Marioo Ajivunia Kuleta Sound Mpya Afrika Mashariki

Marioo Ajivunia Kuleta Sound Mpya Afrika Mashariki

Staa wa muziki wa Bongo Fleva, Marioo, amesema anajivunia kuwa miongoni mwa wasanii walioweza kuleta sound mpya katika ukanda wa Afrika Mashariki, hatua ambayo imemuwezesha kutengeneza hits kadhaa. Akizungumza na Mpasho akiwa nchini Kenya, Marioo amesema kuwa sound aliyotumia kwenye nyimbo zake “Oluwa,” “Hahaha,” na “Dunia” zinafanana kwa sababu zimetengenezwa kwa mtindo mmoja aliouamini tangu mwanzo. Kwa mujibu wake, uamuzi wa kusimamia sound hiyo ulimsaidia kutoa hit tatu mfululizo. Marioo amesema mafanikio hayo yamempa imani kubwa kuwa yeye ndiye aliyeileta sound hiyo kwa mara ya kwanza katika soko la muziki la Afrika Mashariki, akisisitiza kuwa kujiamini na ubunifu ndivyo nguzo kuu za mafanikio yake. Kauli ya Marioo imeendelea kuzua gumzo miongoni mwa wadau wa muziki, wengi wakimtaja kama msanii mwenye maono mapya na mchango mkubwa katika mabadiliko ya sound ya Bongo Fleva na muziki wa Afrika Mashariki kwa ujumla.

Read More
 Marioo Akanusha Madai ya Kununua Views YouTube

Marioo Akanusha Madai ya Kununua Views YouTube

Msanii wa Bongo Fleva, Marioo, ameibuka na kukanusha vikali madai yanayosambaa mitandaoni kwamba alinunua watazamaji (views) wa YouTube kwa ajili ya wimbo wake mpya Oluwa. Kupitia mitandao yake ya kijamii , Marioo amesisitiza kuwa idadi kubwa ya watazamaji walioupokea wimbo huo ni halali kabisa na inatokana na mapenzi ya mashabiki wake walio ndani na nje ya Tanzania. Msanii huyo ameonesha kushangazwa na hali ya wimbo wake kushindwa kuingia kwenye orodha ya Trending YouTube, licha ya kufikisha idadi kubwa ya watazamaji ndani ya muda mfupi. Marioo amewataka mashabiki na watu wenye uelewa wa masuala ya TEHAMA (IT) kujitokeza kumsaidia kubaini tatizo linalofanya wimbo wake usiingie trending YouTube, licha ya kufanya vizuri kwa upande wa watazamaji. Kauli ya Marioo imeibua mjadala mpana mitandaoni, ambapo baadhi ya mashabiki wameendelea kumpa moyo na kumpongeza kwa mafanikio ya Oluwa, huku wengine wakijadili kwa kina mfumo wa YouTube na vigezo vyake vya trending.

Read More
 Marioo Atuhumiwa Kutumia Maroboti Kupandisha Views za Wimbo Wake Youtube

Marioo Atuhumiwa Kutumia Maroboti Kupandisha Views za Wimbo Wake Youtube

Msanii wa Bongo Fleva Marioo anatuhumiwa kutumia maroboti kupata views za wimbo wake mpya “Oluwa”, baada ya kazi hiyo kufikisha views milioni moja ndani ya siku mbili pekee tangu kuachiwa kwake. Madai hayo yameibuka miongoni mwa mashabiki na wadau wa muziki mitandaoni, wakidai kasi ya kupanda kwa views hizo haieleweki kirahisi ikizingatiwa hali ya sasa ya soko la muziki nchini Tanzania. Baadhi ya mashabiki wamehoji alipataje idadi hiyo kubwa ya watazamaji kwa muda mfupi, hasa wakati huu ambapo Watanzania wengi wanadaiwa kususia kazi za wasanii kufuatia kujihusisha kwao na siasa za uchaguzi zilizokumbwa na utata. Aidha, wengine wamedai kuwa wimbo wa “Oluwa” hauonekani kwenye orodha ya nyimbo zinazovuma au trending nchini Tanzania, jambo lililozidi kuibua shaka kuhusu uhalali wa takwimu hizo. Mjadala huo unaendelea kushika kasi mitandaoni huku wengi wakisubiri kauli ya msanii huyo au timu yake ya usimamizi.

