BIEN WA SAUTI SOL AKANUSHA KUWA KWENYE UGOMVI NA MUUNGANO WA KISIASA WA AZIMIO LA UMOJA

BIEN WA SAUTI SOL AKANUSHA KUWA KWENYE UGOMVI NA MUUNGANO WA KISIASA WA AZIMIO LA UMOJA

Msanii wa Sauti Sol, Bien amefunguka na kudai kuwa hana ugomvi wowote na muungano wa kisiasa wa Azimio la Umoja kama namna baadhi ya watu wanavyochukulia mtandaoni. Katika mahojiano na kituo kimoja cha redio nchini Bien amesema kile ambacho anakishinikiza kama kundi la Sauti Sol  malipo yao wimbo wa Extravangaza ambao ulitumiwa na muungano huo kwenye shughuli zao kisiasa bila ridhaa yao. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Mbwe Mbwe” amesema mawakili wapo kwenye mazungumzo na Uongozi wa Azimio la Umoja kutatua utata unaozingira wimbo wao  wa extra vangaza huku akidokeza kwamba huenda wakalipa shillingi billioni moja za kenya kwa kuharibiwa brand yao ya muziki. Kauli ya Bien imekuja mara baada ya Ezekiel Mutua kuitaka bendi ya Sauti Sol kuacha kushiriki vita vya mtandaoni na muungano wa Azimio la Umoja na badala yake watumie njia ya mazungumzo kutatua tofauti zao kudai haki yao kwani jambo hilo huenda likaathiri muziki wao. Utakumbuka baada ya Sauti Sol kutishia kuufungulia muungano wa Azimio la Umoja kesi kwa kuitumia wimbo wa Extravaganza kwenye kampeini zao bila ridhaa yao, walipoteza takriban subscribers 2,000 kwenye mtandao wa Youtube na kuifanya channel yao kushuka kutoka subscribers elfu 905 hadi 904.

Read More
 BIEN WA SAUTI SOL AUCHANA MUUNGANO WA KISIASA NCHINI KENYA AZIMIO LA UMOJA

BIEN WA SAUTI SOL AUCHANA MUUNGANO WA KISIASA NCHINI KENYA AZIMIO LA UMOJA

Mwanakikundi wa Sauti Sol, Bien ameamua kurusha jiwe gizani kwenda kwa uongozi wa Azimio la Umoja unaongozwa na Raila Odinga baada ya bendi hiyo kupoteza jumla ya subscribers 2.000 kwenye mtandao wa youtube ndani ya kipindi cha masaa 48. Kupitia Mtandao wa Instagram Bien, ameandika ujumbe wa kimafumbo ambao umetafsiriwa na wajuzi wa mambo kwenye mitandao ya kijamii kuwa bendi hiyo inaegemea upande wa mrengo wa Kenya Kwanza unaongozwa na Naibu wa Rais Dakta William Ruto wakati huu taifa inajiandaa kwa uchaguzi mkuu wa Agosti 9. “Time will reveal. Wale wanashuka washuke saa hii. Stage yao imefika.” Ameandika Instagram. Chapisho hilo kutoka kwa Bien imeibua hisia mbali mbali miongoni mwa wakenya kwenye mitandao ya kijamii, ambapo wengi wamewataka wasaani hao bendi hiyo kujitenga na masuala ya siasa na badala yake wawekeze nguvu zao kwenye suala la kutoa muziki mzuri. Channel ya Youtube ya Sauti Sol ambayo ilikuwa na subscribers elfu 903 kwa sasa ina jumla ya subscribers elfu 903. Jumatatu wiki hii bendi ya Sauti Sol ilitishia kuushtaki Muungano wa Azimio la Umoja kwa kutumia wimbo wao “Extravaganza” bila ridhaa yao kwenye kampeni zao ambapo siku hiyo walikuwa wakimtambulisha Mgombea mwenza wa Raila Odinga, Bi. Martha Karua. Utakumbuka mwaka wa 2021 Sauti Sol walikuwa baadhi ya wasanii Kenya waliojitokeza hadharani na kupinga mchakato wa kuifanyia katiba marekebisho kupitia Mpango wa Maridhiano BBI ambao ulikuwa unaongozwa na kinara wa ODM Raila Odinga.

