OTILE BROWN AKOSHWA NA MFUMO WA MUZIKI WA AFRIKA KUSINI

OTILE BROWN AKOSHWA NA MFUMO WA MUZIKI WA AFRIKA KUSINI

Mwanamuziki kutoka nchini Kenya Otile Brown ameusifia mfumo wa muziki wa Afrika Kusini ambao ameutaja kuulinda zaidi muziki wa ndani kwa kutoupa nafasi muziki wa mataifa mengine ndani ya nchi hiyo. Kupitia nstastory yake kwenye mtandao wa Instagram Otile Brown amedai kuwa kwenye kiwanda cha muziki nchini Afrika Kusini kuna hali kujipa kipaumbele zaidi kwani nyimbo za wasanii wa ndani zinapiga sana kwenye maeneo ya umma tofauti na nchini ya Kenya ambayo imewazingatia sana wasanii wa nje huku akieleza kuwa inaweza kuwa moja kati ya sababu za muziki wao kuwa na thamani ya juu yenye maendeleo. Otile Brown ambaye juzi kati amekuwa nchini Afrika Kusini amesema mfumo wa muziki wa Afrika kusini umewapelekea wasanii wengi kuwa na mafanikio makubwa hata wakiwa na kazi chache walizozifanya kwenye career yao ya muziki ambapo ameonekana kutoa changamoto kwa serikali ya kenya kufuata nyayo za nchi ya Afrika kusini ambayo imetengeneza mazingira ya kutumia sanaa kutoa ajira kwa maelfu ya vijana wake. “Soko la muziki la Afrika Kusini halivumi sana lakini lina utajiri. Serikali imewatengenezea mazingirana wanajipenda sana unaweza kuwa na wimbo mkubwa Afrika na hawaujui maana huwezi sikia wimbo wa nje hata mmoja kwenye klabu, Migahawani au kwenye vyombo vya usafiri wowote”. Otile anaendelea kwa kuandika “Ni ubinafsi ila imenifanya nifikirie Je ni bora uwe hivyo na watu wenu wawe vizuri au uwe muungwana waku support nyimbo za nje na kupoteza nguvu na thamani ya sanaa yenu maana jamaa kimya game wanailinda nakuithamini maana inatengeneza ajira 100% kila siku. Jamaa mtu ananyimbo mbili tu lakini mafanikio makubwa sana.” ameandika kupitia Instastory yake

Read More
 OTILE BROWN AJIZAWADI VIATU YENYE THAMANI YA SHILLINGI 80,000 ZA KENYA

OTILE BROWN AJIZAWADI VIATU YENYE THAMANI YA SHILLINGI 80,000 ZA KENYA

Msanii nyota nchini Otile Brown ameamua kuzitumia ipasavyo pesa anazozikeshea na kuzitolea jasho. Hii ni baada ya kutumia kiasi cha shillingi elfu 80 za Kenya kununua viatu aina Balenciaga Crocs boots kama zawadi ya kumbukizi ya kuzaliwa kwake Machi 21 mwaka 2022. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Hitmaker huyo wa ngoma ya “Fed Up” amechapisha video akionekana akizitoa viatu hivyo kwenye boksi huku akiwashukuru mashabiki zake kwa kusapoti muziki wake na kumfanya kuwa namba moja kwenye kiwanda cha muziki nchini.. Otile Brown ambaye kwa sasa yupo nchini Afrika Kusini kwa ajili kusherekea birthday yake anaungana na rapa Kanye West  kutoka Marekani ambaye hupendelea kuvaa viatu aina ya Balenciaga Crocs Boots

Read More
 OTILE BROWN AIPONDA ALBUM MPYA YA ARROW BOY, ATISHIA KUFUTA WIMBO ALIOSHIRIKISHWA

OTILE BROWN AIPONDA ALBUM MPYA YA ARROW BOY, ATISHIA KUFUTA WIMBO ALIOSHIRIKISHWA

Staa wa muziki nchini Otile Brown ameonesha kukerwa na kitendo cha Arrow Boy kuushirikisha wimbo wao wa pamoja ambao haukuwa umekamilika kwenye album yake mpya iitwayo Focus. Kupitia instastory Otile Brown ametaja Arrow Boy kama mnafiki asiyejali maslahi ya wasanii wenzake kwa hatua yake ya kukwenda kinyume na mkataba wa makubaliano wa kutoachia demo ya wimbo wao wa pamoja huku akisema kwamba kitendo hicho huenda ikamshushia brand yake ya muziki. Hata hivyo wa ngoma ya “Fine By Me” amemtaka Arrow Boy auondowe wimbo wao uitwao “Show Me” kwenye album yake ya Focus kabla hajachukua hatua ya kuishusha mwenyewe wimbo huo kwenye digital platforms mbali mbali za kupakua na kusikiliza muziki duniani.

