TYGA AFUNGUKA KWA MARA YA KWANZA KUHUSU SAKATA LA KUMPIGA EX WAKE

TYGA AFUNGUKA KWA MARA YA KWANZA KUHUSU SAKATA LA KUMPIGA EX WAKE

Rapa kutoka nchini Marekani Tyga amefunguka kuhusu taarifa za kufunguliwa mashtaka kwa madai ya kumpiga ex wake Camaryn Swanson, Jumatatu wiki iliyopita. Tyga alijisalimisha kwenye mikono ya polisi mjini Los Angeles Jumanne  wiki iliyopita ambapo Tovuti ya TMZ ilidai kwamba tayari amefunguliwa mashtaka ya unyanyasaji wa nyumbani. Sasa baada ya kimya cha muda mfupi, Tyga ameamua kuweka wazi sakata hilo. Kupitia ukurasa wake wa instagram rapa huyo amekanusha kwa kusema madai hayo hayana ukweli wowote, kwani hakukamatwa na polisi na wala hakufunguliwa mashtaka yoyote bali alifika kituo hapo kujieleza. Kwa mujibu wa nyaraka za polisi wa Los Angeles, zinaonesha Michael Stevenson maarufu Tyga alishtakiwa kwa makosa ya uhalifu mnamo Oktoba 12 mwaka huu na aliachiwa masaa machache baadaye kwa dhamana ya shillingi millioni 5.5 za kenya.

Read More
 KRG THE DON ATHIBITISHA KUACHANA NA BABY MAMA WAKE.

KRG THE DON ATHIBITISHA KUACHANA NA BABY MAMA WAKE.

Baada ya uvumi wa wiki kadhaa,  Msanii wa muziki wa Dancehall nchini KRG The Don hatimaye amethibitisha kuwa yeye na mke wake sio wapenzi tena. KRG ameweka wazi hilo kupitia Instagram page yake baada ya kupost picha ya mke wake huyo na kusindikiza na caption inayoashiria kuwa wameachana rasmi. Hitmaker huyo “Giddem” amemsuta vikali mke wake huyo kwa madai ya kujihusisha sana na anasa na kusahau kuwahudumia watoto wao. KRG pia ametumia fursa hiyo kukanusha madai yanayosambaa kwenye mitandao kuwa alitoka nje ya ndoa yake na ndio maana uhusiano wake na Baby mama wake ulivunjika. Hata  hivyo, bado haijabainika kama kuna ukweli wowote kuhusu stori za wawili hao kuachana ila kwa sasa wamefuta picha zote walizowahi kupiga wakiwa pamoja kwenye mtandao wa Instagram.

Read More
 WINNIE NWAGI MBIONI KUACHA MUZIKI

WINNIE NWAGI MBIONI KUACHA MUZIKI

Inaonekana msanii wa Swangz Avenue Winnie Nwagi hana furaha kwa sasa kwenye tasnia ya muziki nchini Uganda. Kulingana na posts zake kwenye mitandao ya kijamii hitmaker huyo wa “Musawo” inaonekana anapitia kipindi kigumu kwenye maisha yake ambayo hajawahi kutana nayo tangu aanze safari yake ya muziki. Kupitia ukurasa wake wa twitter mrembo huyo amesema kwamba kama angekuwa na kitu kingine cha kufanya kwenye maisha, angeacha muziki kabisa. Winnie nwagi amesema amechoshwa na kile kinachoendelea kwenye maisha yake kwa sasa a ameomba dua kwa mwenyezi mungu aingilia maisha yake kabla hajachukua maamuzi magumu. Kuthibitisha kwamba Winnie Nwagi hana furaha kabisa alienda mbali zaidi na kuwablock mashabiki wake wote kwenye mtandao wa instagram wasiweze ku comment kwenye post yake. Hata hivyo mrembo huyo hajaweka wazi kinachomsumbua kwa sasa kwenye maisha yake.

Read More
 DADDY OWEN AWABARIKI MASHABIKI ZAKE NA CHAPTER 4 ALBUM

DADDY OWEN AWABARIKI MASHABIKI ZAKE NA CHAPTER 4 ALBUM

Mwanamuziki wa nyimbo za Injili nchini Daddy Owen ameachia rasmi album yake mpya iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu na mashabiki zake. Album hiyo inayokwenda kwa jina la Chapter 4 ina jumla ya singo 15 ya moto huku ikiwa na 6 collabo pekee. Daddy Owen amewashirikisha wasanii kama Nakaaya,Bella Kombo, Judy Stevens,Ivyln Mutua,Danco na Slejj. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa chapter 4 album  Daddy Owen amesema safari ya kuandaa album yake mpya haikuwa rahisi ila anamshukuru mwenyezi mungu kwa kumwezesha kuikamilisha album hiyo licha ya changamoto alizokutana nazo. Chapter 4 ni album ya sita kwa mtu mzima Daddy Owen lakini pia inavunja ukimya wake wa miaka 5 tangu alipoachia album yake ya Vanity iliyotoka mwaka wa 2016.

