Oga Obinna Akataa Penzi la Shabiki wa Miaka 18

Oga Obinna Akataa Penzi la Shabiki wa Miaka 18

Msanii wa vichekesho na mwanahabari, Oga Obinna, amezua mjadala mitandaoni baada ya kukataa waziwazi ombi la kutoka kimapenzi na shabiki wake mwenye umri wa miaka 18. Kupitia picha za skrini shots zilizosambaa mtandaoni, Obinna anaonekana akiweka wazi msimamo wake kwa kuamwambia binti huyo kuwa bado ni mdogo sana na akamshauri aelekeze nguvu zake kwenye masomo na kujijenga kwa ajili ya maisha ya baadaye. Obinna pia ameongeza kuwa ana vigezo maalum linapokuja suala la mahusiano, akisema hupendelea kuchumbiana na kina mama wasio na wenza wenye umri wa miaka 24 na kuendelea kwa sababu ya uelewa na mtazamo wao wa maisha. Tukio hilo lilianza pale shabiki huyo alipohudhuria hafla moja akiwa amebeba bango lililoonyesha nia yake ya kutaka kuchumbiana na Obinna, huku akiweka wazi namba yake ya simu. Baadaye, alidaiwa kuendelea kuwasiliana naye kupitia ujumbe binafsi.

Read More
 Oga Obinna Amtetea Larry Madowo Baada ya Mpambe wa Rais Samia Kupinga Ripoti ya CNN  

Oga Obinna Amtetea Larry Madowo Baada ya Mpambe wa Rais Samia Kupinga Ripoti ya CNN  

Mchekeshaji na mtangazaji wa Kenya, Oga Obinna, ameibuka kumtetea kwa nguvu mwandishi wa habari wa CNN, Larry Madowo, kufuatia kauli ya mpambe wa Rais Samia Suluhu Hassan aliyepinga na kupuzilia mbali ripoti ya chombo hicho kuhusu machafuko ya uchaguzi nchini Tanzania. Akiwa hewani kupitia Obinna TV, Obinna ameonekana kukerwa na hatua ya mpambe huyo kuhoji uhalali wa taaluma ya Madowo. Amesisitiza kuwa Madowo ni mwandishi mwenye tajriba ya muda mrefu katika vyombo vikubwa vya habari duniani na hawezi kuripoti taarifa za uongo kama inavyodaiwa. Obinna ameongeza kuwa ni muhimu viongozi na wasaidizi wao kuheshimu kazi ya wanahabari, hasa wale wanaofanya kazi katika vyombo vya kimataifa, kwani wanahabari hao hufuata misingi ya uandishi wa kitaaluma na huchunguza kwa kina kabla ya kuripoti.

Read More
 Oga Obinna Atimiza Ahadi ya Kukutana na Binti Aliyemlilia Mtandaoni

Oga Obinna Atimiza Ahadi ya Kukutana na Binti Aliyemlilia Mtandaoni

Mtangazaji na mchekeshaji wa Kenya, Oga Obinna, hatimaye ameitikia wito wa mapenzi baada ya kutimiza ahadi yake ya kukutana na binti aliyemlia akimuomba penzi hadharani kupitia video iliyosambaa mitandaoni. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Obinna ameshiriki video ikimuonyesha akiwa kwenye chakula cha mchana na binti huyo, tukio ambalo limevutia hisia mseto kutoka kwa mashabiki wake. Katika video hiyo, binti huyo anaonekana akiwa mwenye wasiwasi na mshangao mkubwa, akiwa haamini macho yake baada ya kukutana na mtu ambaye aliwahi kusema ni ndoto yake maishani. Obinna ameeleza kuwa wakati wa kwanza walipokutana, binti huyo alionekana mnyenyekevu na mwenye hofu, lakini baadaye hali ilirejea kawaida na wakaanza mazungumzo ya kirafiki. Obinna amesema mtoko au date hiyo ilienda vizuri na walizungumza mambo mengi, ikiwemo namna atakavyoweza kumsaidia binti huyo ambaye alionyesha mapenzi ya dhati kwake kupitia video kwenye mtandao wa Tiktok. Kabla ya mtoko huo, binti huyo alifanyiwa make-up kuboresha muonekano wake, huku akipata mavazi mapya yanayoendana na tukio hilo la kipekee kwenye moja ya spa ya kifahari.

