BEBE COOL AFUNGUKA KUHUSU KUSTAAFU MUZIKI

BEBE COOL AFUNGUKA KUHUSU KUSTAAFU MUZIKI

Mwanamuziki kutoka Uganda Bebe Cool amefunguka na kudai kwamba hana mpango wa kustaafu muziki hivi karibuni kwani ana miaka 20 ya kufanya hivyo. Kwenye moja ya onesho lake huko Kawempe Bebe Cool amesema ndio mwanzo anaanza safari yake ya muziki hivyo mashabiki watarajie muziki mzuri kutoka kwake. “Majuzi niliambia Chameleone kuwa nina mpango wa kustaafu muziki miaka 20 ijayo na akaanza kuachia muziki maana alikuwa amelaza damu.”..Amesema Bebe Cool Bebe Cool ambaye ana umri wa miaka 40 ametoa changamoto kwa wasanii wachanga kutia bidii kwenye kazi zao maana wasanii wakongwe hawana mpango wa kuacha muziki. Utakumbuka Bebe Cool ni  mmoja kati ya wasanii wakongwe kwenye muziki nchini Uganda kwani amekuwa kwenye game ya muziki kwa takriban miongo miwili.

Read More
 BEBE COOL ATHIBITISHA KUFUNGA PINGU ZA MAISHA NA BABY MAMA WAKE ZUENA KARIMI

BEBE COOL ATHIBITISHA KUFUNGA PINGU ZA MAISHA NA BABY MAMA WAKE ZUENA KARIMI

Mwanamuziki kutoka nchini Uganda Bebe Cool amekuwa akiahidi kufanya harusi na mke wake Zuena Karimi kwa muda, na namna mambo yanavyoenda ni kama tutashuhudia harusi kubwa kati ya mastaa hao mwaka huu. Kwenye moja ya onesho lake huko Mukono nchini Uganda Bebe Cool amethibitisha kuwa ndani ya mwaka huu ana mpango wa kufunga pingu za maisha na mpenzi wake wa siku nyingi Zuena Karimi. Bosi huyo wa Gagamel amewaambia mashabiki zake kuwa harusi ambayo anaenda kuifanya mwaka huu itavunja historia nchini Uganda. Ni hatua ambayo imepokelewa kwa ukubwa na wafuasi wake wengi kwenye mitandao ya kijamii wakisema kwamba wanangoja harusi hiyo kwa hamu harusi ya wawili hao. Utakumbuka Bebe Cool ni msanii pekee ambaye hajafanya harusi ya kanisani kando na mahasimu wake wa jadi Jose Chameleone na Bobi Wine.

Read More
 BEBE COOL AWAJIBU WALIMWENGU KUHUSU ISHU YA KUTOMSAPOTI ALLAN HENDRICK

BEBE COOL AWAJIBU WALIMWENGU KUHUSU ISHU YA KUTOMSAPOTI ALLAN HENDRICK

Staa wa muziki nchini Uganda Bebe Cool amefunguka kuhusu ishu ya kutomsaidia mwanae Allan Hendrick kutunaua wigo wa muziki wake licha ya kuwa na ushawishi mkubwa Afrika Mashariki. Katika mahojiano yake ya hivi karibuni Bebe Cool amekanusha madai ya kumtelekeza Allan Hendrick kwenye muziki wake huku akisema amekuwa na ukaribu na mwanae huyo kwa muda akimpa ushauri wa namna ya kuboresha muziki wake na kubaki kwenye tasnia ya muziki kwa muda mrefu bila kuchuja. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Gyenvudde” amesisitiza kuwa anaweza kuinua muziki wa Allan Hendrick bila hata kumpa kollabo tofauti na namna watu wamekuwa wakimshinikiza kwenye mitandao ya kijamii. Kauli ya Bebe Cool imekuja siku cha baada ya Chameleone kumwagia sifa Hendrick kwa kipaji chake cha muziki ambapo alienda mbali zaidi na kuahidi kufufua muziki wake ambao umekuwa ukisuasua katika siku za hivi karibuni.

