Oga Obinna Akataa Penzi la Shabiki wa Miaka 18
Msanii wa vichekesho na mwanahabari, Oga Obinna, amezua mjadala mitandaoni baada ya kukataa waziwazi ombi la kutoka kimapenzi na shabiki wake mwenye umri wa miaka 18. Kupitia picha za skrini shots zilizosambaa mtandaoni, Obinna anaonekana akiweka wazi msimamo wake kwa kuamwambia binti huyo kuwa bado ni mdogo sana na akamshauri aelekeze nguvu zake kwenye masomo na kujijenga kwa ajili ya maisha ya baadaye. Obinna pia ameongeza kuwa ana vigezo maalum linapokuja suala la mahusiano, akisema hupendelea kuchumbiana na kina mama wasio na wenza wenye umri wa miaka 24 na kuendelea kwa sababu ya uelewa na mtazamo wao wa maisha. Tukio hilo lilianza pale shabiki huyo alipohudhuria hafla moja akiwa amebeba bango lililoonyesha nia yake ya kutaka kuchumbiana na Obinna, huku akiweka wazi namba yake ya simu. Baadaye, alidaiwa kuendelea kuwasiliana naye kupitia ujumbe binafsi.
Read More