LEO KATIKA HISTORIA OKTOBA 14, ALIZALIWA RAPA KUTOKA MAREKANI LIL DURK

LEO KATIKA HISTORIA OKTOBA 14, ALIZALIWA RAPA KUTOKA MAREKANI LIL DURK

Siku kama ya leo Oktoba 19 mwaka wa 1996 alizaliwa  staa wa muziki wa Hiphop na mwaandishi wa nyimbo kutoka nchini Marekani Lil Durk. Jina lake halisi ni Durk Derrick na alizaliwa huko Chicago Illinois nchini Marekani ambako alianza muziki mwaka wa 2009 lakini alikuja akapataa umaarufu mwaka wa 2011 baada ya kuachia ngoma zake mbili ambazo ni Sneak Dissin na Ima  Hitta zilizopokelewa kwa ukubwa nchini Marekani. Mwaka wa 2012 Lil Durk aliachia mixtape yake inayokwenda kwa jina la   Life Aaint No Joke chini ya lebo ya muziki ya OTF  ikafuatwa na mixtape yake iitwayo Signed To The Street ya mwaka wa 2013 ambayo ilitayarishwa na lebo ya muziki ya Def  Jam  Recordings. Mwaka wa 2014 Lil Durk aliachia mixtape nyingine iitwayo The Sequel to Signed to the Streets ikafuatwa na album yake ya kwanza ya mwaka wa 2015 iitwayo Remember My Name, album ambayo ilikuwa na jumla ya ngoma 10 za moto. Mwaka huo huo wa 2015 Lil Durk aliachia mixtape yake inayokwenda kwa jina la 300 days, 300 Nights ambayo ilikuwa ngoma kama My Beyonce ambayo iliweza kufikia viwango vya mauzo ya gold kwa kuuza zaidi ya nakala laki 5. Mwaka wa 2016 Lil Durk aliachia album yake ya pili iitwayo Lil Durk  2X ambayo ilikuwa na jumla ya ngoma 11 akiwa  amewashirikisha wasaani kama young thug,ty dolla sign na wengine kibao. Hata hivyo tangu Lil Durk aanze kujishughulisha na muziki wa hiphop nchini Marekani mwaka wa 2009 amefanikiwa kufanya jumla ya album tano za muziki,Mixtape 12,Singles 20 na album mbili iliyobeba nyimbo zilitoka pamoja na zile hazikutoka. Lil Durk kwa sasa amesainiwa na lebo ya muziki ya Def Jam Records lakini pia yupo chini ya record lebo  ya Coke Boys inayomilikiwa na rapa French Montana ambayo inafanya kazi pamoja na lebo yake ya muziki ya Only the Family.

Read More
 CHID BENZ AACHIA TRACKLIST YA “WA2 WANGU” ALBUM

CHID BENZ AACHIA TRACKLIST YA “WA2 WANGU” ALBUM

Rapa kutoka nchini Tanzania Chidi Benz amewapa mashabiki wake orodha ya nyimbo zitakazopatikana kwenye album yake mpya ya “Wa2 Wangu” anayoitarajia kuitoa hivi karibuni. Chid benz ambaye ni mshindi mara nne wa Kill Music Awards kupitia tuzo ya msanii Bora wa Hip Hop nchini tanzania, ameorodhesha jumla ya nyimbo 18 kutoka kwenye album hiyo, huku ikiwa na collabo 5 pekee,ambapo amewapa mashavu wasanii kama Badest 47, Brian Simba kusikika kwenye album hiyo. Hata hivyo, Chidi tayari ameshaachia nyimbo 6 kutoka kwenye album hiyo, ambazo ni Nahamia Bar, Jirani, Walete, One, King of the Jungle na Hilo Ngoma. Ikumbukwe kuwa, hii itakuwa ni album ya pili kutoka kwa mtu mzima Chidi Beenz baada ya Dar Es Salaam Stand Up ya mwaka wa 2010

