BAHATI ANYANG’ANYWA CHETI CHA KUWANIA UBUNGE MATHARE

BAHATI ANYANG’ANYWA CHETI CHA KUWANIA UBUNGE MATHARE

Mwanamuziki aliyegeukia siasa Bahati amenyang’anywa tiketi ya kuwania ubunge wa Mathare kupitia chama cha Jubilee ikiwa ni siku chache zimepita tangu ashinde kwenye uchaguzi wa mchujo wa chama hicho. Katika mkao na wanahabari Bahati amesema alishurutishwa kujiuzulu kama mgombea wa kiti cha ubunge wa Mathare katika Uchaguzi Mkuu wa Agosti 9 mwaka huu baada ya muungano wa Azimio la Umoja kuamua kumuunga mkono mgombea wa ODM ambaye ni mbunge wa sasa Tom Oluoch. Hata hivyo, amemtaka Kiongozi wa Chama cha Jubilee Rais Uhuru Kenyatta na kinara wa ODM Raila Odinga kuwapa wakazi wa Mathare nafasi ya kumchagua mbunge wao wanayempenda kwa kuwa alijiunga na siasa baada ya kupewa shinikizo na wapiga kura wa eneo hilo. Utakumbukwa Mnamo Machi 18, Bahati alitangaza kuwa amejiunga na chama tawala cha jubilee na alikabidhiwa tikiti ya moja kwa moja na chama hicho kuwania kiti cha ubunge wa Mathare

Read More
 BAHATI NA DIANA MARUA WATANGAZWA MABALOZI WA OPPO KENYA

BAHATI NA DIANA MARUA WATANGAZWA MABALOZI WA OPPO KENYA

Kampuni ya OPPO inayojishughulisha na  uzalishaji na usambazaji wa simu na vifaa vingine vya kielectroniki imemtangaza rasmi  Bahati na mke wake Diana Marua kuwa mabalozi wake. Katika taarifa rasmi iliyochapishwa kwenye mtandao wa instagram katika page ya Oppo Kenya imeeleza kuwa wamefurahi kumkaribisha Bahati pamoja na Diana Marua kuwa balozi wa Oppo. “We partnered with @wabosha_maxine @bahatikenya @diana_marua to officially introduce you all to our newest model, the OPPO Reno 7!”,  Imesema sehemu ya chapicho hilo. Kwa upande mwingine Bahati amethibitisha pia katika chapisho lake kwenye mtandao wa Instagram kwa kusema kwamba amejisikia faraja kuwa balozi  wa OPPO na kuahidi kuitendea kazi katika kutangaza kampuni hiyo kupitia bidhaa zao za simu. “ANNOUNCEMENT‼️ JUST SIGNED AS THE NEW OPPO Reno 7 BRAND AMBASSADORS 🔥 So excited to partner with @oppo_kenya @wabosha.maxine and Wifey @Diana_Marua as we officially introduce to you the new OPPO Reno 7!”,  imesema taarifa hiyo. Wakati huo huo Oppo imeitambulisha simu yake mpya ya Oppo Reno ambayo imeingia hivi karibuni sokoni, simu hiyo yenye 8GB RAM + 250 GB ROM inatarajiwa kuuzwa kwa bei nafuu zaidi ili kumsaidia kila Mkenya kumiliki smartphone.

Read More
 BAHATI AFUNGULIWA MASHTAKA KWA KUSHINDWA KULIPA DENI LA SHILLINGI 150,000 ZA KENYA

BAHATI AFUNGULIWA MASHTAKA KWA KUSHINDWA KULIPA DENI LA SHILLINGI 150,000 ZA KENYA

Mwanamuziki aliyegeukia siasa nchini Kenya Bahati amefunguliwa mashtaka na kampuni ya ya mawakili ya Katunga Mbuvi & Co Advocates kwa madai ya kushindwa kumlipa mpiga picha mmoja shillingi 150000 baada ya kumfanyia kazi. Kupitia barua rasmi waliyomuandikia Bahati tarehe 30 mwezi machi mwaka huu,  kampuni hiyo imemtaka msanii huyo kumlipa mteja wao aitwaye Jeremiah Mathambu Thomas JT Shillingi 150,000 katika kipindi cha siku saba zijazo la sivyo watamfungulia kesi katika mahakama kuu ya nairobi. Barua hiyo imeibua hisia mseto miongoni mwa wakenya kwenye mitandao ya kijamii ambao wameonekana kupuzilia mbali tuhuma hizo wakisema kuwa ni njema ya kumchafulia jina Bahati ikizingatiwa kuwa Bahati ni msanii mkubwa ambaye tayari ana timu yake ya kupiga picha na kuchukua video hivyo hawezi mkodisha mtu wa nje. Hata hivyo mpaka sasa Bahati hajatoa tamko lolote kuhusu kashfa zilizoibuliwa na kampuni ya ya mawakili ya Katunga Mbuvi & Co Advocates dhidi yake ila ni jambo la kusubiriwa.

