Lizer Classic Amkataa S2kizzy, Asema Hana Historia ya Kuwatoa Wasanii
Prodyuza wa muziki kutoka Tanzania, Lizer Classic, ameibua mjadala baada ya kumkataa S2kizzy kama prodyuza bora wa muziki wa Bongo Fleva. Lizer amesema kuwa licha ya S2kizzy kujinadi sana kuwa ndiye kinara wa utayarishaji wa muziki kwa sasa, hana historia ya kuwatoa wasanii wapya kwenye tasnia. Kwa mujibu wa Lizer, ukubwa wa prodyuza hupimwa si tu kwa hits anazotengeneza, bali pia kwa mchango wake katika kukuza na kulea vipaji vipya. Ametolea mfano Master Jay na P Funk Majani, ambao amewapongeza kwa kuwa nguzo kubwa za muziki wa Bongo Fleva kutokana na lebo zao zilizozalisha wasanii wengi waliokuja kuwa majina makubwa. Kauli ya Lizer imezua mjadala mitandaoni, huku baadhi ya mashabiki wakimtetea S2kizzy kwa ubunifu na kazi kubwa alizofanya, ilhali wengine wakikubaliana na mtazamo wa Lizer kwamba mchango wa kudumu kwenye tasnia hupimwa zaidi kwa kizazi unachoibua.
Read More