Jovial Atangaza Mapumziko ya Mitandao Baada ya Kujifungua

Jovial Atangaza Mapumziko ya Mitandao Baada ya Kujifungua

Mwanamuziki nyota wa Kenya, Jovial, ametangaza kuwa atachukua mapumziko kwenye mitandao ya kijamii baada ya kujifungua mtoto wake. Kupitia taarifa kwa mashabiki wake, msanii huyo amesema ataepuka shughuli za mitandaoni kwa muda ili kufurahia muda wa faragha na mtoto wake mchanga. Amesisitiza kuwa muda huu utamwezesha kujiweka sawa kimwili na kiakili kwa utulivu. Hata hivyo, Jovial amewahakikishia mashabiki wake kwamba mapumziko hayo hayatazuia kazi yake ya muziki. Amefichua kuwa tayari ana nyimbo mpya zilizokamilika na zitaachiwa wakati wa likizo yake ya uzazi. Tangazo hilo limepokelewa kwa pongezi na jumbe za kumtakia heri kutoka kwa mashabiki na wasanii wenzake, wengi wakimsifu kwa kuipa kipaumbele afya yake huku akiendeleza kipaji chake cha muziki.

Read More
 Mr Eazi Afunga Ndoa na Temi Otedola Katika Harusi ya Kifahari Iceland.

Mr Eazi Afunga Ndoa na Temi Otedola Katika Harusi ya Kifahari Iceland.

Mwanamuziki kutoka Nigeria, Mr Eazi, amefunga ndoa na mpenzi wake wa muda mrefu, Mwigizaji Temi Otedola, katika sherehe ya kifahari iliyosheheni usiri mkubwa, iliyofanyika nchini Iceland. Harusi hiyo ilifanyika Ijumaa, tarehe 8 Agosti 2025, ndani ya Kanisa maarufu la Hallgrímskirkja lililopo mjini Reykjavik. Tukio hilo lilihudhuriwa na familia na marafiki wa karibu pekee, akiwemo mama yake bi harusi, Nana Otedola, na dada yake, DJ Cuppy. Miongoni mwa wageni mashuhuri waliohudhuria ni tajiri namba moja barani Afrika, Bilionea Aliko Dangote, ambaye alishuhudia kiapo cha wawili hao waliodumu kwenye mahusiano tangu mwaka 2017. Harusi hiyo imezua gumzo mitandaoni kutokana na uzuri wa mandhari ya Iceland na umakini uliowekwa kuhakikisha inabaki kuwa tukio la kifamilia, likithibitisha kwamba mapenzi ya kweli hayahitaji hadhira kubwa ili kung’aa.

Read More
 Shorn Arwa Awapa Somo Mabinti Baada ya Tukio la Aibu Luo Festival

Shorn Arwa Awapa Somo Mabinti Baada ya Tukio la Aibu Luo Festival

Mwanamitindo maarufu nchini Kenya, Shorn Arwa, ametoa somo kwa wanawake kuhusu maadili na kujithamini, akiwaasa kujitafutia fedha badala ya kutegemea wanaume kwa msaada wa kifedha. Kupitia mitandao ya kijamii, Arwa ameeleza masikitiko yake kufuatia matukio aliyoshuhudia katika tamasha la Luo Festival, akisema baadhi ya tabia zilizojitokeza ni za aibu na zinapaswa kukemewa. Arwa amedai kuwa baadhi ya warembo walijidhalilisha kwa kufanya vitendo vya aibu hadharani ili kupata tiketi za kuingia kwenye tamasha hilo. Ameeleza kuwa wanawake wengi walijikuta wakifanya mapenzi na wanaume kwenye nyasi ili kupata tiketi, hali ambayo ametaja kuwa ya kusikitisha. Mrembo huyo amesisitiza kuwa kila mwanamke ana haki na uwezo wa kufanikisha maisha yake bila kulazimika kupitia njia za kudhalilisha utu wake. Pia amehimiza umuhimu wa wanawake kujitafutia kipato na kuepuka utegemezi wa kupita kiasi kwa wanaume, akiongeza kuwa mustakabali wa wanawake ni wenye matumaini makubwa. Ujumbe huo wa Shorn Arwa umeibua mjadala mitandaoni, wengi wakimuunga mkono kwa kuhimiza wanawake kujitegemea na kulinda heshima zao, huku wengine wakisisitiza umuhimu wa elimu ya kujikimu kimaisha kwa vijana.

