Otile Brown Aachia Rasmi EP Yake Mpya,

Otile Brown Aachia Rasmi EP Yake Mpya,

Msanii wa RnB kutoka Kenya, Otile Brown, amethibitisha rasmi kuachiwa kwa EP yake mpya, akisema kazi hiyo inapatikana sasa kwenye majukwaa yote makuu ya muziki mtandaoni. EP hii, inayokwenda kwa jina “The Real King of the East”, ina ngoma tano zenye mwelekeo wa kisasa wa RnB, zikiwemo kolabo tatu za uzito na wasanii kama The Ben, Jovial, na Okello Max. Kila wimbo umebeba hadithi tofauti, ikiwakilisha mapenzi, kumbukumbu, na hisia za maisha. Otile amewashukuru mashabiki wake kwa kusubiri kwa hamu mradi huu, akisema kuwa kila wimbo umeandaliwa kwa uangalifu ili kutoa muziki wa hali ya juu unaoendana na jina lake kama “The Real King of the East.” EP hii inapatikana sasa kwa kusikilizwa na kupakuliwa kwenye majukwaa yote makuu ya muziki mtandaoni, ikiwemo Spotify, Apple Music, Boomplay, na YouTube Music.

Read More
 Otile Brown Aachia Tracklist ya EP yake Mpya

Otile Brown Aachia Tracklist ya EP yake Mpya

Msanii mahiri wa RnB kutoka Kenya, Otile Brown, ametangaza rasmi orodha ya nyimbo za EP yake mpya inayokwenda kwa jina “The Real King of the East”. EP hii ina jumla ya ngoma tano kali na imebeba kolabo tatu za uzito zinazomshirikisha Jovial, The Ben, na Okello Max. Katika mradi huo, Otile amemshirikisha The Ben katika wimbo “For Life”, akamleta Jovial kwenye ngoma “I Choose You”, na kisha Okello Max katika wimbo “I Love You”. Aidha, EP inajumuisha pia wimbo “Miss the Water” pamoja na “Lala Salama Baba”, ambao ni wimbo wa kumkumbuka na kumuenzi Raila Odinga. EP ya “The Real King of the East” inatarajiwa kuingia sokoni Novemba 21, 2025, na tayari mashabiki wanaonyesha msisimko mkubwa wakisubiri kusikia mwelekeo mpya wa Otile Brown kupitia kazi hii mpya.

Read More
 Otile Brown Atangaza Ujio wa EP Mpya

Otile Brown Atangaza Ujio wa EP Mpya

Msanii nyota wa R&B kutoka Kenya, Otile Brown, ametangaza ujio wa EP yake mpya ambayo amesema itathibitisha hadhi yake kama mfalme halisi wa muziki Afrika Mashariki. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Otile ameshiriki picha ya cover ya EP hiyo aliyoipa jina “The Real King of East Africa”, akieleza kuwa amekuwa akiitayarisha kwa muda mrefu kwa moyo wake wote na sasa muda umefika wa kuiachia rasmi. Kwa mujibu wa msanii huyo, tarehe 21 Novemba 2025 ni siku ya kihistoria kwa mashabiki wa muziki wa Afrika Mashariki, kwani anaenda kuthibitisha kwa vitendo madai yake ya kuwa “The Real King of East Africa.” kwa kuachia EP yake hiyo. Ingawa hajaweka wazi orodha ya nyimbo au majina ya wasanii watakaoshirikiana naye kwenye kazi hiyo, mashabiki wake tayari wameonyesha hamasa kubwa mtandaoni, wengi wakisubiri kwa hamu kazi hiyo mpya ambayo inatarajiwa kuwa na ubora wa juu kama ilivyo desturi ya Otile.

