Otile Brown Aachia Rasmi EP Yake Mpya,
Msanii wa RnB kutoka Kenya, Otile Brown, amethibitisha rasmi kuachiwa kwa EP yake mpya, akisema kazi hiyo inapatikana sasa kwenye majukwaa yote makuu ya muziki mtandaoni. EP hii, inayokwenda kwa jina “The Real King of the East”, ina ngoma tano zenye mwelekeo wa kisasa wa RnB, zikiwemo kolabo tatu za uzito na wasanii kama The Ben, Jovial, na Okello Max. Kila wimbo umebeba hadithi tofauti, ikiwakilisha mapenzi, kumbukumbu, na hisia za maisha. Otile amewashukuru mashabiki wake kwa kusubiri kwa hamu mradi huu, akisema kuwa kila wimbo umeandaliwa kwa uangalifu ili kutoa muziki wa hali ya juu unaoendana na jina lake kama “The Real King of the East.” EP hii inapatikana sasa kwa kusikilizwa na kupakuliwa kwenye majukwaa yote makuu ya muziki mtandaoni, ikiwemo Spotify, Apple Music, Boomplay, na YouTube Music.
Read More