Esther Musila awajibu wakosoaji: “Mali ni zangu, mume ni wangu”

Esther Musila awajibu wakosoaji: “Mali ni zangu, mume ni wangu”

Mke wa msanii wa muziki wa injili Guardian Angel, Esther Musila, amewajibu vikali watu wanaodai kuwa mali anazomiliki ndizo zimemshawishi mume wake kuendelea kusalia katika ndoa yao, licha ya tofauti kubwa ya umri kati yao. Kupitia ujumbe aliouweka Tiktok, Esther ameonyesha kushangazwa na madai hayo akisema hawezi kutishwa na maneno ya watu mtandaoni. Amesisitiza kuwa mume ni wake na mali anazomiliki ni zake, hivyo hana sababu ya kuishi kwa kuogopa mitazamo ya wengine. Esther ameenda mbali zaidi na kuwataka wakosoaji watafute wapenzi wao na wawape pesa kama wanavyoamini yeye anavyomfanyia Guardian Angel, badala ya kutumia muda mwingi kuzungumzia ndoa yake. Mwanamama huyo ambaye amekuwa pamoja na Guardian Angel kwa miaka 6, amedokeza kuwa mwaka 2026 ataendelea kumpenda mume wake zaidi, akisema hilo litawapa wakosoaji jambo jipya la kuzungumzia.

Read More
 Mke wa Guardian Awajibu Wakosoaji Waliodai Ndoa Yao Haitadumu

Mke wa Guardian Awajibu Wakosoaji Waliodai Ndoa Yao Haitadumu

Mke wa Guardian Angel, Esther Musila amewajibu vikali wakosoaji waliodai ndoa yao haitafika mbali kuelekea maadhimisho ya miaka minne ya ndoa na miaka sita tangu waanze kuwa pamoja. Akizungumza kupitia mitandao ya kijamii, Esther amesema kuwa yeye na Guardian Angel bado wapo imara na hawana mpango wa kuachana hivi karibuni, licha ya shinikizo kutoka kwa jamii kuhusu suala la kupata mtoto pamoja na tofauti yao kiumri. Mwanamama huyo wa miaka 55, amesema walimwengu wanapaswa kuwazoea kuwaona pamoja, akisisitiza kuwa ndoa yao haiendeshwi na maoni ya watu bali misingi ya mapenzi, heshima na uamuzi wao binafsi. Hata hivyo amesema kuwa tarehe 4 Januari itakuwa siku maalum sana kwa familia yao, kwani watakuwa wakiadhimisha miaka minne ya ndoa na pia kusherehekea siku ya kuzaliwa ya Guardian Angel. Ameahidi kuwa kutakuwa na jambo kubwa litakalowashangaza wengi na kuwanyamazisha wanaowabeza na kuwashambulia mitandaoni.

Read More
 Mke wa Guardian Angel Afunguka Kuhusu Matusi Mtandaoni

Mke wa Guardian Angel Afunguka Kuhusu Matusi Mtandaoni

Mke wa mwimbaji wa Injili Guardian Angel, anayefahamika kama Esther Musila, ameapa kupambana vikali na wakosoaji wake mtandaoni hadi mwisho wa dunia. Kupitia ukurasa wake wa TikTok, Musila amesisitiza kuwa hatakubali kunyamaza huku akivunjiwa heshima mtandaoni bila kujibu. Mwanamama huyo ameonyesha hasira yake kwa watu wanaojiona wana uwezo wa kudhibiti maisha ya watu wengine, akisema wazi kwamba atajibu matusi kwa matusi inapobidi. Kauli hiyo imekuja kufuatia mijadala iliyoanzishwa na madai ya msanii, Shiru wa GP ambaye hivi karibuni alidai kuwa marehemu Betty Bayo aliogopa sana hali yake ya kiafya kujulikana kwa umma kutokana na hofu ya kuhukumiwa. Shiru wa GP alidai kuwa hofu ya Betty Bayo ilitokana na jinsi alivyokuwa amedhalilishwa na kuhukumiwa mtandaoni miaka kadhaa iliyopita.

Read More
 Mke wa Guardian Angel Atoa Majibu Makali kwa Wakosoaji wa Ndoa Yake

Mke wa Guardian Angel Atoa Majibu Makali kwa Wakosoaji wa Ndoa Yake

Mke wa msanii wa muziki wa injili Guardian Angel, Esther Musila, ametoa majibu makali kwa wakosoaji wanaoendeleza mazungumzo kuhusu ndoa yake, akisisitiza kuwa uhusiano wao si wa kujadiliwa na umma. Kupitia mfululizo wa video alizochapisha kwenye mitandao ya kijamii, Musila amesema kuwa hana haja ya kutoa maelezo kwa mtu yeyote kuhusu ndoa yake, akibainisha kwamba yeye na Guardian Angel hawakuwahi kutafuta idhini ya mtu yeyote kabla ya kufunga ndoa. Musila ameeleza kuwa watu wengi wamekuwa wakimkosoa kwa sababu ya tofauti ya umri kati yake na mumewe, lakini akasisitiza kuwa thamani yake haiwezi kupimwa kwa miaka yake. Ameongeza kuwa Guardian Angel alimchagua kwa sababu ya utu wake na si kwa sababu ya umri. Aidha, amesisitiza kuwa ndoa yao si biashara ya mtu mwingine na kwamba watu waligundua kuhusu ndoa yao kupitia mitandao ya kijamii. Amesema kuwa watu wanaoendelea kumzungumzia kwa msingi wa umri wanapoteza muda kwa sababu yeye ni zaidi ya miaka yake na ana utambulisho wake binafsi. Mwanamama huyo wa watoto watatu amemalizia kwa kueleza kuwa hana mpango wa kuondoka katika ndoa yake, akiwataka wakosoaji wake waache kumfuatilia na waendelee na maisha yao.