Read More
 JOSE CHAMELEONE: SINA MPANGO WA KUREJEA TENA KWENYE SIASA

JOSE CHAMELEONE: SINA MPANGO WA KUREJEA TENA KWENYE SIASA

Bosi wa lebo ya muziki ya Leone Island msanii Jose Chameleone ameweka wazi kwamba hana mpango tena wa kuingia kwenye siasa. Chameleone amesema siasa inataka pesa nyingi sana na kwa mantiki hiyo itakuwa vigumu kwake kuwania wadhfa wowote wa kisiasa. Hata hivyo amesisitiza kwamba licha ya watu kutompigia kura kwa wingi kwenye uchaguzi mkuu uliopita nchini Uganda, anaamini hana vigezo vya kuwa kiongozi na ndio maana wananchi walimchagua mpinzani wake. Ikumbukwe Jose Chameolene alipoteza kwenye uchaguzi wa umeya wa Jiji la Kampala mapema mwaka huu na mpinzani wake Erias Lukwago.

Read More
 NYOTA NDOGO AINGIA UBIA WA KUFANYA KAZI NA KAMPUNI YA JOY MILLERS LIMITED.

NYOTA NDOGO AINGIA UBIA WA KUFANYA KAZI NA KAMPUNI YA JOY MILLERS LIMITED.

Staa wa muziki nchini Nyota Ndogo amelamba dili nono la kuwa balozi wa unga wa ugali wa Raha Premium. Nyota Ndogo ametengaza habari hiyo njema kwa mashabiki zake kupitia ukurasa wake wa instagram huku akieleza kuwa ana furaha kujiunga na familia ya Raha Premium. Lakini pia ameishikuru uongozi wa kampuni ya Joy Miller Limited kwa kutambua nguvu yake na kuhamua kumpatia dili hilo ambalo litamjengea heshima. Nyota Ndogo sasa atatakiwa kutangaza bidhaa za Raha Premium kwa mashabiki zake kupitia mitandao ya kijamii kwa lengo la kuongeza mauzo ya unga hiyo ya ugali. Hitmaker huyo wa “Watu na Viatu” anajunga na msanii Bahati pamoja mke wake Diana Marua ambao pia waliingia ubia wa kufanya kazi na kampuni ya Joy millers limited mwezi Agosti mwaka huu. Ikumbukwe nyota ndogo ni mmoja kati ya wasaani ambao wamewekeza kwenye biashara kuuza vyakula na amekuwa akitumia mitandao ya kijamii kutangaza mgahawa wake ambao ameupa jina la  Nyota Ndogo jikoni.

Read More
 BURNA BOY AKAVA JARIDA LA ES MAGAZINE LA NCHINI UINGEREZA

BURNA BOY AKAVA JARIDA LA ES MAGAZINE LA NCHINI UINGEREZA

Staa wa muziki kutoka nchini Nigeria  Burna Boy ambaye anafanya vizuri kupitia kazi zake mbalimbali, ametokea mbele ya kava la Jarida la Es Magazine la nchini Uingereza. Jarida la Evening Standard Magazine ni jarida kutoka London, Uingereza ambalo hujihusisha kwa kutoa habari za burudani kutoka kwa mastaa wakubwa ulimwenguni. Kwenye Jarida hilo Burna Boy  amefunguka mengi kuhusiana na muziki wake, mpaka kufikia hapo alipo. Uwezo wake mkubwa wa kujaza kwenye Arena, dili mbalimbali alizozipata kama PEPSI, kukutana na mastaa wakubwa, kushiriki kwenye album za wasanii kutokea Marekani. Hata hivyo, Burna boy  anakuwa msanii wa tatu kutoka Afrika kupata nafasi ya kukava jarida la ES, mwaka 2019 WizKid alikava Jarida hilo na mwaka 2020 ikawa zamu ya Davido kutokea kwenye jarida hilo. Ikumbukwe, Burna Boy kupata nafasi ya kukava kwenye jarida hili kubwa ulimwenguni kunampa nafasi ya kuzingatiwa, kuongeza mashabiki na watu kupata nafasi ya kuweza kumfuatilia zaidi.