Read More
 MR. SEED AFUNGUKA MAZITO KUHUSU UKARIBU WAKE NA BAHATI

MR. SEED AFUNGUKA MAZITO KUHUSU UKARIBU WAKE NA BAHATI

Msanii nyota nchini Mr Seed amemuandika waraka mrefu msanii mwenzake Bahati baada ya hitmaker huyo wa ngoma ya Adhiambo kuweka wazi azma yake ya kuwania ubunge wa Mathare kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu. Kupitia waraka huo ambao aliuandika kupitia ukurasa wake wa Instagram Mr. Seed ameeleza namna alivyokula maisha ya taabu na bahati wakiwa wanaishi mathare, kipindi ambacho walikuwa wanajaribu kupenya kwenye kiwanda cha muziki nchini. Kulingana na Hitmaker huyo wa ngoma ya “Around”, umaskini ulikuwa sehemu ya maisha yao na haikuwazuia kuwaza mambo makubwa ambayo walikuwa wanatamani kufanikisha katika maisha yao. Mr. Seed ambaye ni bosi wa lebo y muziki ya Starbon ametangza kumuunga mkono bahati kwenye azma yake ya kuwa mbunge wa mathare kwenye uchaguzi mkuu wa Agosti 9 mwaka wa 2022 ambapo amemtaja msanii huyo kama kiongozi ambaye anawafaa wakaazi wa eneo hilo. Itakumbukwa mapema mwaka wa 2019 mr seed waliingia kwenye bifu na bahati baada msanii huyo kuigura lebo ya muziki ya EMB ambako alikuwa amesainiwa kwa kipindi cha miaka miwili. Lakini ilikuja ikabainika baadae kuwa bifu ya wawili hao ilisababishwa na ugomvi ulioibuka kati ya wake zao.

Read More
 BAHATI ATANGAZA KUFANYA HOME COMING YAKE WIKIENDI HII HUKO MATHARE, NAIROBI

BAHATI ATANGAZA KUFANYA HOME COMING YAKE WIKIENDI HII HUKO MATHARE, NAIROBI

Nyota wa muziki nchini Bahati ametangaza kufanya ziara yake iitwayo ‘Bahati Mtoto wa Mama Home Coming’ Machi 27 mwaka huu katika uwanja wa Huruma grounds, Kaunti ya Nairobi. Kupitia ukurasa wake wa Instagram hitmaker huyo wa ngoma ya “Adhiambo” amesema amehamua kuja na ziara hiyo kwa ajili ya kunadi sera zake kwa wakaazi wa Mathare kama mbunge wao mtarajiwa kuelekea uchaguzi mkuu wa Agosti 9 mwaka huu. Mbali na hayo, amesema kutakuwepo na fainali za soka katika uwanja wa Mathare Grounds ambapo timu ya Asec Huruma FC itachuana na Oostrom FC kwenye fainali huku Lucio FC ikicheza na True Colours FC kwenye mchezo wa kutafuta timu itakayochukua nafasi ya tatu. Hata hivyo Bahati amesema timu ambayo itaibuka kidedea kwenye fainali hizo itatunukiwa shillingi elfu 150 huku nafasi ya pili na tatu ikizawadiwa shillingi elfu 100 na 50 mtawalia. Utakumbuka Bahati anawania kiti cha ubunge eneo la Mathare kupitia tiketi ya chama cha Jubilee.

Read More
 MWANAMUZIKI BAHATI KUWANIA URAIS NCHINI KENYA MWAKA 2037

MWANAMUZIKI BAHATI KUWANIA URAIS NCHINI KENYA MWAKA 2037

Staa wa muziki nchini Bahati ametangaza nia ya kugombea kiti cha Urais nchini Kenya kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2037. Bahati ameyaweka wazi hayo mbele ya waandishi wa habari alipokuwa akizindua azma yake ya kuwania ubunge wa mathare kwenye uchaguzi mkuu wa Agosti 9 mwaka huu kwa kusema kuwa ana nia njema kwa wananchi wa Kenya kwani ana vigezo vya kutosha ya kuwa kiongozi atakayeleta mabadiliko nchini. Hitmaker huyo wa ngoma “Adhiambo” amedai kwamba hana mpango wa kuacha muziki licha ya kwamba ametia nia ya kuomba ridhaa ya ubunge wa eneo la Mathare. Lakini pia Bahati ameweka wazi mpango wa kuachia EP yake mpya mwezi Mei mwaka huu wakati atakapokuwa anaendeleza kampeini yake ya kujipigia debe kwenye azma ya kuwania ubunge wa Mathare.

