Khaligraph Jones Avaa Kinyago cha Alien Kutangaza Wimbo Mpya na Johny Vigeti

Khaligraph Jones Avaa Kinyago cha Alien Kutangaza Wimbo Mpya na Johny Vigeti

Rapa wa Kenya Khaligraph Jones amewasisimua mashabiki wake baada ya kujitokeza hadharani akiwa amevaa kinyago inayofanana na kiumbe wa anga (alien) huku akitangaza ujio wa wimbo wake mpya. Kupitia ujumbe aliouchapisha mtandaoni, Khaligraph amefichua kuwa anajiandaa kuachia wimbo mpya akishirikiana na rapa mwenzake Johny Vigeti. Kulingana na tangazo hilo, wimbo huo unatarajiwa kutoka rasmi tarehe 11 Machi. Khaligraph amesema kuwa mashabiki wanapaswa kujiandaa kwani kazi hiyo itakuwa kali na yenye ushindani mkubwa wa kimuziki. Amesisitiza kuwa ushirikiano huo na Vigeti umeandaliwa kwa ubora mkubwa ili kuwapa wapenzi wa muziki wa hip hop ladha tofauti. Kwa sasa, mashabiki wanasubiri kwa hamu kusikia matokeo ya muunganiko huo wa wasanii wawili wanaoheshimika katika tasnia ya rap nchini Kenya. Wengi wanaamini wimbo huo unaweza kuwa moja ya nyimbo zitakazotikisa majukwaa ya muziki mara tu utakapozinduliwa.

Read More
 Khaligraph Jones Aidharau Orodha ya Shabiki Aliyewataja Wasanii Wanaoweza Kumpa Ushindani

Khaligraph Jones Aidharau Orodha ya Shabiki Aliyewataja Wasanii Wanaoweza Kumpa Ushindani

Staa wa muziki wa hip hop nchini Kenya, Khaligraph Jones, ameonekana kuidharau orodha iliyotolewa na shabiki mmoja mtandaoni iliyowataja marapa wanaodaiwa wanaweza kumzidi uwezo wa kurap. Kwenye orodha hiyo, shabiki huyo alitaja majina kadhaa mazito kwenye game ya hip hop nchini humo, akiwemo Octopizzo, Elisha Elai, Timmy Blanco, Twenny Eights, Femi One, Abbas Kubaff pamoja na Nyashinski. Aliwataja pia Chris Kaiga, Rekles na Elsy Wameyo kama wasanii wenye uwezo wa kumfunika OG. Hata hivyo, Khaligraph ameonekana kutochukulia orodha hiyo kwa uzito. Kupitia majibu yake ya kejeli kwa shabiki, ameonesha kuwa haoni kama listi hiyo ina uzito wowote kwake. Kwa mzaha, amedai kuwa mtoa orodha alisahau kuwaongeza Stivo Simple Boy, Ngesh pamoja na Diana B, akionyesha wazi kuwa anaichukulia kama mjadala wa mitandaoni usio na athari kwake.

Read More
 Khaligraph Jones Aomba Radhi Baada ya Video ya Usipime Kuzua Utata

Khaligraph Jones Aomba Radhi Baada ya Video ya Usipime Kuzua Utata

Rapa Khaligraph Jones, ameomba radhi mashabiki wake baada ya kuzua gumzo mtandaoni kufuatia kuonekana akirusha noti za dola katika video ya wimbo wake mpya uitwao Usipime. Kupitia ujumbe alioutoa, Khaligraph Jones amesema kuwa dola zilizotumika kwenye video hiyo ni prop money maalum kwa ajili ya shooting za video na filamu, na sio pesa halisi. Papa Jones, amesisitiza kuwa hana uwezo wa kugawa pesa kama ambavyo baadhi ya mashabiki walivyodhani, na akawataka waache kumuomba pesa. Kauli yake imekuja mara baada ya kipande cha video wa wimbo wake mpya kusambaa akirusha pesa, kitendo kilichowafanya mashabiki wengi kuanza kumuomba pesa, wakiamini kuwa fedha alizokuwa akirusha ni za kweli.

