Stevo Simple Boy Aachia Diss-Track kwenda kwa Mchekeshaji Eric Omondi

Stevo Simple Boy Aachia Diss-Track kwenda kwa Mchekeshaji Eric Omondi

Msanii Stevo Simple Boy ameachia wimbo uitwao ‘ Haya basi ‘ ambapo ameeleza manyanyaso aliyoyapitia kwenye shoo ambayo alishindwa kutumbuiza huko Mombasa. Kwenye wimbo huo, Stevo amemtolea uvivu mchekeshaji Eric Omondi kwa kupendekeza autimue uongozi wake wa Men In Business. ” Naskia walisema nifute manager kumbe hao ndio mateja wanajifanya huku nyuma wananipenda na kumbe hao hao ndio wananisema.” Stevo Simple Boy ameeleza namna ambavyo Eric Omondi alikuwa anamshinikiza kutoa burudani kwa mashabiki zake bila malipo kwenye tamasha la Sofire fiesta ” Ati Simple kuja show nitakulips baada ya show nakula matumbo, wakaleta zogo.” Msanii huyo amedai kuwa Eric Omondi alitumia sakata lake la kutolipwa na waandaaji wa Sofire fiesta kutafuta kiki ili azungumziwe kwenye mtandaoni ya kijamii. ” Naskia kiki, naskia simple kwenye basi, haya basi, napigwa picha Hadi nikikunywa Maji, naskia vitu mingi Yule Rais ni wa nini?” Utakumbuka Mwishoni mwa mwezi Desemba 2022, Stivo Simple Boy alifichua kwamba alishindwa kutumbuiza huko Mombasa baada ya waandaji wa sofire fiesta kukataa kumlipa pesa zake kabla ya kutoa burudani kwa mashabiki zake. Kitendo hicho kilimkasirisha Eric Omondi ambaye alikashifu  uongozi wa Stevo akiulaumu kwa masaibu yaliyompata mwanamuziki huyo. Omondi  alidai kuwa mameneja hao walizembea kwenye kazi yao kwa kumpeleka Stevo Mombasa bila mpangilio wowote ambapo alienda mbali na kupendekeza wajiuzulu.

Read More
 Sakata la msanii Stevo Simple Boy na waandaaji wa Sofire Fiesta lachukua sura mpya

Sakata la msanii Stevo Simple Boy na waandaaji wa Sofire Fiesta lachukua sura mpya

Mwakilisha wa tamasha la SoFire Fiesta amejibu malalamishi ya msanii Stevo Simple Boy ya kutolipwa kwenye show huko Mombasa Kwenye mkao na wanahabari amethibitisha kuwa Stevo alipewa nafasi ya kutoa buradani kwenye shoo hiyo lakini hakufanikiwa kufanya hivyo kutokana na uongozi wake kuwa kizingiti. Aidha amesema kuwa hakuwa anasimamia wasanii wa Kenya kwenye masuala ya malipo kwa kuwa alikuwa na majukumu mengine ya kuhakikisha wasanii wa kigeni wanalipwa kwa wakati unaofaa. Hata hivyo amesema hawakuwa na mkataba wa kufanya kazi na stevo licha ya kumpa nafasi kutumbuiza kwenye shoo hiyo huku akisisitiza kuwa wangemlipa pesa zake iwapo angepanda jukwaani kuwapa mashabiki waliohudhuria burudani. Kauli yake hiyo imezua maswali mengi miongoni mwa wa Kenya kama ilivyotakiwa huku wakionyoshea kidole cha lawama mapromota kwa kuwapa kipau mbele wasanii wa kigeni huku wakiwachukulia poa wasanii wa ndani.

