Bahati Awashukuru Mashabiki kwa Kumpongeza kwa Muonekano Mpya Licha ya Video Kuzua Maswali

Bahati Awashukuru Mashabiki kwa Kumpongeza kwa Muonekano Mpya Licha ya Video Kuzua Maswali

Mwanamuziki wa Kenya, Bahati, amezua gumzo mitandaoni baada ya kuwashukuru mashabiki wake kwa pongezi walizompa kuhusu muonekano wake mpya bila nywele. Kupitia video aliyochapisha kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii, Bahati alidai kuwa alinyoa rasta zake kufuatia kichapo cha timu yake ya Arsenal mikononi mwa PSG, katika mechi ya hivi karibuni ya UEFA Champions League. Katika ujumbe wake kwa mashabiki, Bahati alisema: “Nimeanza kujipenda zaidi bila nywele. Nimejifunza kuwa upendo wa kweli huanza na wewe mwenyewe.” Hata hivyo, kilichozua utata ni ubora wa video hiyo, ambayo inaonyesha mabadiliko ya haraka ya uhariri (transition), huku dreadlocks zake zikiendelea kuonekana kwa vipindi tofauti ndani ya video hiyo. Baadhi ya mashabiki walihoji iwapo alinyoa kweli au kama ilikuwa ni kiki ya mitandao. Katika sehemu ya maoni, baadhi ya mashabiki walitoa pongezi wakisema muonekano wake mpya unampendeza na unampa sura ya “umakini mpya”, huku wengine wakitilia shaka ukweli wa madai yake. “Bahati hata kama ni kiki, umetuburudisha. Ila tuambie ukweli – hizo rasta bado zipo ama?” aliandika mmoja wa mashabiki. Muimbaji huyo, anayejulikana kwa kubadili mitindo ya maisha hadharani, ameendelea kuvutia vichwa vya habari kwa sababu mbalimbali kuanzia maisha ya ndoa, siasa, hadi mitindo ya uvaaji. Sasa, inaonekana hata nywele zimeingia kwenye orodha ya vitu vinavyoleta mjadala. Hadi sasa, Bahati hajatoa kauli rasmi kuhusu video hiyo au kama kweli alinyoa, lakini haijazuia mashabiki wake kuendelea kutoa maoni mseto kati ya wanaomsifu na wanaohoji ukweli wa mabadiliko yake

Read More
 Willy Paul akosolewa kwa kutumia Kshs millioni 3.5 kuandaa video ya wimbo wake

Willy Paul akosolewa kwa kutumia Kshs millioni 3.5 kuandaa video ya wimbo wake

Staa wa muziki nchini Kenya Willy Paul anazidi kupata ukosoaji mkubwa kutoka kwa mashabiki mbali mbali wa muziki baada ya msanii huyo kuweka wazi kuwa alitumia kiasi cha shillingi millioni 3.5 kuandaa video ya wimbo wake mpya ‘Keki’ aliyomshirikisha Bahati. Kupitia post aliyochapisha kwenye ukurasa wake wa Instagram akijinadi kutumia kiasi hicho cha fedha kwenye uandaaji wa video ya ngoma hiyo, baadhi ya mashabiki walioachia maoni yao kwenye chapisho hilo wameonekana kutofurahia viwango alivyoonesha kwenye nyimbo alizoziachia rasmi Januari 31 ambazo ni Keki pamoja na Paah. Kulingana na kauli za mashabiki, licha ya Willy Paul kutumia nguvu nyingi kutangaza ujio wa kazi hizo, alifeli kwenye suala la uandishi wa nyimbo wakihoji kuwa msanii ameishiwa na ubunifu wa kutoa nyimbo za kuvutia. Aidha wamempa changamoto kuwatafuta waandishi wazuri wa nyimbo na kuwalipa ili waweze kumuandikia nyimbo ambazo zina maudhui ya kuburudisha jamii sambamba na kuelimisha. Katika hatua nyingine wamemshauri kubadilisha prodyuza anayetayarisha kazi zake za muziki kutokana na kukosa ubunifu wa kuandaa nyimbo zinazoendana na nyakati zilizopo. Willy Paul ambaye yupo mbioni kuandaa tamasha lake muziki mnamo Februari 14 mwaka huu amepokea ukosoaji mkubwa sio tu kutoka kwa mashabiki bali pia kutoka kwa maprodyuza wa muziki nchini, wa hivi punde akiwa ni prodyuza Vinc on The Beat ambaye ameonekana kutoridhishwa na kiwango cha msanii huyo baada ya kuachia nyimbo mbili kwa pamoja alizomshirikisha msanii Bahati ambaye ni hasimu wake wa muda mrefu kwenye muziki.

