Waandishi wa nyimbo za Bebe Cool ni bandia – King Saha

Waandishi wa nyimbo za Bebe Cool ni bandia – King Saha

Mwanamuziki King Saha ameibuka na kuwachana watu wanaomuanndikia Bebe Cool nyimbo kwa kusema kwamba hawana vipaji kwenye masuala ya uandishi. Kwenye mohajiano yake hivi karibuni King Saha amesema Bebe Cool amewekeza mamilioni ya pesa kwa waandishi wa nyimbo ilhali kazi zake zinachuja haraka. Aidha ameenda mbali Zaidi na kujinadi kuwa huwa anaandika nyimbo 5 kwa mwaka na zote zinaisha kuwa kubwa zaidi kwenye tasnia ya Afrika Mashariki. Baadhi ya waandishi wa nyimbo wanaofanya kazi kwa ukaribu na Bebe Cool ni  pamoja na Yese Oman Rafiki na Ronnie On Dis One. Utakumbuka Bebe Cool na King Saha hawajakuwa na maelewano mazuri kwa muda mrefu na ugomvi wao ulianza kipindi ambacho Bebe Cool alimshauri hitmaker huyo wa Zakayo aachane na matumizi ya mihadarati kwa kuwa itampoteza kimuziki. Tangu wakati King Saha amekuwa akimrushia vijembe Bebe Cool kila mara anapopata nafasi kwenye mahojiano yake mbali mbali.

Read More
 Mwimbaji wa Marekani Matt B adokeza kufanya kolabo na Bebe Cool

Mwimbaji wa Marekani Matt B adokeza kufanya kolabo na Bebe Cool

Msanii kutoka  Marekani Matt B amefichua mpango wa kufanya kazi  ya pamoja na wasanii wa Uganda. Kupiti ukurasa wake wa Instagram amemtaja Bebe Cool kama mmoja wa wasanii ambao huenda akafanya nao kazi ambapo alienda mbali zaidi na kuwauliza mashabiki namna wimbo wao utakavyosikika masikioni mwao. “Nilipata nafasi ya kukutana na Bebe Cool ilikuwa heshima. Nashangaa namna wimbo wa Bebe Cool na Matt B utasikika,” aliandika kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii. Utakumbuka Matt B ni moja kati ya wasanii walioteuliwa kushiriki tuzo za Grammy 2023 kupitia Wimbo wake na Eddy Kenzo “Gimme Love”. Wawili hao waliotajwa kuwania kipengele cha Best Global Music Performance wanatarajiwa kuchuana na wasanii Burna Boy, Rocky Dawuni na Blvk H3ro, na Bayethe Wouter Kellerman, Zakes Bantwini na Nomcebo Zikode.

Read More
 Gravity Omutujju Ajibu Madai ya Bebe Cool Kwamba Haogi

Gravity Omutujju Ajibu Madai ya Bebe Cool Kwamba Haogi

Rapa Gravity Omutujju amejibu madai ya Bebe Cool kuwa anapaswa kuoga kila mara ili aweze kufikia kiwango chake cha maisha. Hii ni baada ya Omutujju kumtaka bosi huyo wa Gagamel kustaafu muziki na kuwapa nafasi vijana wachanga waendeleze gurudumu la kuupeleka muziki wa Uganda kimataifa. Sasa kupitia mitandao yake ya kijamiii rapa huyo amesema kuwa yeye huwa anazingatia sana masuala ya usafi kwa kuoga kila siku, hivyo Bebe Cool hapaswi kutumia suala hilo kuficha ukweli kwamba anatakiwa kustaafu muziki. “Tunaoga na kuvaa vizuri, kwa kweli hata tunanukia vizuri. Unaogopa uhalisia na mabadiliko. #kizazi kipya kinatawala duniani kote,” Gravity alichapisha kwenye mitandao yake ya kijamii.

