Eric Omondi Akamilisha Safari ya Kutembea Kwa Miguu Kutoka Nairobi Hadi Busia

Eric Omondi Akamilisha Safari ya Kutembea Kwa Miguu Kutoka Nairobi Hadi Busia

Mchekeshaji na mwanaharakati wa masuala ya kijamii Eric Omondi amefanikiwa kukamilisha safari yake ya kutembea kwa miguu kutoka Nairobi hadi Busia ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kuchangisha fedha za kujenga kituo cha uokoaji kupitia mpango wake wa Sisi Kwa Sisi. Kupitia ujumbe alioutuma baada ya kukamilisha safari hiyo, Eric amesema hatua hiyo ilikuwa zaidi ya juhudi zake binafsi, bali ilikuwa ni ishara ya mshikamano wa Wakenya kusaidiana. Omondi ametoa shukrani kwa kila mtu aliyeshiriki katika safari hiyo kwa njia mbalimbali, ikiwemo kutembea naye, kutoa michango, kusambaza ujumbe wa kampeni na kuunga mkono mradi huo tangu mwanzo hadi mwisho. Kupitia kampeni ya Sisi Kwa Sisi, Eric Omondi amekuwa akihamasisha Wakenya kusaidiana badala ya kusubiri msaada kutoka nje, huku mradi wa kituo cha uokoaji ukitarajiwa kusaidia watu wenye mahitaji maalum na wale wanaohitaji msaada wa haraka katika jamii.

Read More
 Eric Omondi Azindua Safari ya Nairobi-Busia kwa Ajili ya Kuchangisha Fedha.

Eric Omondi Azindua Safari ya Nairobi-Busia kwa Ajili ya Kuchangisha Fedha.

Mwanaharakati na mchekeshaji maarufu, Eric Omondi, ameweka wazi azma yake mpya ya kutembea kwa miguu kutoka Nairobi hadi Busia, kwa ajili ya kuchangisha fedha zitakazoendeleza ujenzi wa kituo cha uokozi cha Sisi Kwa Sisi. Kupitia ujumbe wake kwa umma, Omondi amesema safari hiyo ya siku tano inatarajiwa kuanza rasmi tarehe 2 Machi mwaka huu. Amesisitiza kuwa hatasimama hadi ndoto ya kukamilisha kituo cha Sisi Kwa Sisi itimie kwa ajili ya wakenya wenye uhitaji. Hata hivyo mchekeshaji huyo, amewasihi Wakenya watakaokuwa njiani kumpokea na kuendelea kuchangia kile walicho nacho ili kufikia malengo ya mradi huo. Tangazo hili limekuja ikiwa ni siku chache tu tangu Omondi akamilishe ziara nyingine ya kihistoria ya kutembea kwa miguu kutoka Nairobi hadi Mombasa ambapo alifanikiwa kukusanya mamilioni ya fedha yaliyoelekezwa kwenye ujenzi wa miundombinu ya kituo hicho cha Sisi Kwa Sisi.

Read More
 Eric Omondi Aanza Rasmi Ujenzi wa Taasisi ya Sisi kwa Sisi

Eric Omondi Aanza Rasmi Ujenzi wa Taasisi ya Sisi kwa Sisi

Mchekeshaji na mwanaharakati wa kijamii Eric Omondi ameanza rasmi ujenzi wa taasisi ya Sisi Kwa Sisi Rescue baada ya kukamilisha safari ya kutembea kwa miguu kutoka Nairobi hadi Mombasa kwa ajili ya kuchangisha fedha. Kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, Eric amethibitisha kuwa ndoto hiyo sasa imeanza kutimia, akieleza kuwa tayari wameweka jiwe la msingi kwenye ardhi waliyonunua ili kuanza ujenzi wa kituo hicho. Amesema kuwa timu yake iko kazini kwa sasa kuhakikisha mradi huo unafanikiwa. Mradi huo unalenga kujenga kituo cha uokoaji (rescue centre), shule ya sekondari ya bure, ghala la kuhifadhi misaada pamoja na ununuzi wa ambulensi ili kusaidia familia zenye uhitaji katika jamii. Hatua hiyo imepokelewa kwa hisia mseto huku wengi wakimpongeza kwa juhudi zake za kusaidia jamii, hasa baada ya safari yake ndefu ya kutembea mamia ya kilomita kama njia ya kuhamasisha umma kuchangia mradi huo.

