Afande Sele Afunga Ndoa na Mpenzi wake wa Muda Mrefu

Afande Sele Afunga Ndoa na Mpenzi wake wa Muda Mrefu

Msanii mkongwe wa Bongofleva Seleman Msindi, maarufu kama Afande Sele, ameanza ukurasa mpya maishani baada ya kufunga ndoa na mpenzi wake Wema Raphael Makongoro jana, Desemba 6, 2025, katika hafla iliyofanyika mkoani Morogoro. Ndoa hiyo imefungwa kiserikali mbele ya Katibu Tawala wa Wilaya ya Morogoro, Hilary Sagara, na kuhudhuriwa na ndugu, wasanii, marafiki wa karibu pamoja na jamaa mbalimbali waliokusanyika kushuhudia tukio hilo muhimu. Kwa Afande Sele, hili ni penzi jipya baada ya kupoteza mke wake wa kwanza, Mama Tunda, aliyefariki dunia Agosti 14 mwaka 2014. Tukio la jana limeonekana kuwa sura mpya yenye matumaini mapya kwa msanii huyo, ambaye amekuwa mmoja wa sauti muhimu katika muziki wa hip-hop nchini Tanzania. Sherehe za ndoa hiyo zilijawa na furaha, pongezi na hisia za upendo kutoka kwa waliohudhuria, huku mashabiki mtandaoni wakimiminika kumpongeza msanii huyo kwa hatua hiyo muhimu ya maisha.

Read More
 Afande Sele apinga ujio wa kocha mpya Simba

Afande Sele apinga ujio wa kocha mpya Simba

Mkongwe wa muziki wa Bongo Fleva, Seleman Msindi maarufu ‘Afande Sele’ amezijia juu Klabu za Simba na Yanga kwa kuzitaja kama makaburi ya Soka la Bongo. Afande Sele ametumia ukurasa wake wa Instagram akieleza kwenye andiko lake ambapo akizilaumu Simba na Yanga kwa kusema zimekua zikiua Soka la Tanzania na akaenda mbali zadi kwa kutoa shutuma za kupanga matokeo kwa kununua wachezaji wa timu pinzani na waamuzi, ili kushinda michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara, eti kwa kisingizio cha kuwa Mabingwa. Mkongwe huyo pia amegusia suala la Simba kumleta Kocha Mkuu mpya kutoka nchini Brazil, Roberto Oliveira Gonçalves do Carmo ‘Robertinho’, ili hali tayari wamekua na Kocha Mzawa Juma Mgunda, ambaye ameonesha kuwa na mustakabali mzuri wa kuipa matokeo timu katika Michuano ya Kimataifa na ile ya ndani ya Tanzania Bara. Afande Sele yeye anaona Simba haikuwa na sababu ya kuchukua Kocha wa nje wakati huu, anasema hatoshangaa kuona timu ikivurugika na kupoteza mwelekeo zaidi badala ya kuimarika

Read More