KRG THE DON AWAPA SOMO MASHABIKI ZAKE

KRG THE DON AWAPA SOMO MASHABIKI ZAKE

Msaniii Krg the Don ametoa angalizo kwa mashabiki zake kutofuata au kuamini kile anachokiweka mtandaoni. Katika mahojiano hivi karibu bosi huyo Cash Group Entertainment amesema hayuko mtandaoni kuwafurahisha au kuwashauri watu, hivyo wasichukulie kwa uzito kila kitu anachokiandika mtandaoni kwani inaweza kuwasababishia matatizo. Kauli ya Krg The Don imekuja mara baada ya watu kumkosoa mtandaoni kufuatia kitendo chake cha kuweka hadharani taarifa ya mpesa yake inayoonesha kuwa ametumia kiasi cha shillingi millioni 10 za Kenya katika kipindi cha miezi sita iliyopita. Hatua hiyo ilikosolewa na wengi wakimtaka Krg The Don aache kuwapotosha vijana kwa kuwafanya wajiingize kwenye visa vya uhalifu kwa ajili ya kujipatia kipato.

Read More
 KRG THE DON AONYESHA JEURI YA PESA KWA MASHABIKI

KRG THE DON AONYESHA JEURI YA PESA KWA MASHABIKI

Msanii wa muziki wa dancehall nchini Krg The Don ameamua kutuonyesha jeuri ya pesa anazozitolea jasho kila kuchao kwenye shughuli zake za kibiashara. Kupitia instastory kwenye mtandao wa instagram Krg ameshare taarifa ya mpesa yake inayoonesha kuwa ametumia kiasi cha shillingi millioni 10 za Kenya katika kipindi cha miezi sita iliyopita. Katika taarifa yake hiyo amebainisha kuwa kwa wastani anatumia takriban millioni 1.6 kwa mwezi kwenye matumizi yake ya binafsi jambo ambalo limezua gumzo mtandaoni miongoni mwa wakenya. Hata hivyo watumiaji wa mitandao ya kijamii wamemtaka Krg The Don aache kuwapotosha vijana kwa kuwafanya wajiingize kwenye visa vya uhalifu kwa ajili ya kujipatia kipato huku wengine wakionekana kumtolea uvivu msanii huyo kwa madai ya kutumia suala hilo kutengeneza mazingira ya kuzungumziwa mtandaoni.

Read More
 KRG THE DON AWAJIA JUU VIJANA WANAOTUMIA SHENG NCHINI KENYA

KRG THE DON AWAJIA JUU VIJANA WANAOTUMIA SHENG NCHINI KENYA

Mwanamuziki KRG the Don amewatolea uvivu vijana wanaotumia lugha ya Sheng yenye maneno yasiyoeleweka nchini Kenya. Kulingana na KRG, kundi la vijana wanaotumia lugha hiyo ni malimbukeni ambao wana fikra za kikoloni. “Hiyo ni ujinga, hiyo ni primitivity of the highest order! …iko sheng ile poa… You are going backwards !… ata kama mtu alikua anataka kukuambia anakupenda umuambie nakulombotov, si anaenda kama stima…,” Krg amesema kwa masikitiko. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Ushasema” amewataka vijana wajifunze mambo yatakayowasaidia maishani badala ya kutumia lugha isiyokuwa na mashiko kwenye jamii. “Hizo vitu vijana wametoka sijui wamevuta gum…wanaamka wanaanza kuongea vitu sasa ata ukiulizwa hizo vitu…itawasaidia nini?  Utatoka na hiyo vitu uende utafute kazi gani ? Mi naoana hiyo ni kama kurudi reverse kwa Maisha. Kwa sababu badala ujue lugha yenye unaeza kuongea, Ata si afadhali ujifunze kiChinese… Ukiongea Kichenese, sa hizi watu karibu 1. Something billion wananongea Kichenese, unaeza enda ata china ukafanya kazi ,sasa ukianza kuongea vitu yenye ni wewe na beshtee yako munaelewa,”…Amesema KRG Kauli yake imekuja mara baada ya msanii Jeshi Jinga na Madocho kuingia kwenye bifu ya ni nani hasa ndiye muasisi wa lugha bora ya sheng nchini Kenya. Sheng ni lugha legevu isiyozingatia kanuni za kisarufi ambayo mara nyingi huzungumzwa na vijana wengi nchini Kenya kwa kuchanganya Kiswahili na Kingereza pamoja na lugha za ndani vile Kikuyu,Kijaluo na nyingine nyingi.