Read More
 Jose Chameleone na Juliet Zawedde Wazua Gumzo kwa Mabusu Jukwaani

Jose Chameleone na Juliet Zawedde Wazua Gumzo kwa Mabusu Jukwaani

Staa wa muziki kutoka Uganda, Jose Chameleone, amezua mjadala mpya mtandaoni baada ya kuonekana akiwa na ukaribu wa kimahaba na mfanyabiashara maarufu anayeishi Marekani, Juliet Zawedde, katika tamasha la usiku lililofanyika jana. Wawili hao, ambao uhusiano wao wa karibu umekuwa ukileta minong’ono kwa muda mrefu, waliibua shangwe na nderemo kutoka kwa mashabiki waliokuwa ukumbini baada ya kubusiana hadharani jukwaani, hali iliyowafanya mashabiki kuzidi kudai kwa sauti kuwa uhusiano wao upewe hadhi rasmi ya ndoa. Zawedde aliwasili Uganda wiki iliyopita kusherehekea siku yake ya kuzaliwa, huku sherehe kuu ikifanyika Julai 19 katika klabu ya Noni Vie jijini Kampala. Hata hivyo, Chameleone hakuweza kuhudhuria tukio hilo kutokana na kuwa safarini mjini Bujumbura. Lakini jana usiku, wawili hao walipata nafasi ya kukutana tena jukwaani, na tukio hilo lilibadilika kuwa burudani ya kipekee kwa mashabiki waliokuwa wamehudhuria. Video inayosambaa kwa kasi mitandaoni inaonesha Zawedde akipanda jukwaani, kumkumbatia Chameleone kwa nguvu, kisha kumbusu kwa mikono miwili usoni mbele ya umati mkubwa uliokuwa ukishangilia. Kitendo hicho kimewasha moto mpya kwenye mitandao ya kijamii, ambapo mashabiki wengi wamekuwa wakiandika maoni ya kuwataka wawili hao kuhalalisha penzi lao. Hadi sasa, hakuna mmoja kati yao aliyetoa kauli rasmi kuhusu hatua inayofuata katika uhusiano wao, lakini wazi ni kwamba mashabiki wao wana matumaini makubwa kuona penzi hili likibadilika kutoka ‘urafiki wa karibu’ na kuwa rasmi zaidi. Hii si mara ya kwanza wawili hao kuhusishwa kimapenzi, lakini tukio la jana linaonekana kama uthibitisho mpya wa ukaribu wao unaozidi kushika kasi mbele ya macho ya umma.

Read More
 Nay wa Mitego, Billnass na Nandy Wazozana Hadharani

Nay wa Mitego, Billnass na Nandy Wazozana Hadharani

Mzozo mkali wa maneno umeibuka tena kwenye mitandao ya kijamii kati ya wasanii wa muziki wa Bongo Fleva, Nay wa Mitego, Billnass na mkewe Nandy, ukihusisha tuhuma za fitna, chuki na wivu wa maendeleo. Chanzo cha mvutano huo ni kauli ya Billnass aliyodai kuwa alipitia fitna za kutaka kufungwa kwa kesi ya wizi ambayo Nay wa Mitego alihusishwa nayo kwa kauli zisizo rasmi. Billnass, kupitia mahojiano yake na East Africa Radio, alionesha wazi kutoridhishwa na kile alichokiita hila zilizopangwa dhidi yake na watu aliowahi kuwachukulia marafiki. Baada ya maneno hayo, Nay wa Mitego hakusita kujibu kupitia sehemu ya maoni kwenye posti hiyo. Nay alimtaja Billnass kuwa ni msanii mjinga anayependa kiki bila mipaka na kumuita mwizi ambaye alistahili hata kifungo kwa tabia zake. “Acha nikupe unachotaka, wewe ni mwizi, ungeenda jela kwa tabia yako ya wizi. Nina kazi nyingi za kufanya, siwezi kushughulika na kukukandamiza wewe. Mgande Nandy ivyo ivyo ili usije ukaendelea na udokozi,” aliandika Nay wa Mitego. Kauli hiyo iliwasha moto zaidi pale mke wa Billnass, msanii Nandy, alipoamua kumjibu Nay moja kwa moja kwa hasira kali. Kupitia sehemu ya maoni, Nandy alimshutumu Nay kwa wivu na kumuita mvuta bangi, huku akidai kuwa ana chuki kutokana na kushindwa kimaisha. “Nay wa Mitego wewe cho…k…o, jina langu limeingiaje hapo? Mvuta bangi wewe! Una wivu wa maendeleo. Umejaribu kupambana umeshindwa, umebaki kuwa shabiki. Wa kuibiwa muibiwe nyie, na mnacho cha kuibiwa kwanza? Endelea na chaka zako ujikomboe, maisha upande huu mzito boob utasanda! Kithetheeee wewe, fyuu,” aliandika Nandy kwa hasira. Mashabiki kwenye mitandao wamegawanyika, baadhi wakimtetea Nay kwa kusema anasema ukweli bila uoga, huku wengine wakimtaka apunguze maneno ya matusi na wivu. Wengine wamewaomba wasanii hao warekebishe tofauti zao kwa hekima na busara badala ya kurushiana maneno hadharani. Kwa sasa, hakuna dalili za pande hizi kupoa, na mashabiki wanaendelea kufuatilia kwa karibu kuona ni nani atarushia dongo linalofuata.

