Ringtone Apoko Atangaza Kuhutubia Umma Baada ya Kuachiwa kwa Dhamana

Ringtone Apoko Atangaza Kuhutubia Umma Baada ya Kuachiwa kwa Dhamana

Msanii maarufu wa muziki wa injili, Ringtone Apoko, amedokeza kuwa atazungumza na umma wiki hii, katika kile kinachoonekana kama hotuba muhimu kufuatia matukio ya hivi karibuni maishani mwake. Katika ujumbe huo aliyouchapisha Instagram, msanii huyo alionesha shukrani kwa marafiki zake waliomsaidia wakati wa kipindi kigumu, na kumshukuru Mungu kwa kupitia changamoto alizopitia. “WILL BE ADRESS THE NATION THIS WEEK. 4 NOW AM THANK FOR MY FRIENDS AND MY GOD.” aliandika Ingawa hakutoa maelezo kamili kuhusu yaliyomo kwenye hotuba hiyo, ujumbe wake umeibua gumzo kubwa mitandaoni. Mashabiki wake wametoa maoni mbalimbali, baadhi wakimuunga mkono na kumtia moyo, huku wengine wakisubiri kwa hamu kusikia atakachosema. Wengine pia walitafsiri ujumbe huo kama dalili ya kurudi kwa kishindo kwa msanii huyo ambaye kwa muda sasa amekuwa kimya kisanaa. Taarifa hii inakuja siku chache tu baada ya Ringtone kuachiwa kwa dhamana na korti, kufuatia kesi inayohusiana na mgogoro wa ardhi. Kesi hiyo imekuwa ikifuatiliwa kwa karibu na vyombo vya habari na mashabiki wake, na wengi wanatarajia huenda hotuba hiyo itagusia kwa undani sakata hilo. Kwa sasa, macho na masikio ya wapenzi wa burudani na mashabiki wake yameelekezwa kwake, wakisubiri hotuba hiyo ambayo huenda ikafungua ukurasa mpya katika maisha na safari yake ya muziki.

Read More
 Msanii Ringtone Aachiwa kwa Dhamana ya Shilingi Milioni 1

Msanii Ringtone Aachiwa kwa Dhamana ya Shilingi Milioni 1

Msanii wa nyimbo za Injili, Alex Apoko almaarufu Ringtone, aliachiliwa kwa dhamana ya Shilingi milioni 3 au kwa njia mbadala ya bondi ya Shilingi milioni 1, katika kesi inayomkabili ya kula njama ya kutapeli ardhi. Ringtone alifikishwa katika Mahakama ya Milimani siku ya Alhamisi, pamoja na mshukiwa mwenzake Alfred Juma Ayora, wakikabiliwa na shtaka la kula njama ya kumlaghai mwanamke mmoja kipande cha ardhi chenye thamani ya Shilingi milioni 50. Kwa mujibu wa mashtaka, wawili hao wanadaiwa kupanga njama ya kumtapeli Teresiah Adhiambo kipande cha ardhi kilichoko eneo la Karen, Nairobi, chenye nambari ya usajili NAIROBI/BLOCK 99/142 na ukubwa wa takribani ekari 0.1908. Upande wa mashtaka unadai kuwa mnamo au kabla ya Februari 28, 2023, Ringtone na mwenzake walijifanya kuwa wamiliki halali wa ardhi hiyo kwa madai kuwa wameishi humo kwa kipindi cha miaka 20 kwa mujibu wa umiliki wa muda mrefu (adverse possession), jambo ambalo walijua si la kweli. Kesi hiyo imepangiwa kusikizwa katika tarehe ijayo huku washukiwa wakiendelea kupewa masharti ya dhamana walizopewa na mahakama.

Read More
 Mahakama Yakataa Dhamana kwa Ringtone Kufuatia Mashtaka ya Utapeli wa Ardhi ya Shilingi Milioni 50

Mahakama Yakataa Dhamana kwa Ringtone Kufuatia Mashtaka ya Utapeli wa Ardhi ya Shilingi Milioni 50

