KRG Afichua Madhaifu ya Mfumo wa Ulipaji Mirahaba kwa Wasanii Kenya

KRG Afichua Madhaifu ya Mfumo wa Ulipaji Mirahaba kwa Wasanii Kenya

Msanii aliyegeukia biashara kutoka Kenya, KRG the Don, amefichua madhaifu ya mfumo wa ulipaji mirahaba kwa wasanii wa Kenya baada ya kuonesha kiasi cha pesa alicholipwa kama royalty za muziki wake na Chama cha Haki za Wasanii wa Utumbuizaji Nchini Kenya (PRISK) Kupitia ukurasa wake wa Instagram stories, KRG alionesha ujumbe wa M-PESA ikibainisha kuwa alipokea KSh 3,214 pekee kama malipo ya mwaka mzima. Akiwa na kejeli, alieleza kuwa hiyo ndiyo mshahara wa mwaka mzima anayopokea kama msanii nchini Kenya, jambo lililozua mjadala mitandaoni. Kauli hiyo imeibua maswali mapya kuhusu mfumo wa ulipaji wa wasanii nchini Kenya, ambapo mashabiki na wanamuziki kadhaa wamekuwa wakilalamikia malipo duni licha ya kazi zao kuchezwa mara kwa mara kwenye redio, televisheni na majukwaa ya kidijitali. KRG, anayejulikana kwa maisha ya kifahari na uwekezaji katika biashara, alitumia kisa hicho kuonesha changamoto kubwa zinazowakabili wasanii wengi nchini katika kupata fidia stahiki kutoka kwa mashirika ya haki miliki.

Read More
 KRG The Don Apendekeza DNA ya Lazima Kama Hatua ya Kuzuia Ufisadi Kenya

KRG The Don Apendekeza DNA ya Lazima Kama Hatua ya Kuzuia Ufisadi Kenya

Mwanamuziki na mfanyabiashara KRG The Don amezua mjadala mitandaoni baada ya kupendekeza kuwa uchunguzi wa DNA wa lazima kwa kila Mkenya ndio hatua ya kwanza ya kukomesha ufisadi nchini. Kupitia ujumbe aliouchapisha mitandaoni, KRG amesema kuwa changamoto nyingi za maadili na uwajibikaji nchini zinatokana na watu kukosa uwazi kuhusu undugu na majukumu ya kifamilia. Anadai kuwa iwapo kila Mkenya atapimwa DNA, kutakuwa na uwajibikaji bora wa kifamilia na kijamii, hali ambayo itachangia kupunguza visa vya ufisadi serikalini na katika mashirika binafsi. Kulingana naye, utekelezaji wa sera hiyo unaweza kusaidia kurejesha nidhamu, uadilifu na uwajibikaji katika jamii, kwani watu watakuwa na hofu ya kufichuliwa na kushinikizwa kuwajibika kwa vitendo vyao. Kauli ya KRG imepokelewa kwa mitazamo tofauti mitandaoni. Wafuasi wake wengine wamepongeza hoja hiyo wakisema ni wazo jipya lenye kuibua mjadala mpana, huku wengine wakikosoa wakidai haiwezi kuhusiana moja kwa moja na vita dhidi ya ufisadi bali ni suala la heshima na utaratibu wa kifamilia. KRG, ambaye mara nyingi huzua mijadala mikali kwa kauli na mitazamo yake, ameendelea kujitambulisha si tu kama msanii wa muziki wa kizazi kipya, bali pia kama sauti ya uchokozi wa hoja zinazolenga siasa na jamii.