Read More
 Mrembo Aliyetakiwa Kumlipa Obinna Milioni 6 Asema Hana Uwezo wa Kifedha

Mrembo Aliyetakiwa Kumlipa Obinna Milioni 6 Asema Hana Uwezo wa Kifedha

Mrembo aliyekuwa ameamriwa na mahakama kumlipa mchekeshaji wa Kenya Oga Obinna fidia ya shilingi milioni 6 kwa kumdhalalisha, ameibuka akisema hana uwezo wa kulipa kiasi hicho kikubwa cha pesa. Kupitia video inayosambaa mtandaoni, mrembo huyo alionekana akilia kwa uchungu, akieleza kuwa kwa sasa anapitia changamoto kubwa za kiuchumi na hana njia yoyote ya kupata fedha hizo. Kesi hiyo ilitokana na madai kwamba mrembo huyo alitoa maneno ya kumdhalilisha Obinna kwenye mitandao ya kijamii, jambo lililomfanya mchekeshaji huyo kuchukua hatua za kisheria kulinda heshima yake. Kwa sasa, mashabiki wa Obinna na watumiaji wa mitandao wametofautiana mitazamo, baadhi wakimtaka Obinna kumsamehe huku wengine wakisema sheria ichukue mkondo wake.

Read More
 Mahakama Yampa Ushindi Oga Obinna Dhidi ya Radio Jambo

Mahakama Yampa Ushindi Oga Obinna Dhidi ya Radio Jambo

Mchekeshaji na mtangazaji kutoka nchini Kenya, Oga Obinna, ameibuka mshindi katika kesi ya kashfa ya mtandaoni dhidi ya watangazaji wenzake Massawe Japani, Black Cinderella, na kituo cha redio Radio Jambo. Kwa mujibu wa uamuzi wa mahakama uliotolewa jana, Obinna amezawadiwa shilingi milioni sita kama fidia kutokana na maneno ya kumdhalilisha yaliyotolewa kupitia kipindi cha redio mwaka mmoja uliopita. Kupitia ujumbe wake kwa mashabiki, Obinna ameeleza kuwa sasa amepata fidia ambayo anapanga kuitumia kuanzisha ujenzi wa nyumba yake, akisema ushindi huo unamvutia zaidi kwa sababu umetokana na juhudi za kulinda heshima yake. Mchekeshaji huyo, amefafanua kuwa madai yaliyotolewa dhidi yake yalikuwa ya uongo na hayakuwa na ushahidi wowote, jambo lililoathiri taswira yake kitaaluma na kibiashara. Obinna hata hivyo amewataka watumiaji wa mitandao ya kijamii kuwa waangalifu na wanachochapisha mtandaoni, akisisitiza kuwa ni muhimu kuheshimu watu na kuepuka kusambaza taarifa zisizo na msingi kwani hatua za kisheria zinaweza kuchukuliwa.

Read More
 Binti Aliyemlilia Oga Obinna Mtandaoni Apata Mwaaliko wa Chakula

Binti Aliyemlilia Oga Obinna Mtandaoni Apata Mwaaliko wa Chakula

Mtangazaji na mchekeshaji maarufu Oga Obinna ameahidi kumpeleka lunch date binti aliyesambaa mitandaoni baada ya kuonekana akimwaga machozi akieleza wazi mapenzi yake kwake kupitia video iliyosambazwa mitandaoni. Binti huyo alionekana akieleza jinsi anavyompenda Obinna kwa moyo wake wote na kumwomba ampe nafasi ya kuwa naye, jambo lililozua maoni mseto mitandaoni. Obinna kupitia ukurasa wake wa Instagram amejibu ujumbe huo akisema ameguswa na ujasiri wa binti huyo na kwamba atampatia nafasi ya kukutana naye ana kwa ana kwa ajili ya chakula cha jioni. Ameongeza kuwa anathamini mashabiki wake wote, na kwamba hatua hiyo ni njia ya kuonyesha shukrani kwa upendo na uungwaji mkono anaopokea kila siku. Baadhi ya mashabiki wamepongeza hatua hiyo wakisema ni ishara ya utu na unyenyekevu wa Obinna, huku wengine wakidai huenda tukio hilo ni sehemu ya kiki ya mtandaoni.

