Studio ya Nandor Love Yavamiwa na Majambazi Uganda
Msanii wa muziki kutoka Uganda, Nandor Love, anapitia wakati mgumu baada ya studio yake, Ghost Empire Records, kuvamiwa na majambazi na kuporwa vifaa vya thamani usiku wa kuamkia jana. Kwa mujibu wa Nandor Love, wahalifu hao waliiba vifaa kadhaa vya muziki na uzalishaji ambavyo ni muhimu kwa shughuli za kila siku za Ghost Empire Records. Mbali na wizi, studio hiyo pia iliharibiwa vibaya, ikiwa ni pamoja na kutolewa kwa wallpapers zenye nembo za Ghost Empire Records na kukatwa kwa vitambaa vya makochi, hatua inayoashiria uharibifu uliolenga kuleta maumivu ya kihisia pamoja na hasara ya kifedha. Licha ya hasara hiyo kubwa na uharibifu wa mali, Nandor Love amewahakikishia mashabiki wake kuwa timu yake ni thabiti, na wanaamini wataweza kujenga upya, kurejesha mali iliyopotea na kuendeleza kazi yao bila kukata tamaa. Tukio hilo lilitokea wakati Nandor Love na timu yake walipokuwa nje ya jiji la Kampala kwa ajili ya shoo ya muziki.
Read More