Read More
 KRG The Don Atoa Wito wa Amani Kati ya Kenya na Tanzania Kufuatia Kuzuia kwa Wanaharakati

KRG The Don Atoa Wito wa Amani Kati ya Kenya na Tanzania Kufuatia Kuzuia kwa Wanaharakati

Msanii na mfanyabiashara maarufu wa Kenya, KRG The Don, ametoa maoni yake kuhusu tukio la wanaharakati wa Kenya waliokamatwa na kuzuiliwa nchini Tanzania hivi karibuni. Akiwa na mtazamo wa kipekee, KRG amesema licha ya wanaharakati hao kudai kuwa walikuwa wakitetea haki, huenda hawakuzingatia mbinu sahihi za kuwasilisha ujumbe wao, jambo ambalo lilichangia wao kujipata matatani. “Ni kweli wanaharakati wana jukumu la kutetea haki, lakini kuna njia sahihi za kufanya hivyo. Kuna uwezekano walihusishwa na ajenda ya kumtetea kiongozi wa upinzani nchini Tanzania, Mbowe, na pengine walilipwa ili kusukuma ajenda hiyo,” alisema KRG. Aidha, KRG alieleza kusikitishwa na mzozo unaoendelea mitandaoni kati ya Wakenya na Watanzania kuhusu suala hilo. Amesisitiza kuwa Kenya na Tanzania ni mataifa ya kindugu, na haipaswi kuwa na mivutano ya kijamii au kisiasa. “Mimi nimekuwa nikisafiri Tanzania mara nyingi, na kila wakati nimepokelewa kwa heshima na mapenzi makubwa. Sioni sababu ya sisi kuchochea chuki kupitia mitandao ya kijamii,” aliongeza. Katika hatua nyingine, KRG amedokeza kuwa anapanga kusafiri hivi karibuni kwenda Tanzania kwa lengo la kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan katika juhudi zake za kutafuta muhula mwingine wa uongozi. Kauli ya KRG imepokewa kwa mitazamo tofauti mitandaoni, huku baadhi wakimpongeza kwa msimamo wake wa kuhimiza mshikamano wa Afrika Mashariki, na wengine wakitaka uchunguzi huru kuhusu hali ya wanaharakati waliokamatwa.

Read More
 KRG The Don: “Mimi ni Msanii wa Rais, 2027 Niko Kwa Ballot!”

KRG The Don: “Mimi ni Msanii wa Rais, 2027 Niko Kwa Ballot!”

Msanii maarufu wa dancehall nchini Kenya, KRG The Don, amethibitisha nia yake ya kuingia kwenye siasa kwa kishindo. Kupitia kauli kali yenye ujasiri, KRG alitangaza kuwa atawania kiti cha ubunge mwaka 2027 kupitia chama cha UDA, huku akisisitiza kuwa hana hofu ya wakosoaji wake.  “Mimi ni msanii wa President, hakuna mtu anaweza niguza na 2027 niko kwa ballot for MP under UDA party, wa kukasirika akasirike!” alisema KRG kwa msisitizo. Kauli hiyo inaashiria kujitokeza kwake kama mmoja wa wasanii wanaotaka kuleta mabadiliko nje ya muziki na kuingia moja kwa moja katika ulingo wa kisiasa. KRG, anayejulikana kwa mtindo wake wa maisha ya kifahari na kauli zenye utata mitandaoni, anaonekana kuwa tayari kutumia umaarufu wake kama nguzo ya kujenga ushawishi wa kisiasa. Kwa muda, KRG amekuwa akihusishwa na viongozi wa ngazi ya juu serikalini, na kauli yake ya kujitambulisha kama “msanii wa President” inaweza kuashiria uhusiano wake wa karibu na viongozi wa chama tawala. Iwapo ataendelea kushikilia msimamo wake hadi 2027, huenda akaingia kwenye historia kama mmoja wa wasanii wa Kenya waliothubutu kuchukua hatua ya moja kwa moja katika uongozi wa taifa. Hii inaibua maswali mapya kuhusu nafasi ya wasanii katika siasa na uwezo wao wa kuleta mabadiliko kwa jamii kupitia uongozi rasmi.

