ERIC OMONDI NA BIEN WA SAUTI SOL WARUSHIANA MAKONDE KWENYE ONESHO LA KONSHENS

ERIC OMONDI NA BIEN WA SAUTI SOL WARUSHIANA MAKONDE KWENYE ONESHO LA KONSHENS

Mchekeshaji Eric Omondi ameingia kwenye headlines baada ya kutaka kuzichapa na member wa Sauti Sol, Bien baraza usiku wa kuamkia Januari mosi katika onesho la Konshens Jijini Nairobi. Chanzo cha ugomvi huo ni baada ya Omondi kushinikiza kundi la Sauti Sol watumbuize wa mwisho katika orodha ya wasanii kama njia ya kuwapa heshima. Làkini Pia Bien katika moja ya interview amenukuliwa akisema muda wanaopewa kuperfom kama kundi la Sauti Sol katika tamasha haijawahi kuwa tatizo kwao, iwapo atakuwa wasanii wa kwanza au wa mwisho katika orodha ya wasanii. Ikumbukwe kwa muda  sasa eric omondi amekuwa akipaza sauti juu ya wasanii wa kenya kutotendewa haki na waandaaji wa matamasha ya muziki. Hii ni baada ya wasanii wa mataifa mengine kuonekana kupewa kipau mbele kufanya shows nchini huku wasanii wa Kenya wakiwekwa pembeni.

Read More
 SAUTI SOL KUJA NA ONESHO MAALUM KWA MASHABIKI ZAO DISEMBA 13

SAUTI SOL KUJA NA ONESHO MAALUM KWA MASHABIKI ZAO DISEMBA 13

Kundi la muziki nchini Sauti Sol limetangaza kuja na tamasha spesheli kwa mashabiki wao wa kigeni ambao hawatapata nafasi yà kuhudhuria show yao ya Sol Fest wikiendi hii. Kupitia ukurasa wao rasmi wa Instagram Sauti Sol wamesema Desemba 13 mwaka huu wataanda tamasha spesheli kwa mashabiki zao walioko nje ya Kenya kwa ushirikiano na umoja wa ulaya  kenya. Wakali hao wa Ngoma ya “Suzzana” wamesema tamasha hilo litaruka mubashara kupitia channeli yao ya mtandao wa Youtube kuanzia saa kumi alasiri ambapo wametaka mashabiki zao kukaa mkao wa kula kwa show hiyo ambayo itakuwa moto wa kuotea mbali. Ikumbukwe Desemba 12 mwaka huu Sauti Sol wanatarajiwa kutumbuiza jijini Nairobi kwenye tamasha lao la muziki la Sol Fest ambalo wamekuwa wakiipiga upata kwenye mitandao ya kijamii

Read More
 SAUTI SOL WAPOKEA CHETI CHA UTAMBUZI KUTOKA GRAMMY

SAUTI SOL WAPOKEA CHETI CHA UTAMBUZI KUTOKA GRAMMY

Kundi maarufu la muziki nchini, Sauti sol limepokea cheti cha utambuzi yaani (Certificate of Recognition) kutoka kwa waandaji wa tuzo za Grammy.   Cheti hicho ni maalum kwa ajili ya ushiriki wao kama watayarishaji kwenye album ya msanii Burna Boy kutoka Nigeria iitwayo “Twice As Tall” ambayo ilishinda tuzo ya Best Global Music Album kwenye tuzo za 63 za Grammy zilizofanyika mwezi wa tatu mwaka huu.   Sauti sol wameshiriki kwenye uandaaji wa wimbo namba 11 kutoka kwenye album ya “Twice As Tall” uitwao ‘Time Flies’.   Ikumbukwe, Sauti Sol kwa sasa wapo nchini Uingereza kwa ajili ya ziara yao ya kimuziki baada ya mapumziko ya takribani miaka miwili kutokana na janga la Corona.    

Read More
 SAUTI SOL MBIONI KUJA NA ALBUM MPYA

SAUTI SOL MBIONI KUJA NA ALBUM MPYA

Kundi la muziki nchini sauti sol wametangaza mwezi ambao wataichia album yao ya sita tangu waanze safari yao ya muziki. Kupitia barua ya wazi waliyoishare kwenye ukurasa wao wa instagram sauti sol wamesema album yao mpya itaingia sokoni mwezi mei mwaka wa 2022. Wakali hao wa ngoma ya Suzzana wamesema kabla ya kuachia album yao mpya, wataachia singo yao mpya mwezi Disemba mwaka huu ambapo wamesema kwamba wataweka wazi tarehe ambayo wataachia project hiyo. Sanjari na hilo wametusanua kwamba wanakuja na documentary yao iitwayo Alone Together ambayo itazungumzia changomoto ambazo wasanii wa kundi la sauti sol wamepitia tangu ujio wa janga la korona. Kauli ya sauti sol inakuja mara baada ya kufanikisha tamasha lao la kimuziki liitwalo UK residency lilofanyika nchini uingereza mapema mwezi huu.

Read More