AT Amvua Master J Hadhi ya Prodyuza: “Si Mzalishaji Bali Ni Mmiliki wa Studio”

AT Amvua Master J Hadhi ya Prodyuza: “Si Mzalishaji Bali Ni Mmiliki wa Studio”

Msanii wa Bongefleva AT ameibua mjadala mkali katika tasnia ya muziki wa Tanzania baada ya kutoa kauli nzito zinazomvua hadhi Master J kama prodyuza halisi. Kwa mujibu wa AT, Master J si mzalishaji wa muziki bali ni mmiliki wa studio maarufu za MJ Records. Amefafanua kuwa kitaaluma, Master J alisomea masuala ya electronics na sio music production, hivyo uwezo wake unajikita zaidi kwenye upande wa vifaa na ufundi kuliko uandaaji wa muziki. AT ameeleza kuwa ingawa Master J amekuwa na mchango mkubwa kwa sababu ya kumiliki studio na kutoa nafasi kwa wasanii kurekodi, hana ujuzi wa kitaaluma wa kumwezesha kuhesabiwa miongoni mwa maprodyuza wakubwa waliounda historia ya muziki wa Bongofleva. Aidha, AT amefichua kuwa katika moja ya warsha za muziki zilizofanyika nchini Afrika Kusini, Master J aliwahi kushindwa kabisa kuchangia hoja zozote muhimu kuhusiana na studio na uzalishaji muziki, jambo lililomfanya ashuke hadhi mbele ya wenzake. Hata hivyo amempa changamoto Master J kuthibitisha nafasi yake kama prodyuza halisi kwa kuonyesha albamu ambazo amewahi kuzitengeneza yeye mwenyewe kuanzia hatua ya mwanzo hadi mwisho. Kauli ya AT imekuja mara baada ya msanii mkongwe Juma Nature kunukuliwa katika moja ya mahojiano akidai hajawahi kumkubali Master Jay kama producer. Nature alieleza kuwa kipindi cha nyuma Master Jay alitamani kuwa kama P Funk Majani, hali iliyomfanya baba yake mzazi kumnunulia vyombo vya muziki na si kwa ubunifu au kipaji chake binafsi.

Read More
 Kenya Kuandaa Mashindano ya Dunia ya Taekwondo Mwezi Disemba

Kenya Kuandaa Mashindano ya Dunia ya Taekwondo Mwezi Disemba

Kenya itawatumia wachezaji wake wa taekwondo wenye uzoefu katika mashindano ya dunia kwa wachezaji wasiozidi umri wa miaka 21, ambayo yataandaliwa nchini kwa mara ya kwanza katika historia ya mchezo huo. Mashindano hayo ya kimataifa yanatarajiwa kufanyika kuanzia Disemba 3 hadi 6 mwaka huu, katika Uwanja wa Kimataifa wa Kasarani, jijini Nairobi, na kuwavutia zaidi ya wachezaji 3,500 kutoka zaidi ya mataifa 150 duniani. Kwa mujibu wa Shirikisho la Taekwondo nchini, maandalizi ya mashindano hayo yako katika hatua za mwisho, huku tovuti rasmi ya mashindano hayo tayari ikizinduliwa, ikiwa ni jukwaa la kutoa taarifa kwa washiriki na mashabiki kutoka ndani na nje ya nchi. Zaidi ya kuwa jukwaa la michezo, mashindano haya yanatazamiwa kuimarisha sekta ya utalii na kuchangia kwa kiasi kikubwa uchumi wa nchi, sambamba na kuwapa wachezaji wa Kenya nafasi ya kuonyesha vipaji vyao dhidi ya wapinzani wa kimataifa. Timu ya taifa ya Kenya inatarajiwa kuingia kambini rasmi mwishoni mwa mwezi Novemba ili kujiandaa kikamilifu kwa mashindano hayo.