Read More
 KRG The Don Akanusha Uhusiano na Freemasons, Afafanua Alama Zake za Mitandaoni

KRG The Don Akanusha Uhusiano na Freemasons, Afafanua Alama Zake za Mitandaoni

Msanii wa muziki wa dansi na mjasiriamali nchini Kenya, KRG The Don, amevunja ukimya wake kuhusu tuhuma za muda mrefu zinazomhusisha na kundi la kificho la Freemasons. Akiwa kwenye mahojiano ya hivi karibuni, KRG alikanusha vikali madai hayo na kueleza sababu halisi ya kutumia alama zinazodaiwa kuwa za Freemason kwenye picha na mitandao yake ya kijamii. KRG amesema kuwa watu wamekuwa wakitafsiri vibaya ishara anazotumia kwa sababu ya kukosa uelewa wa sanaa na mitindo ya kujieleza kupitia picha. Alisema kuwa alama hizo ni sehemu ya ubunifu wa kisanii na hazihusiani kwa vyovyote na imani au makundi ya kisiri.  “Mimi si Freemason na sijawahi kuwa. Watu wanapenda kuhusisha mafanikio ya mtu na mambo ya ajabu ajabu. Nimefanya kazi kwa bidii, sihitaji kutumia njia za mkato. Hizo ishara ni style tu, ni photography na creativity, si uchawi,” alisema KRG. Kwenye picha nyingi zake mtandaoni, KRG ameonekana akitumia ishara kama kuweka mikono kwa mtindo wa pembetatu au kufunika jicho moja, alama ambazo kwa muda mrefu zimehusishwa na Freemason au kundi la Illuminati. Lakini KRG anasema hayo ni mitindo ya upigaji picha ambayo wasanii wengi duniani hutumia ili kuvutia mashabiki. Aidha, msanii huyo alieleza kuwa kuna watu wanaotumia mitandao ya kijamii kusambaza propaganda na kueneza hofu kuhusu maisha ya watu mashuhuri bila ushahidi wowote. “Sio kila kitu unachoona Instagram ni kiashiria cha mambo ya ajabu. Watu wengi wananitazama kama mfano wa mafanikio, lakini badala ya kujifunza, wanabuni stori za kunivuruga. Wacha waendelee kuongea, mimi naendelea kusonga mbele,” aliongeza. KRG The Don ni mmoja wa wasanii waliopiga hatua kubwa katika tasnia ya muziki nchini Kenya, na pia amejizolea umaarufu kutokana na maisha ya kifahari anayoyaonyesha mitandaoni. Mafanikio haya yamekuwa chanzo cha uvumi mwingi kuhusu maisha yake ya binafsi, ikiwa ni pamoja na madai ya kujiunga na Freemasons ili kufanikisha ndoto zake. Hata hivyo, kwa mara ya kwanza, msanii huyo ameweka mambo wazi na kuwahakikishia mashabiki wake kuwa mafanikio yake yanatokana na juhudi halali, si imani au makundi ya kisiri.

Read More
 KRG The Don afunguka kustaafu muziki

KRG The Don afunguka kustaafu muziki

Msanii Krg The Don amedai kuwa hana mpango wa kustaafu muziki hivi karibuni hadi pale tasnia ya muziki nchini Kenya itazalisha takriban mabilionea 10. Kwenye mahojiano na SPM Buzz amesema wasanii wa Kenya wana uwezo mkubwa wa kuwa matajiri ila wanapaswa kutia bidii zaidi kwenye kazi zao ikiwemo kuwekeza katika suala la kutoa nyimbo zenye ubora. KRG The Don ambaye amekuwa akijinasibu kuwa billionea upande wa tasnia ya muziki nchini amesema kama rapa mkongwe kutoka Marekani Jay Z aliweza kufanikisha mchakato wa kuzalisha mabillionea kama Rihanna na Kanye West, haoni kitu kitakachomzuia kutengeneza mazingira ya wasanii wa Kenya kuingiza kipato kupitia muziki wao.

