Baby Mama wa Mulamwah, Carol Sonnie, Ataka Mtoto Wake na Ruth K WakutanIshwe
Baby mama wa mchekeshaji maarufu nchini Kenya, Mulamwah, Carol Sonnie, ameweka wazi ombi lake kwa baba wa mtoto wake akitaka watoto wao wawili, Calvin na Keilah, wakutane ili wajenge ukaribu na uhusiano wa kindugu. Kupitia kauli yake ya hivi karibuni, Carol amesema ni muhimu kwa watoto hao kukutana mapema ili waweze kufahamiana na kujenga mahusiano ya kudumu kama kaka na dada. Kwa upande wake, Mulamwah ameridhia ombi hilo akisema hana pingamizi watoto wake kukutana. Hata hivyo, ameeleza kuwa kwa sasa mtoto wake Calvin aliyezaa na Baby mama wake mwingine aitwaye Ruth K yupo nyumbani kwao kwa wazazi wake, jambo linalofanya mipango ya mkutano huo ichukue muda kidogo. Ikumbukwe Mulamwah na Carol Sonnie hajakuwa na maelewano mazuri tangu mahusiano yao yavunjika miaka kadhaa iliyopita, jambo ambalo lilipelekea wawili hao kurushiana maneno makali mtandaoni kufuatia hatua ya Mulamwah kuingia kwenye mahusiano mengine na mrembo aitwaye Ruth K.
Read More