Read More
 iPhone 17 Pro Kutambulishwa Rasmi Kesho Usiku na Apple

iPhone 17 Pro Kutambulishwa Rasmi Kesho Usiku na Apple

Kampuni ya Apple inatarajiwa kuzindua rasmi simu zake mpya za mwaka huu usiku wa kesho, katika hafla maalum itakayofanyika saa 2 usiku kwa saa za Afrika Mashariki. Katika uzinduzi huo, Apple inatarajiwa kuonyesha kwa mara ya kwanza hadharani matoleo mapya ya iPhone 17 Pro na iPhone 17 Pro Max, ambayo yamesemwa kuwa yatakuja na mabadiliko makubwa ya kimwonekano na kiteknolojia, ikilinganishwa na vizazi vya awali vya iPhone. Mbali na matoleo hayo, Apple pia inatarajiwa kutangaza simu mpya kabisa kwa jina iPhone Air aina ambayo haijawahi kuwepo katika familia ya iPhone. Taarifa kutoka kwa wachambuzi wa teknolojia zinasema kuwa iPhone Air huenda ikawa simu nyepesi zaidi kwa uzito, yenye kioo cha kisasa na betri yenye ufanisi mkubwa, ikiwa imelenga kuvutia watumiaji wanaopendelea unyumbufu na muonekano wa kifahari. Sambamba na uzinduzi wa simu hizo, Apple pia itatoa toleo jipya la mfumo wa uendeshaji wa iOS, ambalo litaanza kupatikana kwa watumiaji wote wa iPhone kuanzia iPhone 11 hadi iPhone 16. Maboresho hayo yanatarajiwa kuleta vipengele vipya vya usalama, muonekano, pamoja na utendaji wa hali ya juu unaolenga kuboresha uzoefu wa mtumiaji.

Read More
 Ziza Bafana Akanusha Tuhuma za Kufukuzwa Amsterdam

Ziza Bafana Akanusha Tuhuma za Kufukuzwa Amsterdam

Msanii wa dancehall kutoka Uganda, Ziza Bafana, amenyoosha maelezo kuhusu madai yaliyosambaa mtandaoni kwamba alifukuzwa nchini Uholanzi siku chache zilizopita. Akizungumza na wanahabari, Bafana ameeleza kuwa alikuwa amepangiwa maonyesho mawili mjini Amsterdam na Ujerumani. Hata hivyo, alipowasili Amsterdam aliombwa kuonesha kibali cha kazi, ambacho kwa bahati mbaya hakuwa nacho, na hivyo akazuiliwa kuendelea na ratiba yake. Mkali huyo wa Speed Controlle amesisitiza kuwa hakufukuzwa kama baadhi ya wakosoaji walivyodai kwenye mitandao ya kijamii. Badala yake, amefafanua kuwa tatizo lilitokana na ukosefu wa vibali sahihi vya kazi. Bafana ameilaumu mamlaka za usafiri za Uganda kwa kusababisha kuvurugika kwa shoo zake, akisema uzembe wa maandalizi ya nyaraka muhimu ndio uliosababisha kufutwa kwa maonesho yake yaliyokuwa yakisubiriwa kwa hamu na mashabiki wa kimataifa. Kwa sasa, msanii huyo ameahidi kuchukua hatua kuhakikisha taratibu zote za kisheria zinafuatwa ili kuepusha changamoto kama hizo siku za usoni, huku akiomba mashabiki wake waendelee kumpa sapoti licha ya changamoto alizopitia.

