipuzi. Nilishtuka maanake watu walikuwa wanavumisha kupita kiasi” amesema na kuongeza; “Nilishangaa mbona walivumisha kupita kiasi, mimi mwenyewe sikushughulika sana, nilimuuliza Zuhura mbona watu walivumisha sana ama kuna kitu chochote. Aliniambia hamna wala hajawahi kuvunjiwa heshima hata siku moja, mimi nilichukulia kama kitu cha kawaida” alisema Khadija Kopa. Aliendelea kwa kusema; “Diamond mimi ananiona kama mama yake kusema ukweli, tangu zamani, kabla hata huyo Zuchu hajaenda Wasafi, amenichukulia kama mama yake”.

Read More