Mulamwah Ashangazwa na Uamuzi wa Ruth K Kubadili Jina la Mtoto Bila Ridhaa Yake

Mulamwah Ashangazwa na Uamuzi wa Ruth K Kubadili Jina la Mtoto Bila Ridhaa Yake

Mchekeshaji maarufu kutoka Kenya, Mulamwah, amefichua kuwa aliyekuwa mpenzi wake na mama wa mtoto wao, Ruth K, amefanya uamuzi wa siri wa kumbadilishia mtoto wao jina la ukoo kutoka jina la baba Oyando hadi jina lake mwenyewe Wanjiku. Kupitia ujumbe aliouchapisha mtandaoni, Mulamwah alieleza masikitiko yake kwa hatua hiyo, akisema kuwa hakuwahi kuhusishwa wala kupewa taarifa kuhusu mabadiliko hayo muhimu katika maisha ya mtoto wake. “Sikuarifiwa chochote. Kumtoa jina langu na kuweka lake bila hata kuniambia, siyo sawa,” alisema Mulamwah kwa masikitiko. Mulamwah, ambaye jina lake kamili ni David Oyando, alisema kuwa kitendo hicho kimemvunja moyo kama mzazi na kinaibua maswali kuhusu haki za baba katika malezi na maamuzi ya maisha ya mtoto. Aliongeza kuwa licha ya tofauti zao na Ruth K, bado anahisi anapaswa kushirikishwa katika maamuzi muhimu yanayomhusu mtoto wao. Wafuasi na mashabiki wake kwenye mitandao ya kijamii wametoa maoni tofauti, wengine wakimpa pole na kumtaka atafute suluhu ya kibinafsi au kisheria, huku wengine wakisema huenda hatua hiyo ni ya kawaida kwa mzazi anayeishi na mtoto peke yake. Kwa upande wa Ruth K, bado hajatoa majibu rasmi kuhusu madai hayo hadi wakati huu wa kuchapishwa kwa taarifa hii. Tukio hili linaibua mjadala mpana kuhusu haki za wazazi, ushirikiano baada ya kuvunjika kwa uhusiano, na athari za uamuzi wa upande mmoja kwenye maisha ya watoto.

Read More
 Malcom Afichua Siri ya Sakata la Mulamwah na Ruth K

Malcom Afichua Siri ya Sakata la Mulamwah na Ruth K

Mwanamtandao maarufu kwa jina la Malcom amezua mjadala mkali mtandaoni baada ya kudai kuwa mchekeshaji Mulamwah na mama ya mtoto wake Ruth K wanalipwa makusudi ili kuwahadaa Wakenya na kuwapotosha kutoka kwenye masuala muhimu yanayoathiri nchi kwa sasa. Kupitia ujumbe aliouandika kwenye mitandao ya kijamii, Malcom alidai kuwa sakata ya mapenzi kati ya Mulamwah na Ruth K, ambayo imekuwa gumzo mtandaoni kwa wiki kadhaa sasa, si ya kweli bali ni maigizo yaliyopangwa ili kuvuruga akili za raia.  “Ni kama kuna watu wanawalipa hawa wasanii kufanya hizi drama ili Wakenya wasifikirie kuhusu shida zao. Mnatupumbaza na mapenzi ya watu wawili ilhali nchi inateketea,” alisema Malcom. Kauli hiyo imezua maoni tofauti kutoka kwa wafuasi wake na watumiaji wengine wa mitandao ya kijamii. Baadhi waliunga mkono madai hayo wakisema kuna ushahidi wa wazi kwamba wasanii wengi wanatumiwa kama chombo cha kupunguza makali ya ukosoaji dhidi ya serikali, huku wengine wakimtaka Malcom awasilishe ushahidi wa madai hayo badala ya kueneza tuhuma zisizo na msingi. Mzozo kati ya Mulamwah na Ruth K umeendelea kutawala vichwa vya habari, huku wawili hao wakitupiana lawama hadharani kuhusu sababu za kuachana kwao. Hata hivyo, kauli ya Malcom imeongeza mtazamo mpya kuhusu kinachoendelea nyuma ya pazia. Wakati huo huo, baadhi ya wadadisi wa masuala ya kijamii wameshauri umma kuwa makini na kile wanachokiona mitandaoni, wakisema kuwa kuna uwezekano mkubwa wa propaganda na mchezo wa kiakili unaoendeshwa kwa makusudi ili kuelekeza umakini wa wananchi mbali na masuala kama vile ongezeko la gharama ya maisha, maandamano ya wanafunzi, na migogoro katika sekta ya afya na elimu. Hadi kufikia sasa, Mulamwah wala Ruth K hawajajibu hadharani madai hayo mapya kutoka kwa Malcom.

