Waandaaji wa Tamasha la Asake na Gabzy Washtakiwa kwa Uzembe

Waandaaji wa Tamasha la Asake na Gabzy Washtakiwa kwa Uzembe

Familia ya marehemu Karen Lojore imewasilisha rasmi kesi mahakamani ikidai fidia ya Shilingi milioni 100 za Kenya kufuatia kifo cha binti huyo kilichotokea katika tamasha la muziki lililofanyika Uwanjani Nyayo mwezi Disemba mwaka jana. Kwa mujibu wa nyaraka zilizowasilishwa mahakamani, Karen alipoteza maisha baada ya kutokea msongamano mkubwa wa watu (crowd surge) wakati wa tamasha lililowahusisha wasanii Asake na Gabzy. Familia inadai tukio hilo lingeweza kuzuilika iwapo hatua stahiki za usalama zingechukuliwa. Katika kesi hiyo, waandaaji wa tamasha hilo, Tukutane Entertainment, wametajwa kama wadaiwa wakuu, wakituhumiwa kushindwa kuhakikisha usalama wa kutosha kwa mashabiki waliohudhuria hafla hiyo. Familia ya marehemu inaeleza kuwa uzembe katika maandalizi na udhibiti wa umati wa watu ndio uliopelekea kupotea kwa maisha ya Karen. Familia sasa inaitaka mahakama kutoa haki kwa marehemu kwa kuwalazimisha wahusika kuwajibika, huku wakisisitiza kuwa fidia wanayodai ni kwa ajili ya madhara makubwa ya kihisia, kiakili na kifamilia waliyopata kutokana na kumpoteza mpendwa wao.

Read More
 Asake Atoa Tamko la Huzuni Kufuatia Kifo cha Sha Katika Tamasha la Nyayo Stadium

Asake Atoa Tamko la Huzuni Kufuatia Kifo cha Sha Katika Tamasha la Nyayo Stadium

Msanii wa Afrobeat kutoka Nigeria, Asake, ameeleza masikitiko yake makubwa kufuatia kifo cha Karen Lojore, mwenye umri wa miaka 20, aliyefariki dunia baada ya kukanyagwa wakati wa tamasha alilokuwa akiongoza jijini Nairobi, Kenya. Kupitia taarifa, Asake amesema tukio hilo limemuumiza sana na kuacha majonzi makubwa kwake binafsi pamoja na timu yake. Amesema moyo wake uko pamoja na familia, marafiki na wapendwa wa marehemu Karen Lojore katika kipindi hiki kigumu cha majonzi. Aidha, ameahidi kushirikiana kikamilifu na juhudi zote za uchunguzi ili kufahamu kilichosababisha tukio hilo la kusikitisha. Asake pia amesisitiza umuhimu wa uwajibikaji, akieleza kuwa wote waliohusika na uzembe wa kiusalama wanapaswa kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria. Kauli hiyo imekuja huku familia na marafiki wa marehemu wakiendelea kuitaka serikali na vyombo husika kufanya uchunguzi wa kina na kuhakikisha haki inatendeka. Tamasha hilo, lililojulikana kama Asake and Gabzy Live in Nairobi, liliandaliwa na kampuni ya Tukutane Entertainment. Waandaaji hao wamesema wanashirikiana kwa karibu na mamlaka husika ili kubaini chanzo halisi cha tukio hilo na mazingira yaliyosababisha msongamano mkubwa wa mashabiki.

Read More