Read More
 Khaligraph Jones Atikisa Mitandao kwa Kionjo cha Ngoma Mpya

Khaligraph Jones Atikisa Mitandao kwa Kionjo cha Ngoma Mpya

Rapa mkali kutoka Kenya, Khaligraph Jones, ametikisa mitandao ya kijamii baada ya kuachia kionjo (teaser) cha ngoma yake mpya inayotarajiwa hivi karibuni. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, rapa huyo amewashangaza mashabiki kwa kuposti video fupi akionekana anachana kwenye beat kali, akionyesha umahiri wake katika uandishi na utoaji wa mistari mizito. Khaligraph amesindikiza video hiyo na caption iliyosomeka “USPIMEEEE MWANANGU”, kauli ambayo imetafsiriwa tofauti na mashabiki wake. Wengi wameichukulia kama ishara ya ngoma kali inayokuja, huku wengine wakidai ni ujumbe wa kuwachokoza wapinzani wake kwenye game ya rap. Ndani ya muda mfupi tangu kionjo hicho kichapishwe, video imepokea maelfu ya likes na maoni, mashabiki wakimsifia kwa kurejea kwa kishindo kwa bars nzito. Baadhi walionekana kudokeza kuwa huenda ngoma hiyo ikawa sehemu ya mradi mkubwa unaotarajiwa kuachiliwa hivi karibuni. Ingawa bado hajafichua jina la wimbo huo wala tarehe rasmi ya kuachiwa, wengi wanaamini Khaligraph anajiandaa kuachia ngoma kali itakayotikisa anga za muziki wa hip hop Afrika Mashariki.

Read More
 Khaligraph Jones Atangaza Book of Jones Kuwa Albamu Bora Zaidi Kuwahi Kutoka Afrika Mashariki

Khaligraph Jones Atangaza Book of Jones Kuwa Albamu Bora Zaidi Kuwahi Kutoka Afrika Mashariki

Rapa mkali kutoka Kenya Khaligraph Jones ametangaza rasmi kuwa albamu yake Book of Jones ndiyo albamu bora zaidi katika historia ya muziki wa Kenya na Afrika Mashariki, akisisitiza kuwa hakuna mradi wowote kutoka ukanda huo uliowahi kufikia kiwango chake. Kupitia Instastory yake, Khaligraph amesema Book of Jones imeweka viwango vipya katika ubunifu, ubora wa sauti na ujumbe, akieleza kuwa albamu hiyo imebeba hadithi halisi za maisha, mapambano na mafanikio yake kama msanii aliyepitia changamoto nyingi katika muziki. Papa Jones ameongeza kuwa mradi huo uliandaliwa kwa umakini mkubwa, kuanzia utunzi wa nyimbo, uzalishaji hadi ushirikiano na wasanii mbalimbali, jambo linaloifanya kujitofautisha na albamu nyingine zilizowahi kutoka katika ukanda wa Afrika Mashariki. Ikumbukwe Albamu hiyo iliachiwa rasmi mwezi Aprili 2025 ikiwa na jumla ya mikwaju kumi ya moto, akiwashirikisha wasanii kama Nyashinski, Modercai, Dyana Cods, Abbas Kubaff na wengine wengi.

Read More
 Rapa Khaligraph Jones Ajitosa Rasmi Kwenye Boxing

Rapa Khaligraph Jones Ajitosa Rasmi Kwenye Boxing

Rapa kutoka Kenya, Khaligraph Jones, ametangaza rasmi kuingia kwenye mchezo wa masumbwi, hatua inayoongeza sura mpya katika mjadala wa wasanii wanaojitosa kwenye michezo ya ushindani. Kupitia Instastory yake, Khaligraph ameeleza kuwa anatafuta kocha wa ngumi atakayemsaidia kujiandaa kwa mapambano maalum dhidi ya wasanii wengine mwaka 2026. Ingawa hakutaja majina ya wapinzani anaowalenga, ujumbe wake umeibua gumzo miongoni mwa mashabiki na wadau wa burudani na michezo. Khaligraph, ambaye mara kwa mara ameonekana akifanya mazoezi ya nguvu na kujihusisha na mafunzo ya mwili, amekuwa akijielekeza zaidi kwenye shughuli za mazoezi katika miezi ya hivi karibuni, na hatua hii imeonekana kama mwendelezo wa kujitanua nje ya muziki. Kwa sasa, mashabiki wanasubiri updates zaidi kuhusu kocha atakayemsimamia na tarehe rasmi za mazoezi na mapambano yajayo.