Read More
 Mulamwah Apata Ajali ya Barabarani, Atoa Shukrani kwa Kunusurika Bila Majeraha

Mulamwah Apata Ajali ya Barabarani, Atoa Shukrani kwa Kunusurika Bila Majeraha

Mchekeshaji maarufu nchini Kenya, Mulamwah, amenusurika ajali ya barabarani na amethibitisha kuwa yuko salama kupitia ujumbe aliouweka kwenye mitandao ya kijamii. Katika chapisho hilo, Mulamwah alieleza kwamba tukio hilo lilitokea kwa haraka sana, lakini anamshukuru Mungu kwa kuwa hakuna mtu aliyejeruhiwa. “Happened so fast. We are grateful to God that no one was injured,” aliandika Mulamwah kupitia InstaStory yake, sambamba na picha ya gari lililoharibika sehemu ya mbele. Ajali hiyo ilitokea Ijumaa tarehe 20 Juni 2025, wakati mchekeshaji huyo akiwa safarini kwenye shughuli zake za kawaida. Ingawa hakufichua eneo halisi lililotokea ajali hiyo, picha zilizosambazwa mitandaoni zilionyesha gari lake likiwa na uharibifu mdogo upande wa mbele, hali inayodokeza kuwa lilihusika katika mgongano. Mashabiki wake mitandaoni walijitokeza kwa wingi kumpa pole na kumtakia afueni, huku wengi wakimtaka awe mwangalifu zaidi barabarani. Wengine walitumia fursa hiyo kuwakumbusha madereva kuhusu umuhimu wa tahadhari barabarani, hasa kipindi hiki ambacho mvua zinashuhudiwa katika maeneo mbalimbali ya nchi. Mulamwah hakusita kumshukuru Mungu kwa kuendelea kumlinda, akieleza kuwa ingawa tukio hilo lilikuwa la kutisha, anakichukulia kama onyo la kutambua thamani ya maisha na kuwa makini zaidi.  “Ni neema ya Mungu. Tunapaswa kuwa na shukrani kila siku tunayopata nafasi nyingine ya kuamka,” alisema katika mazungumzo mafupi na mashabiki wake. Tukio hili linakuja wakati ambapo Mulamwah amekuwa akigonga vichwa vya habari kutokana na malumbano ya mitandaoni na aliyekuwa mpenzi wake, Ruth K. Hata hivyo, ajali hiyo imeleta mwelekeo mpya na kumbukumbu ya jinsi maisha yalivyo mafupi na ya thamani.

Read More
 Mulamwah na Ruth K Waomba Radhi kwa Mashabiki Kufuatia Mzozo wa Mtandaoni

