Burna Boy Alazika Kufuta Shows zake Baada ya Kuugua Ghafla

Burna Boy Alazika Kufuta Shows zake Baada ya Kuugua Ghafla

Staa wa muziki kutoka Nigeria, Burna Boy, amelazika kufuta shows zake baada ya kuchoka kupita kiasi. Msanii huyo wa muziki wa Afro-fusion ameshare video kupitia Instastory yake ikimuonesha akipatiwa matibabu baada ya kupiga show tatu mfululizo ndani ya masaa 24 bila kupata muda wa kupumzika. Hali hiyo imesababisha kufutwa kwa show yake iliyokuwa imepangwa kufanyika usiku wa leo katika Kia Center, Orlando, ukumbi wenye uwezo wa kubeba takribani watu 20,000. Burna Boy yuko katika mfululizo wa ziara yake ya kimataifa iitwayo “No Sign of Weakness Tour”, ambayo ilianza Novemba 2025 na inatarajiwa kumalizika mwaka 2026. Mashabiki wake wameonyesha wasiwasi na kumtakia nafuu ya haraka, wakisisitiza umuhimu wa wasanii kupumzika ili kuendelea kutoa burudani bila kuathiri afya zao.

Read More
 Burna Boy Aomba Radhi Baada ya Madai ya Kuwadhalilisha Mashabiki wake

Burna Boy Aomba Radhi Baada ya Madai ya Kuwadhalilisha Mashabiki wake

Mwanamuziki nyota wa Afrobeat, Burna Boy, ameomba radhi kwa mashabiki wake kufuatia wimbi la lawama lililotanda mtandaoni, baada ya madai kuibuka kwamba aliwaita baadhi ya wafuasi wake masikini. Kupitia ujumbe mrefu alioutoa mtandaoni, Burna Boy amejitetea akisema kuwa mara nyingi matendo yake mema hayapewi nafasi, lakini akifanya jambo lolote linaloonekana kama kosa, ndipo linapoenezwa kwa kasi kubwa. Mkali huyo wa Afrobeat, amefafanua kuwa maneno yake yalipotoka yalikuwa ni sehemu ya utani aliokuwa akifanya na bendi yake kuhusu jambo tofauti kabisa, lakini yakapotoshwa na kuwasilishwa kana kwamba alidharau mashabiki wake. Hata hivyo ametoa msimamo wake kwamba anawapenda wanaompenda na kuwaheshimu wanaomheshimu. Licha ya kusisitiza kuwa hakukosea katika tukio hilo, Burna Boy amewaomba radhi kwa yeyote aliyekasirishwa au kuhisi kuathirika na tafsiri hiyo, akisema kuwa yeye pia ni binadamu na si mkamilifu.

Read More
 Burna Boy: “Sikulazimisha Mtu Kunipenda, Nataka Mashabiki Wenye Pesa”

Burna Boy: “Sikulazimisha Mtu Kunipenda, Nataka Mashabiki Wenye Pesa”

Mwanamuziki nyota wa Nigeria, Burna Boy, ameibua gumzo mitandaoni baada ya kutoa kauli tata akisema kwamba hakumlazimisha mtu yeyote kuwa shabiki wake na kwamba anawapendelea zaidi mashabiki wenye pesa. Kupitia Instagram Live, Burna Boy, amesisitiza kuwa hakuna mtu anayelazimishwa kufuatilia muziki wake, huku akiongeza kuwa anathamini mashabiki wanaoonyesha uaminifu kwa kazi yake na wanaoweza kumudu huduma anazotoa kama sehemu ya maisha yao ya burudani. Kauli hiyo imekuja siku chache baada ya msanii huyo kuonekana kwenye video inayosambaa mitandaoni akimtoa nje shabiki aliyekuwa amelala wakati wa moja ya maonesho yake ya moja kwa moja. Tukio hilo liliibua mijadala mikali, ambapo baadhi ya mashabiki walimkosoa wakisema kitendo hicho kilikuwa cha kudhalilisha.