Read More
 KRG THE DON AFUFUA BIFU YAKE NA KUNDI LA SAILORS GANG

KRG THE DON AFUFUA BIFU YAKE NA KUNDI LA SAILORS GANG

Msanii wa  muziki nchini KRG The Don amefufua tena bifu yake na wasanii wa sailors gang siku chache baada msanii wa kundi hilo Cocos Juma kudai kuwa lebo ya Black Market Records imesambaratisha muziki wao. Kupitia ukurasa wake wa instagram KRG The Don amesema aliwaonya wasanii wa sailors gang kuhusu muziki wao lakini walimchukulia poa huku akienda mbali zaidi na kusema kwamba tamaa ya kutaka maisha ya haraka ndio imewaponza wasanii hao jambo ambalo analodai lilipelekea kuingia mkataba na lebo ya Black Market Records ambayo iliwapoteza kimuziki. Bosi huyo wa Cash group Entertainment amedai masaibu yanayowaandama wasanii wa Sailors ni kutokana na kiburi waliowaonyesha wadau wa muziki nchini kipindi walipata umaarufu kubwa kwenye tasnia ya muziki nchini. Hata hivyo amewataka wasanii wa Sailors Gang kuwaomba msamaha watu waliowadharau kipindi cha nyuma ili njia zao zianze kufunguka Ikumbukwe KRG The Don na Sailors Gang waliachia  wimbo  wa pamoja uitwao “Nyandus” mwaka wa 2019 lakini lilopokuja suala la kutayarisha video walizozana kuhusiana na ishu ya malipo  na hivyo  ikasambaratisha  mpango wa kuiachia video  rasmi ya wimbo huo.

Read More
 KRG THE DON AZINDUA MAISHA POA APP INAYOJIHUSISHA NA MICHEZO YA KUBASHIRI

KRG THE DON AZINDUA MAISHA POA APP INAYOJIHUSISHA NA MICHEZO YA KUBASHIRI

Mwanamuziki wa Dancehall kutoka Kenya, KRG The Don amezindua programu ya simu inayojihusisha na michezo ya kubashiri iitwayo Maisha POA App, inayolenga kuwasaidia vijana kujikwamua kiuchumi. Katika mkao na wanahabari KRG The Don amesema app hiyio ambayo inapatikana Google Playstore kwa watumiaji wa mfumo wa Android itatoa fursa kwa vijana kujishindia shillingi millioni 1.2 kwa siku. Msanii huyo amesema mtumiaji atatakiwa kulipa shillingi 100 kujiandikisha na kadri mtu anavyozidi kujiandikisha anajitengeneza mazingira ya kushinda pesa taslimu kupitia droo ambayo itafanyika kila siku. Hata hivyo KRG amewakikishia mashabiki zake pamoja na wakenya kwamba app hiyo imeidhinishwa na bodi inayodhibiti michezo ya kubashiri nchini, hivyo haihusiki kivyovyote na masuala ya kuwatapeli watu. Maisha Poa ni app ambayo ipo chini ya kampuni ya Pepe Mtanii ambayo inalenga kuwasaidia vijana kuboresha maisha yao kupitia michongo mbali mbali.