Read More
 Khaligraph Jones Afunguka Sababu za Kwenda Gym Kila Siku

Khaligraph Jones Afunguka Sababu za Kwenda Gym Kila Siku

Rapa Khaligraph Jones amefunguka sababu inayomsukuma kuendelea na utaratibu wa kufanya mazoezi ya gym kila siku. Kupitia Instastory yake, Khaligraph amesema kuwa hofu ya kukosolewa mitandaoni endapo angeonekana kunenepa kupita kiasi ndiyo sababu kuu ya nidhamu yake ya mazoezi. Khaligraph anaamini kuwa mashabiki na wakosoaji mitandaoni mara nyingi hawana huruma na huwa wakali wanapotoa maoni kuhusu muonekano wa wasanii. Rapa huyo amesema hali hiyo imemfanya kujitolea kuhakikisha anabaki katika hali bora ya kiafya na kimwili, ili kuepuka maneno ya kejeli na ukosoaji wa umma. Mashabiki wake wamechukulia kauli hiyo kwa mitazamo tofauti, wengine wakiipongeza kama dalili ya uwazi na kujituma, huku wengine wakisema kuwa wasanii wengi wanaishi chini ya shinikizo la kuhifadhi mwonekano fulani ili kuepuka ukosoaji.

Read More
 Video ya Khaligraph na Toxic Lyrikali Yazidisha Uvumi wa Kolabo, 

Video ya Khaligraph na Toxic Lyrikali Yazidisha Uvumi wa Kolabo, 

Rapa kutoka Kenya, Khaligraph Jones, amewaacha mashabiki na maswali baada ya kuonekana akizungumza na msanii Toxic Lyrikali wakati wa mazoezi ya Sol Fest. Tukio hilo lilinaswa kwenye video na kusambaa haraka mitandaoni, likichochea uvumi kuwa huenda wawili hao wanapanga kufanya kazi pamoja. Kwenye klipu hiyo, wasanii hao wanaonekana wakisalimiana nyuma ya jukwaa, jambo lililowafanya mashabiki kudhani kuwa huenda kuna mipango mipya ya muziki inayonukia. Hii inakuja licha ya kwamba Toxic Lyrikali aliwahi kukataa ombi la kolabo kutoka kwa Khaligraph hapo awali, akieleza kuwa wakati huo haukuwa sahihi. Hata hivyo, kukutana kwao ghafla katika mazoezi ya Sol Fest kumezua matumaini mapya kuwa msimamo huo huenda umebadilika. Ingawa hakuna taarifa rasmi kutoka kwa yeyote kati yao, mashabiki wanaendelea kuonyesha matumaini makubwa kwamba kukutana kwao unaweza kuwa mwanzo wa kolabo inayosubiriwa kwa muda mrefu.

Read More
 Khaligraph Jones Atangaza Ujio wa Duka Kubwa la Mavazi 2026

Khaligraph Jones Atangaza Ujio wa Duka Kubwa la Mavazi 2026

Rapa kutoka nchini Kenya, Khaligraph Jones, ametangaza kuingia rasmi katika ulimwengu wa fasheni kwa mpango mpya unaotarajiwa kuvutia mashabiki na wadau wa mitindo. Kupitia instastory yake, Rapa huyo amesema kuwa atazindua duka lake la mavazi na bidhaa za ubunifu mwaka 2026, hatua inayotafsiriwa kama mwanzo wa sura mpya katika safari yake ya kisanii na kibiashara. Kwa muda mrefu Khaligraph amekuwa akionekana katika mavazi ya kipekee yanayoendana na taswira yake ya uhodari na ubunifu, na sasa anaonekana kutaka kugeuza muonekano huo kuwa biashara madhubuti. Duka hilo litakuwa na mavazi ya kisasa, bidhaa za chapa yake na makusanyo yatakayoakisi mtindo wake wa kipekee unaojulikana na mashabiki wake. Wadau wa muziki na mitindo wanasema huu ni wakati mwafaka kwa rapa huyo kuchukua hatua hiyo, kwani ushawishi mkubwa mitandaoni vinaweza kulifanya jaribio hili kufanikiw­a kwa kiwango cha kimataifa.