Mulamwah na Ruth K Waomba Radhi kwa Mashabiki Kufuatia Mzozo wa Mtandaoni

Baada ya wiki ya taharuki na mivutano ya hadharani iliyopelekea kurushiana lawama mitandaoni, mchekeshaji Mulamwah na aliyekuwa mpenzi wake Ruth K wameamua kufunga ukurasa wa mgogoro huo kwa kuomba msamaha kwa mashabiki wao, kila mmoja akielezea majuto yake kwa yaliyojiri. Kupitia ujumbe mrefu aliouchapisha kwenye mitandao ya kijamii, Mulamwah alielezea kwa kina maumivu na majuto aliyobeba kufuatia kile alichokieleza kama msururu wa maamuzi yasiyo ya busara aliyoyafanya akiwa chini ya hisia kali. Alisema kuwa amefanya tafakari ya kina na ametambua kuwa matendo yake yalikuwa ya kuumiza na ya kutozingatia hisia za wengine. “Poleni sana kwa mashabiki wangu wote. Najua nimewaangusha kwa njia nyingi. Nilikuwa nimesukumwa na hisia na hali mbalimbali, lakini hiyo haifai kuwa sababu ya mimi kufanya baadhi ya mambo niliyofanya. Nimejifunza, nimejirekebisha, na nipo tayari kuanza upya,” alisema Mulamwah katika ujumbe wake wa maombi ya msamaha. Mulamwah alihitimisha kwa kueleza kuwa ni wakati wa kutuliza hali, kusonga mbele na kuweka nguvu katika kazi na malezi, huku akimwomba Mungu kuwaongoza katika maamuzi ya baadaye. Kwa upande wake, Ruth K naye hakusita kuonesha unyenyekevu wake kwa mashabiki na familia yake. Katika chapisho lake, aliomba msamaha kwa wale wote waliokwazwa na matendo au kauli zake, na akaahidi kuanza ukurasa mpya wa maisha. “Ninachukua jukumu kamili kwa sehemu yangu ya makosa. Nilikuwa nikipitia wakati mgumu kihisia na kwa kweli mambo mengi yalinitesa. Si kila nilichofanya kilikuwa sahihi, lakini naomba mnisamehe. Nitakuwa bora – kwa ajili yangu, kwa ajili ya mtoto wangu, na kwa ajili yenu,” alisema. Aliongeza kuwa kama mama wa mtoto mmoja, anapitia changamoto nyingi huku akijitahidi kudumisha utu na utulivu. Ruth aliomba msamaha kwa wote walioumizwa au kuvunjwa moyo na matendo yake, na kueleza kuwa huu ni mwanzo mpya wa maisha yenye maadili na nidhamu. Kuomba radhi kwao kumepokelewa kwa hisia mseto na wafuasi wao, wengi wakikiri kuwa ni hatua muhimu ya ukomavu na uwajibikaji. Wengi wana matumaini kuwa huu ni mwanzo wa ukurasa mpya katika maisha yao binafsi na ya kitaaluma.

Read More
 Bahati Aingilia Kati Drama ya Mulamwah na Ruth, Atoa Wito wa Amani

Bahati Aingilia Kati Drama ya Mulamwah na Ruth, Atoa Wito wa Amani

Msanii maarufu wa muziki nchini Kenya, Bahati, ametoa wito wa amani na msamaha kwa wasanii wenzake Mulamwah na Ruth K, akiwataka kuweka tofauti zao binafsi mbali na mitandao ya kijamii kwa ajili ya mustakabali wa mtoto wao. Kupitia ujumbe wa kugusa moyo aliouandika kwenye ukurasa wake wa Instagram, Bahati alisema kuwa hajazoea kuingilia mambo ya watu binafsi, lakini hali inayoshuhudiwa kati ya Mulamwah na Ruth imemsikitisha sana kama mzazi na mwanajamii. “Siwezi kuingilia sana mambo ya watu binafsi, lakini sipendezwi kuona familia zikivunjika . Naomba umma tuwaombee vijana hawa wawili, na zaidi ya yote, Mungu arejeshe kile walichopoteza wakati wa sakata hili, aponye mioyo yao na amkinge mtoto asiye na hatia,” aliandika Bahati. Bahati, ambaye pia ni mzazi na mume wa Diana Marua, alisema kuwa ameshindwa kuwapata Mulamwah na Ruth kwa simu, na hivyo kuamua kuwafikia kwa njia ya umma ili kuwataka waepuke kulifanya suala hilo kuwa la hadhara. “Ombi langu kwa wazazi wenzangu Mulamwah na Ruth (kwa sababu siwezi kuwafikia kwa simu)… tafadhali acheni kuanika haya mitandaoni… ni jambo la kusikitisha lakini naamini litakuwa sawa kwa jina la Yesu .” aliongeza. Alihitimisha ujumbe wake kwa maandiko ya Biblia kutoka Yakobo 1:20, akisisitiza umuhimu wa kudhibiti hasira wakati wa migogoro ya kifamilia: “Hasira ya mwanadamu haizai haki ya Mungu,” aliandika Bahati Kauli ya Bahati imepokelewa kwa hisia kali na wafuasi wake, wengi wakimpongeza kwa kuonesha uelewa na huruma, huku wengine wakitumaini kwamba ujumbe huo utakuwa mwanzo wa mazungumzo ya suluhu kati ya wawili hao. Hali ya sintofahamu kati ya Mulamwah na Ruth K imekuwa gumzo mitandaoni hapo jana, huku kila mmoja akitoa maelezo yake kuhusu sababu za kutengana kwao, hali ambayo imewaacha mashabiki wakiwa na maoni tofauti.