Read More
 Krg The Don ajitolea kumsaidia Director wa video za muziki nchini Kenya Tiger Mind Vision

Krg The Don ajitolea kumsaidia Director wa video za muziki nchini Kenya Tiger Mind Vision

Mwanamuziki wa dancehall nchini Krg The Don ameamua kujitolea kumsaidia mwongozaji wa video nchini Tiger Mind Vision ambaye anadaiwa kuwa hana makaazi. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Krg the Don amewataka watu walio na ukaribu na Tiger Mind Vision wawasiliane naye ili aweze kufanikisha mchakato mzima wa kumsaidia. “Someone put me in contact wirth Dir, Tyga or Tell him to come to Casavera lounge from 4pm We see how we can help”, Ameandika instastory. Kauli ya Bosi huyo wa Cash group Entertainment inakuja mara baada ya Picha za Tiger Motions kusambaa mtandaoni akiwa anaisha maisha ya uchochole kutokana na kukosa makaazi ya kuishi. Utakumbuka Tiger Motion ni moja kati ya waongozaji wa video za muziki nchini aliyeacha alama kwenye tasnia ya muziki nchini kupitia video za nyimbo kama Mama ya Bahati, Lala Salama ya Willy Paul, Ndio yako ya Gloria Muliro, Tenda Wema ya Ringtone na nyingine nyingi.

Read More
 KRG THE DON AKANUSHA TUHUMA ZA KUFANYA BIASHARA YA ULANGUZI WA PESA

KRG THE DON AKANUSHA TUHUMA ZA KUFANYA BIASHARA YA ULANGUZI WA PESA

Msanii asiyeishiwa na matukio kila leo kutoka Kenya KRG The Don amekanusha madai yanayotembea mtandaoni kuwa anajihusisha na biashara ya ulanguzi wa pesa bandia (Wash Wash). Akipiga stori na Mpasho hitmaker huyo wa “Wano” amesema madai hayo hayana ukweli wowote bali yaliibuliwa na watu wanaomuonea wivu kutokana na mafanikio ambayo ameyapata akiwa na umri mdogo. Bosi huyo wa Cash Group Entertainment amesema anamiliki biashara mbali mbali ambazo zinamuingizia kipato ambacho kinafadhili maisha yake ya kifahari. Hata hivyo amemalizia kwa kusema kuwa utajiri wake wa sasa umechangiwa pakubwa na hatua ya yeye kuwakimbia marafiki wabaya ambao kipindi cha nyuma alikuwa anatumia nao pesa kiholela kwa kujihusisha na vitendo vya anasa.

Read More
 KRG THE DON AAMBULIA MATUSI MTANDAONI KISA BEI YA MAFUTA

KRG THE DON AAMBULIA MATUSI MTANDAONI KISA BEI YA MAFUTA

Mwanamuziki KRG The Don amejipata pabaya kwenye mitandao ya kijamii baada ya wakenya kumshambulia kwa madai ya kuwavunjia heshima kutokana na hatua ya serikali kuondoa ruzuku ya mafuta. Kwenye ujumbe wake aliochapisha kwenye mtandao wa Instaram KRG aliwataka wakenya waache kulalamika kuhusu bei ya mafuta kupanda ikizingatiwa kuwa wengi wao hawamiliki magari yanayohitaji bidhaa hiyo muhimu. Hakuishi hapo alienda mbali zaidi na kuwaponda wakenya kwa kusema kuwa kulalamika kwao kumewafanya watu kuhisi wanapitia maisha magumu wakati sio kweli. “Unalalamika mafuta imepanda na hauna gari? Sisi watu tuko na 6.3L engine na German machines hatulalamiki. Unalalamika na unatembea na slippers yako na footsubishi? Nyinyi ndio mnafanya nchi ikae ni kama watu wanateseka na watu hawateseki.” Ameandika Sasa ujumbe huo umeonekana kuwakera watumiaji wa mitandao ya kijamii ambao wameshushia kila aina matusi msanii huyo huku wakisema bei ya mafuta inamuathiri kila mkenya bila kuzingatia utajiri alionao. Hata hivyo wamemalizia kwa kumtaka KRG The Don aanze kutoa misaada kwa watu wenye uhitaji katika jamii kama kweli ana utajiri mkubwa badala ya kuisha maisha ya kuigiza kwenye mitandao ya kijamii. Utakumbuka juzi kati Serikali ya rais William Ruto iliondoa ruzuku ya mafuta kwa sababu imekuwa haiwasaidii raia wa Kenya wanaoendelea kulalamikia kupanda kwa gharama ya maisha