Read More
 Burna Boy Apuzilia Mbali Uvumi wa Nguvu za Kichawi Kwenye Kwapa Lake

Burna Boy Apuzilia Mbali Uvumi wa Nguvu za Kichawi Kwenye Kwapa Lake

Msanii nyota wa Nigeria, Burna Boy, amefafanua kuhusu uvumi unaozagaa mtandaoni kwamba mafanikio yake ya kimataifa yanahusishwa na nguvu za kichawi zinazodaiwa kufichwa kwenye kwapa lake. Akizungumza na Apple Music, Burna Boy amesema baadhi ya watu nchini Nigeria wanaamini kuwa uamuzi wake wa kutonyoa kwapa ni ishara ya nguvu za ajabu, wakifananisha hali hiyo na simulizi la Biblia kuhusu Samson ambaye nguvu zake zilihusishwa na nywele zake. Burna Boy amekanusha madai hayo kwa maneno makali, akiyaita ya kipuuzi. Amesisitiza kuwa kutonyoa kwapa ni uamuzi wake binafsi wa maisha, na hakuna uhusiano wowote na imani za kishirikina au nguvu za kichawi. Staa huyo, amesema kuwa mafanikio yake katika muziki yametokana na kazi ngumu, nidhamu, na msaada wa mashabiki wake duniani kote, na sio imani za kichawi kama inavyodaiwa na baadhi ya watu.

Read More
 Burna Boy Aachia Albamu Mpya, “No Sign of Weakness”

Burna Boy Aachia Albamu Mpya, “No Sign of Weakness”

Nyota wa muziki wa kimataifa kutoka Nigeria , Burna Boy, ameachia rasmi albamu yake ya nane inayokwenda kwa jina la No Sign of Weakness. Albamu hiyo imeachiwa usiku wa kuamkia leo, Ijumaa, Julai 11, ikitimiza ahadi yake aliyotoa takribani miezi minane iliyopita kwa mashabiki wake. Albamu hii ina jumla ya nyimbo 16 na inaonesha ushawishi mkubwa wa kimataifa kwa kuwa Burna Boy ameshirikiana na mastaa wakubwa wa muziki duniani, akiwemo: Travis Scott, Mick Jagger, Stromae na Shaboozey Kushirikiana na majina haya makubwa kunathibitisha kasi na ukuaji wa Burna Boy katika kuleta sauti za Afrika kuungana na muziki wa kimataifa. Albamu hiyo sasa inapatikana kwenye majukwaa yote ya kusikiliza muziki, na tayari mashabiki wameshajawa na shauku kubwa katika kupokea kazi hii mpya. Kwa mashabiki wa Afro-fusion na muziki wa dunia kwa ujumla, No Sign of Weakness inaonekana kuwa ni kazi iliyosukwa kwa ubora wa hali ya juu, ikionyesha ufanisi mkubwa wa Burna Boy katika taaluma yake

