Marioo Adai Hajawahi Kuandikiwa Wimbo, Mashabiki Wahoji Bifu na Mbosso

Marioo Adai Hajawahi Kuandikiwa Wimbo, Mashabiki Wahoji Bifu na Mbosso

Msanii nyota wa Bongo Fleva, Marioo, amefunguka kuhusu safari yake ya muziki, akisema licha ya mafanikio makubwa aliyopata hajawahi kubebwa na lebo kubwa wala kuandikiwa wimbo na mtu yeyote. Kupitia Instastory, msanii huyo amesema kuwa yeye ndiye msanii pekee mwenye hits “back to back”, akiongeza kuwa tayari ameshinda mara kadhaa tuzo za Msanii Bora wa Mwaka (Bongo Fleva), jambo linaloashiria ukubwa wa mchango wake katika tasnia. Marioo, ambaye kwa sasa anatamba na kibao chake “Dunia”, pia amewajibu mashabiki waliokuwa wakimtaka kutoa, “Global Song”, akiahidi kwamba wimbo huo utapatikana kwenye Deluxe Version ya albamu yake “The God Son”, iliyotoka rasmi mwezi Novemba 2024. Kauli hiyo ya Marioo imepokewa kwa mitazamo tofauti, huku baadhi ya mashabiki wakidai huenda ujumbe huo umemlenga aliyekuwa staa wa WCB, Mbosso, ambaye juzi kati Diamond Platnumz alidai kwamba ndiye aliyeandika wimbo wake maarufu “Pawa.” Hali hiyo imezidisha minong’ono ya uwepo wa bifu la chini kwa chini kati ya Marioo na Mbosso, hasa ikizingatiwa kuwa wote wanahesabika kati ya waimbaji wenye mashabiki wengi na nyimbo zinazotamba kwa sasa.

Read More
 Marioo Aendeleza Mafanikio ya The Goson Album kwa Toleo la Deluxe

Marioo Aendeleza Mafanikio ya The Goson Album kwa Toleo la Deluxe

Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Marioo, sasa anajiandaa kuachia rasmi Deluxe Edition ya albamu yake “The Goson”, ikiwa ni miezi saba imepita tangu atoe albamu yake hiyo iliyopata mapokezi makubwa kutoka kwa mashabiki zake. Kwa mujibu wa taarifa, Marioo ameongeza nyimbo kadhaa mpya kwenye toleo hilo maalum, hatua ambayo inalenga kuwapa mashabiki wake ladha zaidi ya kazi zake za kisanaa. Ingawa hajatangaza rasmi orodha kamili ya nyimbo zitakazojumuishwa kwenye Deluxe, vyanzo vya karibu na msanii huyo vinaashiria kuwa baadhi ya nyimbo hizo tayari zimekamilika na zinasubiri muda sahihi wa kuachiwa. Hii si mara ya kwanza kwa Marioo kutumia mbinu ya Deluxe Edition. Wafuasi wake watakumbuka kuwa albamu yake ya awali, The Kid You Know, nayo ilipata toleo la Deluxe ambalo lilijumuisha vibao vipya kama Nikazama na Sing, ambavyo vilipata mapokezi makubwa.

Read More
 Aliyekuwa Shemeji wa Diamond Platnumz aingilia sakata la Marioo kusainiwa WCB

Aliyekuwa Shemeji wa Diamond Platnumz aingilia sakata la Marioo kusainiwa WCB

Bado sakata la mwanamuziki Marioo kudaiwa kumuomba Diamond Platnumz amsaini katika record label ya WCB Wasafi linazidi kuibua mapya mengine, baada ya aliyekuwa shemeji wa mwanamuziki Diamond Platnumz, Msizwa kufichua kuwa jambo hilo limegeuzwa na kwamba Diamond Platnumz  ndiye aliyekuwa akitaka kumsani Marioo na sio Marioo kutaka kusainiwa na Diamond. Msizwa ambayee kupitia ukurasa wake wa Instagram ameeleza kuujua ukweli, amedai kwamba alikuwa sehemu ya shuhuda wakati wa mazungumzo ya Diamond Platnumz kutaka kumsaini Marioo kipindi wapo wasafi village, ambapo Marioo alionesha kutoafiki jambo hilo kwa wakati huo kiasi cha kuomba ushauri kutoka kwake. Hata hivyo Msizwa ameeleza kuwa kama kuna siku nyingine wawili hao waliongea kuhusu hilo jambo na yeye hakuwepo ni sawa ,lakini kama ni kipindi hicho alicho sema Baba Levo basi yeye alikuwepo kama shuhuda pamoja na Baba Levo pia.