Read More
 Bebe Cool afunguka sababu za kutofanya tamasha la muziki mwaka 2022

Bebe Cool afunguka sababu za kutofanya tamasha la muziki mwaka 2022

Msaniii mkongwe Bebe Cool amefunguka sababu za kutofanya tamasha la muziki mwaka 2022 kama wasanii wenzake. Kwenye mahojiano yake amekiri kupata changamoto ya kifedha kwa kuwa amekuwa akiwalipia karo watoto wenye uhitaji katika jamii maeneo mbali mbali nchini uganda. Hitmaker huyo wa “Gyevude” amesema watoto wengi kutoka familia zisozijiweza wanamtegemea hivyo hawezi kuwaacha wakitabiaka. Hata hivyo walimwengu kwenye mitandao ya kijamii wamehoji kuwa sababu za Bebe Cool kutoandaa tamasha lake la muziki hazina mashiko kwa kuwa hajaachia wimbo wowote mkali.

Read More
 Bebe Cool amjibu Gravity Omutujju kuhusu kustaafu muziki

Bebe Cool amjibu Gravity Omutujju kuhusu kustaafu muziki

Mwanamuziki kutoka nchini Uganda Bebe Cool amemjibu Gravity Omutujju baada ya rapa huyo kumshauri astaafu muziki kwa kuwa ana umri mkubwa. Kwenye mahojiano yake hivi karibuni Bebe Cool amemtaka rapa huyo kumlipa pesa kama anatamani aache muziki. Utakumbuka baada ya Gravity kupata mapokezi kwenye show yake miezi kadhaa huko Cricket Oval, Lugogo aliibuka na kuwachana wasanii bebe cool jose chameleone na Bobi wine akiwashauri wageukia masuala ya kilimo na kuachia wasanii kizazi kipya kuendelea na muziki. Alienda mbali zaidi na kutoa orodha ya wanamuziki bora nchini Uganda na kuwaacha nje wasanii hao watatu.

Read More
 Wanamuziki wa Uganda wataendelea kushinda tuzo za kimataifa- Bebe Cool

Wanamuziki wa Uganda wataendelea kushinda tuzo za kimataifa- Bebe Cool

Bosi wa Gagamel, Msanii Bebe Cool ana imani kuwa wasanii wa Uganda wataendelea kung’aa kimataifa kupitia muziki wao. Kwenye mahojiano yake hivi karibuni, Bebe Cool amebainisha kuwa kuteuliwa kwa Eddy Kenzo kwenye tuzo za Grammy 2023 itawafungulia wasanii wengi nchini humo milango ya kushiriki tuzo kubwa duniani. Ikumbukwe kipindi cha nyuma Bebe Cool alikuwa kwenye ugomvi (bifu) na Eddy Kenzo mara baada ya hitmaker huyo wa “Nsimbudde” kukimbia na msanii wake Rema Namakula ambaye alikuwa chini ya Gagamel Entertainment. Lakini wawili hao walikuja wakaweka kando tofauti zao kwa manufaa ya tasnia ya muziki nchini Uganda.

Read More
 Bebe Cool achoshwa na wasanii wa Nigeria kutumbuiza nchini Uganda

Bebe Cool achoshwa na wasanii wa Nigeria kutumbuiza nchini Uganda

Msanii mkongwe nchini Uganda Bebe Cool amechoshwa na hatua ya wasaniii wa Nigeria kutumbuiza nchini humo kila wiki. Bebe cool amesema kitendo hicho imewafanya wasaniii wa Nigeria kujiona kuwa wana mashabiki wengi kuwashinda wasanii wa ndani huku akiwataka mashabiki kuwaonyesha upendo wasanii wa Uganda pindi wanapofanya matamasha kama njia ya kuwapa changamoto mapromota muziki kuwazingatia kwenye maonyesha yao. “We are tired of Nigerian artists coming here and acting as though they have more fans here. I implore everyone who has supported Kenzo to also come for Jose Chameleone’s concert dubbed “Gwanga Mujje” next year at Cricket Oval,” Alisema Bebe Cool. Bosi huyo wa Gagamel ametoa kauli hiyo alipokuwa anawarai mashabiki kumuunga mkono msanii jose chameolene kipindi hiki yupo kwenye maandalizi ya onesho lake ambalo litafanyika mapema mwaka 2023. Ikumbukwe ndani ya mwaka huu wasanii kumi kutoka Nigeria tayari wametumbuiza nchini Uganda akiwemo Tiwa Savage, Rema, Ruger, na wengine wengi.

