Vijana Wanaofanana na Mastaa wa Bongofleva Watikisa Mitandao ya Kijamii
Vijana wanaofanana kwa karibu na mastaa wakubwa wa Bongo Fleva akiwemo Jux, Diamond Platnumz, Rayvanny, Mbosso, Marioo pamoja na Jay Melody wamezua gumzo kubwa mitandaoni, baada ya picha na video zao kusambaa kwa kasi katika majukwaa mbalimbali ya kijamii. Katika video hiyo inayosambaa mtandaoni, vijana hao wanaonekana wakiwa wamevaa na kujipamba kwa mitindo inayofanana kabisa na ya wasanii hao maarufu, kuanzia mavazi, nywele hadi muonekano wa jumla. Vijana hao wamewashangaza wengi kutokana na uwezo wao wa kuiga kwa usahihi mkubwa muonekano na mitindo ya wasanii hao wakubwa wa Tanzania. Wengi wameeleza kuwa kwa mara ya kwanza walidhani ni mastaa hao kabla ya kubaini kuwa ni watu wengine wanaofanana nao. Hata hivyo walimwengu wamewapa baraka vijana hao, wakisema kuwa hali hiyo inaweza kuwa mwanzo wa safari mpya kwa vijana hao, hasa katika ulimwengu wa sanaa na biashara za matangazo.
Read More