Mwimbaji maarufu wa muziki wa injili nchini Kenya, Alex Apoko, Maarufu Ringtone, amepata pigo kubwa hapo jana baada ya Mahakama ya Nairobi kukataa ombi lake la kuachiliwa kwa dhamana. Ringtone na mshukiwa mwenzake Alfred Juma Ayora wanashtakiwa kwa kosa la kula njama ya kutapeli ardhi yenye thamani ya shilingi milioni hamsini, inayodaiwa kumilikiwa na Bi. Teresiah Adhiambo katika mtaa wa kifahari wa Karen, jijini Nairobi. Kwa mujibu wa hati ya mashtaka, wawili hao wanadaiwa kutoa madai kuwa wameishi katika ardhi hiyo kwa zaidi ya miaka ishirini na kwa hivyo wanastahili kupewa umiliki wa ardhi hiyo kwa mujibu wa sheria ya “adverse possession”, inayomruhusu mtu kumiliki  ardhi au mali isiyokuwa yake kisheria  endapo atakuwa ameimiliki kwa muda mrefu bila pingamizi kutoka kwa mmliki halali. Hata hivyo, upande wa mashtaka unasema madai hayo ni ya kupangwa kwa lengo la kuipora ardhi hiyo kwa njia ya hila na nyaraka za uongo. Mahakama iliielezwa kuwa wamiliki halali wa ardhi hiyo hawajawahi kuondoka wala kuachia umiliki kwa washitakiwa. Katika uamuzi wake, mahakama ilitaja sababu kadhaa za kukataa dhamana, ikiwemo uzito wa kosa, historia ya mshtakiwa kuhusishwa na kesi kama hizi hapo awali, na hatari ya kuingilia ushahidi au mashahidi. Kumbuka, mwaka 2016, Ringtone alihusishwa na mgogoro wa nyumba ya kifahari katika mtaa wa Runda. Aidha, mwaka 2023, familia ya raia wa Sudan Kusini ilimshtaki kwa madai ya kuvamia mali yao huko Karen na kuharibu vitu vyao. Ringtone, kwa upande wake, amekanusha mashtaka haya, akisema ni njama ya kumchafua hadharani na kumvunjia heshima kama mtu wa imani. Amekuwa akidai kuwa yeye ni mpangaji halali wa ardhi hiyo kwa muda mrefu. Kwa sasa, Ringtone na mshukiwa mwenzake wataendelea kuzuiliwa rumande hadi kesi itakapoanza kusikilizwa rasmi. Mahakama imesisitiza kuwa mchakato wa haki utafuatwa kikamilifu, na uamuzi wa mwisho utategemea ushahidi wa pande zote mbili

Read More
 Ringtone Apoko amchana Eric Omondi kwa kutumia mbwa wake kutafuta umaarufu

Ringtone Apoko amchana Eric Omondi kwa kutumia mbwa wake kutafuta umaarufu

Msanii asiyeishiwa na matukio kila leo Ringtone Apoko amemtolea uvivu Eric Omondi baada ya mchekeshaji huyo kutamba na mbwa wake kwenye uzinduzi wa onesho la Laugh & Jazz mwishoni mwa juma lillopita. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Ringtone amedai kuwa Omondi alimuomba mbwa hao kwa ajili ya kutengeneza mazingira ya kuzungumziwa kwenye vyombo vya habari nchini. Hitmaker huyo wa “Ombi Langu” amesema licha ya kumsaidia Omondi kufanikisha jambo lake amekerwa na kitendo cha mchekeshaji huyo kumregeshea mbwa wake wakiwa wachafu na wachovu. Hata hivyo watumiaji wa mitandao ya kijamii wamemuashia moto Ringtone kwa madai ya kutafuta kiki kupitia jina la Omondi.

Read More
 Ringtone afunguka sababu za kuwaponda Willy Paul na Bahati

Ringtone afunguka sababu za kuwaponda Willy Paul na Bahati

Hitmaker wa Ombi Langu, Ringtone Apoko amefunguka sababu ya kuwakosoa wasanii Willy Paul na Bahati kila mara kwenye majukwaa mbali mbali. Kwenye mahojiano yake hivi karibuni amesema wawili hao walimvunjia heshima mwenyezi Mungu kwa kutumia vibaya kiwanda cha muziki wa injili kwa ajili ya kujilimbikizia mali na kisha wakageukia muziki wa kidunia. Msanii huyo ameenda mbali zaidi na kusema kuwa kitendo cha Willy Paul na Bahati kutumia njia haramu kuchuma mali wanayomiliki kwa sasa imewaponza kisanaa kiasi cha kutopata mafanikio kwenye muziki wao. Katika hatua nyingine Ringtone ametetea utajiri wake kwa kusema kuwa ana vyanzo vingi halali vinavyomuinguzia kipato huku akikanusha tuhuma za kujihusisha na biashara haramu ya ulanguzi wa pesa kwani inakwenda kinyume na maandiko matakatifu.