Read More
 Ruth K Atoa Maneno Mazito Dhidi ya Mulamwah kwa Kutoheshimu Faragha Yake

Ruth K Atoa Maneno Mazito Dhidi ya Mulamwah kwa Kutoheshimu Faragha Yake

Mama wa mtoto wa mchekeshaji maarufu Mulamwah, anayefahamika kwa jina la Ruth K, amezua gumzo mitandaoni baada ya kumtolea uvivu mzazi mwenzake, kufuatia hatua ya msanii huyo kuchapisha picha yake kwenye mitandao ya kijamii bila idhini. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Ruth K aliandika ujumbe wa hisia akieleza jinsi alivyojeruhiwa kihisia tangu kuvunjika kwa mahusiano yao takribani miezi mitatu iliyopita. Anasema kuwa ukimya wake umechukuliwa kimakosa kuwa ni udhaifu, na sasa ameamua kusimama kidete kudai heshima yake. “Mara nyingine kimya huchukuliwa kuwa udhaifu. Haijapita hata miezi mitatu tangu tuachane, lakini tayari nimepitia fedheha na ukosefu wa heshima hadharani – na zaidi kwa faragha,” aliandika Ruth K. Katika ujumbe huo, Ruth alieleza kuwa anapitia wakati mgumu wa kupona kihisia lakini hali hiyo imekuwa ya kuchosha kutokana na matendo ya dharau kutoka kwa Mulamwah. Alifichua kuwa Mulamwah alimtumia pesa kiasi cha shilingi 5,000 kisha akazirudisha haraka, jambo ambalo alilitaja kuwa ni la dharau. Lakini kilichomuudhi zaidi ni kitendo cha Mulamwah kupakia picha aliyoweka juhudi kubwa kuipiga na kuitayarisha, bila ridhaa yake. “Unatuma elfu tano halafu unairejesha, kisha unathubutu kuscreenshot picha niliyoitolea jasho? Kiburi ni kikubwa mno,” alisema kwa msisitizo. Kwa hasira na uchungu, Ruth K alihitimisha ujumbe wake kwa kusema ameamua kuchukua heshima yake tena, akiahidi kuwa ipo siku atasimulia hadithi yake yote kwa umma. “Siku moja nitaeleza simulizi langu,” aliandika kwa hisia. Hali hii imezua mjadala mkubwa mitandaoni huku wafuasi wa wawili hao wakigawanyika, wengine wakimuunga mkono Ruth kwa ujasiri wake wa kujieleza, huku wengine wakimtaka aepuke kusambaza mambo ya kifamilia kwenye mitandao ya kijamii. Hadi kufikia sasa, Mulamwah bado hajatoa kauli rasmi kuhusiana na tuhuma hizo mpya dhidi yake.

Read More
 Dufla Amvamia Mulamwah Kwa Maneno Makali Mtandaoni

Dufla Amvamia Mulamwah Kwa Maneno Makali Mtandaoni

Msanii wa muziki wa dancehall nchini Kenya, Dufla Diligon, amemkemea hadharani mchekeshaji maarufu Mulamwah, akimtuhumu kwa vitisho na usumbufu wa simu. Kupitia ujumbe mkali aliouweka katika ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, Dufla alieleza hasira zake na kuonyesha kutoridhishwa na tabia ya Mulamwah. “Mulamwah stop threatening me!! Mimi mahali nimezaliwa wewe hata hauwezi survive. Hizi vitisho punguza… ama unaona mimi sina sauti, I mean I don’t have bass?!! On a serious note, stop calling me na kunitishia, mimi ni warrior, am not a coward!!!!” Dufla aliandika Instagram. Ujumbe huo umeibua gumzo mitandaoni, huku mashabiki wa muziki na wafuasi wa burudani wakitaka kufahamu chanzo cha mvutano huo. Wengi wameunga mkono msimamo wa Dufla, wakisema kuwa watu maarufu wanapaswa kutumia ushawishi wao kwa njia ya kujenga, si ya kuharibu.  Siku chache kabla ya taarifa hiyo, Dufla alikuwa amedai kwamba Mulamwah alimblock kwenye Instagram bila sababu ya msingi. Katika ujumbe huo, Dufla alimshauri Mulamwah kuacha kuwa na “feelings” kupita kiasi na kuzingatia mambo ya maana. Mvutano kati ya wawili hao ulianza miaka michache iliyopita, kufuatia madai kuwa Dufla alikuwa anamnyemelea baby mama wa Mulamwah, Carol Sonnie, jambo ambalo lilizua taharuki kubwa kwenye mitandao ya kijamii wakati huo. Ingawa hakuna uthibitisho wa moja kwa moja kuhusu uhusiano kati ya Dufla na Sonnie, hali hiyo ilisababisha sintofahamu kubwa kati yao.

