Esther Musila awajibu wakosoaji: “Mali ni zangu, mume ni wangu”
Mke wa msanii wa muziki wa injili Guardian Angel, Esther Musila, amewajibu vikali watu wanaodai kuwa mali anazomiliki ndizo zimemshawishi mume wake kuendelea kusalia katika ndoa yao, licha ya tofauti kubwa ya umri kati yao. Kupitia ujumbe aliouweka Tiktok, Esther ameonyesha kushangazwa na madai hayo akisema hawezi kutishwa na maneno ya watu mtandaoni. Amesisitiza kuwa mume ni wake na mali anazomiliki ni zake, hivyo hana sababu ya kuishi kwa kuogopa mitazamo ya wengine. Esther ameenda mbali zaidi na kuwataka wakosoaji watafute wapenzi wao na wawape pesa kama wanavyoamini yeye anavyomfanyia Guardian Angel, badala ya kutumia muda mwingi kuzungumzia ndoa yake. Mwanamama huyo ambaye amekuwa pamoja na Guardian Angel kwa miaka 6, amedokeza kuwa mwaka 2026 ataendelea kumpenda mume wake zaidi, akisema hilo litawapa wakosoaji jambo jipya la kuzungumzia.
Read More