Read More
 AKOTHEE AREJEA TENA KEMPINSIKI BAADA YA KUUSUTA VIKALI UONGOZI WAKE

AKOTHEE AREJEA TENA KEMPINSIKI BAADA YA KUUSUTA VIKALI UONGOZI WAKE

Nyota wa muziki nchini Akothee amerejea tena katika hoteli ya kifahara ya Kempinski,ikiwa ni wiki mbili imepita baada ya kuhapa kutokanyaga kwenye hoteli hiyo. Hatua hiyo ya Akothee imeonekana kuwakera wakenya kwenye mitandao ya kijamii wengi wakisema msanii huyo ni mnafiki na kauli  chafu aliyoitoa juu ya hoteli ya Kempinski haiwezi haribu brand ya hoteli hiyo. Akothee alikuwa anahudhuria hafla ya kusherekea mafanikio ambayo kinara wa ODM Raila Odinga ameiletea taifa la Kenya wikiendi hii iliyopita. Ikumbukwe wiki kadhaa zilizopita Akothee aliichana hoteli ya kifahari ya Kempinski iliyoko jijini Nairobi kwa madai ya kuwa na uongozi mbaya kwani mameneja wa hoteli hiyo walimsumbua sana kipindi anasherekea mwaka mmoja wa kuzinduliwa kwa wakfu wake wa Akothee Foundation katika hoteli hiyo.

Read More
 KHALIGRAPH JONES AFUNGUKA KUWAHI KUTAKA KUACHA MUZIKI.

KHALIGRAPH JONES AFUNGUKA KUWAHI KUTAKA KUACHA MUZIKI.

Rapa Khaligraph Jones ametusanua kuhusu changamoto alizokutana  nazo katika safari yake ya muziki ambayo ilimpelekea kutaka kuchukua maamuzi magumu kwenye maisha yake. Kupitia ukurasa wake wa instagram amepost picha akiwa jukwaani katika chuo kikuu cha St. Pauls limuru mwaka wa 2012 na kusema kwamba mashabiki waliikata perfomance yake na kumtimua jukwaani jambo ambalo lilimfanya kufikiria kuacha muziki. Lakini baada ya kujitafakari upya na kuweka bidii kwenye kazi zake za muziki aliweza kuwaaminisha watu waliombeza kipindi hicho kwamba anaweza kwenye tasnia ya muziki nchini. Khalighraph jones ni moja kati ya marapa maarufu barani afrika na licha ya kutimuliwa jukwanii mwaka wa 2012 nchini Kenya ametumbuiza kwenye majukwaa makubwa ya muziki duniani lakini pia ameshinda tuzo kadhaa za muziki ikiwemo B.E.T na Sound city Africa.

Read More
 TEKASHI 69 ADUKULIWA AKAUNTI YAKE YA SPOTIFY

TEKASHI 69 ADUKULIWA AKAUNTI YAKE YA SPOTIFY

Akaunti ya Spotify ya Rapa Tekashi 69 kutoka Marekani imedukuliwa (Hacked)  na wadukuzi. Hii imekuja mara baada ya ghafla kubadilishwa kwa Profile Pic (DP) kwenye akaunti yake hiyo na kuwekwa picha ya Rapa Trippie Red na Lil Durk. Sio hayo tu  Bio ya rapa huyo pia imebadilishwa ambapo kwa wale waliofikia akaunti hiyo kwa muda huo walikutana na ujumbe ulioandikwa kuwa Tekashi 69 amekuwa akiishi kwa kutamani kuja kuwa kama rapa Trippie Red na Lil Durk. Mashabiki wa Trippie Red na Lil Durk  wametajwa kuhusika na udukuzi huo ikizingatiwa kuwa Tekashi 69 ana bifu na marapa hao wawili.

Read More
 STREAMS ZA BOOMPLAY KUHESABIKA BILLBOARD

STREAMS ZA BOOMPLAY KUHESABIKA BILLBOARD

App namba moja ya kupakua na kusikiliza muziki Afrika,Boomplay imefanikiwa kuingiza kazi za wasanii katika chati za Billboard kama sehemu yake ya kuendelea kusaidia tasnia ya muziki wa Afrika kutanua wigo wake kamili. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa umma na Kampuni ya Transsnet Music Limited ambayo ndiyo inayomiliki Programu tumuishi (App) ya Boomplay,  itaanza kuingiza kazi za wasanii katika chati maarufu za Billboard Hot 100, Billboard 200, Artist 100 na Billboard Global 200, na pia chati zingine zote za Billboard Marekani na kimataifa ambazo zinajumuisha kazi za kupakua na kusikiliza muziki. Aidha, pamoja na mamilioni ya nyimbo za Kiafrika kusikilizwa kupitia programu hiyo duniani kote, kujumuishwa kwa taarifa za Boomplay katika chati hizo kubwa za muziki kunawapa wasanii wa Kiafrika na Kimataifa fursa ya kuonekana zaidi kwenye majukwaa makubwa duniani. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, ndani ya jukwaa la Music Connect la MRC Data, kazi za Boomplay zitajumuishwa kwenye kapu moja la takwimu linalojumuisha mahitaji ya sauti na picha ambapo picha zimeanza kuonekana kuanzia Oktoba 12, 2021 na miito Oktoba 8, 2021. Streams za Boomplay ziliizoingizwa kwenye chati za Billboard zinawakilisha streams kutoka kwa wasikilizaji waliojisaliji kawaida na wale wa kulipia huku kila stream kutoka kwa msikilizaji wa kundi husika vikipimwa kwa uzito wake.