Read More
 Stevo Simple Boy amfuta kazi meneja wake kwa tuhuma za wizi na usaliti

Stevo Simple Boy amfuta kazi meneja wake kwa tuhuma za wizi na usaliti

Msanii Stevo Simple Boy amemtimua meneja wake mmoja kwenye uongozi wake wa Men In Business baada ya sakata la kukosa kutumbuiza kwenye shoo ya SolFire Fiesta huko Mombasa. Kupitia video aliyoposti Instagram amesema amechukua hatua hiyo kutokana na usaliti wa meneja ambaye anadaiwa alishirikiana na wandaji kumtapeli pesa zake. Hata hivyo amewahakikisha mashabiki zake kuwa kila kitu kipo shwari kati yake na mameneja wake wawili waliosalia, hivyo watarajie mambo mazuri kutoka kwake mwakani. Kauli yake imekuja mara baada ya uongozi wake kupuzilia mbali madai ya Mchekeshaji Eric Omondi kuwa walishinda kumkingia kifua Stevo alipwe pesa zake kabla ya kutumbuiza kwenye tamasha la SolFire Fiesta. Kwenye mkao na waandishi wa habari uongozi wake ulisema madai ya Omondi hayana ukweli wowote, wakimtaja kuwa msaliti kutokana na kitendo chake cha kuwashinikiza wamruhusu Stevo atokee kwenye shoo kabla ya malipo.

Read More
 Eric Omondi afunguka baada ya Stevo Simple Boy kukosa kutumbuiza kwenye tamasha la SolFire Fiesta.

Eric Omondi afunguka baada ya Stevo Simple Boy kukosa kutumbuiza kwenye tamasha la SolFire Fiesta.

Mchekeshaji Eric Omondi amewatolea uvivu mameneja wa msanii Stevo Simple Boy kwa kushinda kumkingia kifua msanii huyo alipwe pesa zake kabla ya kutumbuiza kwenye tamasha la SolFire Fiesta. Kupitia instastory yake mchekeshaji huyo ameandika ujumbe wa masikitiko kwenda kwa uongozi wa Stevo ambao kwa mujibu wake ulitumia kiasi cha shilling 84,000 kwa chakula huku wakimuacha msanii huyo akiwa hajalipwa chochote. Aidha ametaka uongozi wa Men In Business kujiuzulu mara moja la sivyo atahakikisha wanafungulia mashataka ya utapeli huku akihoji ni kwa nini Stevo Simple Boy anasimamiwa na mameneja wanne tofauti na wasanii wengine. Kauli ya Omondi imekuja siku moja baada ya stevo na uongozi wake kutoa taarifa kwa umma wakieleza ghadhabu zao kwa waandaji wa SolFire Fiesta kwa kushindwa kutoa malipo yote kabla ya Stevo kupanda jukwaani.

Read More
 Stevo Simple Boy afunguka sababu za kususia show ya Mombasa

Stevo Simple Boy afunguka sababu za kususia show ya Mombasa

Msanii Stevo Simple Boy amewaomba radhi mashabiki zake baada ya kukosa kutumbuiza kwenye tamasha la So Fire Fiesta lilofanyika Nyali, Kaunti ya Mombasa. Kupitia taarifa aliyotoa kupitia ukurasa wake wa Instagram amewalaumu waandaji wa tamasha hilo kwa kushindwa kumlipa pesa zake kabla ya kupanda jukwaani. “Naomba msamaha kwanza kwa mashabiki wangu na kushukuru management yangu MIB Africa mumejaribu Kadri wa uwezo wenu na mnapigania Sana kuniona juu kila wakati..Tunajaribu Sana kama wasani ila wakenya wenzetu ndo wanatudhulumu”, Alisema. Stevo ambaye alikuwa alipaswa kutumbuiza kwenye show hiyo ambaye Ruger wa Nigeria alikuwa msanii kinara amesema kitendo cha kususia kupanda jukwaani kulimpelekea kufungiwa hoteli aliyokuwa amekodishwa na waandaji wa So Fire Fiesta. “Tulifungiwa hotelini kwa sababu tumekataa kuperfom bila kulipwa na kampuni ya sofire fiesta Ni tendo ambalo limenifika kooni kama Msanii na imenikataa moyo Sana ila sikati tamaa kabisa ntazidii kupambana na nawapenda sana wakenya wanao ni support.”, Aliongeza. Hata hivyo mashabiki wamechukizwa na hatua ya waandaji wa So Fire Fiesta kutaka kumdhulumu Stevo Simple Boy huku wakionekana kumnyoshea kidole cha lawama mchekeshaji Eric Omondi kwa masaibu yaliyompata msanii huyo kwa kusema kuwa huenda alishirikiana na wasimamizi wa tamasha hilo kumfanyia mchezo mchafu.