Read More
 BIFU LA KRG THE DON NA KUNDI LA MBOGI GENJE LACHUKUA SURA MPYA

BIFU LA KRG THE DON NA KUNDI LA MBOGI GENJE LACHUKUA SURA MPYA

Inaonekana bifu ya Mbogi Genje na Krg The Don haitapoa hivi karibuni hii ni baada ya wasanii wa kundi hilo kuibuka na kumchana Krg The Don kutokana na kauli aliyotoa majuzi kuwa wasanii wa mbogi genje ni wasanii wa mashinani. Wakiwa kwenye moja ya Interview wasanii hao wakiongozwa na Militant wamesema Krg The Don aache kujipiga kifua kuwa ni msanii wa kimataifa wakati ana idadi ndogo ya wafuasi kwenye mitandao kustream muziki duniani huku wakisema kama kweli Krg The Don angekuwa na pesa angewalipa baada ya kufanya nao kolabo kupitia wimbo wa Zible. Wasanii hao wa Mbogi Genje wameenda mbali zaidi na kusema kuwa hawana muda wa kupishana na Krg The Don ila hawakufurahishwa na hatua ya msanii huyo kukiuka mkataba wa maelewano kuhusu umiliki wa wimbo wa Zible baada ya kupakia video ya wimbo huo kwenye Youtube channel yake bila ridhaa yao. Mapema wiki Krg The Don aliibuka na kuwachana wasanii Mbogi Genje kuwa hawakugharamia chochote kwenye mchakato wa kuandaa audio na video wa wimbo wa Zible,  hivyo hawana haki ya kudai umiliki wa wimbo huo. Hii ni baada ya mbogi genje kudai kuwa Krg The Don aliwasiliti baada ya kukiuka mkataba wa maelewano kuhusu umiliki wa wimbo wa Zible alipoahamua kupakia video wa wimbo huo kwenye channel yake ya youtube bila idhini yao

Read More
 KRG THE DON AWATOLEA UVIVU WASANII WA MBOGI GENJE KWA KUDAI WIMBO WA ZIBLE NI WAO

KRG THE DON AWATOLEA UVIVU WASANII WA MBOGI GENJE KWA KUDAI WIMBO WA ZIBLE NI WAO

Mwanamuziki wa dancehall nchini KRG The Don amenyosha maelezo kuhusu umiliki wa wimbo wa Zible aliowashirisha wasanii wa kundi la Mbogi Genje baada ya kundi hilo kudai kuwa KRG aliiba ubunifu wao. Katika mahojiano yake hivi karibuni KRG The Don amesema wasanii wa Mbogi Genje hawakugharamia chochote kwenye mchakato wa kuandaa wimbo huo, hivyo hawana haki ya kudai mirabaha ya wimbo wa Zible. KRG The Don amewatolea uvivu wasanii wa Mbogi Genje kwa kutumia lugha isiyokuwa na mashiko kuwasilisha ujumbe kwa mashabiki, kitu ambacho amedai kuwa imekuwa kizingiti kwa muziki wao kusikilizwa na watu wa umri wote katika jamii. Hitmaker huyo wa “Full kishunzi” amepuzilia mbali madai ya wasanii wa Mbogi Genje kuwa walimuandikia wimbo wa zible kwa kusema kwamba madai hayo hayana msingi wowote kwani alihusika pakubwa kuandika wimbo huo bila usaidizi wa mtu yeyote. Kauli ya KRG The Don imekuja mara baada ya wasanii wa kundi la mbogi genje kumtuhumu kuwa alishindwa kuwalipa alipowashirikisha kwenye wimbo wake uitwao Zible ambapo walienda mbali zaidi na kusema kwamba wao ndio walihusika kwa asilimia moja kwenye uandishi wa wimbo huo.

