ERIC OMONDI AWAPA SOMO WASANII WA KENYA KUJITUMA ZAIDI

ERIC OMONDI AWAPA SOMO WASANII WA KENYA KUJITUMA ZAIDI

Mchekeshaji Eric Omondi amewashauri wasanii kuwa na uthubutu katika kazi zao ili waweze kufikia malengo yao. Akizungumza na Mungai Eve msanii huyo amesema kuwa kupitia sanaa ya ucheshi aliyoifanya kwa muda mrefu amejifunza zaidi kuthamini kile anachokifaanya na kujenga maudhui ambayo yanafurahisha jamii, kitu ambacho kimempa umaarufu zaidi. Katika hatua nyingine Omondi amewasisitiza wasanii kuichukulia sanaa kama kazi nyingine huku akiwataka wajenge tabia ya kuwekeza na kuweka akiba. Hata hivyo amewataka wasanii wanaochipukia kuwa na subira, uvumilivu pamoja na kufanya kazi zenye manufaa na kujenga zaidi jamii zao badala ya kuwa na fikra za kutaka kuwa matajari haraka.

Read More
 ERIC OMONDI AZIDI KUANIKA MADHAIFU YA WASANII WA KENYA

ERIC OMONDI AZIDI KUANIKA MADHAIFU YA WASANII WA KENYA

Mchekeshaji Eric Omondi amekuwa akichefukwa na Kiwanda cha Muziki nchini Kenya, leo ameibuka tena baada ya Diamond Platnumz kutumbuiza kwenye hafla ya mwisho ya mkutano wa kisiasa wa Azimio la Umoja One Kenya katika uwanja wa Kasarani ambapo inadaiwa Chibu alilipwa kiasi cha Ksh. Millioni 10 kutumbuiza kwa dakika 30 tu. Eric Omondi ambaye kwa muda mrefu amekuwa akipigana kwa udi na uvumba kutetea muziki wa humu nchini huku akitamba taasisi zote na washikadau kukumbatia kucheza miziki ya Kenya kwa asilimia 75, alisema kwamba hana ubaya na Diamond Platnumz ila inasikitisha sana kwamba katika halfa ya kihistoria kama ile ya Kasarani, hakuna msanii hata mmoja wa humu nchini alipata kutambulika na kuoenekana kuwa wa thamani. Mchekeshaji huyo alionekana kuwalaumu wasanii wa Kenya kwa kutojijenga vizuri na kujikuza (SHOWBIZ) kwa njia inayoweza kuwapeleka kwenye majukwaa makubwa na ya kihistoria kama hayo. Omondi alitolea mfano kwa kuweka orodha ya wasanii wanaosikilizwa zaidi Kenya ambapo Top 5 wamekaa wasanii wa Tanzania.

Read More
 ERIC OMONDI KUFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA KUKWEPA KULIPA DENI.

ERIC OMONDI KUFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA KUKWEPA KULIPA DENI.

Mchekeshaji Eric Omondi anatarajiwa kufikisha kortini Mei 27 mwaka huu kwa tuhuma za kukwepa kulipa deni la shillingi la 4 za Kenya. Taarifa hiyo imethibitisha na mwanamitindo wa masuala ya urembo nchini Melina kwenye mahojiano na Presenter Ali ambapo amesema kwamba mchekeshaji huyo ameshindwa kuheshimu agizo la mahakama la kumlipa deni lake kwa awamu mbili. Mrembo huyo ameenda mbali zaidi na kusema kwamba amesikitishwa na kitendo cha Omondi kukwepa simu zake kila mara anapojaribu kumuulizia kuhusu deni hilo jambo analosema limemlazimu kufufua tena kesi lilokuwa linamuandama. Hata hivyo amesema hatalegeza msimamo wa kumchukulia Omondi hatua kali za kisheria na ana Imani mahakama itamtendea haki ili iwe funzo kwa wanaokimbia madeni ya watu. Utakumbuka Melina amekuwa akimvalisha Eric Omondi kwenye shughuli zake lakini mchekeshaji huyo aliingiwa na jeuri baada ya kushindwa kulipa huduma aliyopewa na mrembo huyo.