Read More
 Marioo akanusha madai ya Diamond kutaka kujiunga na WCB

Marioo akanusha madai ya Diamond kutaka kujiunga na WCB

Staa wa Muziki wa Bongo Fleva Marioo amekanusha stori za kutaka kujiunga na Lebo ya WCB kama ilivyoelezwa na Mkurugenzi wa Lebo Hiyo na Staa wa Muziki Diamond Platnumz . Kabla ya Show ya Cheers 2023 ya Diamomd kufanyika, Staa huyo alifanya Mahojiano na Kituo cha habar cha WasafiFm na kudai kwamba Marioo aliwahi kumfuata na kuomba kisainiwa kwenye lebo ya WCB kitu ambacho Diamond alikataa kutokana na ukubwa alionao kwa sasa. Marioo Amekanusha stori hiyo kwa kumjibu shabiki ambaye alitaka kujua kama kuna ukweli wowote

Read More
 Marioo aachia rasmi Tracklist ya Album yake mpya

Marioo aachia rasmi Tracklist ya Album yake mpya

Mkali wa Bongo Fleva Marioo ameachia Tracklist ya Album yake mpya The Kid You Know ambayo itatoka rasmi Disemba 9 mwaka huu. Album hiyo ya kwanza kwa Marioo, ina jumla ya mikwaju 17 huku ndani akiwashirikisha wakali kama Ali Kiba, Harmonize, Rayvanny, Jux, Ladipoe na wengine wengi. Ikumbukwe, hii inakuwa ni album ya kwanza kwa Marioo  katika safari yake ya muziki.

Read More
 Marioo kuachia historia fupi ya maisha yake kabla ya kutoa Album yake mpya mwezi Desemba 2022

Marioo kuachia historia fupi ya maisha yake kabla ya kutoa Album yake mpya mwezi Desemba 2022

Baada ya kuachia cover ya album yake mpya iitwayo “The Kid You Know” anayotarajia kuitoa Desemba 9, 2022, mwimbaji wa Bongofleva Marioo ametangaza kuwa ataachia historia fupi ya maisha yake kabla ya ujio wa album yake mpya. Marioo ameeleza hilo kupitia insta story yake. Pia amebainisha kwa sasa unaweza ukai Pre-Order “The Kid You Know” kupitia Africori. Album hiyo ya Marioo itakuwa na jumla ya nyimbo 18, huku nyimbo 3 toka kwenye album hiyo tayari zimeshatoka ambazo ni “Mi Amor”, “Naogopa” pamoja na “Dear EX”, nyimbo 15 zilizobaki zote ni mpya.

Read More
 Marioo atamba na album yake mpya, Asema ni moto wa kuotea mbali.

Marioo atamba na album yake mpya, Asema ni moto wa kuotea mbali.

Staa wa muziki wa Bongofleva, Marioo ni kama tayari ameikamilisha Album yake mpya ambayo huenda ikaingia sokoni hivi karibuni. Kupitia insta story kwenye mtandao wa Instagram Mkali huyo wa ngoma ya Dear Ex amesema ngoma zilizopo kwenye album yake hiyo ni za moto lakini pia kuna nyimbo ambazo zimebaki na anashindwa aziweke wapi. “Yaani kwenye albamu mangoma yamejaa halafu yote moto, halafu bado nipo na mawe mengine, hata sijui nayafanyia nini na bado nipo na mood ya kurekodi” amesema Marioo. Kwenye andiko lake hilo ameishia kwa kusema anafikiria kuwabariki mashabiki zake na zawadi ambayo walimwengu wametafsiri huenda msanii huyo ana mpango wa kuachia EP kabla ya Album. Utakumbuka juzi kati Marioo alitudokezea kuwa ngoma zake kama Mi Amor, Naogopa na Dear EX zitakuwepo kwenye albamu yake mpya.

Read More
 MAPANCH NA MARIOO WATUPIANA LAWAMA KUHUSU WIMBO WA “MY LOVE”

MAPANCH NA MARIOO WATUPIANA LAWAMA KUHUSU WIMBO WA “MY LOVE”

Agosti 10, msanii wa Bongfleva Mapanch aliachia video ya ngoma yake My Love aliyomshirikisha Marioo. Hata hivyo takriban siku nne baadaye, video hiyo iliondolewa youtube. Mapanch anadai aliyeiondoa ni Marioo ambaye alituma malalamiko ya hakimiliki. Msanii huyo amesema amechukizwa na kitendo hicho kwa kueleza kuwa Marioo ni mnafiki na mbaya zaidi ni yeye ndiye aliyetaka kuwepo kwenye wimbo huo. Hata hivyo Marioo amezungumza kwanini hakutaka video ya My Love aliyoshirikishwa na mapanch itoke. Marioo amesema ngoma hiyo ilikaa sana ndani licha ya kuwahimiza mara kadhaa wawaiache kuitoa kwa sababu muziki wake unabadilika kadri siku zinavyokwenda.

