Mwijaku Aumizwa na Kitendo cha Ndoa Yake Kuvunjika

Mwijaku Aumizwa na Kitendo cha Ndoa Yake Kuvunjika

Mtangazaji na mdau wa burudani kutoka Tanzania, Mwijaku, amefunguka kwa uchungu baada ya mke wake kukataa kurudiana naye licha ya kuomba msamaha. Kupitia ukurasa wake wa Instastory, Mwijaku ameeleza kuwa kinachomuumiza zaidi ni mazoea ya muda mrefu, kwani wameishi pamoja kwa zaidi ya miaka 15 na sasa ndoto yao ya kifamilia inavunjika kwa kosa moja. Ameonyesha maumivu makubwa kutokana na hali hiyo, akisisitiza kuwa ni vigumu kukubali kuvunjika kwa ndoa hiyo kwa kuwa wameishi pamoja kwa miaka mingi. Taarifa zinaeleza kuwa mke wa Mwijaku alikataa miito ya kurudiana, akisema hana tena hisia za kimapenzi kwake. Inadaiwa kuwa chanzo cha mgogoro huo ni madai ya usaliti, ambapo Mwijaku alihusishwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamke mwingine, kitendo kilichomkasirisha mke wake na kuamua kuvunja ndoa yao.

Read More
 Mwijaku Aonya Wanaodhoofisha Brand ya Harmonize

Mwijaku Aonya Wanaodhoofisha Brand ya Harmonize

Mwanahabari na mchanganuzi wa masuala ya burudani, Mwijaku, ameibuka rasmi kumtetea msanii Harmonize katika sakata linaloendelea kati ya Konde Boy na Baba Levo, huku akisema kuwa kauli za Harmonize zinapaswa kuheshimika kama sheria ndani ya tasnia ya muziki. Kupitia ujumbe wake mzito, Mwijaku amesema kuwa anamfahamu vyema Harmonize, na kwamba kwa msanii huyo kufikia hatua ya kusema yale yaliyo Moyoni, basi kuna jambo kubwa limefika mwisho. Ametaka watu waachane na shobo zinazodhoofisha brand ya msanii huyo na badala yake waheshimu misimamo yake. Ameeleza kuwa kuna wasanii ambao hawawezi kupelekwa pelekwa na mitazamo ya watu wengine kama vibaraka wa mwambino wanaomramba miguu, akimaanisha wale wanaojipendekeza kwa baadhi ya vigogo wa muziki ili kupata nafasi au kutengeneza kiki. Mwijaku amesema wazi kuwa kauli za Harmonize hazipaswi kupuuzwa, akizilinganisha na katiba ya nchi au kanuni za chama kikuu cha upinzani, akizipa jina la utani Konde Statment Sharia, ishara ya uzito anaouona katika msimamo wa msanii huyo.

Read More
 Mwijaku Akanusha Taarifa za Kuachana na Mke Wake

Mwijaku Akanusha Taarifa za Kuachana na Mke Wake

Mwanamitandao maarufu nchini Tanzania, Mwijaku, amekanusha taarifa zilizosambaa mitandaoni zikidai kuwa ameachana na mke wake. Akizungumza na moja ya vyombo vya habari nchini humo, amesisitiza kwamba bado wako pamoja licha ya mke wake kuondoka nyumbani kwa muda. Mwijaku ambaye anafahamika kama DC wa Instagram, amefafanua kuwa hatua ya mke wake kutohonekana nyumbani haimaanishi kuvunjika kwa ndoa yao, kwani anafahamu aliko na wanawasiliana. Ameeleza kuwa taarifa zilizoenezwa mtandaoni zimetiwa chumvi, akibainisha kuwa hakuna mgogoro wa mali kati yao kama inavyodaiwa. Kwa mujibu wa Mwijaku, kila mali waliyonayo ina jina la muhusika, na mali pekee wanayomiliki kwa pamoja ni kiwanja. Kauli ya Mwijaku imekuja kufuatia mjadala ulioibuka kwenye mitandao ya kijamii kuhusu mustakabali wa ndoa yake, na amesisitiza kuwa wanashughulikia mambo yao kwa utulivu pasipo ushawishi wa taarifa za mitandaoni.

Read More
 DC wa Instagram Mwijaku Afunguka Kuhusu Hali Ya Kumuenzi MC Polepole

DC wa Instagram Mwijaku Afunguka Kuhusu Hali Ya Kumuenzi MC Polepole

Mtangazaji maarufu nchini Tanzania, Mwijaku, ametuma ujumbe mzito kwa vijana na watumiaji wa mitandao ya kijamii akiwataka kumuenzi marehemu MC Polepole kwa kumuombea dua badala ya kupakia picha zake mtandaoni. Kupitia mitandao yake ya kijamii, Mwijaku amesema kuwa imekuwa kawaida kwa watu wengi kushindana kupost picha za marehemu kwenye mitandao, huku wakisahau kuwa namna bora zaidi ya kuwaenzi wapendwa ni kwa maombi na matendo mema. Mwijaku ambaye anafahamika kama DC wa Instagram, ameeleza kuwa kama kulikuwa na haja ya kushirikiana au kumwonyesha upendo MC Polepole mitandaoni, hiyo ilipaswa kufanyika wakati akiwa hai, na si baada ya kifo chake. Hata hivyo amehimiza vijana kutumia muda huu kumuombea marehemu ili Mungu aipokee roho yake na amweke mahali pema peponi, akibainisha kuwa hilo ndilo jambo la maana na lenye heshima zaidi kwa marehemu kuliko kusambaza picha zake mitandaoni.

Read More