Otile Brown awaomba mashabiki kumrejeshea laptop zake zilizoibiwa Tanzania

Otile Brown awaomba mashabiki kumrejeshea laptop zake zilizoibiwa Tanzania

Staa wa muziki nchini Kenya Otile Brown ametoa rai kwa mashabiki zake wa Tanzania kumrejeshea kompyuta zake mbili za mkononi zilizopotea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere. Kupitia instagram live amesema yupo radhi kutoa kiasi chochote fedha kwa mtu yeyote atakayemrejeshea laptop hizo kwani zimemkosesha usingizi. Aidha ameahidi kuwa hana mpango wa kufungulia mashtaka mtu yeyote atakajitokeza kumrudishia kompyuta zake aina MacBook kutokana na uhitaji wa stakabadhi zake muhimu zilizomo ndani.

Read More
 Otile Brown aibiwa laptop mbili nchini Tanzania

Otile Brown aibiwa laptop mbili nchini Tanzania

Nyota wa muziki nchini, Otile Brown amedai kuibiwa laptop zake mbili aina ya MacBook akiwa kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam. Kupitia insta story yake Otile ambaye ametua nchini Tanzania asubuhi ya leo kwa ajili ya shughuli zake za kimuziki ameeleza kuwa walinzi pamoja na watoa huduma walikataa kumpa ushirikiano ikiwa ni pamoja na kuchunguza tukio zima kupitia kamera za CCTV zilizopo eneo hilo. “”So kwenye airport ya Julius Nyerere nimeibiwa Mac/laptop mbili ila walinzi na watoa huduma wamekataa kutusaidia ndani ya masaa 3 wamekataa kuchunguza kwenye cctv … longest night of my life.Tumetoa hadi report ya police ambayo ndio utaratibu lakini wakakataa… nimeumia sana,” Ameandika. Hata hivyo hakufichua thamani ya vifaa vyake vya kielektroniki ambavyo vimetoweka katika uwanja wa ndege.

Read More
 Otile Brown aachia rasmi Extended Playlist yake mpya

Otile Brown aachia rasmi Extended Playlist yake mpya

Mwanamuziki kutoka Kenya Otile brown ameachia rasmi Extended playlist yake mpya baada ya ukimya wa miezi mitatu EP hiyo iitwayo Terminator ina jumla ya nyimbo tano za moto akiwa amewashirikisha wakali kama Vivian, Ilogos na The Ben. Terminator EP ina nyimbo kama Kolo Kolo, Terminator, By My Side, Hatima, Do It na inapatikana Exclusive kwenye majukwaa yote ya kupakua na kusikiliza muziki mtandaoni. Hii ni EP ya pili kwa mtu mzima Otile Brown baada ya Uptown Flex iliyotoka mapema mwaka huu ikiwa na jumla ya singles 4 za moto.

Read More
 Otile Brown awajibu waliomjia juu kuhusu Kiswahili

Otile Brown awajibu waliomjia juu kuhusu Kiswahili

Mwanamuziki nyota nchini Otile Brown ameamua kuwajibu wanaoendelea kumponda mtandaoni baada ya kutoa maoni yake kuwa lugha ya Kiswahili inayotumika na wasanii wa Kenya ndio sababu kubwa inayowafanya wasifanye vizuri kimataifa kama wanavyofanya wasaniii wa Nigeria. Kupitia mfululizo wa instastory yake kwenye mtandao wa Instagram Otile amesema kuwa lugha ya Kiswahili ndio lugha ambayo imempa mafanikio makubwa kisanaa huku akiwataka wanaomkosoa kuelewa kwanza alichokisema kabla ya kuleta ubishi. Hitmaker huyo “I Need You” amesema hakuwa na nia ya kuishusha lugha ya Kiswahili ambayo imemtoa kimuziki ila alikuwa anajaribu kuanzisha mjadala utakaowasaidia wasanii wa Kenya kuchanganya lugha ya Kiingereza kwenye nyimbo ili waweze kupenya kimataifa. Hata hivyo amemalizia kwa kusisitiza kuwa ataendelea kuimba nyimbo zake kwa lugha ya Kiswahili huku akitoa changamoto kwa jumuiya ya Afrika Mashariki kuendeleza mjadala wa lugha kwenye nyimbo za wasanii kama njia moja ya kupata suluhu ya kizingiti inayokwamisha muziki wa ukanda huu kufika kimataifa.