Read More
 KRG THE DON ASHAMBULIWA MTANDAONI KISA KUTIA NIA YA KUJIUNGA NA SIASA ZA UCHAGUZI MKUU NCHINI KENYA

KRG THE DON ASHAMBULIWA MTANDAONI KISA KUTIA NIA YA KUJIUNGA NA SIASA ZA UCHAGUZI MKUU NCHINI KENYA

Walimwengu kwenye mitandao ya kijamii wamemshambulia mwanamuziki wa dancehall nchini KRG The Don mara baada ya msanii huyo kuomba ushauri awanie kiti gani cha kisiasa kwenye uchaguzi mkuu wa Agosti 9. Kupitia instagram page yake KRG The Don alidai kuwa amekuwa akipokea shinikizo kutoka kwa marafiki zake wa karibu kujiunga na siasa. Sasa kupitia uwanja wa comment wa post yake mashabiki wamemtolea uvivu Krg The Don wakisema kuwa hapaswi kuwania kiti chochote cha kisiasa kwani hana  kabisa vigezo vya kuwa kiongozi. Haikushia hapo wameenda mbali zaidi na kumshauri KRG The Don aendelee kufanya muziki wa Gengetone huku wengine wakidai kuwa msanii huyo anajaribu kutengeneza mazingira ya kuzungumziwa kwenye media ikizingatiwa kuwa muziki umemshinda.

Read More
 MENEJA WA KUNDI LA MBOGI GENJE AMVUA NGUO KRG THE DON KISA KUWAADA WAKENYA

MENEJA WA KUNDI LA MBOGI GENJE AMVUA NGUO KRG THE DON KISA KUWAADA WAKENYA

Meneja wa kundi la Mbogi Genje Eastlando President amemtolea uvivu msanii KRG The Don kwa madai ya kuwadanganya wakenya kuwa yeye ndiye mmliki wa ukumbi wa burudani wa Casavara. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Eastlando president amesema kuwa mmiliki halisi waCasavara ni msanii wa dancehall kutoka jamaica Konshens ila KRG amepewa kazi ya kuipromote ukumbi huo wa starehe. Eastlando President ameenda mbali kumtaka KRG aache suala la kujigamba na badala ajifunze kuwa heshimu watu wengine kwani pesa ambazo analipwa na konshens zimempa kiburi. Kauli ya Eastlando president imekuja mara baada ya KRG The Don kushindwa kuwalipa wasanii wa kundi la Mbogi Genje pesa zao baada ya kuwashirikisha kwenye wimbo wake uitwao Zible ambao ulikuwa umefutwa kwenye mtandao kwa madai ya hakimiliki.

Read More
 WIMBO MPYA WA MSANII KRG THE DON WAFUFTWA YOUTUBE KWA MADAI YA HAKIMILIKI

WIMBO MPYA WA MSANII KRG THE DON WAFUFTWA YOUTUBE KWA MADAI YA HAKIMILIKI

Mwanamuziki KRG The Don amepata pigo baada ya wimbo wake uitwao Zible aliyomshirikisha msanii wa kundi la Mbogi Genje, Guzman kuondolewa kwenye mtandao wa Youtube kwa madai ya hakimiliki. Kulingana na ujumbe ambao KRG alishare kwenye ukurasa wake wa instagram wimbo huo ulifutwa na msanii chipukizi aitwaye Zoja K Worldwide ambaye anadai kuwa KRG alisample mdundo wake na akautumia kwenye wimbo wake , Zible na Guzman wa Mbogi Genje. Hitmaker huyo wa “Giddem” amewakosoa washindani wake akidai kuwa wanauone  muziki wake wivu huku akiwataka mashabiki zake wawe na subra wakati huu uongozi wake unaifanyia kazi  suala la kurejesha wimbo wake wa zible kwenye mtandao wa youtube. Hata hivyo walimwengu kwenye mitandao ya kijamii wameonekana kutofautiana kimawazo na krg wakidai kuwa msanii huyo huenda msanii huyo amefuta wimbo huo mwenyewe ili azungumziwe kwenye mitandao ya kijamii ikizingatiwa kuwa amekuwa akipenda kujihusisha sana na kiki.