Read More
 BAHATI ATANGAZA MSIMAMO WAKE KISIASA, AACHIA WIMBO UNAOMPIGIA DEBE RAILA ODINGA KWENYE AZMA YAKE YA URAIS.

BAHATI ATANGAZA MSIMAMO WAKE KISIASA, AACHIA WIMBO UNAOMPIGIA DEBE RAILA ODINGA KWENYE AZMA YAKE YA URAIS.

Staa wa muziki nchini Bahati amehamua kutangaza msimamo wake wa kisiasa ikiwa ni siku chache imepita tangu msanii mwenzake Willy Paul atangaze kumuunga mkono kinara wa ODM Raila Odinga. Kupitia wimbo wake mpya uitwao Fire ambao amemshirika Raila Odinga bahati ameonekana kumwagia sifa kinara huyo wa chama odm jambo ambalo limetafsiriwa moja kwa moja kuwa amehamua kumuunga mkono odinga kwenye azma yake ya kuwania urais kwenye uchaguzi mkuu wa Agosti 9 mwaka huu kupitia muungano wa Azimio la umoja. Hata hivyo wimbo huo wa Bahati umeibua hisia mseto miongoni mwa mashabiki zake ambapo wengi wameonekana kumpongeza kwa hatua ya kuweka msimamo wake kisiasa huku wengine wakimkosoa kwa hatua ya kuukimbia mrengo wa kenya kwanza ambao unaongozwa na naibu wa raias dakta William Ruto kupitia chama chake cha UDA. Utakumbuka mwaka wa 2021 Bahati pia alitangaza kumuunga mkono naibu rais dakta William Ruto kwenye azma yake ya kuliongoza taifa kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Read More
 BAHATI AMSHAURI MUNA LOVE ASIBADILI DINI KUTOKA UKRISTO KWENDA UISLAMU

BAHATI AMSHAURI MUNA LOVE ASIBADILI DINI KUTOKA UKRISTO KWENDA UISLAMU

Baada ya Muigizaji na mjasiriamali kutoka nchini Tanzania Muna Love kuweka wazi matamanio yake ya kubadili dini kutoka Ukristo kwenda Uislamu, Staa wa muziki nchini Bahati ameonekana kutofautiana kimawazo na mrembo huyo. Kupitia comment aliyoachia kwenye post ya Muna Love kwenye mtandao wa Instagram Bahati amemshauri mrembo huyo abaki katika dini yake ya Ukristo kwa kudai kuwa njia ya wokovu ina mambo mengi. Kauli ya Bahati imekuja siku moja baada ya Ali Kiba kuahidi kuhakikisha kuwa mrembo huyo ana stirika katika dini ya Uislamu ambapo alienda mbali zaidi na kusema kuwa atashirikiana nae vyema katika kumbadili endapo atakuwa tayari kufanya hivyo. Ikumbukwe kuwa miaka kadhaa nyuma Muna Love alitangaza kuokoka na kuwa Mlokole ambapo amekuwa akitumia nafasi hiyo pia kuwashawishi watu wengine kuingia katika dini yake hiyo.

Read More
 BAHATI AWAJIBU WALIMWENGU BAADA YA KUTILIA SHAKA ZAWADI ANAZOMPA MKE WAKE DIANA MARUA

BAHATI AWAJIBU WALIMWENGU BAADA YA KUTILIA SHAKA ZAWADI ANAZOMPA MKE WAKE DIANA MARUA

Staa wa muziki nchini Bahati amewajibu watu wanaotilia shaka vitu vya thamani ambavyo amekuwa akimzawadi mke wake Diana B katika miaka ya hivi karibuni. Kupitia ukurasa wake wa Instagram bahati amesema kuwa vitu vyote ambavyo amekuwa akimpa mke wake vinatoka kwa mungu ambaye alimtoa kwenye lindi la umaskani katika mitaa ya mabanda ya mathare. Hitmaker huyo wa ngoma “Adhiambo” ameenda mbali na kuwapa changamoto watu wanaombeza mitandao wawe na imani pamoja na subira katika maisha kwani mungu pekee ndiye ana uwezo wa kubadilisha maisha ya mtu. Kauli ya Bahati inakuja mara baada ya shabiki mmoja mapema wiki hii kuhoji kuwa wawili hao ni jirani zake lakini hajawahi mwona diana akiendasha magari mawali aina Mercedez ambazo alipatiwa awali ila amekuwa akimwona akiendesha gari aina na vitz. Siku ya valentines Bahati alimzawadi Diana Marua gari la shillingi million 10 aina ya Land Cruiser TX pamoja na jumba la kifahari lilogharimu shillingi million 27. Tukio hili lilipelekea mashabiki kwenye mitandao kuhoji kuwa huenda ni kiki wawili hao wanafanya