Read More
 Wakili wa Cardi B Ajibu Kesi ya Kipaza Sauti

Wakili wa Cardi B Ajibu Kesi ya Kipaza Sauti

Wakili wa rapa kutoka Marekani Cardi B, Drew Findling, ameibuka na kuikosoa vikali kesi mpya ya madai iliyofunguliwa dhidi ya mteja wake, akisema ni jaribio la kutaka kumpora pesa kwa kutumia jina lake maarufu. Kauli ya Findling imekuja kufuatia mwanamke mmoja, anayetambulika kama Jane Doe, kufungua kesi ya madai dhidi ya Cardi B kwa tuhuma za shambulio la mwili, uzembe na dhuluma ya kihisia, akidai kuwa alijeruhiwa baada ya kurushiwa kipaza sauti na rapa huyo wakati wa tamasha la Drai’s Beachclub huko Las Vegas mnamo Agosti 2023. Kwa mujibu wa maelezo ya Jane Doe, Cardi B alikuwa akitumbuiza katika hafla ya mchana iliyokuwa ikifanyika wakati wa joto kali, ambapo aliwaomba mashabiki wamwagie maji ili kupooza. Mwanamke huyo anasema alifanya hivyo kwa nia njema, lakini alichokutana nacho ni kurushiwa kipaza sauti kwa nguvu na Cardi B, kitendo ambacho sasa anadai kilimsababishia madhara ya kimwili na kiakili. Ingawa tukio hilo lilichukua sura kubwa mitandaoni wakati huo, uchunguzi wa polisi haukupelekea kufunguliwa kwa mashtaka yoyote ya jinai dhidi ya Cardi B. Polisi waliamua kufunga jalada hilo baada ya kukosa ushahidi wa kutosha, na kesi hiyo haikuwahi kufika kwa Mwendesha Mashtaka wa Kaunti. Hata hivyo, Jane Doe sasa ameamua kufungua kesi ya madai miaka miwili baadaye, akidai kuwa hata mnada wa kipaza sauti hicho kwa ajili ya shughuli za hisani ulimvuruga kisaikolojia na kumrudisha katika hali ya huzuni aliyoipitia baada ya tukio hilo. Mashabiki wa Cardi B wamejitokeza mitandaoni wakimtetea msanii huyo, wengi wakisema mwanamke huyo alitafuta kiki na sasa anajaribu kutumia tukio la zamani kujinufaisha kifedha. Hadi sasa, Cardi B hajatoa tamko la moja kwa moja kuhusu kesi hiyo mpya, lakini timu yake ya kisheria imeweka wazi kuwa wataipinga vikali hadi mwisho.

Read More
 Google Yazindua Mfumo Mpya wa Kudhibiti Ad Blockers kwa Chrome

Google Yazindua Mfumo Mpya wa Kudhibiti Ad Blockers kwa Chrome

Kampuni ya teknolojia ya Google imeanzisha mfumo mpya wa kudhibiti na kuzuia matumizi holela ya extensions (viongezo) vinavyotumika kuzima matangazo kwenye kivinjari chake cha Chrome. Hatua hii inalenga kulinda mapato yanayotokana na matangazo, ambayo ni chanzo kikuu cha fedha kwa kampuni hiyo. Kwa mujibu wa taarifa rasmi kutoka Google, mfumo huo mpya utahakikisha kuwa extensions zote zinazozuia matangazo zinatekeleza sera mpya za usalama na uwazi. Hii ni pamoja na matumizi ya Manifest V3, mfumo wa kisasa unaolenga kudhibiti namna viongezo vinavyoingiliana na tovuti na taarifa za watumiaji. Hatua hiyo imeibua mjadala mkubwa miongoni mwa watumiaji wa intaneti na wapenda faragha, kwani wengi walitegemea extensions kama AdBlock na uBlock Origin kuondoa matangazo yanayokera na kurahisisha matumizi ya mtandao. Google imesema haitapiga marufuku moja kwa moja extensions zote za kuzuia matangazo, lakini zile ambazo hazitazingatia viwango vipya, zitafutwa kutoka kwenye Chrome Web Store. Kampuni hiyo imesisitiza kuwa inalenga kuweka uwiano kati ya faragha ya mtumiaji, utendaji wa kivinjari, na kulinda mazingira ya watengenezaji maudhui wanaotegemea mapato ya matangazo. Wadau wa teknolojia wameonya kuwa mabadiliko haya huenda yakapunguza uhuru wa watumiaji kuchagua namna wanavyotumia mtandao, huku wengine wakitafsiri kama juhudi za Google kuhakikisha kuwa matangazo yake yanaonekana zaidi kwa watumiaji wa Chrome duniani kote.