Read More
 Dufla Diligon Amlalamikia Mulamwah kwa Kumblock Instagram

Dufla Diligon Amlalamikia Mulamwah kwa Kumblock Instagram

Msanii wa muziki wa Kenya, Dufla Diligon, amezua mjadala mtandaoni baada ya kufichua kuwa amefungiwa (blocked) na mchekeshaji maarufu Mulamwah kwenye mtandao wa Instagram. Kupitia Instastory yake, Dufla alisimulia tukio hilo kwa mshangao na utani, akisema kuwa aligundua amefungiwa wakati alipokuwa akitafuta akaunti ya Mulamwah akiwa katika mazungumzo na msanii Lyanii.  “Jana tulikuwa na mazungumzo na @officialiyanii, halafu nikaamua kutafuta akaunti ya Mulamwah kwenye IG. Nilishangaa kuona nimefungiwa. Kumbe mimi na Obinna tuko kwa listi moja!” aliandika Dufla. Katika ujumbe wake, Dufla hakusita kuonyesha mshangao wake na hata kumtaka Mulamwah “kupunguza hisia”, akionekana kutofahamu chanzo cha hatua hiyo ya mchekeshaji huyo.  “Punguza feelings buda!!!” aliongeza, kwa mtindo wa utani lakini uliobeba ujumbe mzito. Hadi sasa, Mulamwah hajatoa majibu yoyote hadharani kuhusu hatua hiyo, wala kueleza sababu ya kuwazima Dufla na Obinna kwenye ukurasa wake wa Instagram. Hata hivyo, mashabiki wa pande zote wameendelea kutoa maoni tofauti, wengine wakisisitiza haja ya kuwepo kwa mawasiliano ya moja kwa moja kati ya wahusika badala ya kupeana block mitandaoni.

Read More
 Mulamwah Atumia Akiba ya Harusi Kununua Gari la Kifahari Aina ya Mercedes S-550

Mulamwah Atumia Akiba ya Harusi Kununua Gari la Kifahari Aina ya Mercedes S-550

Mchekeshaji maarufu wa Kenya, Mulamwah, ameibua gumzo mitandaoni baada ya kufichua kuwa alitumia akiba aliyokuwa ameweka kwa ajili ya harusi na mpenzi wake wa zamani, Ruth K, kununua gari la kifahari aina ya Mercedes Benz S-550 kama zawadi ya kuzaliwa kwake. Kupitia mitandao ya kijamii, Mulamwah alisema aliamua kujipa zawadi hiyo ya kifahari baada ya uhusiano wao kuvunjika. Badala ya kuendelea kuhifadhi pesa hizo kwa ajili ya tukio lisilotekelezeka tena, aliona ni busara kujiwekea kumbukumbu ya mafanikio yake binafsi. “Pesa za harusi zilienda kwa Mercedes. Life must go on. At least now nacheka kwa comfort,” alisema kwa utani huku akionesha gari hilo jipya. Mercedes Benz S-550 ni gari la hadhi ya juu linalojulikana kwa ubora, kasi, na starehe – ishara kuwa Mulamwah ameamua kuweka thamani katika faraja yake binafsi baada ya kuachana na Ruth K. Taarifa hiyo imepokelewa kwa hisia mseto na mashabiki wake, wakipongeza uamuzi wa kujipa thamani binafsi, huku wengine. huku wengine wakikosoa matumizi ya fedha kwa njia hiyo, wakisema huenda pesa hizo zingetumika katika uwekezaji wa muda mrefu. Mulamwah, ambaye amejizolea umaarufu kwa ucheshi na maudhui yake mtandaoni, anaendelea kuwa mmoja wa wanahabari wa burudani wanaofuatiliwa sana nchini, huku maisha yake ya kibinafsi yakizidi kuvutia macho ya mashabiki.