Read More
 Ruger amkataa Stevo Simple Boy

Ruger amkataa Stevo Simple Boy

Hitmaker wa “Girlfriend”, Msanii Ruger amemkataa hadharani Stevo Simple Boy baada ya kuulizwa na waandishi wa habari kama ana wimbo wa pamoja na msanii huyo wa Men In Business. Ruger ambaye yupo nchini kwa ajili ya shughuli zake za kimuziki amesema hamjui kabisa msanii huyo huku akithibitisha ujio wa ngoma yake na kundi la Sauti Sol ambayo itapatikana kwenye album yake mpya mwakani. Utakumbuka juzi kati Eric Omondi alithibitisha ujio wa kolabo ya Stevo Simple Boy pamoja na msanii huyo kutoka nchini Nigeria mara tu atakapotua nchini. “At this rate wacha sisi tutengeneze Pesa watu ni Viziwi hawaskii maneno. The only Event happening in Mombasa this December. 28th December Wild waters. Na Stivo Somple boy ashajishindia Collabo na Ruger. GET YOUR TICKETS from my BIO @sofire_53 @sofire_fiesta”, Aliandika Instagram Ruger anatarajiwa kutoa burudani leo kwenye tamasha la So Fire Fiesta litakalofanyika Nyali, Mombasa.

Read More
 Stevo Simple Boy akiri hana mpenzi kwa sasa

Stevo Simple Boy akiri hana mpenzi kwa sasa

Hitmaker wa “Freshi Barida”, Msanii Stevo Simple Boy ameweka wazi kuwa kwa sasa hana mpenzi na anafurahia maisha yake mapya Msanii wa huyo wa Men in Business ameweka wazi hilo kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo amefungua milango kwa waliokuwa wanamumezea mate kujaribu bahati yao. “Mapenzi ya siku hizi jamani, sasa niko single naenjoy. Jamani kua single raha, akinipenda baba na mama inatosha, lakini ata mnivunje roho na mbavu, nikipata mwingine napenda tena”, Ameandika. Kauli ya Stevo Simple Boy imekuja siku chache baada ya kuvunjika kwa mahusiano yake na mchumba wake Gee, mahusiano ambayo yalidumu kwa kipindi cha miezi sita.

Read More
 Penzi la Stevo Simple Boy na Jenny Wangui lavunjika rasmi

Penzi la Stevo Simple Boy na Jenny Wangui lavunjika rasmi

Mahusiano ya Stevo Simple Boy na Mrembo Jenny Wangui yamefika mwisho ikiwa ni miezi miwili tangu wawili hao waanze kuchumbiana. Stevo amefuta picha zote akiwa na mrembo huyo kwenye ukurasa wake wa Instagram siku chache baada ya watumiaji wa mtandao wa Tinder kuibua madai kuwa Jenny Wangui ana akaunti kwenye mtandao huo wa kuwatafuta wapenzi. Utakumbuka jana Jenny Wangui aliibuka na kudai kuwa hakuwahi toka kimapenzi na mkali huyo wa Ngoma ya “Freshi Barida” kwa kuwa mahusiano yao yalikuwa ya kuigiza kwa ajili ya kuutangaza muziki wa Stevo Simple Boy.

Read More
 Gee amuumbua Stevo Simple Boy “Tulipanga tufanye KIKI, Hatuna mahusiano”

Gee amuumbua Stevo Simple Boy “Tulipanga tufanye KIKI, Hatuna mahusiano”

Kama ulidhani mahusiano ya Stevo Simple Boy na Gee yalikuwa ya kweli ni kuambie tu pole, kwa sababu mrembo huyo amejitokeza hadharani na kukiri kuwa hajawahi toka kimapenzi na msanii huyo kama watu wengi wanavyochukulia mtandaoni. Gee ambaye amekuwa akideka sana juu ya huba la Stevo Simple Boy kiasi cha kuwatishia wanawake kutomchumbia hitmaker huyo wa Wedding Day, amesema mahusiano yao yalikuwa ni kiki kwa ajili ya kuutangaza muziki wa Stevo Simple Boy. Hata hivyo kauli ya mrembo huyo imeonekana kuwakera watumiaji wengi wa mitandao ya kijamii ambao wametoa changamoto kwa wasanii kutoa muziki mzuri badala ya kuishi maisha ya kuigiza mtandaoni. Utakumbuka mapema mwaka huu baada ya Stevo Simple Boy kumtambulisha Gee kama mpenzi wake na kumvisha pete ya uchumba alienda mbali zaidi na kuwaaminisha walimwengu kuwa wao ni mume na mke walipofanya harusi ya kitamaduni maarufu kama Ruracio kwa siri.