Read More
 Marioo Aonyesha Muonekano Mpya Baada ya Kuchora Tattoo Maalum

Marioo Aonyesha Muonekano Mpya Baada ya Kuchora Tattoo Maalum

Mwanamuziki nyota wa Bongo Fleva, Marioo, amezua gumzo mitandaoni baada ya kuonesha muonekano wake mpya uliopambwa na tattoo kadhaa zenye maana kubwa maishani mwake. Msanii huyo ameonekana akijivunia mchoro mpya kwenye mkono wake wa kushoto, ambao umebeba kumbukumbu muhimu za safari yake ya muziki na maisha binafsi. Tattoo hizo zinajumuisha tarehe ya kuzaliwa ya mpenzi wake na babymama, Paula, pamoja na tarehe ya kuzaliwa ya mtoto wao Amara, ishara ya upendo na kujitoa kwa familia yake. Mbali na hayo, Marioo pia ameweka jina la wimbo wake maarufu “Dar Kugumu”, ngoma iliyompa umaarufu mkubwa na kumweka imara kwenye ramani ya muziki wa Afrika Mashariki. Hakuishia hapo,msanii huyo pia amechora jina la “Abbah”, likiwa ni heshima kwa Producer Abbah ambaye amechangia pakubwa katika safari yake ya muziki na mafanikio ya nyimbo zake. Muonekano huo mpya umefanya mashabiki na wadau wa muziki kuendelea kumzungumzia, wengi wakimpongeza kwa ubunifu na kujali watu muhimu katika maisha yake.

Read More
 Marioo Atoa Pole kwa Familia za Watanzania Waliofariki Wakati wa Ghasia za Uchaguzi

Marioo Atoa Pole kwa Familia za Watanzania Waliofariki Wakati wa Ghasia za Uchaguzi

Staa wa muziki wa Bongo Fleva, Marioo, ameungana na Watanzania katika kuomboleza vifo vya watu waliopoteza maisha kufuatia ghasia zilizotokea baada ya uchaguzi uliofanyika Oktoba 29. Kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, Marioo ameonyesha huzuni yake kwa matukio hayo na kutoa pole kwa familia, ndugu, na Watanzania wote walioguswa na vifo hivyo. Amesema kuwa taifa la Tanzania linapitia kipindi kigumu kinachohitaji umoja, subira, na maombi. Msanii huyo ameongeza kuwa Mungu awape faraja wale waliopoteza wapendwa wao na kulitakia taifa la Tanzania amani na baraka. Ujumbe wake umepokelewa kwa hisia tofauti, wengi wakimsifu kwa kuhubiri amani katika kipindi ambacho taifa linapitia mivutano ya kisiasa.

Read More
 Marioo Amsifu Paula Kajala Kama Mwanamke Mrembo Zaidi Duniani

Marioo Amsifu Paula Kajala Kama Mwanamke Mrembo Zaidi Duniani

Staa wa muziki wa Bongo Fleva, Marioo, ameonyesha wazi upendo wake wa dhati kwa mpenzi na mama wa mtoto wake, Paula Kajala, kwa maneno ya kimahaba yaliyowagusa mashabiki wengi mitandaoni. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Marioo amemsifia Paula kuwa ndiye mwanamke mzuri kuliko wote duniani, na kwamba akiwa na uhakika wa penzi lake, anachohitaji kwa sasa ni kuendelea kujituma kutafuta hela. Msanii huyo amesema kuwa mapenzi ya kweli huleta utulivu na motisha katika maisha, jambo ambalo linalomfanya azidi kujikita katika kazi yake ya muziki na kuhakikisha Paula anaishi maisha bora. Marioo na Paula wamekuwa pamoja kwa muda sasa, wakiendelea kuthibitisha uimara wa penzi lao kupitia picha na video wanazoshiriki mara kwa mara kwenye mitandao ya kijamii.