Read More
 Mchekeshaji Eric Omondi Atangaza Nia ya Kugombea Nafasi ya Kisiasa 2027

Mchekeshaji Eric Omondi Atangaza Nia ya Kugombea Nafasi ya Kisiasa 2027

Mchekeshaji na mwanaharakati wa kijamii, Eric Omondi, ametangaza rasmi nia yake ya kuwania nafasi ya kisiasa kama Mwakilishi wa Vijana katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2027, hatua inayoongeza orodha ya wasanii wanaoingia katika ulingo wa siasa nchini Kenya. Kwenye mahojiano yake hivi karibuni, Omondi amesema kuwa ushiriki wa vijana katika mchakato wa kupiga kura ni jambo la msingi endapo Kenya inataka kushuhudia mabadiliko ya kweli. Amesisitiza kuwa vijana wana nguvu kubwa ya kuamua hatima ya nchi, hivyo wanapaswa kuchukua nafasi za uongozi badala ya kuachwa pembeni. Mchekeshaji huyo amefichua kuwa iwapo atachaguliwa, atashinikiza mabadiliko makubwa ya kikatiba baada ya uchaguzi, yakiwemo mapendekezo ya kupunguza idadi ya kaunti pamoja na kuondoa baadhi ya nyadhifa za kuchaguliwa, akisema hatua hizo zitapunguza gharama za uendeshaji wa serikali na kuleta ufanisi. Hata hivyo, Eric Omondi amewakosoa vikali baadhi ya viongozi wa kisiasa kwa kile alichokitaja kuwa ni kuwadhalilisha na kuwadharau vijana, akiongeza kuwa matukio ya hivi karibuni nchini Kenya yanaonyesha wazi dhana potofu inayotumiwa dhidi ya vijana licha ya mchango wao mkubwa katika maendeleo ya taifa.

Read More
 Eric Omondi azindua rasmi mpango wa Youth 47

Eric Omondi azindua rasmi mpango wa Youth 47

Msanii na mwanaharakati wa kijamii Eric Omondi amezindua rasmi mpango wa Youth 47, hatua aliyotaja kuwa ni mwanzo wa safari kuelekea Kenya mpya inayoongozwa na vijana. Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Eric Omondi amesema zaidi ya asilimia 70 ya wapiga kura nchini Kenya ni vijana, hivyo sauti zao lazima zisikike na kuthaminiwa. Amesema kupitia YOUTH 47, vijana hawatabaki tena kuwa wapiga kura wanaotumiwa wakati wa uchaguzi pekee, bali watakuwa viongozi wanaochukua nafasi za maamuzi katika ngazi zote za uongozi. Kwa mujibu wake, kaunti zote 47 za Kenya ziliwakilishwa katika uzinduzi huo, ishara ya umoja na dhamira ya kitaifa. Amewatakia heri vijana hao katika safari yao ya uongozi, akisema ana imani kuwa mpango huo utaleta mabadiliko makubwa kwenye masuala ya uongozi nchini Kenya.

Read More
 Eric Omondi Aokoa Familia Iliyovunjiwa Mlango kwa Kukosa Kodi

Eric Omondi Aokoa Familia Iliyovunjiwa Mlango kwa Kukosa Kodi

Mchekeshaji na mwanaharakati wa kijamii Eric Omondi amekutana na familia changa iliyogusa nyoyo za wengi baada ya kupitia masaibu makubwa ya maisha, ikiwemo kuvunjiwa mlango wa nyumba na mwenye nyumba kwa kushindwa kulipa kodi.. Kupitia wakfu wake wa Sisi kwa Sisi, Eric Omondi ameahidi kusimama na familia hiyo kwa vitendo. Amesema wako tayari kuwafungulia biashara ndogo itakayowawezesha kujitegemea kiuchumi, na pia ameeleza mpango wa kununua kiwanja ambacho watajengewa nyumba ili kuwaondolea mzigo wa kodi na kuwapa makazi ya kudumu. Eric Omondi pia ametoa wito kwa Wakenya wenye nia njema kushirikiana kupitia TEAM SISI KWA SISI ili kuibadilisha maisha ya familia hiyo. Ameeleza kuwa msaada wowote, mdogo au mkubwa, utakuwa na mchango mkubwa katika kuinua maisha yao. Familia hiyo, inayoundwa na Ishmael na mkewe Grace, ina mtoto mchanga wa miezi nane na imekuwa ikipambana kutafuta riziki ya kila siku. Ishmael ameeleza kuwa huuza mayai ili kuisaidia familia yake kupata mahitaji ya msingi, lakini kipato hicho hakijatosha kukidhi gharama za maisha, hali iliyosababisha mgogoro wao na mwenye nyumba.