Read More
 STEVO SIMPLE BOY AFUNGA NDOA YA KITAMADUNI NA MCHUMBA WAKE JENNY WANGUI

STEVO SIMPLE BOY AFUNGA NDOA YA KITAMADUNI NA MCHUMBA WAKE JENNY WANGUI

Msanii Stivo Simple Boy amefunga ndoa ya kitamudani maarufu kama Ruracio na mchumba wake Jenny Wangui ikiwa ni miezi kadhaa tangu amvishe pete ya uchumba. Kupitia ukurasa wake wa instagram Stivo ameposti ujumbe mrefu wa mahaba kwa mrembo huyo na kusema kwamba amechukua maamuzi hayo kama njia ya kuwathibitishia wazazi wa Jenny Wangui kuwa hafanyi mzaha katika mahusiano yake bali ameamua kwa kauli moja kuingia kwenye maisha ya ndoa. Hitmaker huyo “Freshi Barida” ambaye amepongezwa na mashabiki zake kwa hatua hiyo kubwa maishani, amemuondolea hofu mpenzi wake kwa kumueleza kuwa penzi lake ni la kweli, hivyo asitishwe na watu mitandaoni. Hii ni baada ya mwanamke mmoja kujitokeza na kudai kuwa amemzia kimapenzi Stivo the Simple Boy, kitendo kilichomfanya gee kuwa na wasi wasi juu ya hatma ya mahusiano yake na msanii huyo wa Men in Business.

Read More
 STIVO AKANUSHA TUHUMA ZA KUKIMBIA NA MCHUMBA WA MTU

STIVO AKANUSHA TUHUMA ZA KUKIMBIA NA MCHUMBA WA MTU

Msanii Stivo Simple Boy kwa mara ya kwanza amefunguka kuhusu tuhuma za kumuibia rapa Rapdon mpenzi wake. Katika mahojiano yake ameonyosha maelezo kuhusu na madai hayo kwa kusema kwamba madai hayo hayana ukweli wowote na yameibuliwa rapa huyo kwa ajili ya kujitengenezea mazingira ya kuzungumzia kwenye mitandao ya kijamii. Hitmaker huyo wa “Freshi Barida” amesema uhusiano wake na mpenzi wake ni wa kweli na sio kiki kama namna watu wanavyochukulia mitandaoni. Sanjari na hilo mpenzi wa Stivo amepuzilia mbali madai ya kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na rapa don kwa kusema walikuwa marafiki kipindi cha nyuma ila hajawahi toka kimapenzi. Kauli yao imekuja mara baada ya rapa Rapdon kujitokeza wazi wazi na kudai kuwa Stivo Simple Boy alimvunjia heshima kwa hatua ya kumunyanganya mpenzi wake.

Read More
 STEVO SIMPLE BOY ATAJWA KUWANIA TUZO ZA ZIKOMO

STEVO SIMPLE BOY ATAJWA KUWANIA TUZO ZA ZIKOMO

Msanii wa Men In Business, Stevo The Simple Boy ametajwa kuwania vipengele viwili katika Tuzo za Kimataifa za Zambia ziitwazo Zikomo Awards. Stevo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na video ya wimbo wake “Fresh Barida”, anawania tuzo hizo kupitia vipengele vya BEST UPCOMING ARTIST OF THE YEAR na BEST SONG OF THE YEAR. Kumpigia kura Stevo The Simple Boy ni rahisi, ingia kwenye tovuti ya tuzo hizo http://www.zikomoawards.com kisha nenda kwenye category iliyoandikwa Music & Film, baada ya hapo unamu-nominate.

Read More