Read More
 TYGA AFUNGUKA KWA MARA YA KWANZA KUHUSU SAKATA LA KUMPIGA EX WAKE

TYGA AFUNGUKA KWA MARA YA KWANZA KUHUSU SAKATA LA KUMPIGA EX WAKE

Rapa kutoka nchini Marekani Tyga amefunguka kuhusu taarifa za kufunguliwa mashtaka kwa madai ya kumpiga ex wake Camaryn Swanson, Jumatatu wiki iliyopita. Tyga alijisalimisha kwenye mikono ya polisi mjini Los Angeles Jumanne  wiki iliyopita ambapo Tovuti ya TMZ ilidai kwamba tayari amefunguliwa mashtaka ya unyanyasaji wa nyumbani. Sasa baada ya kimya cha muda mfupi, Tyga ameamua kuweka wazi sakata hilo. Kupitia ukurasa wake wa instagram rapa huyo amekanusha kwa kusema madai hayo hayana ukweli wowote, kwani hakukamatwa na polisi na wala hakufunguliwa mashtaka yoyote bali alifika kituo hapo kujieleza. Kwa mujibu wa nyaraka za polisi wa Los Angeles, zinaonesha Michael Stevenson maarufu Tyga alishtakiwa kwa makosa ya uhalifu mnamo Oktoba 12 mwaka huu na aliachiwa masaa machache baadaye kwa dhamana ya shillingi millioni 5.5 za kenya.

Read More
 KRG THE DON ATHIBITISHA KUACHANA NA BABY MAMA WAKE.

KRG THE DON ATHIBITISHA KUACHANA NA BABY MAMA WAKE.

Baada ya uvumi wa wiki kadhaa,  Msanii wa muziki wa Dancehall nchini KRG The Don hatimaye amethibitisha kuwa yeye na mke wake sio wapenzi tena. KRG ameweka wazi hilo kupitia Instagram page yake baada ya kupost picha ya mke wake huyo na kusindikiza na caption inayoashiria kuwa wameachana rasmi. Hitmaker huyo “Giddem” amemsuta vikali mke wake huyo kwa madai ya kujihusisha sana na anasa na kusahau kuwahudumia watoto wao. KRG pia ametumia fursa hiyo kukanusha madai yanayosambaa kwenye mitandao kuwa alitoka nje ya ndoa yake na ndio maana uhusiano wake na Baby mama wake ulivunjika. Hata  hivyo, bado haijabainika kama kuna ukweli wowote kuhusu stori za wawili hao kuachana ila kwa sasa wamefuta picha zote walizowahi kupiga wakiwa pamoja kwenye mtandao wa Instagram.

Read More
 WINNIE NWAGI MBIONI KUACHA MUZIKI

WINNIE NWAGI MBIONI KUACHA MUZIKI

Inaonekana msanii wa Swangz Avenue Winnie Nwagi hana furaha kwa sasa kwenye tasnia ya muziki nchini Uganda. Kulingana na posts zake kwenye mitandao ya kijamii hitmaker huyo wa “Musawo” inaonekana anapitia kipindi kigumu kwenye maisha yake ambayo hajawahi kutana nayo tangu aanze safari yake ya muziki. Kupitia ukurasa wake wa twitter mrembo huyo amesema kwamba kama angekuwa na kitu kingine cha kufanya kwenye maisha, angeacha muziki kabisa. Winnie nwagi amesema amechoshwa na kile kinachoendelea kwenye maisha yake kwa sasa a ameomba dua kwa mwenyezi mungu aingilia maisha yake kabla hajachukua maamuzi magumu. Kuthibitisha kwamba Winnie Nwagi hana furaha kabisa alienda mbali zaidi na kuwablock mashabiki wake wote kwenye mtandao wa instagram wasiweze ku comment kwenye post yake. Hata hivyo mrembo huyo hajaweka wazi kinachomsumbua kwa sasa kwenye maisha yake.

Read More
 DADDY OWEN AWABARIKI MASHABIKI ZAKE NA CHAPTER 4 ALBUM

DADDY OWEN AWABARIKI MASHABIKI ZAKE NA CHAPTER 4 ALBUM

Mwanamuziki wa nyimbo za Injili nchini Daddy Owen ameachia rasmi album yake mpya iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu na mashabiki zake. Album hiyo inayokwenda kwa jina la Chapter 4 ina jumla ya singo 15 ya moto huku ikiwa na 6 collabo pekee. Daddy Owen amewashirikisha wasanii kama Nakaaya,Bella Kombo, Judy Stevens,Ivyln Mutua,Danco na Slejj. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa chapter 4 album  Daddy Owen amesema safari ya kuandaa album yake mpya haikuwa rahisi ila anamshukuru mwenyezi mungu kwa kumwezesha kuikamilisha album hiyo licha ya changamoto alizokutana nazo. Chapter 4 ni album ya sita kwa mtu mzima Daddy Owen lakini pia inavunja ukimya wake wa miaka 5 tangu alipoachia album yake ya Vanity iliyotoka mwaka wa 2016.