Read More
 Otile Brown afunguka kuhusu kujipendekeza kwa mpenzi wake wa zamani Nabayet

Otile Brown afunguka kuhusu kujipendekeza kwa mpenzi wake wa zamani Nabayet

Staa wa muziki nchini Otile Brown amewajibu wanaodai kuwa anajipendekeza kwa mpenzi wake wa zamani Nabayet licha ya mahusiano yao kuvunjika. Otile ambaye amerejea nchini baada ya kukamilisha ziara ya miezi miwili nchini marekani amewashangaa wanaomsema vibaya kuwa bado anamzimia kimapenzi mrembo huyo kwa kusema kuwa hajutii kitendo cha kumtumia salamu za heri kwenye kumbukizi ya kuzaliwa kwake kwani ni moja kati ya watu ambao anawapenda sana. Otile Brown na Nabayet walikuwa kwenye mahusiano kwa kipindi cha miaka miwili lakini mahusiano yalikuja kuvunjika mwaka wa 2020 kutokana na umbali kati yao. Utakumbuka mwaka wa 2019 Otile Brown aliachia wimbo wa kusifia urembo wa Nabayet baada ya penzi lao kunoga.

Read More
 Kiswahili inawakwamisha wasanii wa Kenya kutusua kimataifa – Asema Otile Brown

Kiswahili inawakwamisha wasanii wa Kenya kutusua kimataifa – Asema Otile Brown

Msanii nyota nchini Otile Brown amefunguka kuwa miongoni mwa vitu vinavyowakwamisha wasanii wa Kenya kufanya vizuri kimataifa ni lugha. Katika mkao na waandishi wa habari Otile amedai kuwa endapo wasanii wa Kenya wangekuwa wanaimba kwa lugha ya kingereza basi wangekua na uwanja mkubwa wa kusikika kimataifa zaidi na kupata shows tofauti tofauti za nje ya nchi. Hitmaker huyo wa “Run Up” ameenda mbali zaidi na kusema kuwa tofauti ya muziki wa Kenya na Nigeria ni lugha pekee na ndio sababu kubwa ambayo hawawezi kushindana na wasanii kutoka taifa hilo la Afrika Magharibi. Hata hivyo ametoa changamoto kwa wasanii nchini kuanza kutumia lugha ya kiingereza kwenye nyimbo zao ili muziki wa Kenya uweze kufika mbali zaidi. Utakumbuka Otile Brown amekuwa nchini Marekani kwa miezi miwili ambako amekuwa akifanya shows kwenye miji mbali mbali nchini humo.

Read More
 Meneja wa Otile Brown awapa mapromota utaratibu mpya wa kumpata msanii wake

Meneja wa Otile Brown awapa mapromota utaratibu mpya wa kumpata msanii wake

Meneja wa Otile Brown, Noriega amewapa utaratibu mpya mapromota wa kimataifa watakaompatia msanii wake shows. Kupitia instastory Noriega amewataka wahakikishe kuwa wanamtumia Otile Brown na timu yake ndege binafsi. Aidha amesema nyakati za Otile brown kugharamikia nauli ya ndege kusafiri nje ya nchi kwa ajili ya shows zimepita na wakati huku akisema kuwa ni lazima ndege binafsi itajumuishwa kwenye mkataba kati ya uongozi wa Otile na mapromota wa kigeni. ” This before … Sahizi ni Private Jet kwa contract,” Ujumbe wa Noriega unasomeka instastory. Kauli ya Noriega imekuja mara baada ya promota aliyempa mwaliko msanii otile brown nchini marekani kugharamia usafiri wa msaniii huyo kupitia ndege binafsi ya daraja la juu.

Read More
 OTILE BROWN AINGILIA SAKATA LA MSANII FAVE KUDHULUMIWA NA PROMOTA

OTILE BROWN AINGILIA SAKATA LA MSANII FAVE KUDHULUMIWA NA PROMOTA

Nyota wa muziki nchini Otile Brown amefunguka kuhusu sakata la msanii wa Nigeria Fave kudhulumiwa na promota baada ya kukamilisha ziara yake ya kimuziki nchini. Kupitia instastory Otile amesema pana haja ya mapromota wa Kenya kuchukulia biashara kama suala la muda mrefu badala ya kuwadhulumu washirika wao ambao wana mchango mkubwa kwenye mafanikio ya shughuli zao. Hitmaker huyo wa “Celebration” amewakosoa mapromota waliomleta Fave nchini Kenya kwa kutokuwa na mipango mizuri ya kufanikisha show ya msanii huyo huku akisisitiza kuwa mawasiliano ni jambo la msingi kwenye biashara yeyote yenye mafanikio.

Read More
 OTILE BROWN AZUA GUMZO MTANDAONI NA SOKSI YA KSHS. 32,000

OTILE BROWN AZUA GUMZO MTANDAONI NA SOKSI YA KSHS. 32,000

Msanii nyota nchini Otile Brown ameamua kuzitumia ipasavyo pesa anazozikeshea na kuzitolea jasho. Mkali huyo wa “Celebration” kupitia Instastory ametuonesha soksi ambazo kwa mujibu wake zilimgharimu shillingi 32,000 za Kenya. Hatua hiyo imeonekana kuleta ukakasi miongoni mwa mashabiki zake, wengi wakionekana kumkejeli kwa kusema kuwa anatumia suala hilo kutengeneza mazingira ya kuzungumziwa mtandaoni Hii sio mara ya kwanza kwa Otile Brown kuanika vitu vya thamani anavyovimiliki, mapema mwaka huu alitusanua kuwa alitumia kiasi cha shillingi elfu 80 za Kenya kununua viatu aina Balenciaga Crocs boots.