Read More
 Bahati adokeza ujio wa kolabo yake na Harmonize

Bahati adokeza ujio wa kolabo yake na Harmonize

Wakati bado Bahati anaendelea kufanya vizuri na wimbo wake mpya ‘Nowe Sweety,’ ameonyesha kuwa hataki kulaza damu kuhusu muziki,ameonekana ujio wa kazi yake mpya na msanii wa BongoFleva Harmonize. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Bahati amepost picha akiwa na Harmonize na kuandika ‘2023 are You Ready for Us??? Brother  @Harmonize_tz ‘ na Harmonize akajibu kwa kuandika ‘SEND IT BRO I HAVE ONLY ONE WATSP NUMBER LOVE YOU NO MARA WAA !!! GETO BOYS ‘. Iwapo Bahati atafanikiwa kuachia wimbo wake na Harmonize atakuwa ameongeza orodha ya wasanii wa Bongoflava aliofanya nao kazi ikizingatiwa kuwa ana kazi ya pamoja na  Rayvanny, Mbosso na Aslay.

Read More
 Diana B ashindwa kuficha hisia zake kwa mume wake Bahati

Diana B ashindwa kuficha hisia zake kwa mume wake Bahati

Mwanamitandao aliyegeukia muziki nchini Diana B ameamua kuwapa somo wanawake wa Kenya jinsi ya kuwaonyesha upendo wapenzi zao. Mama huyo wa watoto watatu ameshea video hii kwenye ukurasa wake wa Instagram akiwa anamlisha mume wake Bahati ambaye kwa sasa anaumwa. Kwenye posti yake hiyo ameandika ujumbe mzito wa mahaba kwenda kwa mume wake huyo ambaye alionekana kudeka na kitendo hicho huku akimhakikishia kumpenda kwa shida na raha. “In Sickness and in Good Health, Mapenzi Tight kama kifuniko ya gas “, Aliandika. Hata hivyo watumiaji wa mitandao ya kijamii wameonekana kukoshwa na upendo wa wawili hao huku wengi wakiahapa kufuta nyayo zao kwa ajili ya kuboresha mahusiano yao. “Mapenzi wewe any time I pass through dee and bahaa…. I feel I need a man in my life… 2023 wewe lazima mr right akuwe nimechokaa kuangalia ya wenyewe,” Mtumiaji mmoja wa mitandao ya kijamii aliandika.

Read More
 Weezdom akiri kupatwa na msongo wa mawazo kisa Bahati

Weezdom akiri kupatwa na msongo wa mawazo kisa Bahati

Msanii Weezdom amefunguka kupatwa na msongo wa mawazo baada ya kuachana na aliyekuwa bosi wake chini ya label ya EMB Records, Bahati. Kwenye mahojiano na Podcast ya EMM, amesema tangu uhusiano wake na Bahati kuingiwa na ukungu, ilikuwa vigumu kwake kujikimu kimaisha jambo lilimpelekea kuchukua maamuzi magumu na kuanza kubugua pombe kupindukia kama njia ya kukimbia changomoto za maisha. Msanii huyo amesema ulevi ulimfanya kupoteza mweelekeo kiasi cha kusahau kufanya muziki. Hata hivyo amesema anamshukuru mwenyezi Mungu kwa kumtoa kwenye tatizo la ulevi baada ya wasamaria wema kujitokeza na kumsaidia kuondokana na matumizi ya pombe.

Read More
 Bahati akoshwa na wimbo wa Dullah Makabila, “Pita Huku”

Bahati akoshwa na wimbo wa Dullah Makabila, “Pita Huku”

Mwimbaji nyota wa muziki toka Kenya, Bahati ameonyesha kukoshwa na ubunifu alioutumia staa wa Singeli nchini, msanii Dulla Makabila kwenye video ya wimbo wake mpya Pita Huku ulioibua mijadala juu ya mengi kufuatia yaliyo zungumziwa kwenye wimbo huo. Akiacha koment kwenye video hiyo katika mtandao wa YouTube, ujumbe wa Bahati unasomeka, “Huu ni Ubunifu Kaka Yangu. Hongera kwa Muziki mzuri”. Mbali na Bahati pia na wengine wengi wameacha komenti zao wakiusifia ubunifu uliofanywa kwenye kazi hiyo. Wimbo wa “Pita Huku” ambao umetoka Jumatatu ya wiki hii umefanikiwa kupata mapokezi makubwa kutoka kwa wadau mbalimbali wa muziki pamoja na mashabiki kwa ujumla.