Read More
 STAA WA MUZIKI NCHINI KENYA BAHATI AMZAWADI MKE WAKE DIANA B MJENGO WA KIFAHARI

STAA WA MUZIKI NCHINI KENYA BAHATI AMZAWADI MKE WAKE DIANA B MJENGO WA KIFAHARI

Upendo wa Staa wa muziki nchini Bahati kwa baby mama wake Diana B unazidi kuongezeka kila uchao. Baada ya kumnunulia gari aina Prado TX kama zawadi ya siku ya wapendanao duniani amekuja na suprise nyingine kwa mke wake huyo. Kupitia ukurasa wake wa instagram hitmaker huyo wa ngoma ya “Adhiambo” amepost mjengo wa kifahari ambao amezawadi mke wake Diana B  na kusema kwamba ameahamua kumpa zawadi hiyo kama njia ya kumuonyesha upendo kwa kusimama nae kwenye shida na raha. Hata hivyo mashabiki na mastaa mbali mbali wameonekana kufurahishwa na hatua ya Bahati kumuonyesha upendo baby mama wake huku wakimpongeza kwa mafanikio makubwa maishani.  

Read More
 DAVID WONDER ANYOSHA MAELEZO KUHUSU BIFU LAKE NA BAHATI

DAVID WONDER ANYOSHA MAELEZO KUHUSU BIFU LAKE NA BAHATI

Msanii wa nyimbo za injili nchini David Wonder amefunguka kuhusu ishu ya kuwa kwenye bifu na staa wa muziki nchini Bahati mara baada ya nyimbo zake alizofanya na msanii huyo akiwa chini ya lebo ya EMB kufutwa kwenye mtandao wa Youtube. Akipiga stori na mwanahabari Nicholas Kioko kwenye mtandao wa Youtube David Wonder amesema hana ugomvi wowote na msanii huyo licha ya kwamba amekuwa akimzungumzia vibaya kwenye mahojiano mbali mbali. Hitmaker huyo wa “Naenda na Yesu” amekanusha ishu ya kupotea kimuziki kwa kusema kwamba amekuwa akiachia ngoma bila kupoa ila vyombo vya habari nchini Kenya vimekuwa vikiwangazia wasanii ambao wamekuwa na drama nyingi kwenye tasnia ya muziki huku wasanii wanaotoa muziki mzuri wakisahulika Hata hivyo amedokeza kuachia album yake mwaka huu wa 2022 huku akiwataka mashabiki zake kukaa mkao wa kula kupokea ujio wake mpya ambao ameutaja kama  wakitofauti zaidi.

Read More
 WEEZDOM AKANUSHA MADAI YA KUFUTWA KAZI NA BAHATI

WEEZDOM AKANUSHA MADAI YA KUFUTWA KAZI NA BAHATI

Msanii wa muziki nchini Weezdom amenyosha maelezo kufuatia post aliyoweka kwenye mtandao wa Instagram akisema kwamba Bahati akome kufutilia maisha yake. Akipiga stori na mwana youtube Presenter Ali Weezdom amesema alikasirishwa na kauli ya Bahati kwamba alimfuta kazi kama meneja wake baada ya kuzembea katika majukumu yake. Msanii huyo amekanusha madai yaliyoibuliwa na bahati kwamba alifuta kazi kama meneja wake kwa kusema madai hayo sio ya kweli kwani yeye binafsi ndiye aliamua kuacha kazi kama meneja wake. Amesema ameshangazwa na hatua ya Bahati kukosa shukran kwake licha ya kumsaidia mambo mengi kwenye muziki wake ikiwemo kumuandikia wimbo wa barua uliompa mafanikio makubwa kwenye tasnia ya muziki. Weezdom amesema bahati amemfanya aonekane mbaya kwenye jamii kwa kukodisha watu wamtusi kwenye mitandao ya kijamii ambapo amesema hatotishwa na jaribio hilo la kumzima kwani yeye ni moja kati ya watu ambao huwa hajali jinsi watu wanamchukulia. Hata hivyo amemtaka bahati aache kuwafanyia wasanii wengine mabaya hata kama aliwashika kipindi cha nyuma kwani yeye pia mafanikio ambayo ameyapata yametokana na watu waliomtangulia kumuonyesha njia. Kauli ya Weezdom imekuja mara baada ya Bahati kunukuliwa kwenye moja ya interview akisema kwamba watu waache kumuuliza kuhusu habari za weezdom ambaye alishindwa kutekeleza majukumu ya kusimamia kazi zake wakati alimpa wadhfa wa umeneja.

Read More