Read More
 Mulamwah adokeza ujio wa mpya wa msanii wake Val Wambo

Mulamwah adokeza ujio wa mpya wa msanii wake Val Wambo

Mchekeshaji Kendrick Mulamwah ametangaza  ujio mpya wa msanii wake val wambo ambaye yupo chini ya lebo yake ya muziki ya Mulamwah Ent. Kwenye mahojiano na podcast ya VIncent Mboya, Mulamwah amesema msanii wake huyo kwa sasa yupo chimbo anaanda ep yake mpya, hivyo mashabiki zake watarajie muziki mzuri kutoka kwake. Mulamwah aidha amebainisha kuwa hana mpango wa kumsajili msanii mwingine kwenye lebo yake kutokana na changamoto ya kifedha. Ikumbukwe mapema mwaka huu val wambo alitambulishwa chini uongozi wa mulamwah ent na amefanikiwa kuachia nyimbo tatu ambazo ni Umenilemea na Serereka akiwa ammshirikisha Ruth K.

Read More
 MULAMWAH ATISHIA KUMSHTAKI BABY MAMA WAKE CAROL SONNIE

MULAMWAH ATISHIA KUMSHTAKI BABY MAMA WAKE CAROL SONNIE

Mchekeshaji Mulamwah ametishia kumchukulia hatua kali za kisheria Baby Mama wake Carol Sonnie kwa hatua ya kumtumia vibaya mtoto wao mtandaoni. Kwenye mahojiano yake hivi karibuni Mulamwah ametoa ya moyo kwa kusema kuwa amechukizwa na kitendo cha Baby mama wake huyo kumtumia mtoto wao kama kitega uchumi, jambo ambalo amedai kuwa si cha kingwana kwani amekiuka haki ya faragha ya mtoto wao. Mchekeshi huyo ameenda mbali zaidi na kwa kudai kwamba kinachomuuma zaidi ni hatua ya mrembo huyo kumzushia madai ya uongo kwenye vyombo vya habari kuwa kuna kipindi alimshushia kichapo cha mbwa akiwa mja mzito, madai ambayo Mulamwah ameyakanusha vikali. Mapema wiki hii Mulamwah na Baby Mama Carol Sonnie walitupiana maneno makali mtandaoni kwenye kumbukizi ya kuzaliwa kwa mtoto wao baada ya mchekeshaji huyo kudai kuwa mzazi mwenzie amekuwa akimpa wakati mgumu kwenye suala la kutoa matunzo kwa binti yake.

Read More
 CAROL SONIE AKANUSHA VIKALI KURUDIANA NA MULAMWAH

CAROL SONIE AKANUSHA VIKALI KURUDIANA NA MULAMWAH

Mpenzi wa zamani wa mchekeshaji Mulamwah, Carol Sonie amekanusha taarifa za kurudiana na mchekeshaji huyo. Hii ni baada ya Mulamwah kuposti video jana kupitia ukurasa wa Instagram na kuandika ujumbe ulioashiria kuwa wamerudiana jambo lilowaaminisha walimwengu wawili hao wamezika tofauti zao. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Sonie amesema madai ya mulamwah hayana msingi wowote huku akisisitiza kuwa hawajasuluhisha mgogoro uliopo kati yao kama inavyoripotiwa mitandaoni. Mrembo huyo amesema Mulamwah alitokea ghafla na kuivamia shughuli zake za kupiga picha na ndipo akataka wazungumzie nae jambo analodai lilipelekea kitu k mapaparazi kuchukua video akiwa na mchekeshaji huyo. Hata hivyo amewataka watumiaji wa mitandao ya kijamii kupumzilia mbali taarifa za kurudiana ambapo mbali zaidi na kumtaka mulamwah aombe familia, mashabiki pamoja binti yao msamaha kwa kumzushia madai ya uongo. Utakumbuka katika kipindi cha wiki moja iliyopita Mulamwah alikamata headlines za habari mtandaoni baada ya kujitokeza na kudai kwamba aliachana baby wake Carol Sonie mwaka wa 2021 baada ya mrembo huyo kumsaliti kimapenzi kwa kuzaa na mwanaume mwingine ambapo alienda mbali zaidi na kudai kuwa Keilah Oyando sio mtoto wake.

Read More