Read More
 KRG THE DON AWEKA WAZI THAMANI YA UTAJIRI WAKE

KRG THE DON AWEKA WAZI THAMANI YA UTAJIRI WAKE

Msanii asiyeishiwa na vituko kila leo Krg the Don amejigamba kuwa ana utajiri wa kima cha kati ya shillingi billioni 6 na 8 za Kenya. Katika mahojiano yake bosi huyo Cash Group Entertainment amesema katika kipindi cha miaka kumi ijayo thamani ya mali yake itakuwa imeongezeka hadi shillingi trillioni moja za Kenya kwani anazidi kuwekeza kwenye nyanja mbali mbali itakakayomuingizia kipato zaidi. KRG ambaye anafanya vizuri na singo yake mpya “Wano” amesema mafanikio makubwa ambayo ameyapata akiwa na umri mdogo ndio yamewafanya baadhi ya watu kuanza kumchukia na hata kumzushia tuhuma za uongo mitandaoni, jambo ambalo amedai alitamkatisha tamaa kwenye suala la kujitafutia riziki na kuishi maisha yake ya kifahari. Utakumbuka katika siku za hivi karibuni utajiri wa msanii huyo umekuwa ukitiliwa shaka huku wengi wakihoji kwamba huenda chanzo cha utajiri wake umetokana na yeye kushiriki kwenye biashara ya ulanguzi wa dawa za kulevya madai ambayo amekuwa akipuzilia mbali.

Read More
 NDOA YA KRG THE DON NA MKEWE LINAH WANJIRU LAFIKIA KIKOMO

NDOA YA KRG THE DON NA MKEWE LINAH WANJIRU LAFIKIA KIKOMO

Ndoa ya Krg The Don na mke wake Linah Wanjiru imevunjika rasmi baada ya miaka 8. Hii ni kufuatia mahakama kutangaza rasmi kwamba Krg anaweza kuendelea na maisha yake ya U-single. Pia mahakama hiyo imeliondoa jina la Krg kwenye majina matatu ya Linah Wanjiru  baada ya mchakato wa talaka kukamilika wiki hii. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Krg ameshabiki hatua hiyo ya mahakama akisema kwamba watashirikiana kutoa matunzo kwa watoto wao huku akimtakia kila la heri aliyekuwa mke wake Linah Wanjiru kwenye maisha yake mapya. Ikumbukwe, wawili hao wamedumu kwenye ndoa kwa takribani miaka 8 na wamebarikiwa kupata watoto wawili.

Read More
 KRG THE DON ADOKEZA KUANZA ZIARA YA MUZIKI NJE YA KENYA

KRG THE DON ADOKEZA KUANZA ZIARA YA MUZIKI NJE YA KENYA

Msanii wa dancehall nchini KRG The Don amefunguka tusiyoyajua kuhusu muziki wake. Katika mahojiano yake hivi karibuni amesema alilazimika kusitisha ziara yake ya muziki nje ya Kenya kwa sababu migogoro iliyokuwa inazingira ndoa yake mapema mwaka huu. Hitmaker huyo wa Ushasema amesema kwa sasa ametatua changamoto zilizokuwa zinamuandama kipindi cha nyuma, hivyo yupo mbioni  kuanza kufanya ziara yake ya kimuziki kimataifa. Katika hatua nyingine amewachana wasanii wa nyimbo za injili nchini waache unafiki na badala yake waugeukia muziki wa kidunia ambao una pesa nyingi. KRG amesema hayo alipotua nchini akitokea Sudan Kusini ambako alienda kutumbuiza kwenye moja ya show aliyokuwa amealikwa wikiendi hii iliyopita.

Read More