Read More
 Bebe Cool ampa Eddy Kenzo maua yake akiwa angali hai kuelekea Tamasha lake Novemba 12

Bebe Cool ampa Eddy Kenzo maua yake akiwa angali hai kuelekea Tamasha lake Novemba 12

Msanii mkongwe kwenye muziki Bebe Cool ameamua kumpa maua yake Eddy Kenzo akiwa angali hai licha ya watu kuhisi kuwa ana bifu (ugomvi) na Bosi huyo wa Big Talent. Mkali huyo ngoma ya “Boss Lady” ametoa wito kwa mashabiki wa muziki mzuri kujitokeza na kuhudhuria tamasha la msanii huyo Novemba 12 huko Kololo Airstrip huku akithibitisha kuwa atakuwa moja kati ya wasanii watakaotoa burudani kwenye tamasha hilo. Ikumbukwe miaka kadhaa iliyopita Eddy Kenzo alimualika Bebe Cool kwenye tamasha lake la muziki katika hoteli ya Serena viungani mwa Jiji la Kampala na kupitia tamasha hilo ndipo alimaliza bifu yake na Bobi Wine.

Read More
 BEBE COOL ALIPWA LAKI SITA ZA KENYA KWA WIMBO WA NYEGE NYEGE

BEBE COOL ALIPWA LAKI SITA ZA KENYA KWA WIMBO WA NYEGE NYEGE

Wakati walimwengu wanaendelea kumkosoa Bebe Cool mtandaoni kwa kuachia wimbo wake wa Amapiano uitwao “Nyege Nyege”, msanii huyo ameripotiwa kulipwa takriban shillingi laki 6 za Kenya. Kulingana na chanzo cha karibu na bosi huyo wa Gagamel, waandaji wa tamasha la Nyege Nyege walimlipa kiasi hicho cha fedha kwa kutunga wimbo huo uliokuwa unasifia tamasha hilo la siku nne linaloendelea kwa sasa huko Jinja nchini Uganda. “Alilipwa shillingi millioni 20 za Uganda kwa kutoa wimbo huo, hivyo hajali na hatishiki kabisa na maneno ya watu wanaomsema vibaya mtandaoni”, Chanzo hicho kimeiambia jarida moja la Habari nchini Uganda. Utakumbuka baada ya Bebe Cool kuachia wimbo wa Nyege Nyege alipata ukosoaji mkubwa kutoka kwa mashabiki na baadhi ya wasanii akiwemo Mr. Lee wa B2C na King Saha ambao walihoji kuwa wimbo huo hauna ubora wowote. Mapema wiki iliyopita tamasha la Nyege Nyege lilisitishwa kwa muda na bunge la Uganda kwa misingi ya kueneza uesharati lakini Waziri mkuu nchini Uganda Robinah Nabanjja alikuja akatengua uamuzi huo wa bunge na kuruhusu tamasha hilo kuendelea.

