Mwijaku Aumizwa na Kitendo cha Ndoa Yake Kuvunjika
Mtangazaji na mdau wa burudani kutoka Tanzania, Mwijaku, amefunguka kwa uchungu baada ya mke wake kukataa kurudiana naye licha ya kuomba msamaha. Kupitia ukurasa wake wa Instastory, Mwijaku ameeleza kuwa kinachomuumiza zaidi ni mazoea ya muda mrefu, kwani wameishi pamoja kwa zaidi ya miaka 15 na sasa ndoto yao ya kifamilia inavunjika kwa kosa moja. Ameonyesha maumivu makubwa kutokana na hali hiyo, akisisitiza kuwa ni vigumu kukubali kuvunjika kwa ndoa hiyo kwa kuwa wameishi pamoja kwa miaka mingi. Taarifa zinaeleza kuwa mke wa Mwijaku alikataa miito ya kurudiana, akisema hana tena hisia za kimapenzi kwake. Inadaiwa kuwa chanzo cha mgogoro huo ni madai ya usaliti, ambapo Mwijaku alihusishwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamke mwingine, kitendo kilichomkasirisha mke wake na kuamua kuvunja ndoa yao.
Read More