Mwijaku: Diamond Aliiba Nyota ya Kassim Mganga Usiku wa Valentine

Mwijaku: Diamond Aliiba Nyota ya Kassim Mganga Usiku wa Valentine

Mdau wa burudani Mwijaku amezua mjadala mkali mitandaoni baada ya kudai kuwa msanii wa Bongofleva Kassim Mganga ameisha kimuziki kufuatia tukio la Diamond Platnumz kubusu viatu vyake akiwa jukwaani usiku wa Valentine’s. Akizungumza kupitia majukwaa ya kijamii, Mwijaku amedai kuwa tukio hilo halikuwa la kawaida, akisema Diamond alitumia fursa hiyo kuiba nyota ya mafanikio ya msanii huyo. Katika hatua nyingine, Mwijaku amemtaja Jay Melody akisema aliwahi kuibiwa nyota kwa njia kama hiyo, jambo ambalo amedai mpaka sasa imeathiri muziki wa mkali huyo wa ngoma ya Sugar. Mwanamitandao huyo hakuishia hapo, ameenda mbali zaidi na kufichua kuwa kitendo cha Jay Melody kuonekana kususia kumpa mkono Diamond jukwaani katika hafla ya Garravallentines ilikuwa ni ishara ya kujingika kiimani.

Read More
 Mwijaku Amtolea Uvivu Chief Godlove Kuhusu Magari ya Kifahari Bila Parking

Mwijaku Amtolea Uvivu Chief Godlove Kuhusu Magari ya Kifahari Bila Parking

Mtangazaji na mdau wa burudani, Mwijaku, amezua gumzo mitandaoni baada ya kumtolea uvivu Chief Godlove, akigusia suala la umiliki wa magari ya kifahari bila kuwa na maegesho binafsi. Kupitia clip aliyoposti akiwa nyumbani kwake, Mwijaku ameonyesha magari yake yakiwa yameegeshwa kwenye parking ya nyumba yake, akisema haiwezekani mtu kudai kumiliki magari ya kifahari ilhali hana parking yake mwenyewe kwa sababu anaishi nyumba za kupanga. Kwa mujibu wa Mwijaku, umiliki wa magari ya thamani kubwa unapaswa kwenda sambamba na makazi yenye maegesho salama, akisisitiza kuwa hilo ni suala la mipango ya maisha na si kujionyesha tu. Kauli hiyo imekuja baada ya Chief Godlove juzi kati kuonekana kwenye clip nyingine akionesha mashabiki wake gari lake lililovunjwa kioo. Katika clip hiyo, Godlove alionekana ameegesha gari lake kwenye parking iliyojaa magari mengi, hali iliyozua maswali na mjadala mkubwa mitandaoni.

Read More
 Mwijaku Arudiana na Mke Wake Baada ya Mgogoro wa Ndoa

Mwijaku Arudiana na Mke Wake Baada ya Mgogoro wa Ndoa

Mtangazaji na mdau wa burudani, Mwijaku, ameripotiwa kurudiana na mke wake miezi kadhaa baada ya ndoa yao kugubikwa na mgogoro mkubwa uliovuma sana mitandaoni na kwenye vyombo vya habari. Mwijaku amethibitisha hilo kwa kuposti video kwenye mitandao ya kijamii akiwa pamoja na mkewe wakikagua ujenzi unaoendelea wa jumba lao la kifahari (mansion) Katika video hiyo, Mwijaku amesikika akimbembeleza mke wake kwa maneno ya upole huku mwanamama huyo akionekana akideka kwa madaha, hatua iliyoashiria wazi kuwa wameamua kuyaweka nyuma yaliyopita na kuendelea na maisha ya ndoa yao. Taarifa za kutengana kwa wawili hao ziligonga vichwa vya habari mwishoni mwa mwaka jana, ikidaiwa kuwa mke wa Mwijaku alimkimbia kutokana na madai ya tabia ya Mwijaku ya kutembea kimapenzi na wanawake wengine, jambo lililozua mjadala mkubwa mitandaoni.