Read More
 WhatsApp Kuleta Muhtasari wa Meseji Kupitia Teknolojia ya Akili Bandia

WhatsApp Kuleta Muhtasari wa Meseji Kupitia Teknolojia ya Akili Bandia

Kampuni ya Meta, inayomiliki WhatsApp, imetangaza kuwa inafanyia majaribio kipengele kipya cha akili bandia (AI) kitakachowezesha watumiaji wake kufupisha mazungumzo marefu kwenye meseji. Kwa kutumia teknolojia ya AI, WhatsApp itawaruhusu watumiaji kupata muhtasari wa haraka wa mazungumzo yao, jambo ambalo linalenga kusaidia wale wanaopokea ujumbe mwingi au ambao hawakuwahi kufuatilia kila ujumbe mmoja mmoja. Kipengele hiki kinatarajiwa kufanya kazi kwa kuchambua mazungumzo ya kundi au mtu binafsi, kisha kutoa muhtasari wa mambo muhimu yaliyojadiliwa, huku kikihifadhi usalama na faragha ya watumiaji kwa kutumia teknolojia ya usimbaji wa mwisho kwa mwisho (end-to-end encryption). Taarifa kutoka kwa baadhi ya watumiaji waliopata toleo la majaribio zinasema kuwa kipengele hicho kiko chini ya sehemu ya “Chat Summary,” ambapo AI inaweza kutoa dondoo fupi kuhusu mazungumzo yaliyopita. Hii ni moja kati ya hatua kadhaa ambazo Meta imeanza kuzitekeleza ili kuimarisha matumizi ya AI kwenye majukwaa yake, ikiwa ni pamoja na kuanzisha wasaidizi wa kidijitali ndani ya WhatsApp na Messenger. Hadi sasa, Meta haijatoa tarehe rasmi ya kuachia kipengele hicho kwa watumiaji wote, lakini matarajio ni kuwa kitakuwa sehemu ya masasisho yajayo ya WhatsApp mwaka huu

Read More
 6ix9ine Akiri Kumiliki Madawa ya Kulevya, Hukumu Yasubiriwa Septemba

6ix9ine Akiri Kumiliki Madawa ya Kulevya, Hukumu Yasubiriwa Septemba

Rapa wa Marekani, Tekashi 6ix9ine, amekiri makosa ya kumiliki madawa ya kulevya kufuatia msako uliofanywa katika nyumba yake mjini Miami mwezi Machi mwaka huu. Kwa mujibu wa taarifa za mahakama, 6ix9ine alikiri mbele ya jaji kuwa alikuwa na dawa za kulevya aina ya cocaine na MDMA (ecstasy), jambo ambalo linakiuka masharti ya probation aliyowekewa baada ya kesi yake ya mwaka 2018 inayohusiana na kundi la uhalifu la Nine Trey Gangsta Bloods. Msako huo wa Machi 2025 uliendeshwa na polisi wa Miami baada ya kupata taarifa za uhusiano wa rapa huyo na shughuli za uhalifu. Madawa hayo yalipatikana kwenye nyumba yake, na uchunguzi zaidi ukaonesha uvunjifu wa masharti ya muda wake wa majaribio (probation). Mahakama imepanga kutoa hukumu ya kesi hiyo mwezi Septemba 2025, huku wengi wakisubiri kuona iwapo 6ix9ine atapewa kifungo cha gerezani au adhabu mbadala. Kesi hii inaongeza msururu wa matatizo ya kisheria yanayomkabili rapa huyo, ambaye tangu afungue ukurasa mpya baada ya kutoa ushahidi dhidi ya wanachama wa genge la Nine Trey, amekuwa akigonga vichwa vya habari kwa matukio ya utata.