Read More
 Bien Akutana na Burna Boy BBC Studios, Adokeza Wimbo Mpya

Bien Akutana na Burna Boy BBC Studios, Adokeza Wimbo Mpya

Msanii nguli wa Afro-pop kutoka Kenya, Bien-Aimé Baraza, ameonekana akiendelea kupanda ngazi za kimataifa baada ya kukutana na msanii mashuhuri wa Nigeria, Burna Boy, katika studio za BBC Radio 1 mjini London. Mkutano huo, ambao umevutia maelfu ya mashabiki mtandaoni, unazua tetesi za uwezekano wa ushirikiano wa kisanii kati ya wawili hao. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Bien alipakia video akiwa kwenye studio pamoja na mchekeshaji wa Kimataifa, Edie Kadi, huku akidokeza ujio wa wimbo mpya. “Onwards and upwards! Had a good time with @comediekadi at @bbcradio1. New single loading… stay tuned. 🔥🎶 Get your tickets for Hamburg, O2, and Kenya tour. Link in bio! Don’t suffer like your enemies,” Bien aliandika kwenye Instagram yake baada ya mkutano huo. Kauli hiyo imeibua msisimko mkubwa, hasa ikizingatiwa kuwa mkutano wake na Burna Boy umetokea muda mfupi kabla ya ujumbe huo. Ingawa Bien hakutaja moja kwa moja kuhusu ushirikiano na Burna Boy, mashabiki wameanza kuunganisha nukta na kutarajia collabo ya kimataifa inayoweza kutikisa muziki wa Afrika. Bien, ambaye kwa sasa anazunguka Ulaya kwa ajili ya ziara na mahojiano, ameendelea kujijenga kama msanii wa kujitegemea tangu kundi la Sauti Sol lipumzike kwa muda. Kwa upande mwingine, Burna Boy anaendelea kutamba duniani na amekuwa mstari wa mbele kuipeperusha bendera ya Afrobeats kwenye majukwaa ya kimataifa.

Read More
 Burna Boy Kupiga Tamasha la Bure Burkina Faso Kwa Heshima ya “The African Giant”

Burna Boy Kupiga Tamasha la Bure Burkina Faso Kwa Heshima ya “The African Giant”

Msanii nyota wa muziki wa Afrobeats kutoka Nigeria, Burna Boy, ametangaza mpango wa kufanya tamasha la bure kabisa nchini Burkina Faso kwa ajili ya kuwatunuku raia wa taifa hilo na kuonyesha mshikamano wa Kiafrika. Kupitia ujumbe aliouandika mtandaoni, Burna Boy alisema kuwa tamasha hilo litafanyika wakati wowote ndani ya mwaka huu, iwapo kila kitu kitaenda sawa, kwa heshima ya “The African Giant” na upendo kwa watu wa Burkina Faso. “Ikiwezekana, itakuwa ni heshima kwangu kuwapigia watu wa Burkina Faso tamasha la bure la Burna Boy wakati wowote mwaka huu, Insha Allah,” aliandika msanii huyo maarufu duniani. Burna Boy alieleza kuwa sababu ya kufanya tamasha hilo bure ni kuleta watu pamoja na kuonyesha upendo kwa wale ambao husimama imara licha ya kutotambuliwa au kupewa heshima na dunia kwa ujumla. Ametaja kuwa anavutiwa na uthabiti wa watu wa Burkina Faso, hasa chini ya uongozi wa Captain Ibrahim Traoré, ambaye amekuwa maarufu barani Afrika kwa msimamo wake wa kizalendo na wa kupinga ubeberu. Tangazo hili limepokelewa kwa furaha na mashabiki wengi barani Afrika, huku wengi wakimsifu Burna Boy kwa moyo wake wa kujitolea na kwa kutumia jina lake kubwa kusherehekea mshikamano wa Waafrika. Ikiwa litatimia, tamasha hilo linatarajiwa kuwa tukio la kihistoria sio tu kwa Burkina Faso, bali kwa bara zima la Afrika.

Read More
 Burna Boy atajwa tena kutumbuiza Coachella mwaka 2023

Burna Boy atajwa tena kutumbuiza Coachella mwaka 2023

Staa wa muziki kutoka Nigeria Burna Boy ametajwa tena kutumbuiza kwenye tamasha kubwa la Muziki nchini Marekani Coachella mwaka 2023. Burna Boy ametajwa kwenye orodha ya wasanii ambao watatumbuiza Aprili 14 pamoja na wakali Bad Bunny, Pusha T, Becky G, Metro Boomin na wengine. Tamasha hilo ambalo huenda kwa wikendi mbili, mwaka huu litaongozwa wakali kama Calvin Harris, Frank Ocean, Blackpink na Bad Bunny. Hii inakuwa mara ya pili kwa Burna Boy kutumbuiza kwenye jukwaa kuu la tamasha hilo.

