KRG Afichua Madhaifu ya Mfumo wa Ulipaji Mirahaba kwa Wasanii Kenya
Msanii aliyegeukia biashara kutoka Kenya, KRG the Don, amefichua madhaifu ya mfumo wa ulipaji mirahaba kwa wasanii wa Kenya baada ya kuonesha kiasi cha pesa alicholipwa kama royalty za muziki wake na Chama cha Haki za Wasanii wa Utumbuizaji Nchini Kenya (PRISK) Kupitia ukurasa wake wa Instagram stories, KRG alionesha ujumbe wa M-PESA ikibainisha kuwa alipokea KSh 3,214 pekee kama malipo ya mwaka mzima. Akiwa na kejeli, alieleza kuwa hiyo ndiyo mshahara wa mwaka mzima anayopokea kama msanii nchini Kenya, jambo lililozua mjadala mitandaoni. Kauli hiyo imeibua maswali mapya kuhusu mfumo wa ulipaji wa wasanii nchini Kenya, ambapo mashabiki na wanamuziki kadhaa wamekuwa wakilalamikia malipo duni licha ya kazi zao kuchezwa mara kwa mara kwenye redio, televisheni na majukwaa ya kidijitali. KRG, anayejulikana kwa maisha ya kifahari na uwekezaji katika biashara, alitumia kisa hicho kuonesha changamoto kubwa zinazowakabili wasanii wengi nchini katika kupata fidia stahiki kutoka kwa mashirika ya haki miliki.
Read More