Read More
 Esther Musila Awajibu Wanaomshauri Aache Kujibizana na Watu Mtandaoni

Esther Musila Awajibu Wanaomshauri Aache Kujibizana na Watu Mtandaoni

Mwanamitindo na mpenzi wa muziki wa injili Esther Musila ametoa majibu kwa wakosoaji wanaomshauri aache kujibizana na watu wanaomkejeli kwenye mitandao ya kijamii. Musila, ambaye ni mke wa msanii wa injili Guardian Angel, amekuwa akilengwa mara kwa mara na maneno ya kashfa mtandaoni, hasa kuhusu umri wake na uhusiano wake na mwanamuziki huyo. Baadhi ya wafuasi wake wamekuwa wakimshauri apuuze maneno hayo na asiwajibu wanaomkosoa. Hata hivyo, kupitia ukurasa wake wa Instagram, Musila alisema kuwa watu wengi hudhani ukikaa kimya ni udhaifu, lakini kwake, kujibu ni njia ya kuonesha kujitambua na kujiheshimu. Alieleza kuwa hana tatizo kujitetea pale anapohisi kushambuliwa, kwani kufanya hivyo hakumaanishi hana busara bali ni kutetea utu wake kama binadamu. Kauli yake imezua hisia mseto mtandaoni, huku baadhi ya mashabiki wakimpongeza kwa kusimama kidete kujilinda, ilhali wengine wakimshauri aendelee kupuuza maneno ya chuki na kuzingatia mambo chanya. Musila na Guardian Angel wameendelea kuonesha kuwa hawajali maneno ya watu, wakionekana mara kwa mara wakishirikiana kwenye matukio mbalimbali na kuonesha mapenzi yao hadharani bila woga.

Read More
 ESTHER MUSILA ATOA WITO KWA WANAWAKE KUWAWEKA WAUME ZAO KWA MAOMBI

ESTHER MUSILA ATOA WITO KWA WANAWAKE KUWAWEKA WAUME ZAO KWA MAOMBI

Mke wa msanii Guardian Angel,Esther Musila ametoa changamoto kwa wanawake walio kwenye ndoa kujenga tabia ya kuwaweka waume zao kwenye maombi. Akipiga stori na SPM BUZZ Musila amesema maombi yana nguvu kubwa sana katika maisha ya ndoa kwa kuwa inaleta familia pamoja lakini pia inawasaidia wanandoa kufanikisha baadhi ya mipango yao. Mwanamama huyo wa miaka 52 amesema amekoshwa sana na mienendo ya mama taifa Bi Rachel Ruto ya kumtanguliza Mungu kwa kila jambo ambapo amehapa kwamba atafuata nyayo zake kuhakikisha mume wake Guardian Angel anafanikisha ndoto zake katika maisha. Utakumbuka Guardian Angel na mke wake Esther Musila ni miongoni mwa wasanii watakao toa burudani Septemba 13 katika hafla ya kuapishwa kwa Rais mteule wa Kenya Dkt. William Samoe Ruto kwenye uga wa kamataifa wa Kasarani.

Read More
 GUARDIAN ANGEL AFUNGA NDOA YA SIRI NA MCHUMBA WAKE ESTHER MUSILA

GUARDIAN ANGEL AFUNGA NDOA YA SIRI NA MCHUMBA WAKE ESTHER MUSILA

Nyota wa muziki wa injili nchini Guardian Angel ameripotiwa kufunga ndoa ya siri na mchumba wake Esther Musila  baada ya kuwa kwenye mahusiano kwa takribani mwaka mmoja. Kulingana na wajuzi mambo kwenye mitandao ya kijamii,Harusi hiyo ambayo inadaiwa kuwa ya siri imiefanyika leo jijini Nairobi na kuhudhuriwa na wageni wasiozidi 20, ikiwemo ndugu wa pande zote mbili za familia zao. Hata hivyo mashabiki wengi kwenye mitandao ya kijamiii wamefurahia kwa hatua ya wawili hao kuhalalisha mahusiano yao huku wengine wakiwa na mshangao kwanini ndoa hiyo imekuwa ya siri japokuwa ni jambo la kheri kwa kila mwanadamu Uhusiano wa kimapenzi wa hao ulianza mapema mwaka jana 2021, huku Guardian Angel akithibitisha mahusiano hayo rasmi baada ya ukaribu wake na mwanamama huyo mwenye umri wa miaka 51 gumzo mtandaoni ambapo  wengi walishangazwa na hatua ya msanii huyo kutoka kimapenzi na mtu ambaye amemzidi umri.

Read More