Dogo Sajent Afunguka Sababu za Kutaka Kuondoka ‘Wanaman Gang’

Dogo Sajent Afunguka Sababu za Kutaka Kuondoka ‘Wanaman Gang’

Mwanamuziki chipukizi kutoka Tanzania Dogo Sajent hatimaye amefunguka kuhusu sababu zilizomfanya kutaka kuondoka kwenye lebo ya muziki ya Chino Kid, inayojulikana kama Wanaman Gang. Akizungumza na wanahabari, Dogo Sajent alieleza kuwa changamoto kuu iliyomsukuma kufikiria kuondoka ilikuwa ni malipo madogo aliyokuwa akipokea kutoka kwa lebo hiyo, ambayo hayakuweza kukidhi mahitaji ya familia yake. Aidha, aliongeza kuwa uhusiano wao wa kikazi haukuwa rasmi kwa kuwa hawakuwa na mkataba wa maandishi uliokuwa ukieleza majukumu na haki za pande zote. Msanii huyo amesema kwamba kwa sasa wameweka tofauti zao pembeni na kufikia makubaliano mapya na Chino Kid. Amesema wametia saini mkataba rasmi wa kazi ili kuhakikisha ushirikiano wao unaendelea kwa msingi wa uwazi na manufaa ya pande zote. Hata hivyo Dogo Sajent, amesema ana matumaini makubwa kuwa hatua hiyo mpya italeta mwelekeo bora katika safari yake ya muziki chini ya Wanaman Gang.

Read More