Read More
 Marioo Atishia Kuanika Wanaomtongoza Mke Wake

Marioo Atishia Kuanika Wanaomtongoza Mke Wake

Msanii wa Bongo Fleva, Marioo, amefunguka kwa hasira akilalamikia watu maarufu, wanasiasa na marafiki wanaodaiwa kumtongoza mke wake Paula Kajala. Kupitia instastory, amesema amekuwa akivumilia kwa muda mrefu vitendo vya baadhi ya watu maarufu wanaojaribu kuingilia uhusiano wake, lakini sasa ameamua kuweka mambo hadharani. Hitmaker huyo wa Dunia, ameeleza kuwa ataweka wazi majina na ushahidi wa mazungumzo ya watu wanaomtongoza mchumba wake, akisisitiza kuwa hana tena uvumilivu. Msanii huyo pia amefichua kuwa kipindi mpenzi wake alipokuwa na ujauzito, baadhi ya watu walimshawishi kutoa mimba kwa kisingizio kwamba hangemfaa tena, lakini amesema anamshukuru mama mtoto wake kwa kuonyesha ujasiri na msimamo. Ujumbe huo umechochea maoni mseto mtandaoni, huku mashabiki na wadau wa muziki wakitafsiri maneno ya Marioo kama dalili za msongo wa mawazo au hasira kutokana na mambo ya uhusiano. Wengine wameshauri msanii huyo kutuliza hasira na kushughulikia masuala binafsi nje ya mitandao ya kijamii.

Read More
 Wivu wa Paula Wamchelewesha Marioo Kuachia Video Mpya

Wivu wa Paula Wamchelewesha Marioo Kuachia Video Mpya

Msanii wa Bongo Fleva, Marioo, amefunguka kuwa kuchelewa kwake kuachia video yake mpya kumetokana na wivu wa mpenzi wake, Paula Kajala, ambaye ni binti wa muigizaji maarufu Frida Kajala. Kupitia Instagram, Marioo amesema alitarajia kutoa video hiyo jana kama alivyoahidi kwa mashabiki wake, lakini Paula alimzuia kutokana na baadhi ya vipande vilivyomo kwenye video hiyo ambavyo hakuridhika navyo. Mkali huyo wa ngoma ya Dunia, ameeleza kuwa mpenzi wake alionyesha wivu mkubwa akisema kuna sehemu ambazo hazimpendezi, ingawa yeye binafsi hakuona tatizo lolote katika picha hizo. Marioo ameongeza kuwa amewekeza fedha nyingi katika utayarishaji wa video hiyo, na kuchelewa kwake kumeathiri ratiba aliyokuwa amepanga kwa ajili ya mashabiki wake. Hadi sasa, Marioo hajatangaza tarehe mpya ya kuachia video hiyo, lakini amesema anafanya jitihada za kutatua tofauti hizo ili mashabiki wake wapate kazi hiyo muda si mrefu.

Read More
 Marioo Adai Hajawahi Kuandikiwa Wimbo, Mashabiki Wahoji Bifu na Mbosso

Marioo Adai Hajawahi Kuandikiwa Wimbo, Mashabiki Wahoji Bifu na Mbosso

Msanii nyota wa Bongo Fleva, Marioo, amefunguka kuhusu safari yake ya muziki, akisema licha ya mafanikio makubwa aliyopata hajawahi kubebwa na lebo kubwa wala kuandikiwa wimbo na mtu yeyote. Kupitia Instastory, msanii huyo amesema kuwa yeye ndiye msanii pekee mwenye hits “back to back”, akiongeza kuwa tayari ameshinda mara kadhaa tuzo za Msanii Bora wa Mwaka (Bongo Fleva), jambo linaloashiria ukubwa wa mchango wake katika tasnia. Marioo, ambaye kwa sasa anatamba na kibao chake “Dunia”, pia amewajibu mashabiki waliokuwa wakimtaka kutoa, “Global Song”, akiahidi kwamba wimbo huo utapatikana kwenye Deluxe Version ya albamu yake “The God Son”, iliyotoka rasmi mwezi Novemba 2024. Kauli hiyo ya Marioo imepokewa kwa mitazamo tofauti, huku baadhi ya mashabiki wakidai huenda ujumbe huo umemlenga aliyekuwa staa wa WCB, Mbosso, ambaye juzi kati Diamond Platnumz alidai kwamba ndiye aliyeandika wimbo wake maarufu “Pawa.” Hali hiyo imezidisha minong’ono ya uwepo wa bifu la chini kwa chini kati ya Marioo na Mbosso, hasa ikizingatiwa kuwa wote wanahesabika kati ya waimbaji wenye mashabiki wengi na nyimbo zinazotamba kwa sasa.