Read More
 OTIILE BROWN AFUNGUKA KUHUSU MAISHA YAKE YA MAHUSIANO

OTIILE BROWN AFUNGUKA KUHUSU MAISHA YAKE YA MAHUSIANO

Nyota wa muziki nchini Otile Brown, amesema licha ya kusumbuliwa na warembo kwa sasa hayupo kwenye mahusiano,yaani yupo ‘Single’. Mkali huyo anayefanya vizuri na EP yake mpya Uptown Flex amedai kwa sasa hataki kukurupuka kuingia kwenye mahusiano ya mapenzi kutokana na matukio aliyopitia kipindi cha nyuma. Otile Brown amefunguka hayo  kwenye Instagram live, mara baada ya mashabiki zake kutaka kujua upande wa maisha yake ya mahusiano baada ya kutangaza kuachana na mrembo mwenye asili ya nchi ya Ethiopia Nabayet wiki kadhaa zilizopita.

Read More
 OTILE BROWN AHITAJI MAOMBI KUHUSU AFYA YAKE

OTILE BROWN AHITAJI MAOMBI KUHUSU AFYA YAKE

Siku chache tu baada ya kufanyiwa upasuaji, mwanamuziki kutoka Kenya, Otile Brown amewaacha mashabiki wake katika hali ya wasiwasi kutokana na chapisho lake kwenye mitandao ya kijamii. Otile Brown ametoa taarifa fupi kuhusu afya yake akifichua kwamba anashuhudia maumivu makali sana mwili mwake. Kupitia ukurasa wake wa Instagram amewasihi mashabiki wake kumkumbuka katika maombi yao huku akiendelea kuuguza maumivu yanayomkabili. “Nina maumivu makali sana, ombeeni Obizee” Brown ameandika kwenye ukurasa wake wa Instagram. Utakumbuka takriban siku tano zilizopita mwanamuziki huyo alifanyiwa upasuaji katika hospitali moja jijini Nairobi. Hata hivyo,hakueleza sehemu ya mwili wake ambayo ilifanyiwa upasuaji wala kilichokuwa kinamsumbua.

Read More
 OTILE BROWN KUACHIA UPTOWN FLEX EP ALHAMISI HII

OTILE BROWN KUACHIA UPTOWN FLEX EP ALHAMISI HII

Msanii nyota nchini Otile Brown ametangaza kuachia EP mpya chini ya  lebo yake ya muziki ya Just in Love ambayo ni zawadi kwa mashabiki zake kuelekea siku ya wapendanao maarufu kama Valentines Day. EP hiyo inakwenda kwa jina la Uptown Flex itakuwa na jumla ya nyimbo 5 ambazo amezifanya mwenyewe bila kumshirikisha msanii yeyote. Kupitia ukurasa wake rasmi wa Instagram Otile Brown ameshare artwork pamoja na Tracklist ya EP hiyo ambayo ina nyimbo kama  Double up, Realer, Fine By Me,  Run Up na Sempre. Hata hivyo amewataka mashabiki zake kukaa mkao wa kula kuipokea Uptown Flex  EP ambayo itaingia sokoni rasmi Februari 10 mwaka wa 2022. Hii inaenda kuwa EP ya kwanza kwa mtu mzima Otile Brown ikizingatiwa kuwa mwaka wa 202o aliwabariki mashabiki zake na Album iitwayo Just In Love ambayo ilikuwa na jumla ya mikwaju 11 ya moto.