Read More
 Mwijaku Adai Chief God Love Amembebesha Ujauzito Msanii Wake Pipi Jojo

Mwijaku Adai Chief God Love Amembebesha Ujauzito Msanii Wake Pipi Jojo

Mdau wa burudani asiyeishiwa na matukio kila leo, Mwijaku, amezua gumzo mtandaoni baada ya kudai kuwa Bilionea Chief God Love amembebesha ujauzito msanii wake, Pipi Jojo. Kwa mujibu wa Mwijaku, Pipi Jojo aliwahi kupata ujauzito wa awali ambao aliupoteza kupitia tukio la kuharibika kwa mimba (miscarriage). Hata hivyo, anadai kwa sasa msanii huyo ana ujauzito mwingine, na anasisitiza kuwa mimba hiyo ni ya Chief Godlove. Mwijaku amesema hali hiyo ndiyo sababu kubwa inayomfanya Pipi Jojo asionekane sana mitandaoni na kwenye shughuli za kawaida za kazi siku za hivi karibuni. Mwijaku ameenda mbali zaidi kwa kumtolea changamoto Chief Godlove, akimtaka ajitokeze hadharani na kumposti Pipi Jojo kama uthibitisho iwapo madai hayo ni ya uongo. Mwijaku ameonyesha kujiamini na kusisitiza kuwa anachokizungumza anakifahamu vizuri

Read More
 Mwijaku Aapa Kumkingia Kifua Mkubwa Fella Licha ya Kumdharau

Mwijaku Aapa Kumkingia Kifua Mkubwa Fella Licha ya Kumdharau

Mtangazaji na mdau wa burudani, Mwijaku, amefunguka kwa uchungu namna meneja wa wasanii Mkubwa Fella aliwahi kumdharau kipindi cha nyuma kiasi cha kutomsalimia. Akizungumza kwa hisia kali, Mwijaku amesema Mkubwa Fella hakutaka kumuona karibu yake na mara nyingi alikuwa akipuuza salamu zake kama mtu asiyefaa katika jamii. Mwijaku amesema licha ya kudharauliwa, ataendelea kumkingia kifua serikalini ili apate msaada wa matibabu. Anasema alipopata taarifa ya kuumwa kwake hakusita kutumia nafasi na ushawishi wake kuwasilisha ajenda hiyo kwa mamlaka husika, akiamini kuwa utu na ubinadamu vinapaswa kuwa mbele kuliko chuki za zamani. Mwijaku amedai kuwa jambo linalomuuma zaidi ni kuona baadhi ya watu waliokuwa karibu sana na Mkubwa Fella, wakitajwa kumtoroka kipindi hiki kigumu anapitia matatizo ya kiafya.

Read More
 Mwijaku Akanusha Madai ya Kukosa Makazi kwa Kutamba na Mali zake

Mwijaku Akanusha Madai ya Kukosa Makazi kwa Kutamba na Mali zake

Mtangazaji na mdau wa burudani, Mwijaku, amejigamba waziwazi kuhusu mali anazodai kumiliki, huku akimshambulia vikali msanii mkongwe Dudu Baya kwa madai ya kukosa makazi na maisha ya uhakika. Akizungumza kupitia moja ya mitandao ya kijamii, Mwijaku ametamba kuwa ana nyumba yake binafsi, magari pamoja na runinga kubwa ya inchi 100 huku akisisitiza kuwa mafanikio hayo yametokana na juhudi na kazi yake binafsi. Mwijaku hakusita kumrushia Dudu Baya maneno mazito, amedai kuwa msanii huyo anaishi kwenye baa na hana maisha aliyoyapanga. Ameongeza kuwa Dudu Baya amekuwa akiombaomba watu wamchangie na kumkopesha kodi ya nyumba. Kwa mujibu wa Mwijaku, mafanikio hayo yanamtofautisha pakubwa na Dudu Baya ambaye amedai hana maisha.

