KRG THE DON ATHIBITISHA UJIO WA KOLABO YAKE NA MKALI WA DANCEHALL KUTOKA JAMAICA KONSHENS

KRG THE DON ATHIBITISHA UJIO WA KOLABO YAKE NA MKALI WA DANCEHALL KUTOKA JAMAICA KONSHENS

Habari nzuri kwa mashabiki wa muziki nchini ni kwamba tutarajie muda wowote ujio wa Collabo kati ya mwanamuziki KRG The Don na Star wa muziki wa dancehall duniani Konshens. Kupitia insta story ya KRG The Don kwenye mtandao wa Instagram ameshare taarifa hiyo nzuri kwa mashabiki na wadau wa muziki nchini kwa kuthibitisha kuwa tayari wawili hao wamefanya kazi ya pamoja. Endapo collabo hiyo itatoka itamfanya KRG The Don kuwa msanii wa pili nchini baada ya Ethic Entertainment kufanya kazi ya pamoja na mwanamuziki huyo nyota kutoka Jamaica. Itakumbukwa kwenye mkesha wa kuamkia mwaka mpya 2022 Konshens alipiga shoo ya kufa mtu kwenye onesho la NRG Wave Concert, shoo ambayo iliyoaacha wapenzi wa muziki mzuri wa dancehall wakitaka burudani zaidi kutoka mkali huyo

Read More
 SAKATA LA NDOA YA MSANII KRG THE DON LACHUKUA SURA MPYA

SAKATA LA NDOA YA MSANII KRG THE DON LACHUKUA SURA MPYA

Sakata la ndoa ya msanii KRG The Don  na mkewe Linah wanjiru linaendelea kuwaka moto. Mtandao wa Nairobi gossip umeripoti kwamba, Linah Wanjiru ameorodhesha kiasi ambacho anataka alipwe na KRG The Don baada ya kuachana.  Linah amesema anahitaji kiasi cha shillingi elfu 350  za kenya kwa mwezi kwa ajili ya matunzo yaani Spousal Support. Linah ambaye amezaa motto mmoja na KRG The Don, anayatolea macho mamilioni ya pesa ya msanii huyo wa muziki ambapo pia amemtaka amlipie ada ya mawakili wake kwa ajili ya mchakato mzima wa kufungua shauri la talaka miezi michache iliyopita.

Read More
 KRG THE DON AFUNGUA SHAURI LA TALAKA MAHAKAMANI

KRG THE DON AFUNGUA SHAURI LA TALAKA MAHAKAMANI

Msanii wa muziki wa dancehall nchini KRG The Don amefungua shauri la talaka mahakamani dhidi ya mke wake Linah Wanjiru, shauri hilo limefunguliwa katika Mahakama ya Milimani Jijini Nairobi. KRG ameweka wazi hilo kupitia instagram page yake baada ya kupost  nyaraka za kisheria kuhusiana na mchakato wa talaka na kusindikiza na caption inayosomeka “kwa wale waliyokuwa wanachukulia kwa mzaha, poleni” Hitmaker huyo Giddem alifunga ndoa na mke wake huyo mwaka wa 2014 na wamejaliwa kupata wawili kwa pamoja. Hatua ya KRG kufungua shauri la talaka dhidi mke wake inakuja siku chache baada ya kumsuta vikali mke wake huyo kwa madai ya kujihusisha sana na anasa na kusahau kuwahudumia watoto wao.

Read More
 KRG THE DON ATHIBITISHA KUACHANA NA BABY MAMA WAKE.

KRG THE DON ATHIBITISHA KUACHANA NA BABY MAMA WAKE.

Baada ya uvumi wa wiki kadhaa,  Msanii wa muziki wa Dancehall nchini KRG The Don hatimaye amethibitisha kuwa yeye na mke wake sio wapenzi tena. KRG ameweka wazi hilo kupitia Instagram page yake baada ya kupost picha ya mke wake huyo na kusindikiza na caption inayoashiria kuwa wameachana rasmi. Hitmaker huyo “Giddem” amemsuta vikali mke wake huyo kwa madai ya kujihusisha sana na anasa na kusahau kuwahudumia watoto wao. KRG pia ametumia fursa hiyo kukanusha madai yanayosambaa kwenye mitandao kuwa alitoka nje ya ndoa yake na ndio maana uhusiano wake na Baby mama wake ulivunjika. Hata  hivyo, bado haijabainika kama kuna ukweli wowote kuhusu stori za wawili hao kuachana ila kwa sasa wamefuta picha zote walizowahi kupiga wakiwa pamoja kwenye mtandao wa Instagram.

Read More