Read More
 Otile Brown Atangaza Wimbo wa Kumbukumbu kwa Baba Raila Odinga

Otile Brown Atangaza Wimbo wa Kumbukumbu kwa Baba Raila Odinga

Staa wa muziki wa Bongo RnB, Otile Brown, ametangaza ujio wa wimbo mpya wa kumbukumbu kwa Baba Raila Odinga, siku chache tu baada ya kiongozi huyo kuzikwa. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Otile amesema kuwa mwezi Novemba atatoa wimbo ulio karibu sana na moyo wake, akisema ni wimbo wa heshima na kumbukumbu kwa Raila na kwa wote waliopoteza wapendwa wao. Msanii huyo amesisitiza kuwa baadhi ya matukio ni zenye nguvu kiasi kwamba haziwezi kunyamaziwa, na kwamba muziki wake utakuwa njia ya kuenzi maisha na urithi wa Baba. Mashabiki wengi wamepongeza hatua ya Otile Brown wakisema ni njia ya heshima na kumbukumbu kwa kiongozi ambaye amegusa maisha ya Wakenya wengi.

Read More
 Otile Brown Aandaa Wimbo Maalum Kumheshimu Hayati Raila Odinga

Otile Brown Aandaa Wimbo Maalum Kumheshimu Hayati Raila Odinga

Mwanamuziki nyota wa Kenya, Otile Brown, ametangaza kuwa yuko mbioni kukamilisha wimbo maalum wa kumuenzi aliyekuwa Waziri Mkuu wa Kenya, hayati Raila Amolo Odinga. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Otile ameshiriki kipande cha video akiwa studioni akirekodi mradi huo wa kihisia, akieleza kuwa alihitaji muda wa kuhakikisha kazi hiyo inatoka kwa moyo wake kabisa. Msanii huyo amesema kuwa hayati Raila alikuwa mtu wa heshima kubwa na anastahili kutambuliwa kwa mchango wake mkubwa kwa taifa la Kenya. Otile ameahidi kutoa wimbo huo hivi karibuni kama njia ya kutoa heshima na upendo wake kwa kiongozi huyo aliyegusa maisha ya wengi. Taarifa hii inakuja siku ambayo Raila Odinga amepumzishwa kwenye nyumba yake ya milele huko Bondo, Kaunti ya Siaya, katika mazishi yaliyohudhuriwa na viongozi wa kitaifa, wageni wa kimataifa na maelfu ya waombolezaji waliokusanyika kumuenzi.

Read More
 Otile Brown Asema Kifo cha Raila Kumfundisha Utu

Otile Brown Asema Kifo cha Raila Kumfundisha Utu

Mwanamuziki nyota wa R&B kutoka Kenya, Otile Brown, ameonyesha kuguswa kwa kina na kifo cha aliyekuwa kiongozi wa upinzani nchini Kenya, Raila Amolo Odinga, akisema kimebadilisha mtazamo wake kuhusu maisha na maana halisi ya uongozi. Kupitia ujumbe wake kwenye mitandao ya kijamii, Otile Brown ameeleza kuwa kifo cha Raila kimemfanya kutafakari kuhusu maisha, akisema kimeonyesha wazi kwamba dunia ni kubwa kuliko mwanadamu na kwamba hatuna mamlaka ya kudumu ndani yake. Msanii huyo amesema tukio hilo limemnyenyekeza sana na kumfanya kutambua thamani ya kuwa na uongozi wenye misingi ya utu na upendo kwa watu. Ameongeza kuwa viongozi wanapaswa kujifunza kutokana na maisha ya Raila Odinga, ambaye licha ya changamoto alizokumbana nazo, aliendelea kujitolea kujenga jamii bora. Kwa mujibu wa Otile, kiongozi mzuri ni yule anayejenga jamii imara na anayeacha alama nzuri hata baada ya kuondoka. Amesisitiza kuwa pesa pekee haitoshi kujenga kizazi bora katika jamii iliyovurugika kimaadili, akieleza kuwa mali haina maana ikiwa mtu hana moyo wa kuridhika na kufanya mema. Hata hivyo, Otile Brown, amehitimisha ujumbe wake, akiwataka Wakenya kuendelea kupendana na kujenga taifa lao kwa umoja na moyo wa uzalendo, akisema ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha nchi inaendelea kuwa mahali bora kwa vizazi vijavyo.