Read More
 BEB COOL MBIONI KUWAFUNGULIA MASHTAKA WANAOMPAKA TOPE NCHINI UGANDA

BEB COOL MBIONI KUWAFUNGULIA MASHTAKA WANAOMPAKA TOPE NCHINI UGANDA

Mwanamuziki Moses Ssali maarufu Bebe Cool ni mmoja wa wasanii waliokosolewa zaidi nchini Uganda, lakini huenda wanaomchafulia jina wakijipata hatiani hivi karibuni. Katika mahojiano ya hivi  karibuni na MwanaYouTube wa eneo hilo, bosi huyo wa Gagamel ameeleza kuwa ameanza kukusanya ushahidi dhidi ya wanahabari ambao wamekuwa wakimpaka tope kwa tuhuma za uongo. “Nimejenga brand yangu kwa muda mrefu sana na kwa mwandishi yeyote wa habari kuja kuniongelea upuuzi, nawaahidi nitawapa funzo. Ninakusanya ushahidi, na watalipa,” alisema. Hata hivyo Bebe Cool amesema washukiwa wakuu ni watangazaji wa redio na TV ambao wamekuwa wakitoa maoni hasi dhidi yake.

Read More
 GRAVITY OMUTUJJU: BEBE COOL SIO RAFIKI YANGU WA KARIBU, SIMPENDI

GRAVITY OMUTUJJU: BEBE COOL SIO RAFIKI YANGU WA KARIBU, SIMPENDI

Rapa kutoka Uganda Gravity Omutujju amefunguka na kudai kuwa hataki kuwa rafiki wa msanii mwenzake Bebe Cool licha ya kufanya wimbo wa pamoja. Katika mahojiano yake ya hivi karibuni Omutujju amesema hana ugomvi wowote na msanii huyo ila hajawahi pata amani akiwa karibu na bebe cool kwa sababu ni mnafiki mkubwa. Bebe Cool na Gravitty Omuttuju walifanya wimbo wa uitwao “Kerere” mwaka wa 2017 lakini hawakuweza kutoa video ya wimbo huo. Mwaka wa 2020 kwenye moja ya mahojiano gravity omutujju alimulaumu Bebe Cool kwa kushindwa kuandaa video ya wimbo huo jambo ambalo limetafsiriwa na wajuzi wa mambo kwenye mitandao ya kijamii kuwa huenda ndio sababu ya wawili hao kutokuwa na mahusiano mazuri.

Read More
 ZIZA BAFANA AMCHANA BEBE COOL KISA ORODHA YAKE YA WASANII WALIOFANYA VIZURI MWAKA 2021

ZIZA BAFANA AMCHANA BEBE COOL KISA ORODHA YAKE YA WASANII WALIOFANYA VIZURI MWAKA 2021

Mwanamuziki anayesuasua kimuziki nchini Uganda Ziza Bafana hana furaha kabisa baada ya kutoonekana kwenye orodha ya wasanii wa kila mwaka ambayo hutolewa na msanii mwenzake Bebe Cool. Bafana, ambaye alifanya vizuri mwaka wa 2021 kwa kuachia magoma makali anadai kuwa Bebe Cool alipoteza mweelekeo katika tasnia ya muziki nchini Uganda kwani siku hizi hajakuwa akiachia muziki mzuri kama kipindi cha nyuma. Hitmaker huyo wa “Embuzi” amesema Bebe Cool,anatumia orodha yake ya kila mwaka ya wasanii waliofanya vizuri kutengeneza mazingira ya kuzungumziwa kwenye vyombo vya habari nchini Uganda. Ikumbukwe Bebe Cool hajawahi kuwa na uhusiano mzuri na mwanamuziki mwenzake Ziza Bafana baada ya msanii huyo kuanza kujihusisha na matumizi ya dawa za kulevya miaka kadhaa iliyopita.

