Marioo Adai Hajawahi Kuandikiwa Wimbo, Mashabiki Wahoji Bifu na Mbosso
Msanii nyota wa Bongo Fleva, Marioo, amefunguka kuhusu safari yake ya muziki, akisema licha ya mafanikio makubwa aliyopata hajawahi kubebwa na lebo kubwa wala kuandikiwa wimbo na mtu yeyote. Kupitia Instastory, msanii huyo amesema kuwa yeye ndiye msanii pekee mwenye hits “back to back”, akiongeza kuwa tayari ameshinda mara kadhaa tuzo za Msanii Bora wa Mwaka (Bongo Fleva), jambo linaloashiria ukubwa wa mchango wake katika tasnia. Marioo, ambaye kwa sasa anatamba na kibao chake “Dunia”, pia amewajibu mashabiki waliokuwa wakimtaka kutoa, “Global Song”, akiahidi kwamba wimbo huo utapatikana kwenye Deluxe Version ya albamu yake “The God Son”, iliyotoka rasmi mwezi Novemba 2024. Kauli hiyo ya Marioo imepokewa kwa mitazamo tofauti, huku baadhi ya mashabiki wakidai huenda ujumbe huo umemlenga aliyekuwa staa wa WCB, Mbosso, ambaye juzi kati Diamond Platnumz alidai kwamba ndiye aliyeandika wimbo wake maarufu “Pawa.” Hali hiyo imezidisha minong’ono ya uwepo wa bifu la chini kwa chini kati ya Marioo na Mbosso, hasa ikizingatiwa kuwa wote wanahesabika kati ya waimbaji wenye mashabiki wengi na nyimbo zinazotamba kwa sasa.
Read More