Read More
 Mwijaku Akubali Kuzichapa na Dudu Baya

Mwijaku Akubali Kuzichapa na Dudu Baya

Mtangazaji na mdau wa burudani, Mwijaku ameonekana kuumizwa na tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake na msanii mkongwe Dudu Baya ambapo amekiri hadharani yuko tayari kuzichapa naye ana kwa ana iwapo itaendelea kuvuka mipaka ya kumvunjia heshima. Akizungumza kwa hasira, Mwijaku amesema amechoshwa na kile alichokitaja kuwa ni tuhuma za uongo na za kumdhalilisha, akidai Dudu Baya hana uwezo wa kumshinda kwa hali yoyote iwe kifedha, kiuchawi wala kiunguvu. Mwijaku amekanusha vikali madai yaliyotolewa na Dudu Baya kuwa hana makazi na kwamba aliwahi kuwa shoga wakati wa masomo yake chuoni, akisisitiza kuwa taarifa hizo hazina msingi wowote na zinalenga kumharibia jina. Hata hivyo, Mwijaku ameonya kuwa hatamvumilia tena Dudu Baya endapo ataendelea kumvunjia heshima kwa kumzushia taarifa za uongo, akisema yuko tayari kuchukua hatua kali ili kulinda jina na heshima yake mbele ya umma.

Read More
 Mwijaku Amsuta Vikali Dudu Baya Kwa Kumvunjia Heshima Mkubwa Fella

Mwijaku Amsuta Vikali Dudu Baya Kwa Kumvunjia Heshima Mkubwa Fella

Mtangazaji na mdau wa burudani, Mwijaku, amemsuta vikali msanii mkongwe wa Bongo Fleva Dudu Baya kufuatia kauli yake tata kuhusu Mkubwa Fella, ambapo Dudu Baya alinukuliwa akisema kuwa ikitokea Mkubwa Fella amefariki, hawezi kwenda kumzika. Akizungumza kuhusu sakata hilo, Mwijaku ameeleza kusikitishwa kwake na kauli hiyo, akimtaka Dudu Baya kuwa na heshima na utu bila kujali tofauti au migogoro iliyowahi kutokea kati yao. Mwijaku amesisitiza kuwa hakuna mwanadamu aliye mkamilifu chini ya jua, hivyo ni vyema watu kujifunza kusamehe na kuacha chuki hasa pale masuala ya afya na uhai yanapohusika. Kauli ya Mwijaku imekuja muda mfupi baada ya Dudu Baya kudai kuwa kwa sasa hakuna msanii anayeweza kumsaidia Mkubwa Fella katika kipindi hiki ambacho anaumwa, akieleza kuwa aliwanyonya na kuwapoteza wasanii wengi kwenye tasnia ya muziki wa Bongofleva..

Read More
 Mwijaku Asikitishwa na Wasanii Kumkataa Mkubwa Fella Akiwa Mgonjwa

Mwijaku Asikitishwa na Wasanii Kumkataa Mkubwa Fella Akiwa Mgonjwa

Mtangazaji na mdau wa burudani, Mwijaku, ameonyesha kusikitishwa na kitendo cha baadhi ya wasanii kumkataa kumsaidia meneja wa wasanii wa Bongofleva, Mkubwa Fela, wakati huu anapitia kipindi kigumu cha kuumwa. Akizungumza kwa uchungu, Mwijaku amesema ameumia kumuona mtu aliyejitolea kwa muda mrefu kuwasaidia wasanii, anatengwa wakati huu anapitia matatizo ya kiafya. Ameongeza kuwa ameshangazwa na kitendo cha baadhi ya wasanii wakubwa kumkataa kumsaidia Mkubwa Fella licha ya kuwa na utajiri mkubwa. Kwa mujibu wake, tukio hilo linapaswa kuwa funzo kwa jamii, akisisitiza kuwa si kila mtu anafaa kusaidiwa katika maisha. Ameeleza kuwa kuna watu ambao hubadilika mara wanapopata nafuu katika maisha. Katika hatua nyingine, Mwijaku ametoa wito kwa mkongwe wa muziki wa Bongofleva Mwana FA kuingilia kati na kusaidia gharama za matibabu ya Mkubwa Fela, akisema mchango wa meneja huyo katika kulea vipaji na kukuza tasnia ya muziki hawezi kupuuzwa.