Read More
 BEBE COOL AKANUSHA TETESI ZA KUKUTWA NA KIRUSI CHA OMICRON

BEBE COOL AKANUSHA TETESI ZA KUKUTWA NA KIRUSI CHA OMICRON

Msanii mkongwe kwenye muziki nchini Uganda Bebe Cool amefunguka kuhusu ugonjwa uliompelekea kukimbizwa hospitali mwishoni mwa juma lilopita. Kupitia ukurasa wake wa Facebook Bebe Cool ameweka wazi kuwa alikuwa anaugua malari, ugonjwa ambao hakuwa fikiria utampata. Hitmaker huyo “Gyenvudde” amesema kwa sasa amepata ufahamu wa kwanini Wizara Afya nchini Uganda imekuwa mstari wa mbele kusisitiza umuhimu wa kukabiliana na ugonjwa wa malaria. Tamko la Bebe Cool limekuja mara baada ya tetesi kusambaa kwenye mitandao ya kijamii zikidai kuwa msanii alikimbizwa hospitali baada ya kukutwa na kirusi cha Omicron

Read More
 BEBE COOL KUZINDUA TUZO YAKE YA MUZIKI AMBAYO ITAGHARIMU SHILLINGI MILLIONI 127

BEBE COOL KUZINDUA TUZO YAKE YA MUZIKI AMBAYO ITAGHARIMU SHILLINGI MILLIONI 127

Msanii mkongwe kwenye muziki nchini Uganda Bebe Cool alitangaza mwishoni mwaka 2021 aliahidi kuzindua tuzo yake ya kila mwaka kwa ajili ya kutambua juhudi za wasanii wanaofanya vizuri kwenye tasnia ya muziki nchini Uganda. Kwenye mahojiano yake ya hivi karibuni Bebe Cool amesema ametanga shillingi millioni 127 za Kenya ambayo itatumika kuendesha shughuli ya kuzindua tuzo yake ambayo inatarajiwa kuanza mwaka huu. Hitmaker huyo “Gyenvudde” amesema waasanii watatunukiwa pesa taslimu badala ya tuzo za glassi ambazo wamekuwa wakipewa na waandaaji wa tuzo zenye thamani ya takriban shillingi elfu 63 za Kenya. “Tuzo za Uganda hazina maana. Nazindua tuzo yangu ambayo itakuwa tofauti. Tuzo ya Bebe Cool itaghrarimu kati ya shillingi billioni 1.5 hadi  billioni 2 pesa za Uganda..alisema kwenye mahojiano na runinga moja nchini Uganda. Bebe cool amesisitiza kuwa katika kipindi cha miaka miwili ijayo tuzo yake itakuwa yenye bora afrika mashariki na kati.

Read More
 BEBE COOL AWACHANA WAANDAJI WA TUZO ZA MUZIKI UGANDA

BEBE COOL AWACHANA WAANDAJI WA TUZO ZA MUZIKI UGANDA

Mkongwe wa muziki kutoka nchini Uganda Bebe Cool amewatolea uvivu waandaji wa tuzo za muziki nchini humo kwa kuwapa wasanii tuzo ambazo hazina muhimu wowote. Akiwa kwenye moja ya Interview Bebe Cool amesema waandaji wa tuzo nchini Uganda wamekuwa na mazoea ya kuwapa wasanii tuzo ambazo msanii hawezi uuza na akapata pesa za kujikimu kimaisha. Bosi huyo wa Gagamel amedokeza mpango wa kuja na tuzo yake mwakani na washindi watapokezwa kati ya shillingi laki moja na laki tatu kulingana na kipengele ambacho msanii husika atakuwa ameteuliwa kushiriki. Kauli ya Bebe Cool imekuja  siku chache mara baada ya Spice Diana kuwachana waandaji wa tuzo nchini uganda wasimteue  kwenye tuzo zao bila kumshirikisha.

Read More