Read More
 AMBER LULU: NAMTAMANI SANA JUX

AMBER LULU: NAMTAMANI SANA JUX

Msanii wa Bongofleva Amber Lulu amemtaja Juma Jux kuwa ndio mwanaume anayetamani kupata naye mtoto kwa sababu ana akili, yupo smart na atamuongoza vyema lakini pia amekuwa akimfuatilia msanii huyo kwa muda mrefu. Mrembo huyo ambaye anafanya poa na singo yake mpya iitwayo Nimeachika amesema amepanga kuzaa watoto 5 kila mmoja na baba yake sababu akizaa na baba mmoja kisha akafariki yeye ataishia kupata tabu na watoto. Ikumbukwe pia Amber Lulu kipindi cha nyuma alishaweka wazi kutamani kuwa kwenye mahusiano na Diamond Platnumz, lakini hata hivyo nafasi ya kuwa na Diamond inaonekana ni nyembamba sababu baada ya hitmaker huyo wa Naanzaje kuzaa watoto 4 na wanawake tofauti amekiri hivi karibuni kuwa kwa sasa kuwa kwenye mahusiano na wanawake sio kipaumbele chake bali nguvu amezielekeza kwenye kuzidi kufanya kazi ili kuendelea kufanikiwa kiuchumi.

Read More
 VERA SIDIKA:NITAZAA KWA UPASUAJI

VERA SIDIKA:NITAZAA KWA UPASUAJI

Socialite  maarufu Afrika Mashariki Vera Sidika amesisitiza kwamba atajifungua kwa njia ya upasuaji na siyo kwa njia ya kawaida kwa sababu anaogopa uchungu wa leba. Vera ambaye anatarajia kujifungua muda wowote anasema kwamba, alifanya uamuzi kuwa atajifungua kwa njia ya upasuaji hata kabla hajapata ujauzito. Mrembo huyo ambaye anatarajia mtoto wake wa kwanza ameapa kwamba hakuna yeyote ambaye anaweza kubadilisha uamuzi wake. Mpenzi huyo wa mwanamuziki Brown Mauzo amesema kwamba ni heri avumilie kipindi cha uponyaji baada ya kufanyiwa upasuaji kuliko akabiliane na machungu ya leba.

Read More
 TWITTER KUWEKA MATANGAZO KATIKA SEHEMU YA REPLIES

TWITTER KUWEKA MATANGAZO KATIKA SEHEMU YA REPLIES

Mtandao wa Twitter umeanza majaribio ya kuweka matangazo katika sehemu ya Replies/comments. Ni style mpya ya kuonyesha matangazo katikati ya comments/replies. Inaonekana matangazo yataonekana sana katika Tweets za watu maarufu na akaunti ambazo zina watu wengi wanaoshiriki katika comments. Bado haijaonekana kama mwenye akaunti atafaidika na matangazo ambayo yataonekana katika Replies za Tweets zake. Tayari imeanza kwa watumiaji wa App ya Beta katika iOS na Android.

Read More
 KIM KARDASHIAN ASHINDA KIPENGELE CHA UMILIKI WA NYUMBA KWENYE SHAURI LA TALAKA

KIM KARDASHIAN ASHINDA KIPENGELE CHA UMILIKI WA NYUMBA KWENYE SHAURI LA TALAKA

Mahakama ya mjini Los angeles nchini marekani imempatia ushindi Kim Kardashian wa umiliki wa nyumba kwenye shauri la talaka linaloendelea dhidi yaKkanye West. Kim ameshinda kipengele hicho na sasa ni mmiliki wa nyumba ambayo walianzia maisha na Kanye West na kuanzisha familia pamoja. Jumba hilo lenye thamani ya shilling billion 6.7  lipo mjini Hidden Hills California, mwaka wa 2014 walilinunua pamoja kwa shilling billioni 2.6 kisha baadaye mwaka wa 2020 Kanye West aliikarabati. Hii imekuja kufuatia mustakabali wa watoto wao ambao wamezoea kuishi mahali hapo. Taarifa hii imekuja ikiwa ni siku chache tangu kanye west aiweke kwenye mnada moja ya ranchi zake zilizopo huko Wyoming nchini kwa shilling billioni 1.2. Mwezi uliopita  Kanye West pia aliripotiwa kununua jumba la kifahari kwenye fukwe za malibu huko marekani kwa shilling billioni 6.3.

Read More