Read More
 Otile Brown Awataka Mashabiki Kumsaidia Kumtafuta Mrembo

Otile Brown Awataka Mashabiki Kumsaidia Kumtafuta Mrembo

Penzi la mjaka mfine, mrembo aliyekutana na Otile Brown katika tamasha la Luo Festival limemkosesha usingizi staa huyo wa R&B. Msanii huyo amekiri waziwazi kwamba alitekwa na mvuto wa mrembo huyo, akidai macho yake na uwepo wake vilimchanganya. Otile Brown, ambaye mara nyingi huweka wazi hisia zake kupitia muziki, safari hii hakuweza kujizuia bali aliamua kutafuta msaada wa mashabiki wake. Kupitia ukurasa wake wa mtandaoni, aliposti picha yake na mrembo huyo wakiwa karibu, akionekana akimnong’oneza kwa upole kana kwamba macho yake yamefungwa na mvuto wa mrembo huyo. Staa huyo wa Dusuma hakuishia hapo, alienda mbali zaidi na kuwaomba mashabiki wake wamfikishie ujumbe mrembo huyo kwa kumtag, ishara kuwa hamtaki kumwachia apotee hivihivi. Mashabiki wake walichangamkia ombi hilo kwa utani na mzaha, huku wengine wakidai huenda Otile anaanza ukurasa mpya wa mapenzi. Kwa upande mwingine, wapo waliotaja tukio hilo kama kiki ya kuitangaza single yake mpya inayokwenda kwa jina la “Not For Me” Kwa sasa macho yote yameelekezwa kwa mjaka mfine huyo, huku mashabiki wakingoja kuona kama utamu wa tamasha la Luo Festival unaweza kugeuka kuwa simulizi jipya la mapenzi kwa Otile Brown.

Read More
 Otile Brown Aumizwa na Habari za Ndoa ya Nabayet, Aandika Ujumbe wa Hisia Kali

Otile Brown Aumizwa na Habari za Ndoa ya Nabayet, Aandika Ujumbe wa Hisia Kali

Mwanamuziki wa Bongo R&B kutoka Kenya, Otile Brown, ameibua hisia mtandaoni baada ya kuonyesha maumivu na mshangao kufuatia habari za aliyekuwa mpenzi wake, Nabayet kutoka Ethiopia, kufunga ndoa. Kupitia Insta Story yake, Otile alionekana kushindwa kuficha hisia zake, hasa kwa kuwa alimtaja Nabayet katika wimbo wake mpya unaotarajiwa kuachiwa. Ameandika:  “How does she go & get married after mentioning her on my new song dropping tomorrow… now I feel dueh…”,  Otile aliandika hisia nyingi Maneno hayo yameibua hisia mseto mitandaoni, huku mashabiki wake wakimfariji na wengine wakihisi kwamba bado ana hisia kwa mrembo huyo. Uhusiano wa Otile Brown na Nabayet ulikuwa wa muda mrefu na wa hadharani, uliovutia mashabiki wengi kutoka Afrika Mashariki na Ethiopia. Wawili hao walionekana kuwa na mahusiano yenye upendo mkubwa kabla ya kuachana kimya kimya miaka michache iliyopita. Kabla ya habari za ndoa ya Nabayet, Otile alikuwa ameonekana kuendelea na maisha, lakini ujumbe huu mpya unaonyesha pengine bado kuna hisia zilizobaki. Mashabiki sasa wanasubiri kwa hamu wimbo mpya wa Otile Brown ili kusikia alivyomzungumzia Nabayet, huku wengi wakijiuliza kama hii itaathiri maudhui au hisia za kazi hiyo.

Read More
 Nabayet, Mpenzi wa Zamani wa Otile Brown, Afunga Ndoa Kwenye Harusi ya Kifahari Ethiopia

Nabayet, Mpenzi wa Zamani wa Otile Brown, Afunga Ndoa Kwenye Harusi ya Kifahari Ethiopia