Read More
 Eric Omondi Afunguka Kiasi Kikubwa cha Fedha Alichowahi Kupata Kupitia Wakfu wa Sisi kwa Sisi

Eric Omondi Afunguka Kiasi Kikubwa cha Fedha Alichowahi Kupata Kupitia Wakfu wa Sisi kwa Sisi

Mchekeshaji na mwanaharakati, Eric Omondi, amesema kiasi kikubwa zaidi kuwahi kukusanywa kupitia mpango wa Sisi Kwa Sisi ni shilingi milioni 15.7 za Kenya, zilizokusanywa ndani ya siku moja na nusu pekee. Akizungumza kwenye podcast ya Chris The Bass, Omondi amesema fedha hizo zilikusanywa hivi karibuni kwa ajili ya kumsaidia mwanamke mmoja kutoka Githurai, ambaye kupitia mchango huo waliweza kumjengea nyumba za kupanga. Omondi amesema aliweka namba ya malipo ya paybill mtandaoni wakati akiwa anasafiri kuelekea Kisumu kwenye moja ya hafla, na baada ya kutua kisumu ndani ya dakika 26, akaunti ya miamala ya simu ilikuwa tayari imepokea zaidi ya shilingi milioni 7.2 Mchekeshaji huyo, ameeleza kuwa mpango wa Sisi Kwa Sisi umeendelea kugusa maisha ya wengi, huku akibainisha kuwa michango mingi hutolewa na Wakenya kwa moyo wa kujitolea, ikiwa ni kiasi ndogo kama shilingi tano, kumi, ishirini au hamsini. Kwa mujibu wa Eric Omondi, kutokana na maoni ya Wakenya, mpango huo sasa umejikita zaidi kusaidia matukio ya dharura, hasa kwa watu wasiokuwa na uwezo wa kujisaidia.

Read More
 Eric Omondi Atangaza Rasmi Kuwania Ubunge Lang’ata

Eric Omondi Atangaza Rasmi Kuwania Ubunge Lang’ata

Mchekeshaji na mwanaharakati, Eric Omondi, ametangaza rasmi nia yake ya kuwania kiti cha Ubunge wa Lang’ata katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2027. Akizungumza na waandishi wa habari, Omondi amesema azma yake kubwa ni kuongoza kampeni kabambe ya kuhamasisha vijana kujisajili kama wapiga kura, akisisitiza kuwa mabadiliko ya kweli ya uongozi yatawezekana tu iwapo vijana watajitokeza kwa wingi kushiriki katika mchakato wa kidemokrasia. Omondi pia amedai kuwa ifikapo mwaka 2027, wabunge wa wazee wataregeshwa nyumbani ili kupisha viongozi vijana wenye nguvu, mawazo mapya na uelewa wa changamoto za kizazi cha sasa. Kwa mujibu wake, wakati umefika kwa vijana kuchukua usukani wa uongozi na kushiriki kikamilifu katika maamuzi ya kitaifa. Hatua ya Eric kuingia rasmi kwenye siasa za Lang’ata imezua maswali kuhusu uhusiano wake na Phelix Odiwour maarufu Jalang’o, mbunge wa sasa wa eneo hilo. Wawili hao waliwahi kuwa marafiki wa karibu na washirika katika tasnia ya burudani, lakini dalili zinaonyesha kuwa huenda mahusiano yao si mazuri kwa sasa, hasa ikizingatiwa msimamo wa Eric wa kutaka mabadiliko ya uongozi katika eneo hilo.

Read More
 Kauli ya Omondi Kwa Vijana Yazua Mjadala Kuhusu Siasa za Lang’ata

Kauli ya Omondi Kwa Vijana Yazua Mjadala Kuhusu Siasa za Lang’ata

Ziara ya mwanaharakati na mchekeshaji Eric Omondi katika eneo la Lang’ata imezidi kuibua gumzo kubwa kuhusu mustakabali wa kisiasa wa mbunge wa sasa Felix Oduor (Jalang’o) kuelekea uchaguzi wa 2027 baada ya umati mkubwa wa vijana kumkaribisha kwa shangwe na nderemo katika mtaa wa Mugumoini. Katika ziara hiyo iliyovutia mamia ya vijana, Omondi alitembea mitaani akiandamana na umati uliokuwa ukimuimbia na kumpa mapokezi ya kishujaa. Mapokezi hayo yamechochea uvumi kuwa huenda anajiandaa kuwania kiti cha ubunge wa Lang’ata, jambo ambalo limeanza kuongeza shinikizo kwa mbunge wa sasa. Hata hivyo, kauli yake kwa vijana imezua mjadala mpya baada ya Omondi kuwataka vijana kujisali kama wapiga kura, akiwahimiza kuonyesha msimamo wao dhidi ya kile alichokitaja kama mfumo unaowatelekeza vijana. Wadadisi wa siasa za Nairobi wanasema kuwa Omondi ana ushawishi mkubwa miongoni mwa vijana, na kauli zake zinaweza kuwa na athari katika mienendo ya kisiasa ya eneo hilo. Hadi kufikia sasa, Eric Omondi hajatangaza rasmi iwapo atawania kiti cha ubunge cha Lang’ata mwaka 2027. Hata hivyo, ziara yake na mapokezi aliyopata yanaendelea kuongeza tashwishi kuhusu ramani ya kisiasa ya Lang’ata katika miaka ijayo.