Read More
 HARMONIZE NA ERIC OMONDI WAMALIZA TOFAUTI ZAO

HARMONIZE NA ERIC OMONDI WAMALIZA TOFAUTI ZAO

Wasanii Harmonize  na Eric Omondi hatimaye wamemaliza tofauti zao kwa kusameheana kufuatia matukio yaliyojiri Jumapili Mei mosi, 2022. Baada ya uvumi wa ugomvi wake na Harmonize, Eric Omondi ameomba radhi kutokana na kisa hicho ambacho kinadaiwa kuwafanya yeye na nyota huyo kutoka Tanzania kukaa karibu siku nzima katika kituo cha polisi cha Kileleshwa jijini nairobi. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Eric Omondi ameweka wazi kuwa walisuluhisha changamoto iliyopelekea kukosekana kwa maelewano kati yao. “Kama kaka mkubwa, kama mshereheshaji na kama msanii mwenzangu wa Afrika Mashariki nataka kuomba radhi kwa yote yaliyotokea,” Eric alisema. Kwa upande wa Harmonize alisema hakuna aliyekamilika na kuongeza kuwa anachukulia kilichotokea kama sehemu ya changamoto za kazi na si vinginevyo huku akikanusha kumshambulia Eric Omondi kwa ngumi. “Bado mimi na kaka yangu tunampenda na kumheshimu hakuna mtu mkamilifu katika dunia hii, mimi niko poa kutoka moyoni mwangu. Kilichotokea ni changamoto za kazi tu na katika ulimwengu huu huwezi kuwa na furaha siku zote sisi ni ndugu,” Harmonize amesema katika instastory yake Instagram. Ikumbukwe Harmonize alikamatwa wikiendi hii iliyopita na kushikiliwa katika kituo cha Polisi cha Kileleshwa kwa madai ya kukiuka makubaliano ya kutokea kwenye club kadhaa za jijini Nairobi baada ya malipo kutolewa. Inasemekana Eric Omondi ndiye alipokea malipo hayo kwa niaba ya Harmonize.

Read More
 HARMONIZE AWATOLEA UVIVU WAANDAAJI WA TAMASHA LA AFRIKA MOJA KISA PICHA YA ERIC OMONDI

HARMONIZE AWATOLEA UVIVU WAANDAAJI WA TAMASHA LA AFRIKA MOJA KISA PICHA YA ERIC OMONDI

Mkali wa muziki wa Bongofleva Harmonize ameonesha wazi kutofurahishwa na poster ya tamasha la Afrika Moja linalotarajiwa kufanyika nchini, Aprili 30 mwaka huu. Kupitia insta story yake kwenye mtandao wa Instagram Boss huyo wa Konde Gang ameeleza kwamba kitendo walichokifanya waandaaji wa tamasha hilo sio cha kiungwana kufuatia picha yake kuonekana kubwa huku picha ya mchekeshaji nyota nchini Eric Omondi ikiwa ndogo. Harmonize ameeleza kuwa Omondi ni mkubwa kwake kiumri na kisanaa pia, huku akidai kuwa picha hiyo imewekwa kama Omondi anakuja kufanya usafi tu katika uwanja wa KICC ambapo tamasha hilo litafanyika. Hata hivyo amewataka waandaaji wa tamasha hilo watengeneze poster nyingine ili aweze kupost kwenye uso wa ukurasa wake wa Instagram.

Read More
 ERIC OMONDI ATOA CHANGAMOTO KWA EZEKIEL MUTUA KUJA NA TUZO ZA MUZIKI NCHINI KENYA

ERIC OMONDI ATOA CHANGAMOTO KWA EZEKIEL MUTUA KUJA NA TUZO ZA MUZIKI NCHINI KENYA

Mchekeshaji Eric Omondi amemshauri mwenyekiti wa mwenyekiti mpya wa chama cha muziki kinachojihusisha na hakimiliki nchini Kenya Ezekiel Mutua kuja na tuzo za muziki kama ana nia njema ya kufufua muziki wa kenya ambao umeonekana kumpoteza mweelekeo katika siku za hivi karibuni. Kupitia ukurasa wake wa instagram Omondi amesema kuandaliwa kwa tuzo hizo za  muziki itatoa nafasi ya kutambua mchango wa wasaniii wanaofanya vizuri kimuziki nchini,  jambo ambalo amedai litawafanya wasanii kurejesha imani kwa chama cha muziki kinachojihusisha na hakimiliki nchini. Hata hivyo Eric Omondi amemtaka ezekiel mutua kuwekeza pesa nyingi kwenye suala la kurejesha tuzo za muziki nchini huku akipendekeza Julai 2 mwaka huu kama siku nzuri ambayo hafla ya ugawaji tuzo inapaswa kufanyika nchini. “Daktari, Life rarely gives us a second chance but when it does then we are called upon to give it our very best. This is your chance to ABSOLVE yourself and here is how you can do it. Artists lost Faith in MCSK and this is a great paradox because if MCSK is here for the Artists and the Artists have no faith in it then it lacks PURPOSE,” amesema Eric Omondi Mchekeshaji huyo ameongeza “HERE IS MY PROPOSAL TO YOU. Let us Establish a MUSIC AWARDS SHOW that will not only recognize but also Award Perfoming Artists. INJECT MONEY BACK INTO THE INDUSTRY.This will help bring back life into the Industry which is currently seriously lacking. July 2nd 2022 is my PROPOSED DATE. KAZI KWAKO!!!,” Licha ya Eric Omondi kuwasilisha mapendekezo yake hayo kupitia mtandao wake wa Instagram Ezekiel Mutua ambaye ni mwenyekiti mpya wa chama cha muziki kinachojihusisha na hakimiliki nchini Kenya hajatoa tamko lolote kuhusu suala hilo ila ni jambo la kusubiriwa.