Read More
 AKOTHEE AREJEA TENA KEMPINSIKI BAADA YA KUUSUTA VIKALI UONGOZI WAKE

AKOTHEE AREJEA TENA KEMPINSIKI BAADA YA KUUSUTA VIKALI UONGOZI WAKE

Nyota wa muziki nchini Akothee amerejea tena katika hoteli ya kifahara ya Kempinski,ikiwa ni wiki mbili imepita baada ya kuhapa kutokanyaga kwenye hoteli hiyo. Hatua hiyo ya Akothee imeonekana kuwakera wakenya kwenye mitandao ya kijamii wengi wakisema msanii huyo ni mnafiki na kauli  chafu aliyoitoa juu ya hoteli ya Kempinski haiwezi haribu brand ya hoteli hiyo. Akothee alikuwa anahudhuria hafla ya kusherekea mafanikio ambayo kinara wa ODM Raila Odinga ameiletea taifa la Kenya wikiendi hii iliyopita. Ikumbukwe wiki kadhaa zilizopita Akothee aliichana hoteli ya kifahari ya Kempinski iliyoko jijini Nairobi kwa madai ya kuwa na uongozi mbaya kwani mameneja wa hoteli hiyo walimsumbua sana kipindi anasherekea mwaka mmoja wa kuzinduliwa kwa wakfu wake wa Akothee Foundation katika hoteli hiyo.

Read More
 KHALIGRAPH JONES AFUNGUKA KUWAHI KUTAKA KUACHA MUZIKI.

KHALIGRAPH JONES AFUNGUKA KUWAHI KUTAKA KUACHA MUZIKI.

Rapa Khaligraph Jones ametusanua kuhusu changamoto alizokutana  nazo katika safari yake ya muziki ambayo ilimpelekea kutaka kuchukua maamuzi magumu kwenye maisha yake. Kupitia ukurasa wake wa instagram amepost picha akiwa jukwaani katika chuo kikuu cha St. Pauls limuru mwaka wa 2012 na kusema kwamba mashabiki waliikata perfomance yake na kumtimua jukwaani jambo ambalo lilimfanya kufikiria kuacha muziki. Lakini baada ya kujitafakari upya na kuweka bidii kwenye kazi zake za muziki aliweza kuwaaminisha watu waliombeza kipindi hicho kwamba anaweza kwenye tasnia ya muziki nchini. Khalighraph jones ni moja kati ya marapa maarufu barani afrika na licha ya kutimuliwa jukwanii mwaka wa 2012 nchini Kenya ametumbuiza kwenye majukwaa makubwa ya muziki duniani lakini pia ameshinda tuzo kadhaa za muziki ikiwemo B.E.T na Sound city Africa.

Read More
 TEKASHI 69 ADUKULIWA AKAUNTI YAKE YA SPOTIFY

TEKASHI 69 ADUKULIWA AKAUNTI YAKE YA SPOTIFY

Akaunti ya Spotify ya Rapa Tekashi 69 kutoka Marekani imedukuliwa (Hacked)  na wadukuzi. Hii imekuja mara baada ya ghafla kubadilishwa kwa Profile Pic (DP) kwenye akaunti yake hiyo na kuwekwa picha ya Rapa Trippie Red na Lil Durk. Sio hayo tu  Bio ya rapa huyo pia imebadilishwa ambapo kwa wale waliofikia akaunti hiyo kwa muda huo walikutana na ujumbe ulioandikwa kuwa Tekashi 69 amekuwa akiishi kwa kutamani kuja kuwa kama rapa Trippie Red na Lil Durk. Mashabiki wa Trippie Red na Lil Durk  wametajwa kuhusika na udukuzi huo ikizingatiwa kuwa Tekashi 69 ana bifu na marapa hao wawili.

Read More