Mwanamitindo maarufu kutoka Ethiopia,Nabayet, ambaye aliwahi kuwa mpenzi wa msanii nyota wa Kenya Otile Brown, ameaga rasmi maisha ya u-single baada ya kufunga ndoa kwenye harusi ya kifahari iliyofanyika nchini mwake mwishoni mwa wiki. Harusi hiyo, iliyohudhuriwa na familia, marafiki wa karibu na watu mashuhuri kutoka sekta ya mitindo na burudani, ilifanyika katika hoteli ya kifahari jijini Addis Ababa. Nabayet alionekana mrembo kupindukia akiwa amevalia gauni jeupe la harusi lililobuniwa na mbunifu maarufu wa mitindo wa Ethiopia. Video na picha za tukio hilo zimeenea kwenye mitandao ya kijamii, huku mashabiki wakimpongeza kwa hatua hiyo mpya katika maisha yake. Ingawa hakufichua jina la mchumba wake, mashabiki walionekana kushangilia penzi jipya la mrembo huyo ambaye amekuwa akipunguza sana kuweka maisha yake ya kimapenzi hadharani. Nabayet aliingia kwenye uhusiano wa kimapenzi na Otile Brown mwaka 2019, na wawili hao walivutia mashabiki wengi kwa mahusiano yao ya kuvutia yaliyokuwa yakisambazwa kupitia mitandao ya kijamii. Hata hivyo, uhusiano huo uliisha baada ya muda kutokana na tofauti zao za kimtazamo. Otile Brown bado hajatoa kauli rasmi kuhusu harusi hiyo ya mpenzi wake wa zamani. Mashabiki wa Nabayet wameendelea kumpongeza kwa hatua hiyo kubwa, wakimtakia heri katika maisha mapya ya ndoa.

Read More
 Otile Brown atangaza ujio wake mpya 2023

Otile Brown atangaza ujio wake mpya 2023

Mwimbaji nyota wa kizazi kipya nchini Kenya, Otile Brown hataki kuwaacha mashabiki wake hivi hivi kabla mwezi huu haujaisha. Hii ni baada ya kutangaza ujio wa ngoma yake mpya ambayo kwa mujibu wake itaingia sokoni Jumanne wiki ijayo, Januari 31. Otile ameitaja ngoma hiyo aliyoipa jina la Shujaa wako kuwa ni kolabo yake ya Kimataifa akiwa na mwanamuziki kutoka nchini Tanzania, Ruby. Hii itakuwa ni Kazi yake ya kwanza kwa mwaka 2023 ikizingatiwa kuwa hajaachia wimbo wowote tangu mwaka jana alipowabariki mashabiki zake na wimbo uitwao Do It alioshirikisha Vivian.

Read More
 Rayvanny na Otile Brown waingia studio kurekodi kolabo yao

Rayvanny na Otile Brown waingia studio kurekodi kolabo yao

Wanamuziki nyota wanaoiwakilisha vyema Afrika Mashariki, wasanii Rayvanny na Otile Brown wameingia studio na wameonekana kwenye upishi wa kazi mpya. Wawili hao wanatajwa kuingia studio usiku wa kuamkia leo katika studio za Next Level Music zilizopo Mbezi Beach jijini Dar es salaam, zilizo chini ya msanii Rayvanny. Hata hivyo, bado haijafamika kuwa hii itakuwa ni kazi ya nani, tarajia kuipata kazi hiyo kutoka kwa wawili hao siku za usoni.

Read More
 Otile Brown arudishiwa laptop zake zilizoibiwa

Otile Brown arudishiwa laptop zake zilizoibiwa

Msanii kutoka nchini Kenya Otile Brown tayari amepata laptop zake mbili zilizoibiwa alipotua nchini Tanzania siku ya jana. Kupitia video aliyochapisha kwenye ukurasa wake wa Instagram Otile amethibitisha kupokea laptops hizo aina Mac Book ambayo alizipoteza katika uwanja wa ndege wa Julius Nyerere Meneja wa msanii huyo Reginald Noriega amefichua kwamba walifanya uchunguzi walifanikiwa kuzipata kompyuta hizo eneo la kinondoni viungani mwa Jijini Dar es Salaam. Kauli ya Otile Brown imekuja mara baada ya kutoa ahadi ya kuwalipa watakaomrejesha laptops hizo kutokana na stakabadhi zake muhimu ambazo zilikuwa ndani.

Read More