Bebe Cool Adai Eddy Kenzo Hana Uelewa wa Masuala ya Hakimiliki
Msanii mkongwe wa muziki wa Uganda, Bebe Cool, amemsuta vikali msanii mwenzake Eddy Kenzo, akidai hana uelewa wa kina kuhusu masuala ya haki miliki (copyright) nchini humo. Akizungumza na wanahabari, Bebe Cool amesema kauli za hivi karibuni za Eddy Kenzo kuhusu mfumo wa usimamizi wa hakimiliki nchini Uganda zimejaa upotoshaji na zinatokana na msanii huyo kutoelewa sheria na taratibu zinazohusu sekta hiyo. Kwa mujibu wa Bebe Cool, Kenzo amekuwa akizungumza kama mtu asiye na taarifa sahihi, hali ambayo inaweza kuwapotosha wasanii wengine na umma kwa ujumla. Bosi huyo wa Gagamel International amesisitiza kuwa masuala ya hakimiliki ni nyeti na yanahitaji uelewa wa kisheria, akiongeza kuwa si kila msanii ana uwezo wa kuyazungumzia kwa usahihi bila kujiridhisha na ukweli uliopo. Hata hivyo amemtaka Eddy Kenzo na wasanii wengine kujifunza zaidi kuhusu sheria za hakimiliki kabla ya kutoa maoni hadharani.
Read More