Read More
 OTILE BROWN AMVUA NGUO MREMBO MWENYE SHAPE MATATA NCHINI KENYA VERA SIDIKA

OTILE BROWN AMVUA NGUO MREMBO MWENYE SHAPE MATATA NCHINI KENYA VERA SIDIKA

Staa wa muziki nchini Otile Brown amemtolea uvivu mrembo mwenye shape matata Vera Sidika baada ya mrembo huyo kuonekana kulitaja jina lake katika siku za hivi karibuni. Kupitia instagram page yake Otile Brown amemtaka Vera Sidika kuitunza ndoa yake ikizingatiwa kuwa hajawahi kuizungumzia ndoa yake na mumewe brown mauzo sehemu yeyote kutokana na heshima aliyonao kwao. “Jaribu kumheshimu mumeo na kulinda ndoa yako kama ninavyojaribu kunyamaza kila unapotaja jina langu. Dont get comfortable.” Ameandika kupitia insta story yake. Kauli ya otile brown imekuja siku chache baada ya vera sidika kusema kuwa ikitokea otile brown anataka kufanya kolabo na mumwe Brown Mauzo ataunga mkono kikamilifu kolabo hiyo. Hili halikutarajiwa kabisa kutoka kwa Vera Sidika ikizingatiwa kuwa alikuwa kwenye mahusiano na Otile Brown kipindi cha nyuma ambapo walikuja wakaachana vibaya baada ya kuingia kwenye ugomvi mbaya. Kutokana na hilo inaonekana kwamba Vera sidika amepata furaha tena na labda alimsamehe Otile Brown ndiyo maana hajawahi kusema jambo lolote baya kumhusu.

Read More
 OTILE BROWN APOKEZWA TUZO YA DHAHABU NA YOUTUBE KWA KUFIKISHA SUBSCRIBERS MILIONI 1.

OTILE BROWN APOKEZWA TUZO YA DHAHABU NA YOUTUBE KWA KUFIKISHA SUBSCRIBERS MILIONI 1.

Staa wa muziki wa nchini  Otile Brown amepokezwa tuzo ya Golden creators na mtandao wa youtube kwa kufikisha jumla ya subscribers millioni 1. Mkali huyo wa “Jeraha” amewashukuru mashabiki zake kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kuendelea kufuatilia kazi zake ambazo zinaendelea kuonyesha mafanikio makubwa huku akiahidi kutoa mzuri kwa ajili yao . Otile Brown anakuwa msanii wa kwanza kutokea Kenya kuwa na wafuasi wengi zaidi katika mtandao wa YouTube huku Dusuma aliyomshirikisha Meddy ikiwa ndiyo video yenye watazamaji wengi zaidi ikiwa na views milioni 35 ndani ya mwaka mmoja. Baadhi ya wasanii kutoka Kenya wanaofuata kwa wafuasi wengi ni pamoja na Bahati Kenya  akiwa na subscribers elfu 902K, Willy Paul 877K, Sauti Sol  856K,  Khaligraph Jones 538K, na Nyashinski 473K.

Read More
 OTILE BROWN ATHIBITISHA KUACHANA NA MPENZI WAKE WA SIKU NYINGI NABAYET

OTILE BROWN ATHIBITISHA KUACHANA NA MPENZI WAKE WA SIKU NYINGI NABAYET

Staa wa muziki nchini Otile Brown, ametangaza kuachana na Mpenzi wake raia wa Ethiopia Nabayet baada ya kuwa kwenye mahusiano kwa muda wa miaka mitatu. Kupitia ukurasa wake wa instagram  Otile Brown amesema amechukua maamuzi ya kuachana na mpenzi wake huyo baada ya kuafikia makubaliano ya pamoja ambapo amedai kuwa wataendelea kuwa marafiki. Hata hivyo chanzo cha wawili hao kuachana hajaweka wazi ila sio mara ya kwanza kufanya hivyo kwani kipindi cha nyuma wamekuwa na mazoea ya kuachana na kisha mwisho wa siku wanarudiana Hata hivyo walimwengu kwenye mitandao ya kijamii wamehoji huenda Otile Brown anatengeza  mazingira ya kumzinguziwa kabla ya ujio wa ngoma yake mpya Ikumbukwe kuwa penzi la Otile Brown na Nabayet lilianza rasmi mwishoni mwa mwaka 2018  miezi kadhaa baada ya kuachana na aliyekua mpenzi wake Verah Sidika.