Read More
 OTILE BROWN AWACHANA WANAOKOSOA MUZIKI WAKE

OTILE BROWN AWACHANA WANAOKOSOA MUZIKI WAKE

Mwanamuziki nyota nchini Otile Brown amewatolea uvivu  baadhi ya mashabiki wanaozidi kumkosoa baada ya kuacha kuimba nyimbo zake kwa lugha ya Kiswahili na kugeukia Kiingereza. Kupitia mfululizo wa insta stories kwenye ukurasa wake wa Instagram, Otile amewataka wanaopinga juhudi zake za kuupeleka muziki wake kimataifa kuanza kujifunza kuhusu mitindo mbali mbali ya muziki huku akienda mbali zaidi na kudai kuwa ataendelea kutoa muziki mzuri kwa lugha ya Kiingereza kwani hatotishwa na maneno ya watu mtandaoni. “Fk the humble shit for a sec … do y’all even to pay to my kizungu songs au kisa mnapenda Kiswahili mnaboeka ata before y’all give it a chance … mimi ukinipa nafasi nakalisha Africa nzima na dunia kwa ujumla kwani ni Siri”, Aliandika Katika hatua nyingine, Hitmaker huyo wa ngoma ya “Celebration” amesema kuwa hana muda wa kuuthibitisha ulimwengu mafanikio yake kisanaa kwa kuwa ana kipaji cha kipekee kwenye tasnia ya muziki barani Afrika na kote duniani. “Na by the way nyimbo za Kiswahili kwangu hamuezi kumaliza msion … sihitaji kuprove chochote uwezo wangu mnaujua … sitochoka kufanya kufanya nyimbo za kimataifa kisa woga … find taste …”  Alisisitiza

Read More
 OTILE BROWN ASHINDWA KUFICHA HISIA ZAKE KWA MICHELE BRAXTON

OTILE BROWN ASHINDWA KUFICHA HISIA ZAKE KWA MICHELE BRAXTON

Mwanamuziki maarufu nchini Otile Brown ameshindwa kuendelea kuficha hisia zake za ndani juu ya mapenzi aliyonayo kwa staa wa muziki wa Rnb kutoka Marekani, Toni Michele Braxton. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Otile ameweka wazi hisia zake  kwa Michele Braxton kwa kudai kwamba amekuwa akimzimia kimapenzi mwanamuziki huyo kwa muda mrefu na bado anaendelea kuhusudu penzi lake. “Still crushing on her,” Otile ameandika. Hitmaker huyo wa ngoma ya Jeraha ameenda mbali zaidi na kumpa maua yake mwanamama huyo mwenye umri wa miaka 54 kwa kusema kwamba ni moja kati ya wanawake warembo zaidi duniani ambao wapo hai. “One of the sexiest women God ever created,” Amesisitiza. Hata hivyo mashabiki wametoa hisia mbali mbali kuhusiana kauli hiyo ya Otile Brown huku wengi wakisema wameumizwa na kitendo cha msanii huyo kumzimia kimapenzi mtu mwingine licha ya kuwa wamekuwa wakimtamani kimapenzi. Utakumbuka Braxton ambaye anatajwa kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na Rapa Birdman amejaliwa kuwapata watoto wawili ambao ni, Diezel Ky Braxton na Denim Cole.

Read More
 OTILE BROWN AFUNGUKA NAMNA WANIGERIA WANATEGEMEA SOKO LA KENYA KUTANGAZA MUZIKI WAO

OTILE BROWN AFUNGUKA NAMNA WANIGERIA WANATEGEMEA SOKO LA KENYA KUTANGAZA MUZIKI WAO

Staa wa muziki nchini Otile Brown Otile Brown amefunguka jinsi ambavyo Wanigeria wanatumia soko la muziki wa Kenya kutangaza muziki wao Kulingana na Otile Brown wasanii wa Nigeria wanategemea soko la Kenya kufanya nyimbo zao ziwe kubwa zaidi kwa kuwa wanatumia pesa nyingi kuhonga vituo vya redio nchini ili viweze kucheza nyimbo zao. Hitmaker huyo ngoma ya “Woman” amesema nyimbo nyingi za Nigeria zimeshindwa kupenya kwenye soko la muziki hadi pale wakenya kwenye mtandao wa tiktok wanapoanza kuzitumia kwenye video zao. Hata hivyo ametoa changamoto kwa vyombo vya habari  nchini kuunga mkono kazi za wasanii wa humu nchini bila kubagua ili muziki wa kenya uweze kutabulika katika mataifa mengine.

Read More