Read More
 ERIC OMONDI AMVUA NGUO NOTI FLOW KWA KUMVUNJIA HESHIMA

ERIC OMONDI AMVUA NGUO NOTI FLOW KWA KUMVUNJIA HESHIMA

Mchekeshaji maarufu nchini Eric Omondi ameingia kwenye headlines mara baada ya kutupia maneno makali mtandaoni na rapa Noti Flow kuhusu magari waliyowanunulia wapenzi wao hivi karibuni. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Omondi amemtaka Noti Flow kutofuatilia maisha yake ya ndani huku akitishia kumfundisha adabu pamoja na mpenzi wake King Alami. “Ambie huyu CHOKORA Asiwahi Ita jina yangu tena!!!!  Ama nitamshika na huyu demu wake NIWAKULE mpaka wakue straight. IDIOT!!!!” Ameandika Omondi. Post hiyo haikupokelewa vyema na Noti Flow ambaye alishuka kwenye uwanja wa comment ya post hiyo na kumchana tena Eric Omondi akisema mchekeshaji huyo amemkasirikia kwa sababu gari lake ni la kukodisha. “He’s mad cz it’s car hire post logbook bruh. Chokora ni wewe na car hire zako. Clout chaser.” Ameandika Noti Flow. Ikumbukwe purukushani kati ya Eric Omondi na Noti Flow ilianza mara baada ya mrembo huyo kumtaka Omondi aoneshe stakabadhi za gari aliyomnunulia mpenzi wake juzi kati ambapo alienda mbali na kujigamba kuwa tangu amnunulie gari mpenzi wake king alami mastaa wengi kutoka kenya wameanza kumuiga kwa kukodisha magari wakati hana lolote katika maisha.

Read More
 ERIC OMONDI AWAPONDA WATAYARISHAJI WA YOUNG, FAMOUS & AFRICAN,ADAI WAMEMUIBIA UBUNIFU WAKE

ERIC OMONDI AWAPONDA WATAYARISHAJI WA YOUNG, FAMOUS & AFRICAN,ADAI WAMEMUIBIA UBUNIFU WAKE

Mchekeshaji maarufu nchini Eric Omondi amezua gumzo mtandaoni mara baada ya kudai kuwa waandaaji wa reality show ya Young, Famous & African waliiba ubunifu wa kipindi chake cha Wife Material. Kupitia ukurasa wake wa Instagram mchekeshi huyo ametilia shaka namna ambavyo maudhui ya show hiyo yenye matukio halisi ina fanana kwa asilimia 100 na ya kipindi chake cha Wife Material huku akisema kuwa kuna uwezekano mkubwa wa watayarishaji wa Young, Famous & African waliiba mawazo yake. Kwa upande wake mtayarishaji wa kipindi cha Wife Material mchekeshaji Eddie Butita amesema yuko tayari kufanya kazi na maprodyuza wa Young, Famous and African kama wataonyesha nia ya kuhitaji huduma zake. Kauli yao Eric Omondi imekuja mara baada ya watumiaji wa mitandao ya kijamii nchini kuzua mjadala na kuhoji ni kwa nini mastaa wa Kenya hawakuhusishwa kwenye show ya Young, Famous and African ambapo wengi walihoji huenda kiburi ndio imewaponza mastaa wengi wa Kenya. Utakumbuka Show ya Young, Famous & african ilianza kuruka kwenye mtandao wa Netflix, Machi 18, 2022 kupitia maonyesho saba yaliyowashirikisha mastaa wakubw, kutoka Afrika kusini, Uganda, Tanzania, na Nigeria ambapo kwa Afrika Mashariki tunawakilishwa na Diamond Platinumz pamoja na Zari TheBossLady.