Read More
 Ringtone aanika siri za Bahati, Adai yupo mbioni kuja na EP mpya

Ringtone aanika siri za Bahati, Adai yupo mbioni kuja na EP mpya

Mwanamuziki asiyeishiwa na matukio kila leo Ringtone Apoko amefunguka tusiyoyajua kuhusu ukimya wa Bahati kwa kusema kwamba amekuwa chimbo akiandaa EP yake mpya. Kulingana na Ringtone hatua ya Bahati kufuta kila kitu kwenye ukurasa wake wa Instagram ilikuwa ni njia ya kutengeneza mazingira ya ujio wa EP hiyo ambayo ina jumla ya nyimbo 6. Katika hatua nyingine Ringtone amewataka mashabiki kumweka Bahati kwa maombi kwa sababu mkali huyo wa ngoma ya “Adhiambo” amekuwa na msongo wa mawazo tangu ashindwe kwenye kinyanganyiro cha ubunge Mathare. Bahati amekuwa kimya baada ya uchaguzi mkuu wa Agosti 9 kukamilika nchini Kenya, jambo ambalo liliwaacha mashabiki zake na maswali mengi kiasi cha kutaka kufahamu ni nini hasa kimemsibu msanii huyo.

Read More
 RINGTONE APOKO ATANGAZA KUACHA MUZIKI WA INJILI

RINGTONE APOKO ATANGAZA KUACHA MUZIKI WA INJILI

Nyota wa muziki kutoka Kenya Ringtone amezua mjadala mkali kwenye  mitandao ya kijamii mara baada ya kutangaza kuachana na kazi za sanaa ya muziki wa injili. Kupitia video aliyoichapisha kupitia ukurasa wake wa Instagram ringtone ameweka wazi kwamba ameamua kujiunga rasmi na muziki wa kidunia ambapo sasa atajikita kwenye uimbaji wa nyimbo za mapenzi. Hitmaker huyo wa ngoma ya Pamela amewashukuru mashabiki zake waliofuatilia nyimbo zake kipindi alikuwa anajihusisha na uimbaji wa nyimbo za injili huku akitoa wito kwa wakenya kumuunga mkono kwenye safari yake mpya ya muziki wa kidunia. Hata hivyo amewataka wasanii wanaofanya muziki wa kidunia wampe ushirikiano kwa kuwa hajajiunga na muziki huo kwa ajili ya ushindani bali kuupeleka muziki wa kenya kimataifa. Ni jambo ambalo limewachanganya mashabiki zake japo kufikia sasa hajataja hasa chanzo cha kufikia uamzi huo ila wajuzi wa mambo kwenye mitandao ya kijamii wanahoji kuwa huenda mwanamuziki huyo alikuwa akipitia changamoto flani kwenye tasnia ya muziki wa injili nchini Kenya. Ikumbukwe kwamba huyu sio msanii wa Kwanza kutoka Kenya kusitisha safari yake ya muziki wa injili na kujiunga na muziki wa kidunia, tumewaona pia wasanii kama Willy Paul, Bahati, Mr. Seed, Weezdom ambao kipindi cha nyuma walikuwa waimbaji wa nyimbo za Injili wakigeukia muziki wa kidunia.  

Read More
 RINGTONE ATAMBA NA SURUALI YA SHILLINGI MILLIONI 1.5 ZA KENYA

RINGTONE ATAMBA NA SURUALI YA SHILLINGI MILLIONI 1.5 ZA KENYA

Mwanamuziki wa nyimbo za injili Ringtone ameingia kwenye headlines kwa mara nyingine, mkali huyo kwa sasa amekuwa ni mtu wa kutupa Breaking News kila uchao hii ni baada ya kusema kuwa yeye ndiye msanii wa kwanza Kenya kumiliki suruali ghali zaidi. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Ringtone ameeleza kuwa licha ya kuwa ana miliki suruali yenye thamana ya shilllingi millioni 1.5 Za Kenya hajawahi kuwa na jeuri ya kutaka kujionesha kuwa ana pesa nyingi kama namna vijana wa siku hizi wanavyofanya mtandaoni. Hata hivyo, hii sio mara ya kwanza kwa Ringtone kutamba kuhusu kumiliki vitu vya thamani kwani mwaka wa 2021 alitusanua kuwa alinunua saa ya shillingi milioni  60 za Kenya aina ya Richard Mille Watch.

Read More
 RINGTONE AFUNGUKA KUINGIA KWENYE NDOA

RINGTONE AFUNGUKA KUINGIA KWENYE NDOA

Mwanamuziki wa nyimbo za injili  Ringtone amefunguka na kusema kwamba hana mpango wa kuoa hivi karibuni. Katika mahojiano na Nichols Kioko hitmaker huyo wa ngoma ya “Sisi ndio tuko” amesema mapenzi yake kwenye muziki ndio yamemfanya haishi maisha mazuri licha ya changamoto anazokutana  nazo. Ringtone Anaamini wanawake wanaweza kumuaharibia shughuli zake za muziki lakini pia kumfilisisha kiuchumi. Hata hivyo amedokeza ujio wa ngoma yake mpya na kundi la muziki wa injili kutoka Tanzania Zabron Singers ambayo kwa mujibu wake itaingia sokoni mwisho mwa wiki hii.

