Sauti Sol Washukuru Mashabiki Baada ya Mafanikio ya Sol Fest 2025
Kundi la muziki kutoka Kenya, Sauti Sol, limewashukuru mashabiki na wadau mbalimbali waliojitokeza kwa wingi na kuunga mkono tamasha lao la Sol Fest 2025, licha ya kuwepo kwa ushindani mkali kutoka kwa tamasha la msanii Asake kutoka Nigeria. Kupitia Insta Story yao, Sauti Sol wameeleza shukrani zao kwa mashabiki kwa kujitokeza kwa wingi na kuupa tamasha hilo mvuto mkubwa, wakisema mashabiki walionekana kupendeza na waliufanya tukio hilo kuwa la kubwa zaidi. Tamasha hilo lilifanikiwa kuuza tiketi zote, ambazo zilikuwa zikipatikana kwa bei ya takribani KSh 1,500 na KSh 25,000, hatua iliyoonesha wazi upendo mkubwa kutoka kwa mashabiki wao. Sol Fest 2025 ilianza Desemba 18 na kukamilika Desemba 20, 2025, ikifanyika katika Bustani ya Uhuru, Nairobi. Tamasha hilo lilivutia maelfu ya mashabiki na kuwashirikisha mastaa wa muziki kutoka Kenya akiwemo Bensoul, Nviiri The Storyteller, Khaligraph Jones, Nameless, Jua Cali, Sanaipei Tande, pamoja na wasanii wengine wengi waliotoa burudani kwa siku tatu mfululizo.
Read More