Polisi Kigoma Wakanusha Taarifa za Msanii Shilole Kupata Ajali

Polisi Kigoma Wakanusha Taarifa za Msanii Shilole Kupata Ajali

Jeshi la Polisi Mkoa wa Kigoma limekanusha rasmi taarifa zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii, hasa TikTok, zikidai kuwa msanii wa muziki Shilole alipata ajali ya gari na kujeruhiwa akiwa safarini kutoka Mkoa wa Kigoma kuelekea Mkoa wa Dodoma. Katika taarifa kwa umma, Polisi wamesema kuwa hakuna taarifa yoyote ya ajali hiyo iliyowasilishwa katika kituo chochote cha Polisi mkoani Kigoma. Polisi wameeleza kuwa taarifa hizo ni za upotoshaji na hazina uthibitisho wa mamlaka husika. Aidha, Jeshi la Polisi Mkoa wa Kigoma limemshauri msanii Shilole kufika katika kituo chochote cha Polisi na kutoa taarifa endapo ajali hiyo ilitokea, ili uchunguzi wa kina uweze kufanyika na hatua stahiki kuchukuliwa. Awali, taarifa hizo za mitandaoni zilidai kuwa gari aina ya Toyota Alphard aliyokuwa akisafiria msanii huyo, ambalo namba zake za usajili hazikufahamika, liligonga ng’ombe katika eneo la Maragalasi wilayani Uvinza na kusababisha ajali hiyo.

Read More
 Msanii Shilole Anusurika Ajali Mbaya ya Gari Akiwa Njiani Kutoka Kigoma

Msanii Shilole Anusurika Ajali Mbaya ya Gari Akiwa Njiani Kutoka Kigoma

Msanii na mjasiriamali kutoka Tanzania, Shilole, amenusurika katika ajali mbaya ya barabarani iliyotokea usiku wa kuamkia jana katika eneo la Malagarasi, mkoani Kigoma, alipokuwa safarini akirejea Dodoma akitokea Kigoma. Kwa mujibu wa taarifa zilizothibitishwa na Mbunge wa Kigoma Mjini, Cleyton Chipando maarufu Baba Levo, Shilole alikuwa akitumia gari aina ya Toyota Alphard lililogonga ng’ombe barabarani, hali iliyopelekea ajali hiyo kutokea. Mbunge huyo ameeleza kuwa Shilole kwa sasa anaendelea kupata matibabu mkoani Tabora, huku juhudi zikiendelea kuhakikisha anapatiwa huduma zote muhimu za kitabibu. Shilole alikuwa miongoni mwa watu waliofanikisha shughuli ya Pilau Day iliyoandaliwa na Mbunge wa Kigoma Mjini kupitia mgahawa wake wa Shishi Food, ikiwa ni sehemu ya sherehe za Mwaka Mpya zilizofanyika mjini Kigoma.

Read More
 Shilole Awatolea Uvivu Wenye Chuki Baada ya Kushinda Tuzo ya ZIKOMO 2025

Shilole Awatolea Uvivu Wenye Chuki Baada ya Kushinda Tuzo ya ZIKOMO 2025

Msanii na mjasiriamali kutoka Tanzania, Shilole, amepokea rasmi tuzo ya ZIKOMO kupitia kipengele cha Tuzo Bora ya Biashara Ndogo ya Mwaka 2025. Katika ujumbe wake wa shukrani alioutoa kupitia mitandao ya kijamii, Shilole ameonyesha furaha kubwa na kuwatolea uvivu wakosoaji wake. Amesisitiza kuwa chuki na maneno ya kubeza hayamzuii kufikia malengo yake, bali huona ni aina ya upendo unaompa nguvu ya kuendelea kupambana. Shilole amewashukuru mashabiki wake kwa sapoti na upendo mkubwa, akisema hajawahi kuchoka kupokea mapenzi yao wala kutoa shukrani zake. Lakini pia, amemshukuru Mungu kwa neema hiyo na kupongeza waandaaji wa tuzo za ZIKOMO kwa kumpa heshima hiyo. Katika ujumbe wake, Shilole ameeleza kuwa tuzo hiyo ni hatua muhimu kuelekea ndoto yake ya kukuza biashara ndogo kuwa biashara kubwa siku za usoni. Amesisitiza kuwa sapoti ya mashabiki na wadau ndiyo nguzo ya mafanikio yake.