Read More
 EZEKIEL MUTU AMKINGIA KIFUA ODINGA KWA KUTUMIA WIMBO WA SAUTI SOL KWENYE SHUGHULI ZAKE ZA KISIASA

EZEKIEL MUTU AMKINGIA KIFUA ODINGA KWA KUTUMIA WIMBO WA SAUTI SOL KWENYE SHUGHULI ZAKE ZA KISIASA

Mwenyekiti wa chama cha hakimiliki ya muziki nchini Ezekiel Mutua amefunguka kuhusu utata unaozingira wimbo wa Extravaganza wa kundi la Sauti Sol, uliotumiwa na mrengo wa azimio la umoja kwenye hafla ya kumtambulisha mgombea mwenza wa Raila Odinga. Kupitia mitandao yake ya kijamii Mutua amesema azimio la umoja walifuata taritibu zote za kupata leseni ya kutumia wimbo wa extravangaza kwenye kampeini zao. Mutua ameenda mbali na kudai kuwa amesikitisha namna ambavyo Bodi ya hakimiliki nchini imezua tafrani/hofu miongoni mwa watumiaji wa mitandao ya kijamii kwa kutoa taarifa kinzani juu kutumika kwa wimbo wa extravagaza ikizingatiwa kuwa jambo hilo lilipaswa kutatuliwa kwa njia ya mazungumzo. Hata hivyo amesema katiba ya Kenya imeipa jukumu chama cha hakimiliki ya muziki nchini kukusanya pesa kwa niaba ya wasanii,  hivyo hakuna namna ambavyo watakwenda kinyume na sheria za hakimiliki. Hata hivyo msanii wa Sauti Sol, Bien amesema hawatalegeza msimamo wao wa kuichukulia hatua  kali za kisheria timu ya raila odinga kwa kukiuka hakimiliki ya bendi hiyo licha ya watu kuwabeza kwenye mitandao ya kijamii. Utakumbuka Mei 17 mwaka huu Raila Odinga alidai kuwa walitumia wimbo huo kama njia ya kuionesha upendo kundi la Sauti Sol ambalo limeipeperusha bendera ya Kenya kimataifa      

Read More
 SAUTI SOL KUFUNGUA KESI MAHAKAMANI DHIDI YA MUUNGANO WA AZIMIO LA UMOJA

SAUTI SOL KUFUNGUA KESI MAHAKAMANI DHIDI YA MUUNGANO WA AZIMIO LA UMOJA

Bendi maarufu kutoka nchini Kenya Sauti Sol, imetishia kuchukua hatua za kisheria dhidi ya Chama cha Azimio la Umoja nchini humo kwa madai ya ukiukwaji wa hakimiliki. Hatua hii inakuja baada ya muungano huo unaoongozwa na Raila Odinga kupiga wimbo wao wa ‘Extravaganza’ wakati wa hafla ya kumtambulisha Mgombea mwenza wa kiti cha urais, iliyofanyika Jumatatu hii katika ukumbi wa KICC. Wakati wa hafla hiyo ya televisheni, Odinga alimtambulisha Mgombea mwenza Martha Karua huku ‘Extravaganza’ ikicheza nyuma, hatua ambayo bendi hiyo inasema haikuidhinishwa. “Hatukutoa kibali cha wimbo huu kwa kampeni ya Azimio la Umoja walahatukutoa kibali chochote kwa matumizi yake katika kutangaza Mgombea wao wa Makamu wa Rais.” Sauti Sol wamesema hawana misimamo yoyote ya kisiasa na kuahidi kuchukua hatua za kisheria dhidi ya timu inayoongozwa na Odinga kwa kukiuka haki miliki ya bendi hiyo. Hata hivyo Raila Odinga kwa upande wake amesema wimbo huo ulipigwa kwa nia ya kuonesha upendo kwa sababu bendi hiyo imepeperusha bendera ya Kenya  Kimataifa na Wakenya wanawashukuru kwa hilo.