Read More
 Khaligraph Jones Azindua Rasmi Rap Battle ya Wimbo Wake Mpya “Weyuat”

Khaligraph Jones Azindua Rasmi Rap Battle ya Wimbo Wake Mpya “Weyuat”

Msanii nguli wa muziki wa rap nchini Kenya, Khaligraph Jones, ameanzisha rasmi rap battle ya wimbo wake mpya “Weyuat” baada ya kupata shinikizo kutoka kwa mashabiki wake mitandaoni. Khaligraph amesema awali hakupanga kufanya challenge hiyo, lakini mashabiki wake waliamua kuigeuza kuwa challenge rasmi. Amesema atapakia instrumental ya wimbo huo ili rappers wote wanaohisi wana uwezo waweze kuonyesha kipaji chao kupitia beat hiyo. Pia ameongeza kuwa endapo mambo yataenda vizuri, huenda wakafanya remix maalum ya wimbo huo. Rapper huyo ameahidi kutoa nafasi sawa kwa washiriki wote, akisisitiza kuwa changamoto hiyo ni jukwaa la kuibua vipaji vipya katika muziki wa rap Afrika Mashariki.

Read More
 Khaligraph Jones Adokeza Kolabo Mpya na Msanii Chipukizi Toxic Lyrikali

Khaligraph Jones Adokeza Kolabo Mpya na Msanii Chipukizi Toxic Lyrikali

Mfalme wa rap nchini Kenya, Khaligraph Jones, amedokeza uwezekano wa kufanya kolabo na msanii anayechipukia kwa kasi, Toxic Lyrikali, huku akimsifia kwa kuendelea kushikilia mizizi ya rap nchini humo. Kupitia mazungumzo yaliyowekwa wazi na mdau wa muziki Thithad3, Khaligraph ameonyesha kuvutiwa na kazi ya Toxic, akisema kuwa kwa sasa ndiye anayeshikilia uhalisia wa rap nchini humo. Ameongeza kuwa iwapo watashirikiana kwenye wimbo, itakuwa ni kwa muda muafaka bila presha wala haraka. Iwapo kolabo hiyo itatimia, itakuwa moja ya ushirikiano unaosubiriwa kwa hamu zaidi katika muziki wa hip hop wa Kenya mwaka huu. Toxic Lyrikali, ambaye amekuwa akipata umaarufu kutokana na mtindo wake wa uandishi wa mashairi makali na uhalisia wa mitaani, anaendelea kutajwa kama mmoja wa wasanii wanaochukua nafasi kubwa katika kizazi kipya cha muziki wa hip hop nchini Kenya.

Read More
 Khaligraph Jones Atoa Heshima kwa Hayati Raila Odinga kwa Kuweka Picha zake Ukutani

Khaligraph Jones Atoa Heshima kwa Hayati Raila Odinga kwa Kuweka Picha zake Ukutani

Rapper Khaligraph Jones ameonyesha heshima yake kwa aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani, hayati Raila Amolo Odinga, kwa kufichua michoro kadhaa (murals) ya kiongozi huyo zilizowekwa ndani ya jumba lake. Katika video iliyosambaa mitandaoni, Khaligraph anaonekana akitembea ndani ya nyumba yake ya kifahari, akionyesha kuta zilizopambwa kwa picha kubwa za Raila Odinga katika mitindo tofauti ya kisanaa. Msanii huyo amesema hatua hiyo ni njia yake ya kuenzi urithi na mchango wa Raila katika siasa na maendeleo ya Kenya, akimtaja kama kiongozi aliyeinua matumaini ya vizazi vingi. Mashabiki wake wengi wamepongeza hatua hiyo, wakisema ni ishara ya heshima na upendo kwa kiongozi ambaye amekuwa na athari kubwa katika historia ya taifa.

Read More