BAHATI AMSHAURI MUNA LOVE ASIBADILI DINI KUTOKA UKRISTO KWENDA UISLAMU

BAHATI AMSHAURI MUNA LOVE ASIBADILI DINI KUTOKA UKRISTO KWENDA UISLAMU

Baada ya Muigizaji na mjasiriamali kutoka nchini Tanzania Muna Love kuweka wazi matamanio yake ya kubadili dini kutoka Ukristo kwenda Uislamu, Staa wa muziki nchini Bahati ameonekana kutofautiana kimawazo na mrembo huyo. Kupitia comment aliyoachia kwenye post ya Muna Love kwenye mtandao wa Instagram Bahati amemshauri mrembo huyo abaki katika dini yake ya Ukristo kwa kudai kuwa njia ya wokovu ina mambo mengi. Kauli ya Bahati imekuja siku moja baada ya Ali Kiba kuahidi kuhakikisha kuwa mrembo huyo ana stirika katika dini ya Uislamu ambapo alienda mbali zaidi na kusema kuwa atashirikiana nae vyema katika kumbadili endapo atakuwa tayari kufanya hivyo. Ikumbukwe kuwa miaka kadhaa nyuma Muna Love alitangaza kuokoka na kuwa Mlokole ambapo amekuwa akitumia nafasi hiyo pia kuwashawishi watu wengine kuingia katika dini yake hiyo.

Read More
 BAHATI AWAJIBU WALIMWENGU BAADA YA KUTILIA SHAKA ZAWADI ANAZOMPA MKE WAKE DIANA MARUA

BAHATI AWAJIBU WALIMWENGU BAADA YA KUTILIA SHAKA ZAWADI ANAZOMPA MKE WAKE DIANA MARUA

Staa wa muziki nchini Bahati amewajibu watu wanaotilia shaka vitu vya thamani ambavyo amekuwa akimzawadi mke wake Diana B katika miaka ya hivi karibuni. Kupitia ukurasa wake wa Instagram bahati amesema kuwa vitu vyote ambavyo amekuwa akimpa mke wake vinatoka kwa mungu ambaye alimtoa kwenye lindi la umaskani katika mitaa ya mabanda ya mathare. Hitmaker huyo wa ngoma “Adhiambo” ameenda mbali na kuwapa changamoto watu wanaombeza mitandao wawe na imani pamoja na subira katika maisha kwani mungu pekee ndiye ana uwezo wa kubadilisha maisha ya mtu. Kauli ya Bahati inakuja mara baada ya shabiki mmoja mapema wiki hii kuhoji kuwa wawili hao ni jirani zake lakini hajawahi mwona diana akiendasha magari mawali aina Mercedez ambazo alipatiwa awali ila amekuwa akimwona akiendesha gari aina na vitz. Siku ya valentines Bahati alimzawadi Diana Marua gari la shillingi million 10 aina ya Land Cruiser TX pamoja na jumba la kifahari lilogharimu shillingi million 27. Tukio hili lilipelekea mashabiki kwenye mitandao kuhoji kuwa huenda ni kiki wawili hao wanafanya

Read More
 STAA WA MUZIKI NCHINI KENYA BAHATI AMZAWADI MKE WAKE DIANA B MJENGO WA KIFAHARI

STAA WA MUZIKI NCHINI KENYA BAHATI AMZAWADI MKE WAKE DIANA B MJENGO WA KIFAHARI

Upendo wa Staa wa muziki nchini Bahati kwa baby mama wake Diana B unazidi kuongezeka kila uchao. Baada ya kumnunulia gari aina Prado TX kama zawadi ya siku ya wapendanao duniani amekuja na suprise nyingine kwa mke wake huyo. Kupitia ukurasa wake wa instagram hitmaker huyo wa ngoma ya “Adhiambo” amepost mjengo wa kifahari ambao amezawadi mke wake Diana B  na kusema kwamba ameahamua kumpa zawadi hiyo kama njia ya kumuonyesha upendo kwa kusimama nae kwenye shida na raha. Hata hivyo mashabiki na mastaa mbali mbali wameonekana kufurahishwa na hatua ya Bahati kumuonyesha upendo baby mama wake huku wakimpongeza kwa mafanikio makubwa maishani.  