Read More
 Bahati adai wakosoaji wake mtandaoni wanampa nguvu ya kutia bidii kimuziki

Bahati adai wakosoaji wake mtandaoni wanampa nguvu ya kutia bidii kimuziki

Mwanamuziki kutoka Kenya Bahati amedai kwamba hana muda wa kuwajibu wanaomkosoa mtandaoni. Hitmaker huyo wa Adhiambo amewaambia watesi wake kuwa chuki anayoipata kwenye mitandao ya kijamii inampa changamoto ya kutia bidii kwenye kazi zake za muziki. “Guys thank you so much for your support. Like we wouldn’t be here without you without your love, without your criticism, negativity, we take them in”, Aliandika Instagram. Bahati alisema hayo alipokuwa akizindua tuzo ya Golden Plaque aliyotunukiwa na mtandao wa YouTube kwa ajili ya kupata wafutialiaji (Subscribers) milioni moja. Bahati na mke wake Diana B wamekuwa wakikosolewa mitandaoni mwaka mzima kwa matukio ambayo wamekuwa wakijihusisha nayo na hawajaathirika kwa namna yeyote kwenye shughuli zao.

Read More
 Bahati apewa tuzo ya heshima Youtube

Bahati apewa tuzo ya heshima Youtube

Staa wa muziki nchini Bahati ametunukiwa tuzo ya Golden Plaque na mtandao wa Youtube baada ya kufikisha jumla ya subscribers millioni moja kwenye channel yake. Bahati ametumia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram kuwashukuru mashabiki zake kwa upendo ambao wanazidi kumuonyesha kupitia kazi zake za muziki huku akiahidi kuendelea kuwapa burudani zaidi. Channel ya youtube ya Bahati  ilifunguliwa rasmi Joined Agosti 7, mwaka 2012 na mpaka sasa imefikisha zaidi ya watazamaji millioni 193,565,094 huku ikiwa na jumla ya subscribers 1,090, 000. Bahati ni msanii wa pili nchini Kenya kupokea golden Plaque baada ya Otile Brown ambaye alikuw msanii wa kwanza nnchini kufikisha jumla y wafuatiliaji million moja YouTube. Itakumbukwa tuzo ya Golden plaque imekuwa ikitolewa kwa watoa maudhui kwenye mtandao wa Youtube ambao channel zao zinafikisha wafuatiliaji (subscribers) kuanzia 100,000 na kuendelea.

Read More
 Bahati athibitisha kufanya kolabo na Nick Minaj

Bahati athibitisha kufanya kolabo na Nick Minaj

Mwanamuziki wa Kenya Bahati amethibitisha kufanya kazi ya pamoja na Rapa kutoka Marekani Nicki Minaj. Bahati ameweka taarifa hiyo kupitia akaunti yake ya Instagram akifichua kuwa wataachia rasmi wimbo wao mwaka 2023. “2023, Bahati na Nicki Minaj imethibitishwa..,” ameandika kupitia Insta stori yake. Baadhi ya Mashabiki wametilia shaka habari hizo ikizingitiwa kuwa mwanamuziki huyo amekuwa akijihusisha sana na kiki kwa ajili ya kutengeneza mazingira ya kuzungumziwa kwenye vyombo vya habari. Kwa upande mwingine baadhi wamesema kuwa taarifa ya Bahati kufanya kolabo na Nicki Minaj inaweza kuwa na ukweli kwa sababu amekuwa akifanya kazi kwa bidii kwenye muziki wake. Hata hivyo mashabiki wake sasa wanasubiri kwa hamu 2023 wakiwa na matumaini makubwa kuwa wimbo huo utakuwa mkali zaidi . Nicki Minaj ambaye ni mmoja wa marapa bora zaidi wa kike duniani, kolabo hii na Bahati ikitoka inakuwa ni kolabo yake ya pili kushirikishwa na mwanamuziki toka Afrika baada ya Davido (Nigeria) kwenye wimbo “Holy Ground” uliotoka mwaka 2020.