Read More
 Shilole Asema Kuchomwa kwa  Mgahawa Wake  Zimeongeza Ari ya Mapambano

Shilole Asema Kuchomwa kwa  Mgahawa Wake Zimeongeza Ari ya Mapambano

Msanii wa muziki na mjasiriamali kutoka Tanzania, Shilole, amefunguka kuhusu tukio la kusikitisha la kuchomwa kwa mgahawa wake, Shishi Food, wakati wa machafuko yaliyojitokeza katika kipindi cha uchaguzi nchini Tanzania. Akizungumza na waandishi wa habari, Shilole amesema licha ya hasara kubwa aliyopata, hana chuki wala kinyongo dhidi ya waandamanaji waliohusika na uharibifu huo. Kwa mujibu wake, waandamanaji hao ni wananchi waliokuwa wamechoka na hali mbalimbali, hivyo haoni sababu ya kuwachukia. Msanii huyo ameeleza kuwa tukio hilo limezidisha ari yake ya kupambana na kusimama imara zaidi. Amesema yeye ni kijana mpambanaji na changamoto hiyo imempa nguvu mpya ya kuendelea kujijenga upya na kusonga mbele katika maisha na biashara. Shilole ameongeza kuwa licha ya maumivu ya kupoteza alichokijenga kwa jasho, hawezi kukata tamaa, akisisitiza kuwa bado ana ndoto kubwa na dhamira ya kufanikiwa zaidi.

Read More
 Wasanii wa Tanzania Wapata Hasara Kubwa Baada ya Maandamano

Wasanii wa Tanzania Wapata Hasara Kubwa Baada ya Maandamano

Maandamano makubwa yaliyolenga kupinga kile kinachoelezwa kuwa udhalimu wa serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) nchini Tanzania, yamegeuka kuwa janga kwa baadhi ya wasanii wa Bongofleva, baada ya biashara zao kuripotiwa kushambuliwa, kuvunjwa na kuchomwa moto na waandamanaji wenye hasira. Jijini Dar es Salaam, mgahawa maarufu wa Shishi Food, unaomilikiwa na msanii wa muziki Shilole, umeungua moto vibaya usiku wa kuamkia leo. Tukio hilo linadaiwa kufanywa na kundi la waandamanaji waliokuwa wakilenga biashara na mali zinazohusishwa na mastaa wanaoonekana kuunga mkono kuchaguliwa tena kwa Rais Samia Suluhu Hassan. Shilole, ambaye kwa muda mrefu amekuwa akionyesha uhusiano wa karibu na serikali, amekumbwa na hasara kubwa kutokana na tukio hilo. Mashuhuda wanasema moto ulianza ghafla baada ya kundi la vijana kuvamia mgahawa huo, wakipiga kelele za kuipinga serikali. Hasara hiyo pia imewapata wasanii wengine akiwemo Billnass, ambaye duka lake limechomwa moto, na Jux, ambaye duka lake limevunjwa na kuporwa mali ikiwemo nguo na vifaa vya thamani. Wakati huo huo, Makjuice Sinza, biashara inayomilikiwa na watu wa karibu na tasnia ya burudani, imeripotiwa kuharibiwa na kuporwa.

Read More
 SHILOLE AWATOLEA UVIVU WANAUME WANAOPENDA KUJIREMBA

SHILOLE AWATOLEA UVIVU WANAUME WANAOPENDA KUJIREMBA

Mwanamuziki na mjasiriamali kutoka Tanzania Shilole amewachana baadhi ya wanaume wa mjini ambao wanapenda sana kujiremba kupita kiasi. Katika mahojiano na Refresh ya Wasafi TV Shilole amewataka wanaumme wa sampuli hiyo kuacha hulka ya kuiga watoto wa kike kwa sababu wanajaribu kushindana na wanawake katika jamii. Lakini pia mwanamama huyo ametoa changamoto kwa wanaume kujituma katika maisha badala ya kushiriki mapenzi ya jinsia moja kwa ajili ya kujipatia kipato. Hata hivyo haijabainika ni kitu gani kilimpelekea mwanamuziki huyo wa Bongofleva kuibua madai hayo ila walimwengu kwenye mitandao wanadai anatengeneza mazingira ya kuzungumziwa katika vyombo vya habari.

Read More