Read More
 Mwijaku Amlaumu Diamond kwa Kuvunja Ndoa Yake

Mwijaku Amlaumu Diamond kwa Kuvunja Ndoa Yake

Mtangazaji na mdau wa burudani, Mwijaku, amemlaumu staa wa Bongo Fleva Diamond Platnumz kwa kudai kuwa ndiye chanzo cha kuvunjika kwa ndoa yake. Akizungumza kupitia mitandao ya kijamii, Mwijaku amesema kuwa tangu aanze kuwa karibu na Diamond, maisha yake ya ndoa yalianza kuyumba na hatimaye kusambaratika. Amedai kuwa ukaribu wake na Diamond ulimuingiza kwenye mtindo wa maisha uliosababisha migogoro ya mara kwa mara ndani ya ndoa yake. Kwa mujibu wa Mwijaku, mazingira na mienendo inayomzunguka Diamond si rafiki kwa watu wenye ndoa au mahusiano ya kudumu, akidai kuwa kuna ushawishi unaovuruga misingi ya familia kwa wale wanaokuwa karibu naye. Hata hivyo Mwijaku, amempa onyo msanii Jux, akimtaka ajitengenezee mipaka na kujitenga na Diamond mapema kabla mambo hayajaharibika katika ndoa yake. Amesisitiza kuwa ushauri huo unatokana na uzoefu wake binafsi na alichokipitia.

Read More
 Mwijaku Asema Kajala Hana Maisha Bila Harmonize

Mwijaku Asema Kajala Hana Maisha Bila Harmonize

Mtangazaji na mdau wa burudani mwenye utata, Mwijaku, amedai kuwa Kajala Masanja hana maisha wala mwelekeo wa kibiashara bila uwepo wa msanii wa Bongo Fleva, Harmonize. Kwa mujibu wa Mwijaku, kipindi ambacho Kajala alikuwa nje ya mahusiano na Harmonize, maisha yake yalidorora kwa kiwango kikubwa, akidai kuwa alifilisika kiuchumi na kukosa kabisa dili za kibiashara. Anasema hakukuwa na brand wala kampuni zilizokuwa tayari kufanya kazi naye hadi pale aliporudiana na Harmonize. Mwijaku ameongeza kuwa licha ya Kajala kutoka kimapenzi na wanaume wengi , hakuna mafanikio ya maana aliyoyapata kutokana na mahusiano hayo. Kwa mujibu wake, kile pekee ambacho Kajala anaweza kujivunia ni kusafiri nje ya nchi na kula bata kwenye mahoteli ya kifahari, mambo ambayo, kwa mtazamo wake, hayajengi msingi wa maisha yenye tija wala heshima ya kibiashara.

Read More
 Mwijaku Amkosoa Baba Levo kwa Kuwalisha Wananchi Chakula cha Bure Mwaka Mpya

Mwijaku Amkosoa Baba Levo kwa Kuwalisha Wananchi Chakula cha Bure Mwaka Mpya

Mtangazaji na mdau waa burudani, Mwijaku, amemkosoa Mbunge wa Kigoma Mjini, Babalevo, kufuatia kitendo chake cha kuwalisha wananchi chakula cha bure siku ya Mwaka Mpya, akidai hatua hiyo haina mchango wa kudumu katika kubadilisha maisha ya watu wa Kigoma. Akizungumza kwenye mahojiano na Rick Media, Mwijaku amesema Baba Levo amepata nafasi kubwa ya kuaminika na wananchi wa Kigoma, jambo linalompa wajibu wa kufanya maamuzi na miradi itakayobadilisha maisha yao kwa muda mrefu badala ya kutatua tatizo la siku moja. Kwa mujibu wa Mwijaku, kutoa chakula cha bure ni jambo jema kwa wakati husika, lakini halitatui changamoto kubwa zinazowakabili vijana na wakazi wa Kigoma, hususan ukosefu wa ajira na fursa za maendeleo. Amesisitiza kuwa wananchi wanahitaji suluhisho endelevu litakalowawezesha kujitegemea. Mwijaku ameongeza kuwa fedha zilizotumika kuwalisha wananchi zingeweza kuelekezwa katika miradi ya maendeleo, akitolea mfano kufunguliwa kwa Hub ya Vijana wa Kigoma ambayo ingewezesha vijana kubadilishana mawazo, kupata mafunzo, kushirikiana kwenye biashara na kufunguliwa kwa fursa mbalimbali za kiuchumi.

Read More