Read More
 BEBE COOL AKANUSHA MADAI YA KUSTAAFU MUZIKI

BEBE COOL AKANUSHA MADAI YA KUSTAAFU MUZIKI

Msanii nguli wa muziki kutoka nchini Uganda Bebe Cool amedai kwamba hana mpango wa kustaafu muziki licha ya kuwa kwenye game kwa takriban miongo miwili. Akizungumza kwenye moja ya interview Hitmaker huyo wa “Boss Lady” ambaye juzi kati alikuwa anasherekea miaka 45 tangu kuzaliwa kwake, amesema hatostaafu muziki katika kipindi cha miaka 5 ijayo kama alivyosema awali, ila ataendelea kufanya kazi hiyo hadi kifo chake. Hata hivyo Staa huyo amesisitiza kuwa kiwanda cha muziki nchini Uganda bado kinamuhitaji ikizingatiwa kuwa bado hajafanikisha ndoto yake ya kuupeleka muziki wa Uganda kimataifa. Utakumbuka mwanamuziki Bebe Cool aliwahi kusema kuwa atastaafu mara tu atakapofikisha umri wa miaka 50, lakini kutokana na kauli yake hii inaoneka ataendelea kuwabariki mashabiki zake na muziki mzuri licha ya walimwengu kuhoji kwamba anatumia ushirikina kuwavuta mashabiki.

Read More
 KING SAHA AMPA ZA USO BEBE COOL, ADAI NI MCHAWI

KING SAHA AMPA ZA USO BEBE COOL, ADAI NI MCHAWI

Mwanamuziki kutoka Uganda King Saha ameibuka na kumtuhumu msanii mwenzake  Bebe Cool kuwa nii mshirikina. Katika perfomance yake juzi kati King Saha amesema Bebe Cool amekuwa akitumia uchawi kuwashusha wasanii wengine. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Zakayo” amesema hatua ya Bebe Cool kutumia nguvu za giza ni kwa ajili ya kubaki kwa muda mrefu kwenye tasnia ya muziki nchini Uganda bila kuchuja. Utakumbuka King Saha amekuwa akirushiana maneno makali na Bebe Cool tangu bosi huyo wa Gagamel amshauri aachane na matumizi ya dawa za kulevya mwaka wa 2021.

Read More
 EDDY KENZO AAPA KUMALIZA UGOMVI WA KING SAHA NA BEBE COOL

EDDY KENZO AAPA KUMALIZA UGOMVI WA KING SAHA NA BEBE COOL

Staa wa muziki nchini Uganda,Eddy Kenzo amefichua kuwa ugomvi unaoendelea kati ya Bebe Cool na King Saha unamchukiza. Katika mahojiano yake hivi karibuni Kenzo amesema wasaniii wanapaswa kuacha kutupiana maneno makali mtandaoni na badala yake waungane kwa ajili kuupeleka muziki wà Uganda kimataifa. “I hate the negativity in this industry. I don’t like artists who fight each other. We don’t need a divided industry. We need to grow first and conquer the international market,” Amesema Eddy kenzo ameahidi kuwaleta pamoja King Saha na Bebe Cool ambao wamekuwa kwenye bifu kwa muda mrefu kwa kuwa ni marafiki zake. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Nsimbudde” ameeleza kuwa tasnia ya muziki nchini Uganda bado ni changa hivyo wasanii wanapaswa kuelekeza nguvu zao kubuni njia za kuingiza kipato na kutoa muziki mzuri badala kupigana vita. “I will work to unite the two because I speak to both. Artists ought to know our industry is still young, we should unite and fight brokenness instead of fighting one another,”  Ameongeza King Saha na Bebe Cool wamekuwa kwenye ugomvi tangu bebe cool amshauri aachane na matumizi ya dawa za kulevya la sivyo atapotea kimuziki. King Saha alikasirisha na kauli hiyo ambapo amekuwa akimchana Bebe Cool kwenye mahojiano mbali mbali na hata akaachia disstrack iitwayo Zakayo ambayo inalenga bossi huyo wa Gagamel. Eddy Kenzo kipindi cha nyuma alikuwa kwenye ugomvi na Bebe Cool lakini baadae wakakuja wakamaliza tofauti zao ambapo kwa sasa wana uhusiano mzuri wa kufanya kazi pamoja.        

Read More