Read More
 DAVID WONDER ANYOSHA MAELEZO KUHUSU BIFU LAKE NA BAHATI

DAVID WONDER ANYOSHA MAELEZO KUHUSU BIFU LAKE NA BAHATI

Msanii wa nyimbo za injili nchini David Wonder amefunguka kuhusu ishu ya kuwa kwenye bifu na staa wa muziki nchini Bahati mara baada ya nyimbo zake alizofanya na msanii huyo akiwa chini ya lebo ya EMB kufutwa kwenye mtandao wa Youtube. Akipiga stori na mwanahabari Nicholas Kioko kwenye mtandao wa Youtube David Wonder amesema hana ugomvi wowote na msanii huyo licha ya kwamba amekuwa akimzungumzia vibaya kwenye mahojiano mbali mbali. Hitmaker huyo wa “Naenda na Yesu” amekanusha ishu ya kupotea kimuziki kwa kusema kwamba amekuwa akiachia ngoma bila kupoa ila vyombo vya habari nchini Kenya vimekuwa vikiwangazia wasanii ambao wamekuwa na drama nyingi kwenye tasnia ya muziki huku wasanii wanaotoa muziki mzuri wakisahulika Hata hivyo amedokeza kuachia album yake mwaka huu wa 2022 huku akiwataka mashabiki zake kukaa mkao wa kula kupokea ujio wake mpya ambao ameutaja kama  wakitofauti zaidi.

Read More
 WEEZDOM AKANUSHA MADAI YA KUFUTWA KAZI NA BAHATI

WEEZDOM AKANUSHA MADAI YA KUFUTWA KAZI NA BAHATI

Msanii wa muziki nchini Weezdom amenyosha maelezo kufuatia post aliyoweka kwenye mtandao wa Instagram akisema kwamba Bahati akome kufutilia maisha yake. Akipiga stori na mwana youtube Presenter Ali Weezdom amesema alikasirishwa na kauli ya Bahati kwamba alimfuta kazi kama meneja wake baada ya kuzembea katika majukumu yake. Msanii huyo amekanusha madai yaliyoibuliwa na bahati kwamba alifuta kazi kama meneja wake kwa kusema madai hayo sio ya kweli kwani yeye binafsi ndiye aliamua kuacha kazi kama meneja wake. Amesema ameshangazwa na hatua ya Bahati kukosa shukran kwake licha ya kumsaidia mambo mengi kwenye muziki wake ikiwemo kumuandikia wimbo wa barua uliompa mafanikio makubwa kwenye tasnia ya muziki. Weezdom amesema bahati amemfanya aonekane mbaya kwenye jamii kwa kukodisha watu wamtusi kwenye mitandao ya kijamii ambapo amesema hatotishwa na jaribio hilo la kumzima kwani yeye ni moja kati ya watu ambao huwa hajali jinsi watu wanamchukulia. Hata hivyo amemtaka bahati aache kuwafanyia wasanii wengine mabaya hata kama aliwashika kipindi cha nyuma kwani yeye pia mafanikio ambayo ameyapata yametokana na watu waliomtangulia kumuonyesha njia. Kauli ya Weezdom imekuja mara baada ya Bahati kunukuliwa kwenye moja ya interview akisema kwamba watu waache kumuuliza kuhusu habari za weezdom ambaye alishindwa kutekeleza majukumu ya kusimamia kazi zake wakati alimpa wadhfa wa umeneja.

Read More
 BAHATI ATUHUMIWA KUIBA IDEA YA WIMBO WA JE UNANIFIKIRIA KUTOKA KWA MARIOO

BAHATI ATUHUMIWA KUIBA IDEA YA WIMBO WA JE UNANIFIKIRIA KUTOKA KWA MARIOO

Mkali wa muziki nchini Bahati ameingia tena katika mijadala kwenye mitandao nchini  baada ya kudaiwa kuiba  idea ya wimbo wa  ‘For You’ wa msanii  wa Bongofleva Marioo Kulingana na ripoti inayosambaa mitandaoni, inadaiwa Bahati ametumia mdundo na ubunifu wa video wa wimbo huo kwenye wimbo wake mpya wa”Je unanifikiria”, hivyo kuibua maswali mengi miongoni mwa wadau wa muziki nchini ambao walienda mbali zaidi na kuhoji kuwa msanii huyo amekosa ubunifu kwenye muziki wake. Hata hivyo Bahati hajetoa tamko lolote kuhusiana na madai hayo yaliyoibuliwa na baadhi ya watumiaji wa mitandao ya kijamii.

Read More
 BAHATI APEWA TUZO BOOMPLAY

BAHATI APEWA TUZO BOOMPLAY

Nyota wa muziki nchini Bahati ametunukiwa tuzo ya silver Plaque na mtandao wa kupakua na kusikiliza muziki wa boomplay Kenya. Hii ni baada hitmaker huyo wa “Pete yangu” kufikisha zaidi ya streams millioni 8 kupitia nyimbo zake zote zilizopakiwa kwenye mtandao  huo. Kupitia ukurasa wake wa Instagram bahati amewashukuru mashabiki zake kwa kuendelea kufuatilia kazi zake ambazo zinazidi kuonyesha mafanikio makubwa ndani na nje ya Kenya. Tuzo hizo maarufu kama ‘Boomplay Plaques’ hutolewa kutambua jitihada za wasanii wanaofanya vizuri kwenye App ya Boomplay.

Read More