Read More
 Cardi B Kizimbani: Ashtakiwa kwa Kumrushia Shabiki Kipaza Sauti

Cardi B Kizimbani: Ashtakiwa kwa Kumrushia Shabiki Kipaza Sauti

Staa wa muziki wa Hip Hop Cardi B anakabiliwa na kesi ya kisheria kufuatia tukio la mwaka 2023 ambapo alinaswa kwenye video akimrushia shabiki wake kipaza sauti wakati wa onyesho moja jijini Las Vegas, Marekani. Kwa mujibu wa hati za mahakama zilizowasilishwa hivi karibuni, shabiki huyo ambaye jina lake halijawekwa wazi, anadai kuwa aliumia baada ya Cardi B kurusha kipaza sauti kwa hasira, kitendo kinachodaiwa kuwa ni shambulio, unyanyasaji wa mwili na uzembe. Tukio hilo lilitokea wakati wa onyesho la Cardi B mwezi Julai 2023, ambapo inasemekana msanii huyo alikasirishwa na kitendo cha shabiki kumrusha kinywaji akiwa jukwaani. Katika kile kinachoelezwa kuwa ni kisasi, Cardi alionekana akirusha kipaza sauti kwa nguvu kuelekea kwenye kundi la mashabiki. Ingawa hakukuwa na mashtaka ya jinai yaliyowasilishwa wakati huo, kesi hii mpya inaweza kumgharimu Cardi B fedha nyingi na kuathiri jina lake kwenye muziki. Wakili wa mlalamikaji anasema mteja wake alipata majeraha ya mwilini na pia mshtuko kutokana na tukio hilo.

Read More
 Marioo Aendeleza Mafanikio ya The Goson Album kwa Toleo la Deluxe

Marioo Aendeleza Mafanikio ya The Goson Album kwa Toleo la Deluxe

Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Marioo, sasa anajiandaa kuachia rasmi Deluxe Edition ya albamu yake “The Goson”, ikiwa ni miezi saba imepita tangu atoe albamu yake hiyo iliyopata mapokezi makubwa kutoka kwa mashabiki zake. Kwa mujibu wa taarifa, Marioo ameongeza nyimbo kadhaa mpya kwenye toleo hilo maalum, hatua ambayo inalenga kuwapa mashabiki wake ladha zaidi ya kazi zake za kisanaa. Ingawa hajatangaza rasmi orodha kamili ya nyimbo zitakazojumuishwa kwenye Deluxe, vyanzo vya karibu na msanii huyo vinaashiria kuwa baadhi ya nyimbo hizo tayari zimekamilika na zinasubiri muda sahihi wa kuachiwa. Hii si mara ya kwanza kwa Marioo kutumia mbinu ya Deluxe Edition. Wafuasi wake watakumbuka kuwa albamu yake ya awali, The Kid You Know, nayo ilipata toleo la Deluxe ambalo lilijumuisha vibao vipya kama Nikazama na Sing, ambavyo vilipata mapokezi makubwa.

Read More
 Eddy Kenzo Atetea Hadhi Yake ya Kimataifa Baada ya Kukejeliwa na Bebe Cool

Eddy Kenzo Atetea Hadhi Yake ya Kimataifa Baada ya Kukejeliwa na Bebe Cool

Msanii maarufu wa Uganda na mshindi wa tuzo za kimataifa, Eddy Kenzo, amemjibu vikali Bebe Cool kufuatia kauli yake aliyodai kuwa hakuna msanii wa kiwango cha kimataifa nchini Uganda kwa sasa akiwemo Kenzo mwenyewe. Katika mahojiano yake na kituo kimoja cha runinga, Kenzo ameeleza kuwa hana haja ya kuthibitisha thamani yake kwa mtu yeyote, kwani mafanikio yake yanajieleza yenyewe. Amemtaja Bebe Cool kama mbinafsi asiye na uelewa wa hali halisi ya soko la muziki duniani. Kauli ya Kenzo imekuja mara baada ya Bebe Cool kudai katika mahojiano na mtangazaji Kasuku kwamba Eddy Kenzo hajafikia kiwango cha kuwa msanii wa kimataifa, licha ya kuwa na tuzo na kutambulika Afrika. Mvutano huu umeibua mjadala mkubwa mitandaoni, huku mashabiki wa pande zote mbili wakitupiana maneno. Wengi wanamtetea Kenzo kama nembo ya muziki wa Uganda duniani, huku wengine wakisema Bebe Cool anaangalia mafanikio ya kimataifa kwa mizani tofauti. Hii si mara ya kwanza wawili hao kutofautiana. Mnamo mwezi Juni mwaka huu, walitupiana maneno makali kuhusu tamasha la Diamond Platnumz lililofanyika huko Ntungamo, kila mmoja akionesha msimamo tofauti.

Read More