Read More
 Oga Obinna Atokwa na Machozi kwenye Mazishi ya Kimani Mbugua

Oga Obinna Atokwa na Machozi kwenye Mazishi ya Kimani Mbugua

Mtangazaji Oga Obinna amejipata akitokwa na machozi ya uchungu wakati wa mazishi ya mwanahabari Kimani Mbugua, tukio lililofanyika katika eneo la Maragua, Kaunti ya Murang’a. Katika hotuba yake, Obinna ameelezea maumivu makubwa aliyoyahisi kutokana na kumpoteza rafiki katika tasnia ya habari, akisema wanahabari na wasanii wengi wanapitia changamoto kubwa za kimaisha na kisaikolojia ambazo mara nyingi hawawezi kuzungumzia hadharani. Ameeleza kuwa tasnia ya habari na burudani imejaa mashindano, presha na upweke unaowafanya wengi kukosa msaada wa kihisia. Amehimiza mastaa kusaidiana na kuinua kila mmoja badala ya kuendeleza mashindano na chuki zisizo na maana. Obinna pia amewakumbusha mashabiki kwamba maisha halisi ni tofauti kabisa na yanayoonekana kwenye mitandao ya kijamii, akibainisha kuwa mitandao hiyo mara nyingi huficha maumivu na mapambano ambayo watu hupitia kimya kimya. Mazishi ya Kimani Mbugua, aliyewahi kuwa mtangazaji mwenye kipaji kikubwa, yalihudhuriwa na watu wengi kutoka sekta ya habari na burudani nchini. Wengi walimkumbuka kama kijana mwenye ndoto kubwa, ubunifu na moyo wa kujituma.

Read More
 Oga Obinna Aonyesha Heshima kwa Hayati Raila kwa Kunyoa Kipara 

Oga Obinna Aonyesha Heshima kwa Hayati Raila kwa Kunyoa Kipara 

Mtangazaji na mchekeshaji Oga Obinna ameonyesha heshima zake za mwisho kwa hayati Raila Odinga kwa kunyoa kipara kamili, kama ishara ya maombolezo na heshima kulingana na tamaduni za jamii ya Wajaluo. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Obinna ameposti picha akionyesha kichwa chake kilichonyolewa kabisa, akifafanua kuwa kitendo hicho kilikuwa njia yake ya kumuenzi kiongozi huyo aliyegusa maisha ya wengi nchini Kenya. Kwa mujibu wa mila za Kijaluo, kunyoa kipara ni ishara ya huzuni, heshima, na mshikamano na familia ya aliyeaga dunia wakati wa msiba. Kitendo hicho kimezua maoni mengi mtandaoni, wengi wakimsifu Obinna kwa kuenzi utamaduni wa Kiafrika na kuonyesha mshikamano na Wakenya wanaoendelea kuomboleza.

Read More
 Oga Obinna Atoa Ushauri kwa Wasanii Kufuatia Uharibifu wa Duka la Willy Paul

Oga Obinna Atoa Ushauri kwa Wasanii Kufuatia Uharibifu wa Duka la Willy Paul

Mtangazaji na mchekeshaji maarufu Oga Obinna ameonya wasanii wa Kenya kuhusu kuendesha biashara zao kwa tahadhari, kufuatia tukio ambapo genge la watu wasiojulikana liliharibu duka la pombe linalomilikiwa na msanii Willy Paul. Kupitia mitandao ya kijamii, Obinna amesisitiza kwamba wasanii wanapaswa kuwa wanyenyekevu na waangalifu wanapoingia katika biashara nje ya muziki ili kuepuka chuki na mashambulizi ya ghafla. Ameongeza kuwa mafanikio ya msanii yanapaswa kwenda sambamba na busara katika kushughulika na umma, akieleza kuwa dunia ya biashara ni tofauti kabisa na ile ya burudani, hivyo inahitaji umakini na nidhamu zaidi. Obinna ametoa kauli hiyo mara baada ya Willy Paul kutangaza kuwa amelikarabati upya duka lake la Pozze Liquor store lilovamiwa na wahuni na kababisha hasara ya mamilioni ya fedha.