Read More
 KRG THE DON ATANGAZA KUWASAJILI WASANII WAPYA KWENYE LEBO YAKE YA FAST CASH GROUP MUSIC

KRG THE DON ATANGAZA KUWASAJILI WASANII WAPYA KWENYE LEBO YAKE YA FAST CASH GROUP MUSIC

Msanii wa muziki wa dancehall nchini KRG The Don ametangaza mpango wa kuwasajili wasanii wapya kwenye lebo ya muziki ya Fast Cash Group music. Kupitia ukurasa wake wa instagram KRG The Don amewataka mashabiki zake wamuunganishe na wasanii wenye vipaji kwenye muziki kwani lebo ya fast cash Group ipo tayari kuwasaidia kimuziki. Hata hivyo amewataka mashabiki na wasanii chipukizi waendelee kufuatilia mitandao ya kijamii ya Fast Cash Group kwa lebo hiyo itatoa tamko rasmi hivi karibuni ya kufanikisha mchakato mzima wa kuwasajili wasanii. “Lebo ya muziki ya Fast Cash Group ina habari njema kwa wasanii wachanga wenye vipaji kama unamjua msanii ambaye ana kipaji mwaambie kwamba lebo ya Fast Cash Group ipo tayari kumsaidia kimuziki ila kwa sasa endeleeni kufuatilia Fast Cash Group music kupitia mitandao yetu ya kijamii mwaka huu tuna mazuri kwa ajili yenu” amesema KRG The Don kupitia Instagram page yake. Utakumbuka lebo ya muziki ya Fast Cash Group ambayo makao yake makuu yapo South B jijini Nairobi ilizinduliwa miaka saba iliyopita na  KRG The Don  kwa ajili ya kurekodi kazi za wasanii na muziki wake mwenyewe.

Read More
 KRG THE DON ADAI ALIHUSIKA KWENYE UDUKUZI WA AKAUNTI YA INSTAGRAM YA MWANABLOGU EDGAR OBARE

KRG THE DON ADAI ALIHUSIKA KWENYE UDUKUZI WA AKAUNTI YA INSTAGRAM YA MWANABLOGU EDGAR OBARE

Mwanamuziki kutoka Kenya KRG The Don amedai kwamba yeye ndiye aliifuta akaunti mpya ya instagram ya mwanablogu mwenye utata nchini humo Edgar Obare. Kupitia instagram page yake KRG ameandika ujumbe wa kejeli kwenda kwa wafuasi wa Edgar Obare kwa kusema kwamba alikuwa ametishia kuifuta akaunti ya mwanablogu huyo ya Instagram ila watu walichukulia kama mzaha. “I had said i will delete BNNKE for this planet they though I was joking” ..alisema  KRG The Don kupitia Instagram yake. Hata hivyo wafuasi wa KRG The Don wameonekana kutofauti kimawazo na msanii huyo kwa kusema kwamba wanamjua aliyedukua akaunti ya Instagram ya Edgar Obare. Utakumbuka KRG The Don aliingia kwenye ugomvi na Edgar Obare baada ya mwanablogu huyo kuchapisha taarifa akihoji kuwa utajiri wa mwanamuziki huyo umetokana na biashara ya ulanguzi wa pesa ambayo amekuwa akifanya kwa muda. Akaunti ya kwanza ya Instagram ya Edgar Obare ilifutwa mara baada ya mwanablogu huyo kuwa kero kwa mastaa mbali mbali nchini kwa kuanika maovu yao yote kupitia ukurasa wake huo. Jaribio lake la kuirejesha akaunti yake ya kwanza ya Instagram iligonga mwamba na ndipo akafungua akaunti nyingine ambayo juzi kati  ilidukuliwa na mtu asiyejulikana ila wajuzi wa mambo kwenye mitandao ya kijamii wanahoji kuwa ni mchekeshaji Jalang’o ndiye alidua akaunti  hiyo kwani hajakuwa na maelewano mazuri na Edgar Obare.

Read More