Read More
 MAHAKAMA YAAHIRISHA KESI ILIYOWASILISHWA NA RINGTONE DHIDI YA MWANABLOGU ROBERT ALAI

MAHAKAMA YAAHIRISHA KESI ILIYOWASILISHWA NA RINGTONE DHIDI YA MWANABLOGU ROBERT ALAI

Mahakama ya Kibera imeahirisha kwa mara nyingine kikao cha kusikiliza kesi iliyowasilishwa na mwanamuziki Ringtone dhidi ya mwanablogu Robert Alai ambaye alimshambulia na kumjeruhi vibaya mwaka wa 2021. Akizungumza nje ya mahakama ya kibera Wakili wa Ringtone Evans Ondiek amesema Kesi hiyo imeahirishwa hadi Juni 3 mwaka wa 2022,baada ya wakili wa Robert alai kukosa kufika mahakamani kusikiliza ushahidi ambao ringtone alipaswa kuwasilisha dhidi ya mteja wake. Ondiek ambaye alifika mahakamani akiwa kwenye kiti cha magurudumu baada ya kupata ajali, amemlaumu wakili wa Robert alai kwa kuihadaa mahakama kila mara kuisukuma mbele kesi ya mteja wake huku akisema kuwa ana njama ya kusambaratisha kesi inayomkabili mshatakiwa. Kwa upande Mwanamuziki Ringtone amesema atakata tamaa kwenye kesi dhidi ya Robert Alai hadi pale mahakama itamtendea haki ikizingatiwa kuwa ana ushahidi wa kutosha dhidi ya mwanablogu huyo ambaye alimjeruhi vibaya kichwani kwa rungu. Hii ni  mara ya tatu kwa kesi hiyo kuaahirishwa, mapema mwezi Februari mwaka huu ilisogeza mbele hadi Mei 9 baada ya mahakama kushikika kwenye majukumu mengine. Utakumbuka Ringtone na Robert Alai waliingia kwenye ugomvi mwezi julai mwaka wa 2021 baada ya wawili hao kuhusika kwenye ajali ya barabarani ambapo ringtone alimtuhumu Alai kwa kumpiga Rungu ya kichwa na kuaharibu gari lake.

Read More
 RINGTONE AMTOLEA UVIVU SIZE 8,ADAI HANA UWEZO WA KUMTOA MTU MAPEPO

RINGTONE AMTOLEA UVIVU SIZE 8,ADAI HANA UWEZO WA KUMTOA MTU MAPEPO

Msanii wa nyimbo za injili nchini Ringtone amemchana msanii mwenzake Size 8 kwa kitendo cha kujaribu kumtoa  mapepo muumimi moja wiki moja iliyopita. Katika mahojiano yake na Presenter Ali, Ringtone amesema Size 8 hana uwezo kuwaomba wakristo hadi kuwatoa mapepo huku akisema kwamba msanii huyo anatumia njia hiyo kujitafutia umaarufu. Kauli hiyo imekuja wiki moja baada ya video ya Size 8 akimuombea muumini moja kanisani kusambaa mtandaoni jambo ambalo lilizua mjadala mzito miongoni mwa wa kenya wengi wakidai kuwa msanii huyo ana uwezo wa kumtoa mtu mapepo.

Read More
 RINGTONE AMKASHIFU NYANSHINSKI KUTOKANA NA TAMASHA LAKE LA SHIN CITY

RINGTONE AMKASHIFU NYANSHINSKI KUTOKANA NA TAMASHA LAKE LA SHIN CITY

Mwimbaji wa nyimbo za injili nchini Ringtone amemtolea uvivu rapa Nyashinski baada ya kuandaa tamasha lake la Shin City wikiendi hii iliyomalizika. Kupitia ukurasa wake wa instagram ringtone amesema kwamba inasikitisha kuona msanii wa haiba ya Nyashinski anaendekeza ufuska na uesharati wakati yeye kama msanii wa injili anaendeleza harakati za kubadilisha kizazi kijacho. “WE IS INVESTING AT FUTURE GENERATIONS AND NYASH @realshinski IS BUSY HELPING PEOPLE DO FONICATE AND ADULTERY SHAME AT U FOR DEMON POSSESSION CONCERT AT CARNIVORE “, Aliandika Ringtone. Kauli hiyo ringtone imeonekana kuwakasirisha watumiaji wa mitandao ya kijamii ambao wamemtaka aache kuwaonea wasanii wengine wivu kwa mafanikio yao na badala yake aandae tamasha lake la muziki litakalo muingizia kipato. Utakumbuka Aprili 16 mwaka Nyashinski alijaza nyomi la mashabiki katika ukumbi wa Carnivore huko Jijini Nairobi ambako walipiga show ya kufa mtu iliyowaacha mashabiki wakiwa na kiu ya kutaka burudani Zaidi kuptia tamasha lake la Shin City.

Read More