BIEN WA SAUTI SOL MBIONI KUKAMILISHA COLLABO YAKE NA KUNDI LA ETHICS
Member wa Sauti Sol Bien na wasanii wa kundi la muziki wa gengetone Ethics Entertainment wameingia studio kwa ajili ya kuandaa kazi yao ya pamoja. Kwenye video inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii wasanii hao wameonekana kuwa katika jukumu la kushirikiana kuandaa wimbo katika mazingira ya Studio wakivibe na mdundo wa kazi yao mpya. Video hiyo imewaacha mashabiki na maswali mengi kama kweli wawili hao wapo kwenye maandalizi ya kazi yao mpya au walikuwa kwenye starehe zao. Hata hivyo iwapo Bien na wasanii wa Ethics Entertainment wataachia collabo yao itakuwa ni kazi yao ya kwanza ikizingatiwa kuwa hawajawahi kufanya kazi ya pamoja.
Read More