Read More
 CHIMANO WA SAUTI SOL AACHIA RASMI EP YAKE MPYA

CHIMANO WA SAUTI SOL AACHIA RASMI EP YAKE MPYA

Mwanachama wa kundi la Sauti sol, Austin Chimano ameachia rasmi Album yake mpya inayokwenda kwa jina la Heavy is The Crown.. EP hiyo ina jumla ya mikwaju 6 ya moto  ambazo amezifanya bila kumshirisha msanii yeyote. Heavy is The Crown EP ina nyimbo kama Stereo, Mad Love, Loser, Hallelujah, Beautiful Day, Freedom na  inapatikana exclusive kupitia digital platforms mbalimbali za kupakulia na kusikilizia muziki duniani ikiwemo Apple Music na Spotify. Sanjari na hilo tayari picha ya bensol imetumika kama cover ya playlist ya mtandao mkubwa wa kuuza nyimbo duniani,wa Apple Music. Apple wamekuwa na utaratibu wa kuweka cover za Mastaa ambao Ngoma zao zinaongoza kwa Mauzo katika mtandao huo , kwenye Playlist zao mbalimbali.

Read More
 SAUTI SOL WAPINGA UTEUZI WA DKT. EZEKIEL MUTUA KUWA MWENYEKITI WA MAMLAKA INAYOSIMAMIA HAKIMILIKI NCHINI KENYA

SAUTI SOL WAPINGA UTEUZI WA DKT. EZEKIEL MUTUA KUWA MWENYEKITI WA MAMLAKA INAYOSIMAMIA HAKIMILIKI NCHINI KENYA

Wasanii wa Sauti Sol, Bien Baraza na Chimano kwa kauli moja wamepinga uteuzi wa Dakta Ezekiel Mutua kama mwenyekiti wa Mamlaka inayosimamia  Hakimiliki nchini Kenya. Kupitia jumbe walizochapisha kwenye mtandao wa Instagram wasanii hao wameonekana kutofurahisha na kitendo cha Mutua kupewa wadhfa huo huku wakisema kuwa hawana imani na uongozi wake ikizingatiwa kuwa alishinda kuiboresha sekta ya filamu kipindi anahudumu kama mwenyekiti wa Bodi ya filamu. Kauli yao imekuja mara baada ya dakta Ezekiel mutua kusema kwamba anafuraha kurejea kwenye sekta ya muziki kama mwenyekiti wa Mamlaka inayosimamia hakimiliki nchini ambapo aliahidi kuwapigania wasanii wa Kenya hadi pale muziki wao utakapowaingiza kipato kwani  muziki ni ajira kwa vijana kwenye mataifa yaliondelea. Utakumbuka Daktari Mutua alihudumu kama afisa mkuu mtendaji katika bodi ya filamu nchini (KFCB) kati ya mwaka 2015 na 2021, ambapo alichukiwa na wengine kwa kujaribu kulainisha kazi za sanaa na maadili nchini. Muda wake katika bodi hiyo ulifikia kikomo mwezi Agosti mwaka 2021 baada ya tume ya kupambana na ufisadi nchini kuanzisha uchunguzi dhidi yake na mmoja wa wanachama wa bodi ya filamu kwa kupokea marupurupu na mishahara kwa njia isiyofaa.

Read More
 BIEN WA SAUTI SOL ATANGAZA KUWEKEZA ZAIDI KWENYE ISHU YA KUFANYA KOLABO NA WASANII WENGINE KAMA MSANII UHURU

BIEN WA SAUTI SOL ATANGAZA KUWEKEZA ZAIDI KWENYE ISHU YA KUFANYA KOLABO NA WASANII WENGINE KAMA MSANII UHURU

Msanii wa Sauti Sol, Bien amefunguka na kudai kwamba mwaka huu atajikita zaidi kwenye suala la kufanya kolabo na kuwashirikisha wasanii wengine kwenye kazi zake atakazo achia. Katika mahojiano na mpasho Bien amesema kuwa amepokea maombi nyingi za wasanii wanaotaka kufanya naye kazi huku akidokeza ujio wa album mpya ya kundi la Sauti Sol ambayo itaingia sokoni mwezi Aprili mwaka wa 2022. Kauli ya Bien inakuja wakati kundi la Sauti Sol linajianda kufanya ziara yao ya kimuziki  Barani Ulaya kuanzia Aprili Mosi, mwaka huu huko Barcelona nchini Uhispania na itafanyika ndani ya miji 19 kwa kipindi cha mwezi mmoja.. Ziara hiyo inatarajiwa kuzunguka kwenye miji mbalimbali nchini Ujerumani, Ureno, Ufaransa, Denmark, Uingereza, Belgium ambapo kilele chake kitakuwa nchini Uholanzi Juni 28 mwaka wa 2022.