Read More
 Vera Sidika Ajibu Madai ya Kuwatelekeza Watoto Wake

Vera Sidika Ajibu Madai ya Kuwatelekeza Watoto Wake

Socialite maarufu nchini Kenya, Vera Sidika, amejibu tetesi kutoka kwa mashabiki waliodai kwamba amewatelekeza watoto wake kwa sababu ya kuwa safarini mara kwa mara. Kupitia ujumbe alioweka mtandaoni, Vera amesisitiza kuwa watoto wake daima wako chini ya uangalizi wa mzazi kila wakati. Amefafanua kuwa anapohitajika kuwa kwenye shughuli zake binafsi au kuendesha mikusanyiko katika nyumba yake ya kifahari, huomba baba ya watoto wake Brown Mauzo kukaa nao muda wote. Aidha,Mwanamama huyo amesema anaposafiri kwenda maeneo mbalimbali duniani, baba ya watoto hubaki nao nyumbani akisaidiana na wafanyikazi wa ndani (nannies) hadi atakaporudi. Kauli hiyo imekuja baada ya walimwengu kwenye mitandao ya kijamii kuibua maswali kuhusu malezi ya watoto wake, baadhi ya watu wakimlaumu kwa kutokuwa karibu nao kutokana na ratiba zake za mara kwa mara za safari na shughuli za kijamii.

Read More
 Bahati Awatolea Uvivu Wasanii Wanaomtukana Diana B kwa Akaunti Bandia

Bahati Awatolea Uvivu Wasanii Wanaomtukana Diana B kwa Akaunti Bandia

Msanii wa Kenya Bahati ameibuka na kuwatolea uvivu wasanii wanaomtukana mkewe, Diana Marua, kupitia akaunti bandia, akisema wanapoteza muda badala ya kuangazia kazi zao. Kupitia Instagram, Bahati, ameonekana kuguswa na matusi anayopokea Diana, akiwashambulia wanaoendesha chuki hizo kwa kusema kwamba badala ya kutumia nguvu kumshusha Diana, wanapaswa kumuomba ushirikiano wa kimuziki. Bosi huyo wa EMB Records amesisitiza kuwa mafanikio ya mkewe hayawezi kuzimwa na chuki, akiwataka wapinzani wake kubadilisha mbinu. Hii inakuja baada ya Diana kuachia wimbo wake mpya “Bibi ya Tajiri” ambao umeibua gumzo mitandaoni na kupata mapokezi makubwa. Video ya wimbo huo tayari imepata zaidi ya views laki nane ndani ya siku tano pekee tangu kuachiwa, hali inayoonesha kupokelewa vizuri na mashabiki licha ya ukosoaji.

Read More
 Socialite Kate Thuku Asema Wanaume wa Kisasa Hawana Mapenzi ya Kweli

Socialite Kate Thuku Asema Wanaume wa Kisasa Hawana Mapenzi ya Kweli

Socialite chipukizi Kate Thuku ameweka wazi sababu zinazomfanya kwa sasa asiwe kwenye mahusiano ya kimapenzi, akidai kuwa wanaume wengi wa kisasa hawana romance. Akiwa mgeni kwenye podcast ya Prezident Law, Kate alisema anatilia maanani upendo, hisia na kujitolea katika uhusiano. Hata hivyo, kwa mtazamo wake, wanaume wa kisasa wamepoteza ule msisimko na ugunduzi wa kimapenzi unaofanya mahusiano yawe ya kipekee. Kate amefichua pia hapendezwi na wanaume wa mashinani kwa sababu, kwa mtazamo wake, mara nyingi huja na masharti makali yanayomnyima uhuru wake. Badala yake, anatamani mwanaume wa kisasa anayeweza kumfanya ajisikie malkia kupitia vitendo vidogo vya kimapenzi kama kumnunulia maua au hata kumwandikia barua za mapenzi. Kwa sasa, Kate anasisitiza kuwa hana haraka ya kuingia kwenye uhusiano iwapo matarajio yake ya kimapenzi hayatatimizwa, akisema anajipa kipaumbele kujitengenezea furaha na kuendeleza maisha yake binafsi. Kauli yake imezua mazungumzo makubwa mitandaoni, baadhi ya mashabiki wakimpongeza kwa kuweka wazi vigezo vyake, huku wengine wakimkosoa wakisema anatafuta mapenzi ya hadithi za vitabuni ambazo si rahisi kupatikana katika maisha ya kawaida.

