Burna Boy Apuzilia Mbali Uvumi wa Nguvu za Kichawi Kwenye Kwapa Lake
Msanii nyota wa Nigeria, Burna Boy, amefafanua kuhusu uvumi unaozagaa mtandaoni kwamba mafanikio yake ya kimataifa yanahusishwa na nguvu za kichawi zinazodaiwa kufichwa kwenye kwapa lake. Akizungumza na Apple Music, Burna Boy amesema baadhi ya watu nchini Nigeria wanaamini kuwa uamuzi wake wa kutonyoa kwapa ni ishara ya nguvu za ajabu, wakifananisha hali hiyo na simulizi la Biblia kuhusu Samson ambaye nguvu zake zilihusishwa na nywele zake. Burna Boy amekanusha madai hayo kwa maneno makali, akiyaita ya kipuuzi. Amesisitiza kuwa kutonyoa kwapa ni uamuzi wake binafsi wa maisha, na hakuna uhusiano wowote na imani za kishirikina au nguvu za kichawi. Staa huyo, amesema kuwa mafanikio yake katika muziki yametokana na kazi ngumu, nidhamu, na msaada wa mashabiki wake duniani kote, na sio imani za kichawi kama inavyodaiwa na baadhi ya watu.
Read More