KRG THE DON AFUNGUA SHAURI LA TALAKA MAHAKAMANI

KRG THE DON AFUNGUA SHAURI LA TALAKA MAHAKAMANI

Msanii wa muziki wa dancehall nchini KRG The Don amefungua shauri la talaka mahakamani dhidi ya mke wake Linah Wanjiru, shauri hilo limefunguliwa katika Mahakama ya Milimani Jijini Nairobi. KRG ameweka wazi hilo kupitia instagram page yake baada ya kupost  nyaraka za kisheria kuhusiana na mchakato wa talaka na kusindikiza na caption inayosomeka “kwa wale waliyokuwa wanachukulia kwa mzaha, poleni” Hitmaker huyo Giddem alifunga ndoa na mke wake huyo mwaka wa 2014 na wamejaliwa kupata wawili kwa pamoja. Hatua ya KRG kufungua shauri la talaka dhidi mke wake inakuja siku chache baada ya kumsuta vikali mke wake huyo kwa madai ya kujihusisha sana na anasa na kusahau kuwahudumia watoto wao.

Read More
 KRG THE DON ATHIBITISHA KUACHANA NA BABY MAMA WAKE.

KRG THE DON ATHIBITISHA KUACHANA NA BABY MAMA WAKE.

Baada ya uvumi wa wiki kadhaa,  Msanii wa muziki wa Dancehall nchini KRG The Don hatimaye amethibitisha kuwa yeye na mke wake sio wapenzi tena. KRG ameweka wazi hilo kupitia Instagram page yake baada ya kupost picha ya mke wake huyo na kusindikiza na caption inayoashiria kuwa wameachana rasmi. Hitmaker huyo “Giddem” amemsuta vikali mke wake huyo kwa madai ya kujihusisha sana na anasa na kusahau kuwahudumia watoto wao. KRG pia ametumia fursa hiyo kukanusha madai yanayosambaa kwenye mitandao kuwa alitoka nje ya ndoa yake na ndio maana uhusiano wake na Baby mama wake ulivunjika. Hata  hivyo, bado haijabainika kama kuna ukweli wowote kuhusu stori za wawili hao kuachana ila kwa sasa wamefuta picha zote walizowahi kupiga wakiwa pamoja kwenye mtandao wa Instagram.

Read More