Read More
 Burna Boy awaomba radhi mashabiki

Burna Boy awaomba radhi mashabiki

Staa wa muziki nchini Nigeria Burna Boy amewaomba radhi mashabiki zake hii ni baada ya kuchelewa kupanda jukwaani kwenye show yake huko Lagos. Burna Boy amefunguka kuwa haikuwa dhamira yake kuchelewa kupanda jukwaani ila miundombinu ya tamasha hilo haikuwa sawa mfano muziki ulikuwa hauko vizuri jambo ambalo lilimlazimu kusubiri mpaka mambo yakae sawa. Lakini pia Burna Boy amewaalika wawekezaji kuwekeza kwenye sekta ya muziki haswa kwenye vifaa vinavyowezesha wasanii kufanya show bora.

Read More
 Burna boy atangaza kufanya onesho katika uwanja wa London.

Burna boy atangaza kufanya onesho katika uwanja wa London.

Staa wa muziki kutoka Nigeria Burna Boy anaenda kuandika historia nyingine kwenye Muziki wake, ametangaza kuwa atafanya onesho kwenye uwanja wa (London Stadium) uliopo nchini Uingereza, Juni 3 mwaka 2023. Uwanja huo una uwezo wa kubeba watu 66,000. Burna Boy atakuwa msanii wa kwanza toka barani Afrika kufanya onesho kama msanii Kinara (Headliner) kwenye uwanja nchini Uingereza. Mshindi huyo wa Tuzo ya Grammy, tayari anaishikilia rekodi ya kuwa msanii wa kwanza barani Afrika kufanya onesho katika ukumbi wa Madison Square Garden Jijini New York.

Read More
 Wasanii wa Nigeria Tems na Burna Boy watajwa kuwania Grammy 2023

Wasanii wa Nigeria Tems na Burna Boy watajwa kuwania Grammy 2023

Wasanii wa muziki kutokea nchini Nigeria, Burna Boy na Tems wametajwa kuwania vipengele viwili kila mmoja katika Tuzo za Grammy 2022. Burna Boy ametajwa kwenye vipengele viwili, “Best Global Music Performance” kwa ngoma yake ya “Last Last” na kingine ni “Best Global Music Album” – Love Damini. Naye Tems ametajwa kwenye vipengele viwili kama “Best Melodic Rap Performance” kupitia ngoma aliyoshirikishwa na future Ft Drake – Wait For You na pia “Best Rap Song” – Wait For You.

Read More
 Burna Boy ashinda tuzo ya Msanii Bora MTV Europe Music Awards 2022

Burna Boy ashinda tuzo ya Msanii Bora MTV Europe Music Awards 2022

Mwanamuziki kutoka nchini Nigeria, Burna Boy ameshinda tuzo ya MTV Europe Music Awards (MTV EMA) 2022 kama Best African Act. Hiyo ni baada ya kuwabwaga Tems na Ayra Star, wote kutokea Nigeria, pia kuna Musa Keys wa Kenya, Black Sherif wa Ghana na Zuchu wa Tanzania. Tuzo hizo zimetolewa usiku wa kuamkia leo Novemba 14, 2022 katika ukumbi wa PSD Bank Dome huko Duesseldorf, Ujerumani ikiwa ni mara ya sita kwa nchi hiyo kuwa mwenyeji. Utakumbuka hii ni Tuzo ya pili kwa Burna Boy, alishinda tena Tuzo hiyo mwaka 2019. Tuzo hizo zinazotolewa na Paramount International Networks kuheshimu wasanii na muziki katika utamaduni wa Pop, tangu mwaka 2007. Hadi tuzo za mwaka 2021, Justin Bieber ndiye anashikilia rekodi ya kushinda tuzo nyingi zaidi zikiwa ni 22, huku msanii wa kike anayeongoza akiwa ni Lady Gaga aliyeshinda 12. Kwa upande wa makundi, BTS ndio vinara upande wa wanaume wakishinda 14, huku upande wa wanawake, Little Mix waking’ara na tuzo saba.

Read More