Burna Boy Aachia Albamu Mpya, “No Sign of Weakness”
Nyota wa muziki wa kimataifa kutoka Nigeria , Burna Boy, ameachia rasmi albamu yake ya nane inayokwenda kwa jina la No Sign of Weakness. Albamu hiyo imeachiwa usiku wa kuamkia leo, Ijumaa, Julai 11, ikitimiza ahadi yake aliyotoa takribani miezi minane iliyopita kwa mashabiki wake. Albamu hii ina jumla ya nyimbo 16 na inaonesha ushawishi mkubwa wa kimataifa kwa kuwa Burna Boy ameshirikiana na mastaa wakubwa wa muziki duniani, akiwemo: Travis Scott, Mick Jagger, Stromae na Shaboozey Kushirikiana na majina haya makubwa kunathibitisha kasi na ukuaji wa Burna Boy katika kuleta sauti za Afrika kuungana na muziki wa kimataifa. Albamu hiyo sasa inapatikana kwenye majukwaa yote ya kusikiliza muziki, na tayari mashabiki wameshajawa na shauku kubwa katika kupokea kazi hii mpya. Kwa mashabiki wa Afro-fusion na muziki wa dunia kwa ujumla, No Sign of Weakness inaonekana kuwa ni kazi iliyosukwa kwa ubora wa hali ya juu, ikionyesha ufanisi mkubwa wa Burna Boy katika taaluma yake
Read More