Read More
 MARIOO AFIKISHA VIEWS MILLIONI 100 YOUTUE

MARIOO AFIKISHA VIEWS MILLIONI 100 YOUTUE

Kuizuia nyota ya Marioo ni sawa na kuziba mwanga kwa kiganja cha mkono. Nyota huyo  kutoka Tanzania anaendelea kugonga vichwa vya habari na mara hii ni kuhusiana na idadi ya views youtube. Good news kwa mashabiki wa mkali huyo ni kwamba amefikisha watu Milioni 100 waliotazama kazi zake mbalimbali katika channel yake ya mtandao wa Youtube. Marioo alijiunga na mtandao huo Januari 4, mwaka wa 2018 na amepata watazamaji wengi kutokana na kazi zake mbalimbali anazoziweka katika mtandao huo. Baadhi ya matukio anayoyaweka katika mtandao huo ni video, shoo anazozifanya na utayarishaji wa video za nyimbo zake. Kutokana na idadi hiyo ya watazamaji, marioo amewaacha mbali baadhi ya wasanii wa Afrika wanaofanya vizuri katika tasnia ya muziki.

Read More
 MARIOO AWAPA SOMO WASANII CHIPUKIZI

MARIOO AWAPA SOMO WASANII CHIPUKIZI

Staa wa Muziki wa Bongofleva Marioo ambaye kwa sasa anafanya poa na singo yake “Mi Amor” ameamua kutoa somo kwa wasanii chipukizi. Kupitia Instastory yake kwenye mtandao wa Instagram Marioo amewaambia wasanii hao kuwa wanapohitaji kutoa wimbo wahakikishe wimbo husika unakuwa mkali kuliko nyimbo zilizopo masikioni mwa watu. Mbali na hayo, ameendelea kutusanua kuhusu ujio wa album yake mpya kwa kusema kwamba album yake itaitwa “The Boy You Know” na itaingia sokoni kabla ya mwaka huu haujakamilika. Utakumbuka usiku wa kuamkia Aprili 3 kwenye hafla ya ugawaji wa tuzo za Tanzania Music Awards Marioo alishinda tuzo ya Msanii Bora wa Kiume wa Bongofleva na Wimbo Bora wa Bongo Fleva wa Mwaka kupitia ngoma yake ya “Beer Tamu”

Read More
 WIMBO WA MARIOO “MI AMOR” WAFIKISHA STREAMS MILIONI 10 BOOMPLAY

WIMBO WA MARIOO “MI AMOR” WAFIKISHA STREAMS MILIONI 10 BOOMPLAY

Disemba 24 mwaka wa 2021 Staa wa muziki wa Bongofleva Marioo alitubariki na singo inayokwenda kwa jina la “Mi Amor” akiwa amemshirikisha msanii wa kike nchini Jovial. Habari njema kwa mashabiki wa Marioo ni kwamba Wimbo huo umefanikiwa kufikisha jumla ya streams millioni 10 kwenye mtandao wa kupakua na kusikiliza muziki wa Boomplay. Sanjari na hilo wimbo wa “Mi Amor” pia unazidi kufanya vizuri kwenye mtandao wa youtube kwani mpaka sasa video yake imeweza kutazamwa zaida ya mara millioni 3.3 tangu ipakiwe kwenye mtandao huo Februari 25, 2022. “Mi Amor” unakuwa wimbo wa kwanza kutoka kwa Marioo kuwa na idadi hiyo kubwa ya STREAMS, ikizipita nyimbo kama “For You” wenye streams Milioni 4.9 ulitoka mwaka jana, “Beer Tamu” wenye streams Milioni 3.8 na watatu katika top 3 ya kazi za Marioo ilizofikisha streams zaidi ya Milioni ni “Mama Amina” wenyewe una streams Milioni 1.6

Read More
 NIKKI MBISHI:  MARIOO ALISTAHILI KUPEWA MIRABAHA NA COSOTA KUTOKA KAZI ZAKE KUPIGWA SANA KWENYE MEDIA

NIKKI MBISHI: MARIOO ALISTAHILI KUPEWA MIRABAHA NA COSOTA KUTOKA KAZI ZAKE KUPIGWA SANA KWENYE MEDIA

Rapa kutoka nchini Tanzania Nikki Mbishi amesema Marioo kupitia wimbo wake “BIA TAMU” alistahili kuwa namba moja kwenye orodha ya wasanii ambao wamepata gawio la mirabaha kutoka Chama cha Hatimiliki Tanzania – COSOTA. Kupitia ukurasa wake wa Twitter Nikki mbishi amesema wimbo wa Bia Tamu umepigwa kuliko wimbo wowote nchini Tanzania katika kipindi cha miezi 7 iliyopita. “Yaani mtu unakuja na hoja jenzi ambayo pengine ingewapa hamasa Con Boi na Rapcha watu wanahisi umewalinganisha. Jamaa wapo kama COSOTA wakiulizwa vigezo vya kutoa mirabaha, hata mjinga anajua MARIOO alistahili kuwa namba moja BIA TAMU imepigwa kulizo nyimbo zote kwa 7 months ago.” alichomekea Nikki Mbishi wakati akichangia hoja kwenye tweet ya Wakazi iliyoibua mjadala mzito Twitter, tangu juzi. Kwa mujibu wa COSOTA,  Ali Kiba ndiye aliongoza kwa wasanii wa bongo fleva waliopata pesa nyingi za Mirabaha ambapo alipata kiasi cha shilling 3 za Kenya huku Marioo akikosekana hata kwenye TOP 20 ya orodha hiyo.

Read More