Read More
 Marioo Aendeleza Mafanikio ya The Goson Album kwa Toleo la Deluxe

Marioo Aendeleza Mafanikio ya The Goson Album kwa Toleo la Deluxe

Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Marioo, sasa anajiandaa kuachia rasmi Deluxe Edition ya albamu yake “The Goson”, ikiwa ni miezi saba imepita tangu atoe albamu yake hiyo iliyopata mapokezi makubwa kutoka kwa mashabiki zake. Kwa mujibu wa taarifa, Marioo ameongeza nyimbo kadhaa mpya kwenye toleo hilo maalum, hatua ambayo inalenga kuwapa mashabiki wake ladha zaidi ya kazi zake za kisanaa. Ingawa hajatangaza rasmi orodha kamili ya nyimbo zitakazojumuishwa kwenye Deluxe, vyanzo vya karibu na msanii huyo vinaashiria kuwa baadhi ya nyimbo hizo tayari zimekamilika na zinasubiri muda sahihi wa kuachiwa. Hii si mara ya kwanza kwa Marioo kutumia mbinu ya Deluxe Edition. Wafuasi wake watakumbuka kuwa albamu yake ya awali, The Kid You Know, nayo ilipata toleo la Deluxe ambalo lilijumuisha vibao vipya kama Nikazama na Sing, ambavyo vilipata mapokezi makubwa.

Read More
 Aliyekuwa Shemeji wa Diamond Platnumz aingilia sakata la Marioo kusainiwa WCB

Aliyekuwa Shemeji wa Diamond Platnumz aingilia sakata la Marioo kusainiwa WCB

Bado sakata la mwanamuziki Marioo kudaiwa kumuomba Diamond Platnumz amsaini katika record label ya WCB Wasafi linazidi kuibua mapya mengine, baada ya aliyekuwa shemeji wa mwanamuziki Diamond Platnumz, Msizwa kufichua kuwa jambo hilo limegeuzwa na kwamba Diamond Platnumz  ndiye aliyekuwa akitaka kumsani Marioo na sio Marioo kutaka kusainiwa na Diamond. Msizwa ambayee kupitia ukurasa wake wa Instagram ameeleza kuujua ukweli, amedai kwamba alikuwa sehemu ya shuhuda wakati wa mazungumzo ya Diamond Platnumz kutaka kumsaini Marioo kipindi wapo wasafi village, ambapo Marioo alionesha kutoafiki jambo hilo kwa wakati huo kiasi cha kuomba ushauri kutoka kwake. Hata hivyo Msizwa ameeleza kuwa kama kuna siku nyingine wawili hao waliongea kuhusu hilo jambo na yeye hakuwepo ni sawa ,lakini kama ni kipindi hicho alicho sema Baba Levo basi yeye alikuwepo kama shuhuda pamoja na Baba Levo pia.

Read More
 Marioo akanusha madai ya Diamond kutaka kujiunga na WCB

Marioo akanusha madai ya Diamond kutaka kujiunga na WCB

Staa wa Muziki wa Bongo Fleva Marioo amekanusha stori za kutaka kujiunga na Lebo ya WCB kama ilivyoelezwa na Mkurugenzi wa Lebo Hiyo na Staa wa Muziki Diamond Platnumz . Kabla ya Show ya Cheers 2023 ya Diamomd kufanyika, Staa huyo alifanya Mahojiano na Kituo cha habar cha WasafiFm na kudai kwamba Marioo aliwahi kumfuata na kuomba kisainiwa kwenye lebo ya WCB kitu ambacho Diamond alikataa kutokana na ukubwa alionao kwa sasa. Marioo Amekanusha stori hiyo kwa kumjibu shabiki ambaye alitaka kujua kama kuna ukweli wowote

Read More