STEVO SIMPLE BOY AMTOLEA UVIVU EX WAKE PRITTY VISHY KISA MAHARI YA SHILLINGI MILLIONI 2

STEVO SIMPLE BOY AMTOLEA UVIVU EX WAKE PRITTY VISHY KISA MAHARI YA SHILLINGI MILLIONI 2

Msanii Stevo Simple Boy amepuzilia mbali mahari ya shillingi millioni 2 ambayo mpenzi wake wa zamani Pritty Vishy aliweka wazi kwa wanaume wanaotaka kumchumbia. Katika mahojiano na mpasho Stevo amesema mrembo huyo anatumia suala kutafuta mazingira ya kuzungumziwa kwenye mitandao ya kijamii  kwani dhamani yake haiendani na kiwango cha mahari alichodai. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Freshi Barida” ameweka wazi sababu zilizompelekea kuachana na Vishy kwa kusema kwamba mrembo huyo alimsaliti kimapenzi kwa kutoka kimapenzi na wanaume wengine. Hata hivyo amekanusha madai ya Pritty Vishy kuwa amekuwa akimlilia warudiane kwa kusema kwamba  penzi lao lilivunja kitambo na hawezi kumrudia kutokana na tabia zake ambazo hazikumfurahisha hata kidogo. Mbali na hayo msanii huyo ambaye chini ya lebo ya muziki ya Men in Business amedokeza ujio wa tamasha lake la Freshi Barida ambalo linalenga kukuza vipaji vya vijana chini.

Read More
 STEVO SIMPLE BOY APATA HAKIMILIKI YA NEMBO YAKE YA FRESHI BARIDA

STEVO SIMPLE BOY APATA HAKIMILIKI YA NEMBO YAKE YA FRESHI BARIDA

Mwanamuziki Stevo Simple Boy ameripotiwa kusajili jina lake la biashara ambalo ni Freshi Barida. Taarifa hiyo imethibitishwa na lebo ya muziki ya Men In Business kupitia ukurasa wake rasmi wa Instagram ikisema kuwa Stevo kwa sasa ndiye mmiliki halisi wa jina la Freshi Barida kwa mujibu wa sheria ikizingatiwa tayari amepewa hakimiliki za jina hilo na Ofisi ya Patent ya Kenya. Lebo hiyo ambayo inasimamia kazi za Stevo Simple Boy imetoa angalizo kwa atakayetumia nembo hiyo bila ridhaa ya msanii huyo na uongozi wake kwa ajili ya shughuli za kibiashara atachukulia hatua kali za kisheria ambayo itajumuisha kulipa faini. Hii taarifa njema kwa Stevo Simple Boy ambaye juzi kati alizindua bidhaa zake za mavazi za Freshi Barida, siku kadhaa tangu atangaze ujio wa kinywaji chake kiitwacho Freshi Barida Energy Drink.

Read More