Read More
 Mercy Kyallo Akanusha Kuwatapeli Wateja Kupitia Yallo Leather

Mercy Kyallo Akanusha Kuwatapeli Wateja Kupitia Yallo Leather

Mjasiriamali na mdogo wake mtangazaji maarufu Betty Kyallo, Mercy Kyallo, ameweka wazi kilichosababisha sintofahamu kuhusu ucheleweshaji wa oda za bidhaa zake maarufu za ngozi chini ya brand yake ya Yallo Leather. Kupitia Instagram, Mercy ameeleza kuwa changamoto hiyo imetokana na wazalishaji wawili wakuu wa malighafi kufunga biashara, jambo lililosababisha upungufu wa vifaa muhimu na hivyo kusababisha mkwamo wa uzalishaji. Mrembo huyo amehakikishia wateja wake kuwa hakuna oda itakayopotea na kwamba kila mteja atapokea bidhaa yake. Lakini pia amekanusha madai ya kutapeli, akibainisha kuwa biashara yake imesimama kwa misingi ya uaminifu na uwazi. Kwa mujibu wa mjasiriamali huyo, Yallo Leather bado ipo imara na changamoto zinazoshuhudiwa kwa sasa ni za muda tu. Ameomba wateja wake waendelee kuwa na subira wakati oda zilizokwama zikikamilishwa. Yallo Leather imekuwa ikivutia wapenzi wa mitindo kwa ubunifu na ubora wa bidhaa zake, na licha ya changamoto hizo za muda mfupi, mashabiki wengi wameendelea kumpa moyo Mercy huku wakisubiri bidhaa zao kwa hamu.

Read More
 Rapa Wakazi Amkingia Kifua Master Jay Dhidi ya Kubezwa na Wasanii

Rapa Wakazi Amkingia Kifua Master Jay Dhidi ya Kubezwa na Wasanii

Rapa Wakazi, ameonyesha kutopendezwa na namna ambavyo mtayarishaji nguli Master Jay amekuwa akibeuliwa na baadhi ya wasanii na producers wa kizazi cha sasa. Kupitia ujumbe alioweka kwenye ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, Wakazi ameeleza kusikitishwa na hali hiyo, akibainisha kuwa mchango mkubwa wa Master Jay katika tasnia ya muziki wa Tanzania haupaswi kusahaulika wala kubezwa. Rapa huyo amesema huenda ukaribu wa Master Jay na wasanii wachanga umewafanya baadhi yao kumpuuza, huku wengine wakisahau historia na mchango wake katika sekta ya burudani. Wakazi pia amesisitiza kuwa tatizo kubwa ni ukosefu wa kumbukumbu na heshima kwa walioweka msingi wa muziki wa Bongofleva, akihimiza wasanii chipukizi na hata wakongwe kutambua mchango wa waliotangulia. Kauli ya Wakazi imeibuka baada ya msanii mkongwe Juma Nature kunukuliwa katika moja ya mahojiano akidai hajawahi kumkubali Master Jay kama producer. Nature alieleza kuwa kipindi hicho Master Jay alitamani kuwa kama P Funk Majani, hali iliyomfanya baba yake mzazi kumnunulia vyombo vya muziki na si kwa ubunifu au kipaji chake binafsi.

Read More
 Ruth K Amwonya Mpenzi Mpya wa Mulamwah: “Usithubutu Kuzaa Naye!”

Ruth K Amwonya Mpenzi Mpya wa Mulamwah: “Usithubutu Kuzaa Naye!”