Read More
 Eric Omondi Ataka Wasanii Tanzania Kuungana Kupinga Udhalimu

Eric Omondi Ataka Wasanii Tanzania Kuungana Kupinga Udhalimu

Msanii wa vichekesho na mwanaharakati wa kijamii, Eric Omondi, ametoa wito kwa wasanii nchini Tanzania kuungana kupinga udhalimu na kutokubali kutumika kisiasa kwa njia zinazoharibu taswira na brand zao. Akipiga stori na Plug TV, Omondi amesema kuwa muziki na sanaa kwa ujumla hubaki mioyoni mwa watu kwa muda mrefu zaidi kuliko siasa, akisisitiza kuwa wasanii wanapaswa kulinda heshima na ushawishi wao kwa jamii. Kwa mujibu wake, kujihusisha na siasa za upande mmoja kunahatarisha uaminifu wa wasanii kwa mashabiki wao, na badala yake wanapaswa kutumia majukwaa yao kuhamasisha haki, umoja na mabadiliko katika jamii. Kauli yake imekuja baada ya baadhi ya wasanii nchini Tanzania kuunga mkono serikali iliyochaguliwa katika uchaguzi wa Oktoba 28, uchaguzi ambao ulizua utata na kupingwa na wananchi waliodai haukuwa huru na wa haki.

Read More
 Eric Omondi Awakingia Kifua Gen Z kwa Kutoshiriki Uchaguzi Mdogo Kenya

Eric Omondi Awakingia Kifua Gen Z kwa Kutoshiriki Uchaguzi Mdogo Kenya

Mchekeshaji na mwanaharakati Eric Omondi ametetea vijana wa Gen Z kufuatia madai kwamba hawakujitokeza kushiriki uchaguzi mdogo uliofanyika Novemba 27, ambapo idadi ya wapiga kura ilikuwa ndogo kushinda matarajio. Kupitia mitandao ya kijamii, Omondi amesema kutoshiriki kwao hakukuwa dalili ya kutojua umuhimu wa uchaguzi, bali ni hatua ya kujiondoa kwenye michakato ambayo haina manufaa kwao. Amefafanua kuwa uchaguzi huo haukuwa juu ya mustakabali wa vijana, bali ni mapambano kati ya wanasiasa na makundi yenye maslahi yao binafsi, hali aliyoiita vita vya kisiasa. Kwa mujibu wake, vijana walibaki pembeni kwa sababu hawangefaidika lolote kutokana na uchaguzi huo, na hivyo hawakuona sababu ya kushiriki. Amepinga vikali juhudi za kuwalaumu Gen Z kwa idadi ndogo ya waliojitokeza kupiga kura, akisema ni makosa kuwatupia lawama wakati hawahusishwi kikamilifu katika maamuzi yanayowahusu.

Read More
 Eric Omondi Ashinda Tuzo ya People’s Champion of the Year kwenye NGO Awards 2025

Eric Omondi Ashinda Tuzo ya People’s Champion of the Year kwenye NGO Awards 2025

Mchekeshaji na mwanaharakati kutoka nchini Kenya, Eric Omondi, ameendelea kuthibitisha nafasi yake kama sauti ya wananchi baada ya kutangazwa mshindi wa tuzo ya People’s Champion of the Year katika hafla ya NGO Awards 2025. Tuzo hiyo, ambayo hutolewa kwa mtu anayejitolea kupigania haki, ustawi na maslahi ya jamii, imeonekana kuwa uthibitisho wa juhudi za Eric katika kuhamasisha wananchi, kufanya harakati za kijamii, na kusaidia watu wenye uhitaji kupitia kampeni zake mbalimbali. Kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii, Eric Omondi amewashukuru mashabiki wake akisisitiza kuwa ushindi huo ni wao. Katika ujumbe wake, ameeleza kuwa mafanikio hayo yametokana na sapoti na umoja wa mashabiki na wafuasi wake ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakimuunga mkono. Ushindi huu unakuja wakati ambapo Eric Omondi ameendelea kuwa mstari wa mbele katika masuala ya kijamii, ikiwemo kusaidia familia zisizojiweza, kupigania huduma bora, na kuibua mijadala kuhusu changamoto zinazowakumba wananchi wa kawaida.

Read More