Read More
 ALBUM YA OTILE BROWN “JUST IN LOVE” YAWEKA REKODI BOOMPLAY KENYA

ALBUM YA OTILE BROWN “JUST IN LOVE” YAWEKA REKODI BOOMPLAY KENYA

Staa wa muziki nchini, Otile Brown anaendelea kupokea upendo na support kubwa kutoka kwa mshabiki wake kiasi cha kufanya vizuri na album yake  ‘Just In Love’. Hadi kufikia sasa katika mtandao wa boomplay album hiyo imeweza kusikilizwa  zaidi ya mara millioni 17.3 ikiwa ni takriban miaka miwili tangu itokea rasmi. Kwa mafanakio hayo, Album ya just in love  ndio Album iliyosikilizwa zaidi kwenye mtandao wa boomplay kwa wasanii wa humu nchini. Utakumbuka album ya just in love kutoka kwa mtu mzima otile brown iliachiwa rasmi Juni 3 mwaka wa 2020 ikiwa na jumla ya mikwaju 10 ya moto.

Read More
 OTILE BROWN AFIKISHA SUBSCRIBERS MILLIONI MOJA KWENYE MTANDAO WA YOUTUBE

OTILE BROWN AFIKISHA SUBSCRIBERS MILLIONI MOJA KWENYE MTANDAO WA YOUTUBE

Nyota wa muziki Otile Brown anazidi kujikita kileleni kwenye mtandao wa YouTube ambapo kwa sasa amefikisha idadi ya subscribers Milioni 1 kwenye mtandao huo. Hii inamfanya Hitmaker huyo wa “Jeraha” kuendelea kukaa kileleni kama msanii anayeongoza kwa idadi kubwa ya subscribers kwenye Mtandao wa Youtube kwa wasanii wa Kenya. Sanjari na hilo, Mkurugenzi wa lebo ya muziki ya Just in Love na hadi sasa Kupitia channel yake ya YouTube kazi zake zimetazamwa zaidi ya mara milioni  251 tangu ilipofunguliwa rasmi Aprili 20 mwaka 2016. Wasanii wengine kutoka Kenya ambao wapo mbioni kufikisha subscribers millioni moja kwenye mtandao wa youtube ni pamoja na Bahati ambaye ana subscribers laki 9, na Sauti sol ambao wana subscribers laki 8

Read More
 HARMONIZE NA OTILE BROWN WAINGIA LOCATION KUTAYARISHA VIDEO YA WIMBO WAO

HARMONIZE NA OTILE BROWN WAINGIA LOCATION KUTAYARISHA VIDEO YA WIMBO WAO

Msanii wa Bongofleva Harmonize na Otile Brown wameingia location kuitayarisha video ya wimbo wao ambao unahisiwa huenda ukapatikana kwenye EP yao ya pamoja. Harmonize amethibitisha hilo kupitia instastory yake kwenye mtandao wa Instagram kwa kushare misururu ya picha wakiwa chimbo na mkali huyo kutoka Kenya jambo ambalo limewaaminisha mashabiki muziki mzuri Afrika Mashariki kuwa wawili hao wapo kwenye maandalizi ya video ya wimbo wa pamoja. Kupitia post hiyo Harmonize hajaweka wazi nini hasa wanapika na Otile Brown ila wajuzi wa mambo kwenye mitandao ya kijamii wanahoji huenda Otile Brown akawa mmoja wa wasanii atakaotumbuiza Disemba 31 mwaka huu kwenye listening party ya album yake ya High Schoolhuko Palm Village, Mikocheni, Dar e Salaam. Juzi kati Otile Brown alisifia uwezo wa Harmonize katika verse ya wimbo wao wa pamoja waliofanya kwa mara ya kwanza ambapo alisema msanii huyo wa Bongofleva alifanya vizuri katika ngoma hiyo huku akieleza fahari yake kwa mashabiki wa Tanzania na Kenya ambao watakuwa tayari kusikia kazi hiyo Itakumbukwa Harmonize  akiwa nchini katika ziara yake ya kimuziki alitangaza wazi kuja na ‘EP’ itakayo kuwa na nyimbo 5 za pamoja kati yake na Otile Brown.

Read More