Read More
 SAUTI SOL WAZINDUA JUKWAA LA SOL KIDS LITAKALOWAPA WATOTO ELIMU KUPITIA VITABU VYA HADITHI

SAUTI SOL WAZINDUA JUKWAA LA SOL KIDS LITAKALOWAPA WATOTO ELIMU KUPITIA VITABU VYA HADITHI

Kundi la Sauti Sol limezindua rasmi jukwaa la watoto liitwalo Sol Kids Kenya, ambalo linalenga kuja na vitabu vya watoto vitakavyowaelimisha kuhusu haki zao, kujilinda na ujuzi wa kujieleza. Kupitia ukurasa wao wa Instagram  Sauti Sol wamesema jukwaa hilo la mtandaoni litatoa mchango mkubwa katika kuboresha elimu miongoni mwa watoto kwa kutoa vitabu vya vya hadithi na mashairi vitakavyowasaidia kujenga kumbukumbu, uelewa, na kupata ujuzi wa kutatua matatizo. Wakali hao wa ngoma ya Suzzana wamesema wameamua kuja na wazo la Sol kids kutokana na kukosekana kwa jukwaa maalumu linaloshughulikia vitabu vya watoto jambo ambalo limepelekea baadhi ya watoto kumaliza shule bila ya kuwa na uwezo wa kusoma na kuandika. Mbali na hayo member wa sauti sol, Fancy Fingers maarufu kama Polycarp Otieno alipata fursa ya kuzindua kitabu chake cha pili kiitwacho lala land baada ya written in the stars ya mwaka wa 2021 ambayo ni mahsusi kwa ajili ya watoto kujifunza ili kuongeza maarifa. Kitabu chicho cha hadithi  kinapatikana kwenye majukwaa kadhaa ya kuuza vitabu mtandaoni ikiwemo App ya Sauti Sol iitwayo Hustle sasa kwa shillingi 999 za Kenya.

Read More
 SAUTI SOL WAINGIA UBIA WA KUFANYA KAZI NA SHAHARA, JUKWAA LINALOWALENGA WATENGENEZA MAUDHUI MTANDAONI

SAUTI SOL WAINGIA UBIA WA KUFANYA KAZI NA SHAHARA, JUKWAA LINALOWALENGA WATENGENEZA MAUDHUI MTANDAONI

Kundi la Sauti sol limeingia ubia wa kufanya kazi na jukwaa la Shahara lilowapa fursa watengeneza maudhui kutangaza kazi zao za ubunifu kwa njia ya mtandao. Sauti sol wamethibitisha taarifa hiyo njema kwa mashabiki wao kupitia ukurasa wao wa Instagram kwa kushare picha wakiwa wanatia saini mkataba wa maelewano na Shahara huku wakieleza furaha yao ya kujiunga na familia ya Shahara ambayo imekuja na mpango wa kuwasaidia watengeneza maudhui kunufaika na kazi zao za sanaa. Wakali wa ngoma ya “Suzzana” wamesema Shahara itawapa nafasi wanaounda mahudhui kumiliki kazi zao za ubunifu sambamba na kuwafungulia njia ya kuwafikia watu wengi zadi huku wakipata kipato kupitia maudhui wanayopakia kwenye mtandao huo tofauti na majukwaa mengine. Kwa sasa Sauti Sol watatakiwa kutangaza huduma za Shahara kwa mashabiki zake ambao ni wabunifu kupitia mitandao ya kijamii kwa lengo la kuiongeza jukwaa hilo idadi kubwa ya watengeneza maudhui watakaochapisha kazi zao kwa njia ya mtandao.