Read More
 Bahati kufunga ndoa Novemba 30 mwaka huu

Bahati kufunga ndoa Novemba 30 mwaka huu

Mwanamuziki kutoka nchini Kenya Bahati ameashiria kufunga pingu za maisha na mama ya watoto wake Diana B mwishoni mwa mwezi huu. Bahati amedokeza hayo kwa picha ya kupitia ukurasa wake wa Instagram na kisha kuweka ishara ya pete ya ndoa ambayo ameambatanisha na ujumbe unaotaja tarehe 30/11 kufanya jambo la kihistoria. “30TH NOVEMBER 2022 ”, Ameandika. Hata hivyo ujumbe huo umezua hisia mseto miongoni mwa mashabiki zake ambapo wengi wamedai huenda Bahati akahalalisha ndoa yake na Diana B kwa njia ya harusi huku wengine wakihoji ni ujio wa ngoma yake mpya ambayo ana mpango wa kuachia siku hiyo. Ikumbukwe kwa sasa Bahati anafanya vizuri na singles zake mbili “My Beginning” na “Mambo ya Mhesh Remix” ambayo amemshirikisha Sosuun pamoja na Ssaru.

Read More
 Diana B anyosha maelezo kuhusu video iliyosambaa mtandaoni akikiri kutoka kimapenzi na wanaume wengi

Diana B anyosha maelezo kuhusu video iliyosambaa mtandaoni akikiri kutoka kimapenzi na wanaume wengi

Msaniii na  mwanamitandao maarufu kutoka Kenya Diana Marua amefunguka juu ya video iliyosambaa mtandaoni akikiri kuwa alitembea na wanaume wengi kimapenzi kwa ajili ya kukidhi mahitaji yake ya msingi. Kupitia ujumbe mrefu aliochapisha kwenye ukurasa wake wa Instagram Diana amesema aliweka wazi suala hilo kwa umma kwa lengo la kuwapa moyo vijana wanaopitia masha magumu. Lakini pia amewahimiza watoto wa kike kutokata tamaa kwenye ndoto zao na badala yake watie bidii kwani muda wao wa kupata mafanikio utafiki. Diana Marua ameongeza kuwa kama balozi mwema katika jamii anapaswa kuzungumzia magumu aliyoyapitia kwenye maisha yake badala ya kuangazia mazuri tu. Diana alichapisha video hiyo kwenye mitandao yake ya kijamii  mwaka 2020 wakati alipokuwa akipokea gari jipya aina Mercedes Benz alilozawadi na mume wake Bahati. Alikumbuka kipindi alikuwa anaishi maisha ya uchochole ambapo alilazimika kutoka kimapenzi na wanaume tofauti kwa ajili ya kupata pesa lakini pia kuendesha magari ambayo hakuwa anaweza kumudu wakati huo. Kwa sasa Diana ana hesabu baraka zake kama Mama ya watoto watano, Mke na mtengeneza maudhui kwenye mitandao ya kijamii.

Read More
 Diana B azua gumzo mtandaoni baada ya video yake akikiri kutoka kimapenzi na wanaume tofauti kusambaa

Diana B azua gumzo mtandaoni baada ya video yake akikiri kutoka kimapenzi na wanaume tofauti kusambaa

Watumiaji wa mitandao ya kijamii wametoa maoni mbali kuhusu video ya Diana Marua akiri hadharani kutoka kimapenzi na wanaume tofauti kwa ajili ya pesa. Diana alichapisha video hiyo mwaka 2020 mtandaoni ambapo alidai kwamba kabla ya kukutana na mume wake Bahati alikuwa anachepuka na wanaume wengi kwa lengo la kukidhi mahitaji yake ya msingi. Haikushia hapo alienda mbali zaidi na kusema kuwa kipindi ana umri wa miaka 20 pesa haikuwa shida kwake kwani kila mwanaume aliyekuwa kwenye mahusiano naye alikuwa anamhudumia ipasavyo ikiwemo kumlipia kodi sambamba na kumnunulia chakula na mavazi. “I dated guys for money I had people who used to give me 10k, kuna mtu anakupatia 30k, anakupea 20k, nilikuwa na mtu wa kunifanyai shopping ya nyumba , nilikuwa na mtu wa kuni buyia manguo , unajua All I wanted was to live well..”, Alisema Video hiyo ambayo imesambaa kwenye mitandao ya kijamii imeibua hisia mseto miongoni mwa wakenya ambapo wengi wamehoji kuwa Diana B bado ana tamaa ya pesa na huenda akamkimbia bahati ikitokea amefilisika kiuchumi. Hata hivyo wengine wamesema kuwa watu waache kumhukumu mwanamama huyo wa watoto watatu kwa kuwa amebadili mienendo yake ya zamani ikizingatiwa kuwa ametulia na analea familia ya mwimbaji huyo.

Read More