Baby Mama wa Mchekeshaji Mulamwah, Ruth K, ameibua gumzo mtandaoni baada ya kujibu kwa kejeli habari za aliyekuwa mpenzi wake, kuonyesha hadharani mpenzi wake mpya anayefahamika kama Emillianah. Kupitia mitandao ya kijamii, Ruth amemwonya Emillianah dhidi ya kuzaa mtoto na Mulamwah, akisisitiza kuwa mchekeshaji huyo ana historia tata linapokuja suala la malezi ya watoto. Ameonyesha wazi kwamba ingawa hawezi kupinga uhusiano wao, suala la kupata mtoto linaweza kuwa changamoto kubwa kwa upande wa Emillianah. Kauli hiyo imeibua hisia mseto miongoni mwa mashabiki. Wengi wamechukulia ujumbe huo kama dongo kwa Mulamwah ambaye tayari ana mtoto na Ruth, huku changamoto za malezi zikiwa zimewahi kujadiliwa sana mtandaoni. Mashabiki wengine waliunga mkono msimamo wa Ruth wakimtaka Emillianah kuwa makini, huku wengine wakimshutumu Ruth kwa kuingilia maisha mapya ya Mulamwah kwa kuonyesha wivu wa kimapenzi.

Read More
 Abel Mutua Awataka Wakenya Wathamini Maadili Mema Mitandaoni  

Abel Mutua Awataka Wakenya Wathamini Maadili Mema Mitandaoni  

Mtayarishaji maarufu wa filamu, Abel Mutua, ameonekana kushangazwa na tabia ya Wakenya kupendelea kushabikia au kusambaza matukio ya matusi, vurugu, na drama kuliko yale yanayohusisha tabia njema au ujumbe wa heshima. Kupitia Instagram, Abel ameelezea masikitiko yake jinsi baadhi ya watu maarufu nchini wanavyojulikana si kwa matendo yao mema, bali kwa visa vya vurugu. Ametoa mfano wa mhubiri maarufu Pastor James Ng’ang’a, akisema kuwa video zinazopata umaarufu zaidi kwenye mitandao ya kijamii ni zile zinazomwonyesha akiwatukana, akipiga kelele, au akitishia waumini wake. Kwa mujibu wa Abel, hali hii inaonyesha taswira ya jamii ambayo imeanza kuona matusi na fujo kama sehemu ya burudani, huku watu wenye ujumbe wa maana na heshima wakipuuzwa au kutopewa nafasi mitandaoni. Hata hivyo amesema kuwa hali hii si tu inawakatisha tamaa watu wenye maadili mema, bali pia inaathiri kizazi kipya ambacho sasa kinaamini kuwa njia ya kupata umaarufu ni kwa kuwa wa matusi au drama mitandaoni.

Read More
 Khadija Kopa Asema Wakosoaji Wake Mtandaoni Ni Watu Wasiokuwa na Hela

Khadija Kopa Asema Wakosoaji Wake Mtandaoni Ni Watu Wasiokuwa na Hela

Malkia wa Taarab Khadija Kopa ameamua kutoa kauli kali kuhusu wakosoaji wake mitandaoni. Akiwa mgeni katika kipindi cha Tashtiti, Khadija Kopa amesema kuwa haumizwi na kitendo cha watu kumchamba kwenye mitandao ya kijamii, akieleza kuwa mara nyingi wanaofanya hivyo ni watu wasiokuwa na uwezo kifedha. Kwa mujibu wake, wengi wao huishi maisha magumu majumbani mwao lakini wanapofika mtandaoni hujigeuza na kuwa mabingwa wa kutoa maneno makali kwa wengine. Aidha, msanii huyo mkongwe wa Taarab ameongeza kuwa mtu mwenye hela na mafanikio makubwa hana muda wa kupoteza kwenye matusi au malumbano ya mtandaoni. Kauli hiyo imezua mjadala miongoni mwa mashabiki, ambapo baadhi walikubaliana naye wakisema kuwa mitandao imejaa maneno ya watu wasiokuwa na mchango halisi maishani, huku wengine wakihisi kwamba wasanii wanapaswa kukubali ukosoaji kwa kuwa ni sehemu ya maisha ya umaarufu.

Read More