Read More
 SAUTI SOL KUANZA ZIARA YA KIMUZIKI BARANI ULAYA MWEZI APRILI 2022

SAUTI SOL KUANZA ZIARA YA KIMUZIKI BARANI ULAYA MWEZI APRILI 2022

Kundi la muziki nchini Sauti Sol limetangaza ujio wa ziara yao ya kimuziki  Barani ulaya kwa kuanika mkeka wa mataifa ambayo watafanya shows. Kupitia ukurasa wao rasmi wa instagram Sauti Sol, wameipa ziara hiyo jina la Sauti Sol  Europe Tour na itaanza Aprili Mosi, mwaka wa 2022 huko Barcelona nchini Uhispania na itafanyika ndani ya miji 19 kwa kipindi cha mwezi mmoja.. Ziara hiyo inatarajiwa kuzunguka kwenye miji mbalimbali nchini Ujerumani, Ureno, Ufaransa, Denmark, Uingereza, Belgium ambapo kilele chake kitakuwa nchini Uholanzi Juni 28 mwaka wa 2022.

Read More
 BIEN BARAZA WA SAUTI SOL ATANGAZA KUACHA KUTUMIA MITANDAO YA KIJAMII

BIEN BARAZA WA SAUTI SOL ATANGAZA KUACHA KUTUMIA MITANDAO YA KIJAMII

Mwanamuziki mahiri wa kundi maarufu la muziki kutoka nchini Kenya ‘Sauti Sol’ Bien-Aime Baraza ametangaza kubadilisha mfumo wa matumizi yake ya mitandao ya kijamii, kutokana na kile alichodai kuwa mitandao hiyo ni sawa na sehemu ya sumu. Bien ameutumia ukurasa wake wa mtandao wa twitter kubainisha dhamira yake ya kuacha mitandao baada ya kutafakari maisha yake kwa muda mrefu. “Baada ya kujitazama kwa muda mrefu kwenye kioo, nimeamua kubadili njia zangu. Mtandao ni mahali pa sumu sana na ninataka tu kuchukua hatua, Kuna tabia nyingi ambazo nilizichukua na mwaka huu naziacha, Nataka tu kupumzika na kurudi nyuma,” alisema. Hitmaker huyo wa “Mbwe Mbwe” amesema kuwa anajua mchakato wa mabadiliko hautakuwa rahisi, lakini amejipanga kwa safari ndefu inayokuja na kukiri kufikia hatua ya kuacha hata matumizi ya vileo. Kufuatia uamuzi wa nyota huyo, aliungwa mkono na watu mbali mbali licha ya kuwepo kwa waliompinga kiasi cha kubashiri kuwa hatoweza kutekeleza mpango hu .

Read More
 BIEN WA SAUTI SOL ATOA OFA  KWA YEYOTE ATAKAYEMREJESHEA SIMU YAKE ILIYOIBIWA

BIEN WA SAUTI SOL ATOA OFA KWA YEYOTE ATAKAYEMREJESHEA SIMU YAKE ILIYOIBIWA

Member wa Sauti Sol, Bien ameahidi kutoa ofa ya shillingi elfu 50 kama zawadi kwa yeyote atakayemrudishia simu yake ambayo juzi kati iliibiwa katika ukumbi wa burudani wa Carnivore kwenye onesho la NRG Wave Concert. Kupitia ukurasa wake wa Twitter Bien ameandika ujumbe wa masikitiko kwa kusema kwamba aliibiwa simu aina ya Infinix Note 11 Pro na vifunguo vya gari aina ya Porsche Cayenne ambapo amedai kuwa simu yake ilikuwa na data muhimu ya album mpya ya Sauti Sol ambayo inatarajiwa kuingia sokkoni mwezi Aprili mwaka huu. Hitmaker huyo wa “Mbwe Mbwe” ameenda mbali zaidi na  kutania kuwa hangekaa vibaya watu wangemuibia hata mke wake Chiki Kuruka huku akisisitiza kutoa zawadi ya shillingi elfu 50 kwa yeyote atakayemrudhishia simu pamoja na vifunguo vya gari. Sanjari na hilo msanii Ndovu Kuu amethibitisha kuibiwa simu kwenye onesho la NRG Wave Concert lilofanyika katika ukumbi wa Carnivore ambapo pia ameahidi kutoa zawadi kwa yeyote atakayemregeshea simu yake.

Read More