Msanii Chino Afunguka Baada ya Mdogo Sajent Kujiondoa Wanaman Gang

Msanii Chino Afunguka Baada ya Mdogo Sajent Kujiondoa Wanaman Gang

Msanii wa Bongo Fleva Chino ameibua gumzo mitandaoni baada ya kuchapisha ujumbe wa hisia kali kufuatia tangazo la Mdogo Sajent kwamba hatofanya tena kazi na kundi la Wanaman Gang. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Chino ameonyesha wazi maumivu na hisia za usaliti akisema kuwa mara nyingine mtu anaweza kuwa na roho nzuri, lakini bado akafanyiwa roho mbaya na binadamu. Dansa huyo aliyegeukia muziki, ameeleza kushangazwa na hatua ya Mdogo Sajent kuondoka licha ya msaada na jitihada alizowahi kumpa, akiongeza kuwa kitendo hicho kimemuumiza sana na kimemfanya kuamini kuwa binadamu wana maudhi. Hata hivyo, mashabiki mitandaoni wameanza kutilia shaka tukio hilo, wakidai kuwa huenda ni kiki iliyopangwa kimkakati ili kuvutia umakini wa mashabiki kabla ya kuachia kazi mpya. Taarifa kutoka vyanzo vya karibu na wasanii hao zinaeleza kuwa mvutano wao ulianza kutokana na tofauti za kimanagement na malalamiko kuhusu ushirikiano na uongozi ndani ya kundi hilo.

Read More
 Msanii Chino Aomba Maombi Baada ya Kuugua Sana

Msanii Chino Aomba Maombi Baada ya Kuugua Sana

Msanii maarufu wa muziki anayefahamika kwa jina la Chino amewatia mashaka mashabiki wake baada ya kutoa taarifa ya kusikitisha kwamba anaumwa sana na kwa sasa anahitaji maombi kutoka kwa watu wote. Kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, Chino hakufafanua kwa undani kuhusu hali yake ya kiafya, lakini alieleza kuwa anapitia kipindi kigumu na moyo wake unahitaji faraja na sala kutoka kwa wale wanaomjali. Taarifa hiyo imezua hisia tofauti miongoni mwa mashabiki na watu wa karibu, huku wengi wakimiminika kumtakia ahueni ya haraka na kumtia moyo kupitia maoni na ujumbe wa matumaini. Mashabiki na wapenzi wa muziki wake wameombwa kuungana kwa sala na dua ili Chino apate nafuu haraka na kurejea tena katika hali yake ya kawaida. Tunaendelea kumtakia Chino uponyaji wa haraka na nguvu katika kipindi hiki kigumu

Read More