Read More
 Oga Obinna Ajitetea Baada ya Madai ya Kumtumia Dem wa Facebook

Oga Obinna Ajitetea Baada ya Madai ya Kumtumia Dem wa Facebook

Mchekeshaji na mtangazaji maarufu wa Kenya, Oga Obinna, amejibu madai yanayosambaa mitandaoni kuhusu kumfuta kazi ghafla mrembo anayejulikana kama “Dem wa Facebook.” Akizungumza kuhusu suala hilo, Obinna amesisitiza kuwa hakuwahi kumwajiri binti huyo kwa mkataba rasmi wala kufanya makubaliano ya ajira. Ameeleza kuwa ushirikiano wao ulikuwa ni wa kusaidiana kikazi na kwamba lengo lake lilikuwa kumuinua kimaisha na kumpa nafasi ya kukuza kipaji chake. Obinna amesema kuwa hakuwahi kumtumia vibaya binti huyo na kila kipato kilichotokana na kazi walizofanya kwa pamoja kiligawanywa kwa haki. Ameongeza kuwa sehemu kubwa ya mapato hayo alikuwa akimpa kwa uwazi bila kuficha chochote. Kauli yake imekuja mara baada ya madai kuibuka kwamba alivunja mkataba wa makubaliano na kumfuta ghafla Dem wa Facebook bila maelezo yoyote, jambo lililozua mjadala mkubwa kwenye mitandao ya kijamii.

Read More
 Oga Obinna Aumizwa na Tuhuma za Kifo cha Shalkido

Oga Obinna Aumizwa na Tuhuma za Kifo cha Shalkido

Mtangazaji na mchekeshaji maarufu wa Kenya, Oga Obinna, amejikuta kwenye wakati mgumu baada ya baadhi ya wafuasi mitandaoni kumhusisha kwa maneno na kifo cha msanii wa kundi la Sailors, Shalkido. Tuhuma hizo zimeibuka baada ya taarifa za kifo cha Shalkido kusambaa mitandaoni, huku baadhi ya watumiaji wa mitandao wakimtaja Obinna kama mtu aliyekuwa akizungumza mara kwa mara kuhusu changamoto za msanii huyo kabla ya kifo chake. Kupitia machapisho yake kwenye mitandao ya kijamii, Obinna ameonekana mwenye huzuni na kuchoshwa na maneno ya mitandaoni, akieleza kuwa watu wengi hawathamini nia njema. Ameongeza kuwa amejifunza somo kubwa na hatasaidia tena watu wanaopitia changamoto, kwani mara nyingi msaada wake huzua lawama badala ya shukrani. Kwa muda mrefu, Obinna amekuwa akitambulika kwa kusaidia watu wanaopitia matatizo mbalimbali kupitia majukwaa yake ya mitandao ya kijamii. Hata hivyo, sakata hili linaonekana kumgusa kwa undani na huenda likabadilisha mtazamo wake kuhusu kujitolea hadharani.

Read More
 Oga Obinna Amuinua Shalikido Kwa Msaada wa Kifedha na Ajira Mpya

Oga Obinna Amuinua Shalikido Kwa Msaada wa Kifedha na Ajira Mpya

Mtangazaji maarufu na mchekeshaji Oga Obinna, amejiunga na orodha ya mastaa ambao wameamua kumsaidia msanii wa muziki wa Gengetone, Shalikido, ambaye hivi karibuni aliomba umma imsaidie kutokana na maisha kumuendea vibaya. Katika hatua ya kuonyesha upendo na mshikamano kwa wasanii wachanga, Oga Obinna ameamua kumpa Shalikido kazi ya mwaka mmoja kama mshawishi wa mitandaoni (influencer), akimwahidi nafasi ya kukuza kipato chake kupitia majukwaa ya kidijitali. Obinna pia ametoa zawadi za vifaa vya nyumbani kwa Shalikido ikiwemo sofa, godoro na zulia, hatua iliyochukuliwa kama ishara ya kumuwezesha kuanza maisha mapya kwa ustawi na heshima. Zaidi ya hayo, kupitia kipindi chake cha moja kwa moja (live show) kwenye YouTube, Oga Obinna alifanikiwa kuchangisha kiasi cha KSh 62,000 kwa ajili ya kumsaidia msanii huyo kijana. Michango hiyo ilitoka kwa wafuasi wake walioguswa na hali ya Shalikido na waliotaka kuona maisha yake yakibadilika. Hatua hii ya Oga Obinna imepongezwa na wengi kama mfano bora wa usaidizi wa kijamii na kuinua vipaji vya vijana, hasa wale wanaokumbwa na changamoto za kiuchumi. Hatua hii ya Obinna inakuja siku chache tu baada ya mchekeshaji mwingine maarufu, Eric Omondi, kumsaidia Shalikido kwa kumpatia pikipiki mpya na mahitaji mengine muhimu ya nyumbani. Msaada huo ulitolewa baada ya Shalikido kufunguka hadharani kuhusu hali ngumu ya maisha aliyokuwa akipitia, hali iliyomlazimu kushindwa hata kumudu mahitaji ya msingi ya familia yake.

Read More