Read More
 ERIC OMONDI ATANGAZA UJIO WA TAMASHA LA WANAMUZIKI WA KENYA

ERIC OMONDI ATANGAZA UJIO WA TAMASHA LA WANAMUZIKI WA KENYA

Mchekeshaji maarufu nchini Eric Omondi ametangaza ujio na tamasha la muziki ambalo litakuwa mahususi kwa wasanii wa Kenya. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Eric Omondi, amethibitisha kuja na tamasha liitwalo “The Fill Up 254” ambalo litafanyika katika uwanja wa Carnivore, Aprili 2 mwaka huu. Omondi ameeleza kwamba amekuwa akipigania muziki wa Kenya kwa muda sasa na wakati umewadia wa kutekeleza mabadiliko anayotaka kuyaona kwenye kiwanda cha muziki nchini. Hata hivyo kupitia ukurasa rasmi wa tamasha hilo kwenye mtandao wa Instagram, majina ya wasanii watakaotumbuiza kwenye tamasha la  “The Fill Up 254” yametajwa ambapo kundi la muziki wa Hiphop nchini Wakadinali limejumuhishwa kwenye orodha hiyo. Ikumbukwe Eric Omondi amekuwa mstari wa mbele kutetea muziki na wanamuziki wa Kenya kwa kuhimiza vyombo vya habari kucheza kwa kiasi kikubwa nyimbo za wanamuziki wa ndani lakini pia amekuwa akishinikiza wanaoandaa matamasha nchini Kenya kuzingatia wasanii wa ndani badala ya kuwapa kipaumbele wasanii wa kigeni.

Read More
 ERIC OMONDI AUMIZWA NA KITENDO CHA OMAH LAY KUSHINDWA KUFANYA KOLABO NA TANASHA DONNA

ERIC OMONDI AUMIZWA NA KITENDO CHA OMAH LAY KUSHINDWA KUFANYA KOLABO NA TANASHA DONNA

Mchekeshaji maarufu nchini Eric Omond omeonekana kutofurahishwa na kitendo cha Omah Lay kutofanya kazi na mpenzi wake Tanasha Donna licha ya ukaribu wao. Katika mahojiano yake na Plug TV Omondi amesema kitendo cha Omah Lay kufanya kolabo na Justin Bieber inaonyesha ni jinsi gani   hitmaker huyo wa “Godly” hana  mpango wa kuupeleka muziki wa Tanasha Donna kimataifa. Utakumbuka kwa muda sasa Omah Lay amedai kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Tanasha Donna ila wawili hao wamekuwa wakikanusha madai hayo kwa kusema kwamba uhusiano wao ni wa kirafiki tu

Read More
 MCHEKESHAJI ERIC OMONDI AREJELEA HARAKATI ZA KUUPIGANIA MUZIKI WA KENYA

MCHEKESHAJI ERIC OMONDI AREJELEA HARAKATI ZA KUUPIGANIA MUZIKI WA KENYA

Kama kuna kitu ambacho Mchekeshaji Eric Omondi anajivunia kuwa nacho ni kujiamini, baada ya jaribio lake la kwanza la kuikingia kifua muziki wa kenya kutibuka mwaka jana na hata kupelekea kukamatwa kwake, mchekeshaji huyo amerudi tena bungeni kushinikiza mswada kutaka muziki wa Kenya upewe hadhi ujadiliwe. Akizungumza nje ya majengo ya bunge  Omondi amesema hatelekeza msimamo wake wa kutaka  asilimia 75 ya muziki wa Kenya upigwe kwenye vituo vya redio na runinga nchini hadi pale mswaada huo itapitisha kuwa sheria bungeni. Hata hivyo wabunge John Kiarie na David Ole Sankok wameonekana kumuunga mkongo eric omondi katika harakati zake za kupigania maslahi ya wasanii wa Kenya huku wakihapa kwa kauli moja kuhakikisha mswada huo unapitishwa bungeni

Read More
 ERIC MONDI AFUNGUKA SABABU ZA KUMTEMA MSANII MISS P

ERIC MONDI AFUNGUKA SABABU ZA KUMTEMA MSANII MISS P

Mchekeshaji maarufu nchini Eric Omondi amefunguka sababu za kusitisha kufanya kazi na msanii Miss P baada ya kuchukua jukumu la kumsimamia. Katika mahojiano na mungai Eve,  Omondi amesema changamoto kubwa ambayo kampuni yake ilikutana nayo kutoka kwa Miss P, ni msanii huyo kutoonyesha nia ya kutaka kuzisukuma  kazi zake za muziki  mwenyewe. Mchekeshaji huyo amedai kuwa miss p hakuwa mtu wa kutumia mitandao ya kijamii na mara nyingi ilimbidi asitishe shughuli zake kwa ajili ya kusukuma muziki wa Miss P licha ya kutokuwa mwanamuziki. Eric omondi amesema uzembe wa Miss P kusukuma muziki wake kama msanii ilichangia kampuni yake kuvunja mkataba wa kufanya nae kazi. Kauli ya Eric Omondi imekuja siku chache mara baada ya Miss P kwenye mahojiano na mzazi willy tuva kudai kuwa aliacha kufanya kazi na eric omondi kwa sababu ni mtu haeleweki kwani alipoachia wimbo wake wa “Baby Shower” alikata mawasiliano nae.

Read More